Askofu Rweyongeza: Kuna watu na makundi yanayotumia nguvu, risasi na mabomu ya machozi kwa sababu ya kushindwa hoja

Askofu Rweyongeza: Kuna watu na makundi yanayotumia nguvu, risasi na mabomu ya machozi kwa sababu ya kushindwa hoja

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
369,733
Reaction score
855,779
Askofu wa Jimbo Katoliki la Kayanga mkoani Kagera, Mhashamu Almachius Vincent Rweyongeza, amesema kuna watu na makundi katika jamii ya leo yanayotumia nguvu, risasi na mabomu ya machozi kwa sababu ya kushindwa hoja, akifananisha tabia hiyo na akina Herode waliokataa kumpokea Yesu Kristo, Mfalme wa Amani.

Akizungumza katika Homilia yake, Askofu Rweyongeza amesema watu wanaoshindwa katika hoja, tafakari, midahalo na maridhiano mara nyingi hukimbilia matumizi ya nguvu ili kunyamazisha sauti za wanaotumia hoja na fikra.

Amesema kundi la kwanza la watu wasiompokea Yesu ni akina Herode, akiwataja kuwa ni watu wenye ubinafsi, uchu wa madaraka na ukatili, ambao hawapendi kushauriwa, kuonywa wala kusemwa, na badala yake hutumia nguvu pale wanaposhindwa hoja.

Askofu huyo amesema kundi la pili ni Mafarisayo, aliowataja kuwa ni wanafiki wanaotumia dini kama kifuniko cha kufanikisha ajenda binafsi, huku wakijifanya wacha Mungu lakini kwa vitendo wakijihusisha na vitendo vya ufisadi, unyonyaji na uharibifu wa taasisi za dini.

Ameongeza kuwa kundi la tatu ni la Yuda Iskariote, watu wanaomsaliti Yesu kwa busu, yaani wanaoonekana watakatifu kwa nje lakini ndani wakitafuta namna ya kunasa, kuharibu au kunufaika binafsi kupitia mali, sadaka na rasilimali za Kanisa.

Katika homilia yake, Askofu Rweyongeza amesema kundi la nne ni la akina Pilato, watu wanaoujua ukweli lakini huchagua kunawa mikono na kukaa kimya, wakiruhusu dhuluma, uonevu na mauaji ya haki kufanyika bila kuchukua msimamo wa wazi.

Ameeleza kuwa kundi la tano ni la wale aliowafananisha na Wayahudi waliomsulubisha Yesu, akiwataja kuwa ni watu wanaodhalilisha, kuumiza, kupora mali za waathirika, kuwanyonya wanyonge na hata kuwanyima yatima haki zao baada ya vifo vya wazazi wao.

Askofu Rweyongeza amesema makundi hayo bado yapo katika jamii ya leo na yanaendelea kutokumpokea Yesu kwa sura mbalimbali, licha ya kusherehekea Krismasi na kutambua kuzaliwa kwake.

Hata hivyo, amesema bado wapo watu wanaompokea Yesu kwa matendo yao, kwa kuishi katika haki, amani, maridhiano na kulinda utu wa binadamu, jambo ambalo amesema ndilo msingi wa ujumbe wa Krismasi.
1766881556326.jpg
 
Katika homilia yake, Askofu Rweyongeza amesema kundi la nne ni la akina Pilato, watu wanaoujua ukweli lakini huchagua kunawa mikono na kukaa kimya, wakiruhusu dhuluma, uonevu na mauaji ya haki kufanyika bila kuchukua msimamo wa wazi.
 
Askofu Rweyongeza amesema makundi hayo bado yapo katika jamii ya leo na yanaendelea kutokumpokea Yesu kwa sura mbalimbali, licha ya kusherehekea Krismasi na kutambua kuzaliwa kwake.
AAAIIISSEEeeee!

Huyu Askofu kaipanglia kiufundi sana 'homily' yake.

Mimi nawawaza watu kama akina Emmanuel Nchimbi, Nchemba Madilu; akina Wasira, na wengi wengine ndani ya utawala huu. Hawa wanafiti kabisa katika kundi mojawapo ya hayo aliyoyataja.

Kila kundi alilotaja, ukichukwa muda kulielewa vizuri, tunao watu hao katika Tanzania hii ya Samia Suluhu Hassan.
Akina Yuda:-----

Akina Herode:-------

Mafarizayo (wanafiki): Hapo hata usiseme kitu, CCM nzima imejaa watu hawa

Akina Herode (wabinafsi) Akina Kikwete mbali ya unafiki, pia wamejaa ubinafsi
 
AAAIIISSEEeeee!

Huyu Askofu kaipanglia kiufundi sana 'homily' yake.

Mimi nawawaza watu kama akina Emmanuel Nchimbi, Nchemba Madilu; akina Wasira, na wengi wengine ndani ya utawala huu. Hawa wanafiti kabisa katika kundi mojawapo ya hayo aliyoyataja.

Kila kundi alilotaja, ukichukwa muda kulielewa vizuri, tunao watu hao katika Tanzania hii ya Samia Suluhu Hassan.
Akina Yuda:-----

Akina Herode:-------

Mafarizayo (wanafiki): Hapo hata usiseme kitu, CCM nzima imejaa watu hawa

Akina Herode (wabinafsi) Akina Kikwete mbali ya unafiki, pia wamejaa ubinafsi
Watawachokonoa mpaka watoke mmojammoja wote
 
AAAIIISSEEeeee!

Huyu Askofu kaipanglia kiufundi sana 'homily' yake.

Mimi nawawaza watu kama akina Emmanuel Nchimbi, Nchemba Madilu; akina Wasira, na wengi wengine ndani ya utawala huu. Hawa wanafiti kabisa katika kundi mojawapo ya hayo aliyoyataja.

Kila kundi alilotaja, ukichukwa muda kulielewa vizuri, tunao watu hao katika Tanzania hii ya Samia Suluhu Hassan.
Akina Yuda:-----

Akina Herode:-------

Mafarizayo (wanafiki): Hapo hata usiseme kitu, CCM nzima imejaa watu hawa

Akina Herode (wabinafsi) Akina Kikwete mbali ya unafiki, pia wamejaa ubinafsi
📌 📍
 
sasa 'homily' ya namna hii sheikh "mkatavichwa" ataanzia wapi kuielewa?
13Mkamate sana elimu, usimwache aende zake;
Mshike, maana yeye ni uzima wako.
14Usiingie katika njia ya waovu,
Wala usitembee katika njia ya wabaya.
15Jiepushe nayo, usipite karibu nayo,
Igeukie mbali, ukaende zako.
16Maana hawalali isipokuwa wametenda madhara;
Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu.
17Maana wao hula mkate wa uovu,
Nao hunywa divai ya jeuri.
 
Hata hivyo, amesema bado wapo watu wanaompokea Yesu kwa matendo yao, kwa kuishi katika haki, amani, maridhiano na kulinda utu wa binadamu, jambo ambalo amesema ndilo msingi wa ujumbe wa Krismasi.
Haya maneno katika mstari huu; tuseme tuondoe maneno "wanaompokea Yesu"; umpe mtu yeyote mwenye akili iliyotulia ayasome kwa uangalifu mkubwa sana; huyo mtu kweli ataona jambo baya la kukazia shingo?

Raia wanaoishi "katika HAKI, AMANI, maridhiano na kulinda utu wa binaadam...". Kuna tatizo gani hapa hadi tuhimizane kulinda AMANI pekee! Ndilo liwe jambo la kipekee kabisa kama linavyohimizwa na kundi la watu?
 
Uzuri mmoja ni kuwa askofu nae yupo kwenye kundi mojawapo katika aliyoyataja.........pole yake kwani UNAFIKI huwa haumuachi mtu salama.
 
Nilimuuliza adriz mwanamke muislam msagaji anayevaa ushungi na anaswali swala tano na mwanamke ambaye si msagaji havai ushungi na haswali, yupi hapa Allah anamkubali? Na yupi Allah anamkataa? Yupi hapa ana dhambi? Na yupi hapa hana dhambi?

Dogo akala kona na kuzama chaka hadi leo hajanijibu.
 
Askofu wa Jimbo Katoliki la Kayanga mkoani Kagera, Mhashamu Almachius Vincent Rweyongeza, amesema kuna watu na makundi katika jamii ya leo yanayotumia nguvu, risasi na mabomu ya machozi kwa sababu ya kushindwa hoja, akifananisha tabia hiyo na akina Herode waliokataa kumpokea Yesu Kristo, Mfalme wa Amani.

Akizungumza katika Homilia yake, Askofu Rweyongeza amesema watu wanaoshindwa katika hoja, tafakari, midahalo na maridhiano mara nyingi hukimbilia matumizi ya nguvu ili kunyamazisha sauti za wanaotumia hoja na fikra.

Amesema kundi la kwanza la watu wasiompokea Yesu ni akina Herode, akiwataja kuwa ni watu wenye ubinafsi, uchu wa madaraka na ukatili, ambao hawapendi kushauriwa, kuonywa wala kusemwa, na badala yake hutumia nguvu pale wanaposhindwa hoja.

Askofu huyo amesema kundi la pili ni Mafarisayo, aliowataja kuwa ni wanafiki wanaotumia dini kama kifuniko cha kufanikisha ajenda binafsi, huku wakijifanya wacha Mungu lakini kwa vitendo wakijihusisha na vitendo vya ufisadi, unyonyaji na uharibifu wa taasisi za dini.

Ameongeza kuwa kundi la tatu ni la Yuda Iskariote, watu wanaomsaliti Yesu kwa busu, yaani wanaoonekana watakatifu kwa nje lakini ndani wakitafuta namna ya kunasa, kuharibu au kunufaika binafsi kupitia mali, sadaka na rasilimali za Kanisa.

Katika homilia yake, Askofu Rweyongeza amesema kundi la nne ni la akina Pilato, watu wanaoujua ukweli lakini huchagua kunawa mikono na kukaa kimya, wakiruhusu dhuluma, uonevu na mauaji ya haki kufanyika bila kuchukua msimamo wa wazi.

Ameeleza kuwa kundi la tano ni la wale aliowafananisha na Wayahudi waliomsulubisha Yesu, akiwataja kuwa ni watu wanaodhalilisha, kuumiza, kupora mali za waathirika, kuwanyonya wanyonge na hata kuwanyima yatima haki zao baada ya vifo vya wazazi wao.

Askofu Rweyongeza amesema makundi hayo bado yapo katika jamii ya leo na yanaendelea kutokumpokea Yesu kwa sura mbalimbali, licha ya kusherehekea Krismasi na kutambua kuzaliwa kwake.

Hata hivyo, amesema bado wapo watu wanaompokea Yesu kwa matendo yao, kwa kuishi katika haki, amani, maridhiano na kulinda utu wa binadamu, jambo ambalo amesema ndilo msingi wa ujumbe wa Krismasi.View attachment 3521636
Inasikitisha sana
 
AAAIIISSEEeeee!

Huyu Askofu kaipanglia kiufundi sana 'homily' yake.

Mimi nawawaza watu kama akina Emmanuel Nchimbi, Nchemba Madilu; akina Wasira, na wengi wengine ndani ya utawala huu. Hawa wanafiti kabisa katika kundi mojawapo ya hayo aliyoyataja.

Kila kundi alilotaja, ukichukwa muda kulielewa vizuri, tunao watu hao katika Tanzania hii ya Samia Suluhu Hassan.
Akina Yuda:-----

Akina Herode:-------

Mafarizayo (wanafiki): Hapo hata usiseme kitu, CCM nzima imejaa watu hawa

Akina Herode (wabinafsi) Akina Kikwete mbali ya unafiki, pia wamejaa ubinafsi
AkinaHerodi wamejaa, na wengine huwezi kuamini ukiwaona
 
Back
Top Bottom