Mambo haya wanayotaka kuyaweka hadharani sasa ni kwa faida ya nani?Ninathamini sana michango ya wanachama wote wa CDM kuanzia viongozi wakuu na wanachama wa kawaida,ninaamini DR alishirikishwa hatua kwa hatua kwenye hili la kumpokea EL kama hawakuridhiana bado kulikuwa na nafasi ya kuendelea na maridhiano mpaka suluhisho lipatikane,leo hii naona malumbano yanaaza katikati ya mechi ikiendelea,kwa sisi wapenzi wa mpira kocha anaongea na players wake halftime wakiwa changing room,mkijibizana uwanjani katikati wakati mpira unaendelea ni kumpa adui yako nguvu ya kukupiga bao,tena la mkono alilosema Nape.Mzee Mwanakijiji nachelea kusema ya kuwa upinzani wetu bado sana na itatuchukua watanzania miaka nenda rudi kupata mabadiliko,nahisi wananchi tuko tayari ila viongozi wetu hamna dhamira ya dhati,nilifikiri wapinzani wakuu ambao wangevunja UKAWA na kumkataa EL ni CUF,jana nikamuona Duni Hadji(jembe)nikafarijika sana,ila ninaposoma hizi simulizi zenu nikakumbuka ile hadithi ya mwana mpotevu aliepewa sehemu ya urithi wake akaenda kutapanya na makahaba na ailiporejea kwa baba yake kutubu,yule nduguye muaminifu alikasirika aliposikia nduguye karejea na baba amemchinjia ndama alienona na amemfanyia sherehe,Dr hakupaswa kususa,muungwana hanuni kwa mashavu,hununa moyoni.