A Program Note: Tutaweka Hoja Zetu Wazi

A Program Note: Tutaweka Hoja Zetu Wazi

Namheshimu sana Dr SLAA ,naamini ni mapumziko ya muda tu ya kimkakati.mapambano ya kuing'oa ccm yapo palepale.viva UKAWA viva CDM.
Kweli kabisa mkuu
Wala kelele za chura hazimzuwi ngombe kunywa maji!
Chadema ni mpango wa mungu!
Wa Tanzania hatuhitaji ngonjera nyingi kwa muda huu!
 
Mimi napenda kuwa muwazi, ni muumini wadhati wa CCM, ila si mwanachama. Humu kwenye jamvi huwa tuaonesha hisia zetu zaidi, na pengine tunapindisha ukweli.Nilipo msikia mbowe kwa kauli iliyo onyesha wazi imeficha jambo zito ndani yake, kauli iliyo thibitisha hayo ni ile alipo sema chama lazima kisonge mbele bila kujali uwepo wa Slaa, Baregu na Mbowe. Kwa kauli hii inatosha kusema kuwa hata iledhamana mliyopewa na wananchi sasa inarudi kwa CCM. Silaha za kuzitumia tunazo
 
Mkuu
with serious note!

"Hatukukaa kimya kwa watawala walioshindwa wa sasa, na hatuwezi kukaa kimya kwa wanaotaka kuwa wa kesho" MM

Mkuu nimekuuliza una Agenda gani ya siri ambayo hutaki ifahamike?

KWANINI SASA NA SI WAKATI ULE?

Je wadhani watanzania wengi wa sasa wangali na akili za kushikiwa?

SIASA NA UANAHARAKATI NI VITU MBALIMBALI, NARUDIA TENA "HAKUNA ANAETAKA BIASHARA YA HASARA" NA UKITAKA UKWELI ZAIDI HAKUNA YEYOTE ALIYEWAHI KUWA CCM AKAWA MSAFI.

NA JE UNA MAANA MHESHIMIWA DR. SLAA WAKATI ANAGOMBEA UBUNGE KWA TIKETI YA CHADEMA ALIPOTOKA CCM CDM HAWAKUWA NA MGOMBEA?

KAMATI KUU YA CDM SI WENDAWAZIMU, JE MZEE BAREGU NA PRO. SAFARI UNAWAZIDI MAARIFA?

TUNAAMBIWA TUITAZAME AIBU YETU KABLA YA KUISEMA YA WENGINE.

Wakatabahu
 
Mbona mnalialia kwani nyie mmejipangaje? Nyie tulieni atoe hoja.
Kati ya zitto na team mbowe nani wameisaliti cdm kimisingi

Tumetoka huko tunatafuta NJIA SALAMA ya kupita.Usiturudishe nyuma tena
 

Mkuu
The Boss, asante kwa kulizungumzia hili la double standard ya Chadema na wafuasi-waabudu wao!, na kiukweli siku zote huwa naikubali objectivity yako!.

Mimi nimepigia sana kelele suala la kufuatwa kwa sheria, taratibu na kanuni huku baadhi yetu wanajidai kupigania haki, wakinyamaza kimya wakati Chadema ikifanya madudu ya wazi!, lakini sasa inapotokea payback time ya 'karma', what goes around, comes around, eti ndio watu wanasusa!, na kuja na hoja kibao za kutokubaliana na kilichofanyka!, what a double standards!.

Kuna tatizo kwa baadhi ya wapenzi wa Chadema, kuwaabudia baadhi ya viongozi wao na kuwaona kama ni miungu watu!, sasa hii miungu watu wa Chadema, inapopuuzwa, waabudu wao wanaiona hii kama ni blasphemy!, mungu wao amekashifiwa!.

Kuna wakati shetani huwa una disguise as god!, na kuna wakati hata shetani mwenyewe kabla ya kuwa shetani, alikuwa malaika!, hadithi ya Paulo na Sauli ni funzo tosha kwa ujio wa Lowassa ndani ya Chadema!, kama Mungu ndio alipepanga mpango huu, hawa wote wanaoupinga ni mashetani disguised as malaika!.

Ningekuwa mimi ni sehemu ya Chadema, wote hawa ningefukuzia mbali na sio kubembeleza!. Utafiti umeishafanya kuwa kuna watu asilimia 10%, ndani ya Chadema watapinga ujio wa Lowassa, lakini gaini itakuwa ni asilimia 38%, nashauri timulia mbali hii asilimia 10% the sooner the better, gain the 38% safari ya matumaini iendelee!.

Kikukweli Magufuli ni mzuri kuliko Lowassa, na CCM is still stronger than UKAWA kwa ujumla wake wote, ila ushindi kwa UKAWA kupitia kwa Lowassa lies on the "positive will power" kwa wanaotaka mabadiliko ya kweli, sasa hawa kenge kwenye msafara wa mamba, wanatuwekea kiwingu cha "negative will power" ambayo itapunguza margin ya ushindi kwa sababu hata hao nao hizo negative will zao nazo zina power kama alivyo devil or satan mwenyewe!.

NB, pia inawezekana na mimi ndio nikawa wrong kuwa CCM ndio malaika na ndio mpango wa Mungu CCM iendelee kuitawala Tanzania, halafu Lowassa ndio mpango wa shetani, hivyo sisi wote tunaosupport ujio wa Lawassa ndio tunaomtumikia shetani, na wote wanaopinga ujio wa Lowassa Chadema, ndio wanaofanya kazi ya Mungu!, that being the case, naomba kuwaomba radhi hao niliowaita mashetani!, kumbe mashetani ni sisi!.

Pasco.
Pasco your right 100% waache wasuse sisi tunaendelea hakuna namna ccm out 2015 nilazima kwa afya ya nchi yetu mama Tanzania .
 
Mzee Mwanakijiji, hebu turudi nyuma...Flashback 1995, kuna mambo mawili yalitokea;

1. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Augustino Lyatonga Mrema, baada ya kugundua anayo nafasi finyu ya kuteuliwa kugombea Uraisi kupitia CCM, alihamia NCCR - Mageuzi. Mrema hakuwa ametoa mchango wowote katika harakati za mageuzi na badala yake ndiye kinara aliyeongoza majeshi ya Usalama kupinga mageuzi kwa njia ya virungu, mabomu ya machozi na risasi za moto. Wako waliopigwa na kuteswa, wako waliopata ulemavu wa kudumu, wapo waliopoteza kazi na kufungwa na familia zipo zilizosambaratishwa na kusahaulika. Mwaka 1995 ndio mwaka uadui kati ya vyombo vya usalama na raia ulipozaliwa na ni huyo huyo Mrema ambaye awali aliapa kwamba akihamia upinzani laana imkute. Wakati huo tuko wengi wetu tulipinga sana Mrema kukaribishwa NCCR - Mageuzi lakini hatukusikilizwa hadi wengine tukakata tamaa kabisa na kuachana na siasa.

2. Dr. Wilboard P. Slaa aliwekewa mizengwe baada ya kushinda katika kura ya maoni kwa asilimia kubwa tu akiwa CCM na hivyo kuamua kuhamia Chadema na huko akateuliwa kugombea Ubunge. Alishinda kura na kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Karatu na akatokea kuwa moja katika wabunge machachari walioichachafya CCM hadi kujizolea sifa nje na ndani ya bunge. Baada ya muda aliweza kuaminiwa na kila mwanachadema na baadaye uteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho.

Mzee Mwanakijiji, kwa bahati mbaya CCM ni zaidi ya chama cha siasa. CCM ni zao la chama dola na ilirithi kila kitu kilichomilikiwa na chama dola, chama kilichoshika madaraka na chama kilichokuwa na mamlaka ya mwisho katika maamuzi yaliyolihusu taifa hili. Serikali ilikuwa chini ya CCM, Bunge lilkuwa chini ya CCM, mahakama zilikuwa chini ya CCM na vyombo vyote vya dola vilikuwa chini ya CCM. Kuipinga CCM kulitafsiriwa kama uhaini na katiba ya nchi ilifanyiwa marekebisho kwa kuangalia na kutanguliza matakwa ya CCM. CCM ilitumia kila njia kuzuia upepo wa mageuzi na hata pale ilipoonekana wazi kwamba kwa mara ya kwanza wanajaribu kupambana na kile kinachowazidi uwezo, walihakikisha wanayapokea hayo mageuzi kwa maneno lakini si kwa moyo wala matendo.

Waliendelea kuhatamia kila kitu walichokimiliki kama vile vyama vya upinzani havikuwepo, waliendeleza mfumo ule ule kwa nguvu zile zile, wakijilinda kwa mbinu zile zile za wakati wa chama kimoja. Kusema kweli hadi leo hali hii haijabadilika; kinadharia tunavyo vyama vya upinzani lakini kimfumo tunacho chama kimoja, CCM. Mijadala ndani ya Bunge Maalum La Katiba mwanzoni mwa mwaka huu yalizidi kuthibitisha kwamba hatuna upinzani nchini, tunavyo tu vyama vinavyotambulika vitabuni kama vya siasa lakini mchango katika mustakabi wa taifa haupewi umuhimu wowote na CCM. Wakikataa kuunga mkono pendekezo lolote la serikali CCM haijali itaendelea na utekelezaji kama kawaida na wakileta za kuleta, vyombo vya dola vipo kuwadhibiti na kuwatia adabu, kama alivyosema Pinda, wamechoka kuwa wavumilivu hivyo hamna namna na dawa ni kupiga tu.

Mzee Mwanakijiji, CCM kama ilivyo, ni ndoto kuamini kwamba kuna siku itakubali kuachia madaraka kupitia sanduku la kura hata kama wananchi watakuwa wamewachoka. Hii ndiyo sababu wengine tunasema, adui wa nchi hii kwa sasa si Kikwete, si Nape, si Kinana, si Makonda, si Lowassa, si Pinda, hapana, adui wa nchi hii ni mfumo unaoiwezesha CCM kubaki madarakani hata kama haina tena sifa wala uwezo. Katika kipindi kifupi kilichopita serikali yetu imeimarisha sana vyombo vya Usalama, imeagiza mabomu ya machozi, maji ya kuwasha, silaha za moto na vitu kama hivyo. Ukitazama kwa undani, tahayari hizi zote ni katika mipango ya kwadhibiti wananchi na zimetokana na woga, woga wa CCM kuketishwa benchi, woga wa mafisadi kukosa pahala pa hifadhi, CCM na woga wa kuwajibishwa na wananchi kwa vitendo vyao.

Mzee Mwanakijiji, najua yote haya unayafahamu. Najua unajua tahadhari yote hii inatokana na nini. Mwaka 2010 kabla ya Uchaguzi alitokea mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Luteni Jeneral Shimbo, akiwaonya wanachi kuwa tayari kuyapokea matokeo kama yatakavyotangazwa na Tume na kwamba atakayekaidi atashughulikiwa. Siku chache baadaye akatokea Mhariri Mkuu wa Magazeti ya serikali akiapa kwamba katu upinzani hauwezi kutwaa madaraka ya nchi hii. Haya yalikuwa ni matamshi ya hatari sana katika nchi inayoheshimu utawala wa sheria lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa kwa hawa wachochezi. Badala yake tumeshuhudia wakiongezewa myadhifa ndani na nje ya nchi. Swali kubwa hapa ji je kama wananchi tunao uhuru gani wa kujichagulia nani atuongoze?

Mzee Mwanakijiji, CCM kama ilivyo imejizatiti kweli kweli kwa lolote lile kuhakikisha hakiyumbishwi na mtu, kikundi au chama, wako tayari kutumia kila mbinu, kila nyenzo na kila silaha kujilinda hata ikiwa ni pamoja na kuvunja katiba. Kwamba kuna medium, hata kama ni mtu, inaweza kusababibisha kwa namna fulani kulisambaratisha hili zimwi, mimi ni katika wale watakaoikaribisha hiyo medium. Zaidi ya hapo hakuna namna, labda kwa kuchukua silaha na kuingia msituni kitu ambacho sikiafiki hata kidogo. CCM ikipasuka vipande vipande kama ninavyoomba mimi, siku hiyo hata mimi nitamwagika mtaani kushangilia, wewe je? Bila hivyo tuanze tu kunyoa tukjitayarisha kwa maumivu kama yale yale tulioaminishwa yangeisha mwaka 1985, 2000, 2005 na 2010.

Wewe endelea kuflash back .ngoja sisi tuingie field .maana wewe nakushangaa adui yupo mbele yako anasubiri pigo moja la mwisho ushinde vita .wewe unarudi unaanza kuflash back.ngoja baada 25 October tukirudi na ushindi tutakutunuku jina jipya .Mzee wa kuflash back .
 
Tusubiri tamko la kijasusi kutoka kwa wanaojifanya wenye chama hata kama wanaharibu. Huo ndo uwazi.

Tangu kipindi cha ZZK nilipata mshituko na CDM. Ni mwanachama ila macho yangu yanaangaza kila kitu kabla sijaamua kutenda.

mkuu ZZK mpaka leo wana muita msaliti wa chama, nimejifunza kitu kabla ya kumjia mtu juu ni vema nisikize pande zote mbili.la sivyo tutahukumu watu wasio na hatia
 
Hapana mkuu....si sawa kabisa....tuwe honest... wengine tuliwahukumu hatua kwa hatua....kwa mambo mengi.....hii case tusichanganye kabisa na wengine....tafadhali tuheshimu hilo.....
....huwa najiuliza iweje watu leo wanakua so sympathetic na Dr.Slaa alafu wanasahau yeye alivyosimamia kina Zitto kufukuzwa chadema.....na hapa wala Dr. hajafukuzwa hivyo...Ifike mahali tuwe fair bana....kama wanavyosema huko chadema hakuna aliye juu ya chama...hata awe dr.Slaa...
 
Hatuishi kwenye chama kwa sababu ulipigania ili ule matunda,wapo wengi duniani waliipigania kufyeka mapori,Lakini wanaokulamatunda niwajukuu!!

Chadema ni chama cha siasa,na siasa ni watu,tunahitaji watu kukisaidia chama kishinde madaraka,hatuhitaji mtu apiganie chama akusubiri kulipwa fadhila!!

Hata vitabu vya dini havisemi hivyo!
 
Hatuishi kwenye chama kwa sababu ulipigania ili ule matunda,wapo wengi duniani waliipigania kufyeka mapori,Lakini wanaokulamatunda niwajukuu!!

Chadema ni chama cha siasa,na siasa ni watu,tunahitaji watu kukisaidia chama kishinde madaraka,hatuhitaji mtu apiganie chama akusubiri kulipwa fadhila!!

Hata vitabu vya dini havisemi hivyo!

Katika mapambano vita vinapokuwa vikali ushindi ni karibu. Ninaamini kuwa uchaguzi wa mwaka huu 2015 unafungua historia mpya ya mapambano. Kama UKAWA watachukua nchi nao wakajifanya ni miungu tutawatoa kama tutakavyowatoa CCM. Mapambano na CCM yanahitaji silaha zote za maangamizi kama bomu la Nagasaki au Hiroshima. Baada ya kuwapiga kwa" nuclear bomb " lazima kutakuwa na makubaliano ya mustakabali wa nchi hii. Namkubali saaana Dr. na ninaheshimu maamuzi yake, lakini kipindi kilichosalia akubali tufumbe macho na pua tuvuke hadi ng'ambo. Kule ng'ambo kuna uponyaji utakaoponya nchi hii. Hakuna anayeweza kuzuia shauku ya watu wa nchi hii kupata ukombozi, hiki ni kipindi cha " leap forward".
 
MADA YENYEWE IKO HAPA TAFADHALI

PENDEKEZO LA MARIDHIANO

Mzee Mwanakijiji

CDM will go the same way NCCR did post-1995 election, specifically in 1997. Baada ya kushindwa uchaguzi hapo October 2015, CDM wataanza kulumbana na kutupiana mawe na kutimuana. Mwisho wa yote itakuwa kama Mrema na NCCR 1997 kule Tanga, Mkonge Hotel. Itachukua tena muda kuanzan kujenga any meaningful opposition wakati CCM wakitamalaki madarakani....

With Marando present in CC ya CDM (ambaye pia alikuwemo NCCR pale Mkonge Hotel 1997) and Apson eti mshauri wa mgombea wa CDM Lowassa the pattern is unfolding....CDM wanafuata script iliyoandikwa tayari.

CC:The Boss Pasco,
 
Only Blind and deaf will not see this wave!

Dr. Slaa is a hero but personal belief will not win you a political battle my brothers!
 
MM....kwavile Mungu kanipa akili....nitaitumia vyema.....haiwezekani tumpuuze Dr Slaa dakika hii.....wengine tunajua mapito yake....nitasimama nae......

Tuko pamoja mkuu. Moyo wangu umeumia sana. Nguvu ya pesa imevunja vunja misingi mikuu ya chama, hii hakubaliki. Kukaa kimya ni kubariki uharamia huu.
 
Kweli naamini zile hela za CCM zimekufikia..mtu aliyenipa taarifa kuwa umenunuliwa na CCM kuvuruga nilijua utani sasa nimeamini..Ndugu zangu tegemeani maandiko mengi kutoka kwa huyu mtu kuanzia kesho...kama ungekuwa na nia ya dhati ungejua adui yetu ni CCM..ungetumia busara ya kubaki kimya kama ulivyobaki kimya wakati anasulubiwa Zzk..Arfi..Kafulila and the like..Wanachadema wanahitaji kuficha tofauti zao sasa ili kuitoa Ccm

Hivi ni kwa nini CHADEMA wengi humu wanakuwa simple mind kiasi hiki? Hakuna tena logical reasoning zaidi ya kuongozwa na mihemko tu.
 
Mzee Mwanakijiji, tunasubiri kwa hamu kubwa kile mlichoandaa. Tuko wengi kuliko inavyodhaniwa, wale tuliokwazwa na kukatishwa tamaa na mabadiliko ya ghafla ya malengo ya msingi ya CHADEMA. Ukweli pekee ndio utakaokinusuru chama.
 
Last edited by a moderator:
Hayo ni mawazo yako na ofcourse ni sahihi kwako lakini mimi naona hayako sahihi !. Zitto tumeshaachana naye na this time tukishirikiana na vyama vingine katika UKAWA tutachukuwa utawala wa nchi hii.

Hao unaodai wanafikiria kula na wewe unayejiona ndio unafikiria maendeleo weight ya kura yako na zao inalingana !. Kura yako haina weight zaidi ya kura ya mtu mwingine. Its all about numbers and this time we have enough.....

WaTz wengi wakati huu, wameichoka CCM na wanaamini CDM na UKAWA na kwa kura zao tutawapiga chini CCM na kuunda serikali itakayoleta katiba mpya ya wananchi na kuweka mifumo itakayoleta haki kwa wananchi wote na hapo naamini maendeleo yanayoistahili Tanzania ndipo yatakapopatikana !

Hili ni la kuwambia wanaofikiria kula tu na si maendeleo.

Mbowe alikuwa anamuogopa ZZK kuliko CCM. Ni ZZK tu aliyekuwa na uwezo wa kuongoza na kuridhi kiti. Kwa sababu ya kutoruhusu wengine washike chama matokeo yake walitengeneza zengwe ambalo hata sehemu moja huwezi ona uhusika wa ZZK ingawa ndo alikuwa anasakamwa.

Hayo tuache, kwa hili linatotokea ni mwendelezo wa hayo ya familia kuongoza chama. Kwa bahati mbaya imekuwa fedheha kwa baadhi ya wateule.
 
Stay Tuned: Tunatarajia kutengeneza njia mahali hapa ambapo panaonekana hakuna njia. Siyo sahihi kuwaachia nchi na hatima ya nchi watu ambao hawakutoa hata tone moja la jasho kupigania mabadiliko ya siasa.

Iweje leo hii baada ya yote ambayo watu wamesimamia wengine kwa damu na wengine hata kwa uhai wao waje watu wavune wasichopanda kwa ahadi kuwa ati na sisi tutakula nao watakachovuna?

Kesho Inshallah, tutaweka hoja zetu wazi ili wao waamue kama wanataka kuungwa mkono nasi au la; hatutaki wao watuwekee masharti ya sisi kuwaunga wao mkono au kutupigisha mikwara ya kwanini tukae kimya ili wao wafanye wanalotaka.

Hatukukaa kimya kwa watawala walioshindwa wa sasa, na hatuwezi kukaa kimya kwa wanaotaka kuwa wa kesho!

MM

NB: Nitajaribu kutoa majibu ya hoja zilizotolewa na baadhi ya watu (ikiwemo ile mada ya Character X) kuhusiana na kuunga mkono hili la Lowassa.

Mzee Mwanakijiji, nakumbuka kulikuwa na kanzi kako kanazunguka katika maeneo fulani, nilitumai kuwa mida hii katakuwa kamenusanusa zile kurasa tatno ambazo Dr Mwakyembe alikataa kuzisoma kwa kuogopa.

Sijui kama mbwenelehi walikimbia nazo au ka-nzi kanaweza kunusa. Ingekuwa vizuri ukitusaidia. Ni kama watu wanasahau Richmond ni nini, naona kuwa wanaweka jina moja tu wakati ilikuwa na majina mengi, au kwa kuwa RA alifungua vifungo vya gamba yeye amesahaulika? wengine je?

It sickens kusikia watu wanalalamikia fisadi mmoja wakati kuna wengine wengi tu.
 
images




CCM IKO NJIANI KUFA KIFO HIKI
 
Stay Tuned: Tunatarajia kutengeneza njia mahali hapa ambapo panaonekana hakuna njia. Siyo sahihi kuwaachia nchi na hatima ya nchi watu ambao hawakutoa hata tone moja la jasho kupigania mabadiliko ya siasa.

Iweje leo hii baada ya yote ambayo watu wamesimamia wengine kwa damu na wengine hata kwa uhai wao waje watu wavune wasichopanda kwa ahadi kuwa ati na sisi tutakula nao watakachovuna?

Kesho Inshallah, tutaweka hoja zetu wazi ili wao waamue kama wanataka kuungwa mkono nasi au la; hatutaki wao watuwekee masharti ya sisi kuwaunga wao mkono au kutupigisha mikwara ya kwanini tukae kimya ili wao wafanye wanalotaka.

Hatukukaa kimya kwa watawala walioshindwa wa sasa, na hatuwezi kukaa kimya kwa wanaotaka kuwa wa kesho!

MM

NB: Nitajaribu kutoa majibu ya hoja zilizotolewa na baadhi ya watu (ikiwemo ile mada ya Character X) kuhusiana na kuunga mkono hili la Lowassa.

MM KAA UKIJUA MBELE ZA HAKI wa saa 3 asubuhi saa 6 mchana na saa 12 jioni wote watalipwa ujira mmoja hakuna cha kujitetea eti mbona mimi nimefanya kazi tangu asubuhi na huyu kaja jioni halafu tunalipwa ujira sawa
 
Hekima,Busara,Heshima,Utu,Uzalendo,unyenyekevu,na Maono vyatakiwa sana wakati huu kuliko wakati mwingine wowote..Ugomvi wa baba na mama wenye hekima uishia chumbani si mpaka watoto na majirani wajue...Maridhiano yapewe nafasi kwa upendo na uzalendo kwa chama na taifa..tuinuke wamoja,tutembee wamoja,tukimbie mchakamchaka wamoja na tukaketi nchi ya ahadi pamoja!!!! Hakuna Lisilowekana kwa waaminio ktk haki,Kweli,Maridhiano na ushindi...

Hakika umenena vyema sana mwamamichakato,mambo haya wanayotaka kuyaweka hadharani sasa ni kwa faida ya nani?Ninathamini sana michango ya wanachama wote wa CDM kuanzia viongozi wakuu na wanachama wa kawaida,ninaamini DR alishirikishwa hatua kwa hatua kwenye hili la kumpokea EL kama hawakuridhiana bado kulikuwa na nafasi ya kuendelea na maridhiano mpaka suluhisho lipatikane,leo hii naona malumbano yanaaza katikati ya mechi ikiendelea,kwa sisi wapenzi wa mpira kocha anaongea na players wake halftime wakiwa changing room,mkijibizana uwanjani katikati wakati mpira unaendelea ni kumpa adui yako nguvu ya kukupiga bao,tena la mkono alilosema Nape.Mzee Mwanakijiji nachelea kusema ya kuwa upinzani wetu bado sana na itatuchukua watanzania miaka nenda rudi kupata mabadiliko,nahisi wananchi tuko tayari ila viongozi wetu hamna dhamira ya dhati,nilifikiri wapinzani wakuu ambao wangevunja UKAWA na kumkataa EL ni CUF,jana nikamuona Duni Hadji(jembe)nikafarijika sana,ila ninaposoma hizi simulizi zenu nikakumbuka ile hadithi ya mwana mpotevu aliepewa sehemu ya urithi wake akaenda kutapanya na makahaba na ailiporejea kwa baba yake kutubu,yule nduguye muaminifu alikasirika aliposikia nduguye karejea na baba amemchinjia ndama alienona na amemfanyia sherehe,Dr hakupaswa kususa,muungwana hanuni kwa mashavu,hununa moyoni.
 
Back
Top Bottom