A Program Note: Tutaweka Hoja Zetu Wazi

A Program Note: Tutaweka Hoja Zetu Wazi

Mwaka 2009 Zitto hakuzuiwa kugombea. Alitaka kugombea ila aliombwa ajitoe na akakubali angeweza kukataa na kuendelea kama angetaka.....

Mikakati yake ya 2014, ilikuwa kinyuma na taratibu za Chama na taratibu za Chama zilikuwa zinaendelea kumshughulikia kabla ya yeye kukimbilia mahakamani kuzuia mchakato wa chama kumshughulikia....



Hii ya juzi ilikuwa ni attempt ya mara ya pili kwa Zitto kutaka kugombea uenyekiti. Mara ya kwanza alizuiwa na 'wazee wa chama'. Mara ya pili, alitimuliwa wakati anapanga mikakati ya kugombea uenyekiti ambao hat aMbowe alikuwa anautaka. Ingekuwa haina shida kama Zitto angefukuza kwa makosa mengine(maana alikuwa nayo mengi) lakini sio la kupanga mikakati ya kugombea uenyekiti maana inakuwa kama Mbowe alikuwa anaogopa kushindana nae kwenye kura-kitu ambacho kinaua dhana ya demokrasia ndani ya chama.
 
kuna mahali tutakuwa tunakosea sana. Kama kuna kuna hoja na iwekwe wazi ijadiliwe, lakini hili suala la eti 'wageni', na nini sijui, halitawajenga zaidi ya kuzidi kuwagaweni.
Naona ni mwanzo wa kufungua milango ya kubaguana, kuna watu watadai wanaostahili zaidi chamani ni wanachama waishio nchini kuliko waishio nje ya nchi. Itafika mahali kabla ya kugombea uongezi mtadai ili kukidhi vigezo lazima uonyesho ngeu au jeraha mwilini mwako ulilolipata katika harakati za 'kukipigania' chama au ulete ushahidi wa mtu wako wa karibu aliyeuawa katika harakati hizi. Kufikia hapo tayari mnakuwa mmeshasahau objective yenu ya kimsingi kwa sababu ya madaraka.
Misimamo mingine ni upofu tu kuendelea kuing'ang'ania, the true meaning of victory has hidden in the truth that, 'sometimes the better way to win is to loose'.
Nisiwachoshe bwana maana waingereza wana kamsemo kao kanasema "behavior is very comfortable". Hivyo basi maamuzi ni yenu, 'mfe mkiwa maadui au mshinde mkiwa mmeungana'.
Msitusumbue sisi na hiyo misimamo isiyoeleweka unless kuna ukweli mnatuficha.

ndugu kinachoudhi sana hapa, sio kuwa na tabaka za wagombea au mipango ya kubaguana. Ila mtu yoyote anaweza ingia kwenye chama na baada ya hata mwezi akagombea nafasi yoyote ya kiungozi ndani ya chama.
Lakini sio mtu ambaye amekatwa kwenye kinyanganyiro kwenye chama chake akakimbilia chama kingine tena kwa masharti ya lazima yeye ashike sukani tena bila hata ushindani na wanachama wengine waliojijenga miaka kadha ndani ya chama. That’s not ethical at all its corrution and dictatorial behaviour period.
Si unaona sasa kuna mshururu wa vigogo wa ccm walioangushwa kwenye kura za maoni, wamefunga foleni chadema zaidi ikifuatiwa na act, wakijue au wakiwa wamehadiwa na lowassa kuwa atawasaidia.
Lowassa amewaahidi kuwaletea makapi wana chadema. Ndugu usemayo sio kweli, am not a chadema supporter, but am a true tanzanian it will disasterous is a strong opposition party like chadema is destroyed by greed. Leo serekali ya ccm haiwezi kufanya jambo bila ya kujiuliza mara mbili , jee cdm wataleta upinzani gani, a strong cdm is necessary for ccm to perform.
 
Stay Tuned: Tunatarajia kutengeneza njia mahali hapa ambapo panaonekana hakuna njia. Siyo sahihi kuwaachia nchi na hatima ya nchi watu ambao hawakutoa hata tone moja la jasho kupigania mabadiliko ya siasa.

Iweje leo hii baada ya yote ambayo watu wamesimamia wengine kwa damu na wengine hata kwa uhai wao waje watu wavune wasichopanda kwa ahadi kuwa ati na sisi tutakula nao watakachovuna?

Kesho Inshallah, tutaweka hoja zetu wazi ili wao waamue kama wanataka kuungwa mkono nasi au la; hatutaki wao watuwekee masharti ya sisi kuwaunga wao mkono au kutupigisha mikwara ya kwanini tukae kimya ili wao wafanye wanalotaka.

Hatukukaa kimya kwa watawala walioshindwa wa sasa, na hatuwezi kukaa kimya kwa wanaotaka kuwa wa kesho!

MM

NB: Nitajaribu kutoa majibu ya hoja zilizotolewa na baadhi ya watu (ikiwemo ile mada ya Character X) kuhusiana na kuunga mkono hili la Lowassa.
Kwa chama kinachoongozwa na mtu wa level ya Form Four mtategemea sana mabadiliko lakini mtajifunga mabao ya wazi, kama hili la Slaa na Lowassa.
 
Kweli naamini zile hela za CCM zimekufikia..mtu aliyenipa taarifa kuwa umenunuliwa na CCM kuvuruga nilijua utani sasa nimeamini..Ndugu zangu tegemeani maandiko mengi kutoka kwa huyu mtu kuanzia kesho...kama ungekuwa na nia ya dhati ungejua adui yetu ni CCM..ungetumia busara ya kubaki kimya kama ulivyobaki kimya wakati anasulubiwa Zzk..Arfi..Kafulila and the like..Wanachadema wanahitaji kuficha tofauti zao sasa ili kuitoa Ccm

Mbona mnalialia kwani nyie mmejipangaje? Nyie tulieni atoe hoja.
Kati ya zitto na team mbowe nani wameisaliti cdm kimisingi
 
Mzee Mwanakijiji, hebu turudi nyuma...Flashback 1995, kuna mambo mawili yalitokea;

1. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Augustino Lyatonga Mrema, baada ya kugundua anayo nafasi finyu ya kuteuliwa kugombea Uraisi kupitia CCM, alihamia NCCR - Mageuzi. Mrema hakuwa ametoa mchango wowote katika harakati za mageuzi na badala yake ndiye kinara aliyeongoza majeshi ya Usalama kupinga mageuzi kwa njia ya virungu, mabomu ya machozi na risasi za moto. Wako waliopigwa na kuteswa, wako waliopata ulemavu wa kudumu, wapo waliopoteza kazi na kufungwa na familia zipo zilizosambaratishwa na kusahaulika. Mwaka 1995 ndio mwaka uadui kati ya vyombo vya usalama na raia ulipozaliwa na ni huyo huyo Mrema ambaye awali aliapa kwamba akihamia upinzani laana imkute. Wakati huo tuko wengi wetu tulipinga sana Mrema kukaribishwa NCCR - Mageuzi lakini hatukusikilizwa hadi wengine tukakata tamaa kabisa na kuachana na siasa.

2. Dr. Wilboard P. Slaa aliwekewa mizengwe baada ya kushinda katika kura ya maoni kwa asilimia kubwa tu akiwa CCM na hivyo kuamua kuhamia Chadema na huko akateuliwa kugombea Ubunge. Alishinda kura na kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Karatu na akatokea kuwa moja katika wabunge machachari walioichachafya CCM hadi kujizolea sifa nje na ndani ya bunge. Baada ya muda aliweza kuaminiwa na kila mwanachadema na baadaye uteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho.

Mzee Mwanakijiji, kwa bahati mbaya CCM ni zaidi ya chama cha siasa. CCM ni zao la chama dola na ilirithi kila kitu kilichomilikiwa na chama dola, chama kilichoshika madaraka na chama kilichokuwa na mamlaka ya mwisho katika maamuzi yaliyolihusu taifa hili. Serikali ilikuwa chini ya CCM, Bunge lilkuwa chini ya CCM, mahakama zilikuwa chini ya CCM na vyombo vyote vya dola vilikuwa chini ya CCM. Kuipinga CCM kulitafsiriwa kama uhaini na katiba ya nchi ilifanyiwa marekebisho kwa kuangalia na kutanguliza matakwa ya CCM. CCM ilitumia kila njia kuzuia upepo wa mageuzi na hata pale ilipoonekana wazi kwamba kwa mara ya kwanza wanajaribu kupambana na kile kinachowazidi uwezo, walihakikisha wanayapokea hayo mageuzi kwa maneno lakini si kwa moyo wala matendo.

Waliendelea kuhatamia kila kitu walichokimiliki kama vile vyama vya upinzani havikuwepo, waliendeleza mfumo ule ule kwa nguvu zile zile, wakijilinda kwa mbinu zile zile za wakati wa chama kimoja. Kusema kweli hadi leo hali hii haijabadilika; kinadharia tunavyo vyama vya upinzani lakini kimfumo tunacho chama kimoja, CCM. Mijadala ndani ya Bunge Maalum La Katiba mwanzoni mwa mwaka huu yalizidi kuthibitisha kwamba hatuna upinzani nchini, tunavyo tu vyama vinavyotambulika vitabuni kama vya siasa lakini mchango katika mustakabi wa taifa haupewi umuhimu wowote na CCM. Wakikataa kuunga mkono pendekezo lolote la serikali CCM haijali itaendelea na utekelezaji kama kawaida na wakileta za kuleta, vyombo vya dola vipo kuwadhibiti na kuwatia adabu, kama alivyosema Pinda, wamechoka kuwa wavumilivu hivyo hamna namna na dawa ni kupiga tu.

Mzee Mwanakijiji, CCM kama ilivyo, ni ndoto kuamini kwamba kuna siku itakubali kuachia madaraka kupitia sanduku la kura hata kama wananchi watakuwa wamewachoka. Hii ndiyo sababu wengine tunasema, adui wa nchi hii kwa sasa si Kikwete, si Nape, si Kinana, si Makonda, si Lowassa, si Pinda, hapana, adui wa nchi hii ni mfumo unaoiwezesha CCM kubaki madarakani hata kama haina tena sifa wala uwezo. Katika kipindi kifupi kilichopita serikali yetu imeimarisha sana vyombo vya Usalama, imeagiza mabomu ya machozi, maji ya kuwasha, silaha za moto na vitu kama hivyo. Ukitazama kwa undani, tahayari hizi zote ni katika mipango ya kwadhibiti wananchi na zimetokana na woga, woga wa CCM kuketishwa benchi, woga wa mafisadi kukosa pahala pa hifadhi, CCM na woga wa kuwajibishwa na wananchi kwa vitendo vyao.

Mzee Mwanakijiji, najua yote haya unayafahamu. Najua unajua tahadhari yote hii inatokana na nini. Mwaka 2010 kabla ya Uchaguzi alitokea mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Luteni Jeneral Shimbo, akiwaonya wanachi kuwa tayari kuyapokea matokeo kama yatakavyotangazwa na Tume na kwamba atakayekaidi atashughulikiwa. Siku chache baadaye akatokea Mhariri Mkuu wa Magazeti ya serikali akiapa kwamba katu upinzani hauwezi kutwaa madaraka ya nchi hii. Haya yalikuwa ni matamshi ya hatari sana katika nchi inayoheshimu utawala wa sheria lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa kwa hawa wachochezi. Badala yake tumeshuhudia wakiongezewa myadhifa ndani na nje ya nchi. Swali kubwa hapa ji je kama wananchi tunao uhuru gani wa kujichagulia nani atuongoze?

Mzee Mwanakijiji, CCM kama ilivyo imejizatiti kweli kweli kwa lolote lile kuhakikisha hakiyumbishwi na mtu, kikundi au chama, wako tayari kutumia kila mbinu, kila nyenzo na kila silaha kujilinda hata ikiwa ni pamoja na kuvunja katiba. Kwamba kuna medium, hata kama ni mtu, inaweza kusababibisha kwa namna fulani kulisambaratisha hili zimwi, mimi ni katika wale watakaoikaribisha hiyo medium. Zaidi ya hapo hakuna namna, labda kwa kuchukua silaha na kuingia msituni kitu ambacho sikiafiki hata kidogo. CCM ikipasuka vipande vipande kama ninavyoomba mimi, siku hiyo hata mimi nitamwagika mtaani kushangilia, wewe je? Bila hivyo tuanze tu kunyoa tukjitayarisha kwa maumivu kama yale yale tulioaminishwa yangeisha mwaka 1985, 2000, 2005 na 2010.
Mkuu
with serious note!

"Hatukukaa kimya kwa watawala walioshindwa wa sasa, na hatuwezi kukaa kimya kwa wanaotaka kuwa wa kesho" MM
 
Stay Tuned: Tunatarajia kutengeneza njia mahali hapa ambapo panaonekana hakuna njia. Siyo sahihi kuwaachia nchi na hatima ya nchi watu ambao hawakutoa hata tone moja la jasho kupigania mabadiliko ya siasa.

Iweje leo hii baada ya yote ambayo watu wamesimamia wengine kwa damu na wengine hata kwa uhai wao waje watu wavune wasichopanda kwa ahadi kuwa ati na sisi tutakula nao watakachovuna?

Kesho Inshallah, tutaweka hoja zetu wazi ili wao waamue kama wanataka kuungwa mkono nasi au la; hatutaki wao watuwekee masharti ya sisi kuwaunga wao mkono au kutupigisha mikwara ya kwanini tukae kimya ili wao wafanye wanalotaka.

Hatukukaa kimya kwa watawala walioshindwa wa sasa, na hatuwezi kukaa kimya kwa wanaotaka kuwa wa kesho!

MM

NB: Nitajaribu kutoa majibu ya hoja zilizotolewa na baadhi ya watu (ikiwemo ile mada ya Character X) kuhusiana na kuunga mkono hili la Lowassa.

Nakubaliana nawe.Kwani ifike mahali tuone vyama ni vya wananchi na si vya waanzilishi wa vyama hivyo.Hata kama itabidi kuchanga pesa toka kwa wanachama kuwarudishia waanzilishi hao ili waviache vyama viongozwe na wanachama.

Ni kweli mtu mgeni unakaribishwa badala ya kuandaliwa chakula unaingia jikoni mwenyewe eti unatengeneza unachotaka wewe kula.

Hii ipo hapa kwetu.Viongozi wetu wamekosea lakini tusiwaache tuwe wamoja tukimaliza kupambana turudi mezani tukubaliane katika kutokubaliana.
 
Hili ni la kuwambia wanaofikiria kula tu na si maendeleo.

Mbowe alikuwa anamuogopa ZZK kuliko CCM. Ni ZZK tu aliyekuwa na uwezo wa kuongoza na kuridhi kiti. Kwa sababu ya kutoruhusu wengine washike chama matokeo yake walitengeneza zengwe ambalo hata sehemu moja huwezi ona uhusika wa ZZK ingawa ndo alikuwa anasakamwa.

Hayo tuache, kwa hili linatotokea ni mwendelezo wa hayo ya familia kuongoza chama. Kwa bahati mbaya imekuwa fedheha kwa baadhi ya wateule.
Mwaka 2009 Zitto hakuzuiwa kugombea. Alitaka kugombea ila aliombwa ajitoe na akakubali angeweza kukataa na kuendelea kama angetaka.....

Mikakati yake ya 2014, ilikuwa kinyuma na taratibu za Chama na taratibu za Chama zilikuwa zinaendelea kumshughulikia kabla ya yeye kukimbilia mahakamani kuzuia mchakato wa chama kumshughulikia....
 
Kutoa matamko nje ya vikao kutasaidia nini!? Bora mkae kimya muendelee kufunga novena zenu msituharibie chama. Dr.slaa alikuwa na mwanya mzuri wa kupenyeza maoni yake baraza kuu,lkn hata wajumbe wa baraza kuu kawapuuza. Kifupi nimeshaanza kumchukia dr.slaa na wanaomuunga mguu!!

wewe endelaea kuchukia lakini sisi ndio tulioweka agano na sasa tunaliishi agano letu

"Hstukukaa kimya kwa watawala walioshindwa wa sasa, na hatuwezi kukaa kimya kwa wanaotaka kuwa wa kesho"MM
 
Mambo haya si ya leo. Kila wakati watu wengi wamelalamikia mfumo wa kifamilia ndani ya CDM. Wanachama wanaona ni mipango ya CCM kuvuruga chama. Sasa ni kweupe, tumechaguliwa anayetakiwa na familia, tusibaki kulalamika.
Nakubaliana nawe.Kwani ifike mahali tuone vyama ni vya wananchi na si vya waanzilishi wa vyama hivyo.Hata kama itabidi kuchanga pesa toka kwa wanachama kuwarudishia waanzilishi hao ili waviache vyama viongozwe na wanachama.

Ni kweli mtu mgeni unakaribishwa badala ya kuandaliwa chakula unaingia jikoni mwenyewe eti unatengeneza unachotaka wewe kula.

Hii ipo hapa kwetu.Viongozi wetu wamekosea lakini tusiwaache tuwe wamoja tukimaliza kupambana turudi mezani tukubaliane katika kutokubaliana.
 

ndugu kinachoudhi sana hapa, sio kuwa na tabaka za wagombea au mipango ya kubaguana. Ila mtu yoyote anaweza ingia kwenye chama na baada ya hata mwezi akagombea nafasi yoyote ya kiungozi ndani ya chama.
Lakini sio mtu ambaye amekatwa kwenye kinyanganyiro kwenye chama chake akakimbilia chama kingine tena kwa masharti ya lazima yeye ashike sukani tena bila hata ushindani na wanachama wengine waliojijenga miaka kadha ndani ya chama. That’s not ethical at all its corrution and dictatorial behaviour period.
Si unaona sasa kuna mshururu wa vigogo wa ccm walioangushwa kwenye kura za maoni, wamefunga foleni chadema zaidi ikifuatiwa na act, wakijue au wakiwa wamehadiwa na lowassa kuwa atawasaidia.
Lowassa amewaahidi kuwaletea makapi wana chadema. Ndugu usemayo sio kweli, am not a chadema supporter, but am a true tanzanian it will disasterous is a strong opposition party like chadema is destroyed by greed. Leo serekali ya ccm haiwezi kufanya jambo bila ya kujiuliza mara mbili , jee cdm wataleta upinzani gani, a strong cdm is necessary for ccm to perform.


Ndiyo hapo wameshakosea?Sasa suluhu ni nini?Tuendelee kulumbana bila kuwa na suluhisho?Suluhisho ni lazima.Tukae chini tukubaliane,mgeni kaja sawa,mmemkaribisha,na mgeni amewapa masharti mmekubali,sasa wameona wamekosea njia waliyoitumia tuache MELI igonge mwamba?

Nasema HAPANA,Mbowe kaona wamekosea njia,amerudi nyuma kutafuta njia ya kuweza kufika,ametumia BUSARA kusema Dr.Slaa ameomba kupumzika amewaruhusu wao waendelee!!!!!!!!!!!!!!Watu wazima hatuulizi alisema lini,saa ngapi,mlikutana wapi,tunaelewa tunaona hatutakiwi tuambiwe tazamani huku.......nk nk.Ameona amekosea amechukua njia iliyo sahihi.

Wanachama tujadili nini tufanye?Ukiniuliza mimi nitakwambia kwa uhakika siyo Pro-Lowassa wala Team Lowassa,Lowassa afanye press conference aanze kujisafisha mwenyewe kwanza.

Wanachama tujitahidi kwa kila hali kuhakikisha tunapata wabunge wengi wengi ,siyo sababu tunahitaji sana rais,bali tunahitaji zaidi wabunge wa kwenda kuzuia MAGOLI YA MKONO BUNGENI.

MM yupo sahihi,twende mbele tutafute suluhisho,hawa CCM wako busy wanachochea kuni,uzuri KUNI tulizitia maji usiku,ni mbichi hazitawaka,wataishia kupata mafua na kuumwa macho.

PAMOJA TUNAWEZA iwe kauli mbiu yetu.
 
Pasco,

Sure!! Lakini kuna vitu ambavyo ni vya msingi sana kuvijuwa juu yake. Wasiwasi wa wengi umejikita katika mambo mengi sana na si kushinda tu.

1. Kikubwa ni sustainability of the project. Umekiri kuwa Lowassa hana uwezo kama Magufuli na UKAWA hawana uwezo kama CCM. Je Lowassa akishindwa atakuwa na uwezo wa kukaa ndani ya CDM na kukitangaza kwa mapambano kama akina Slaa na wengine walivyojitolea?

2. Ndani ya CDM nani anao uwezo wa kumkanya au kumuongoza Lowassa?

3. Lowassa atakubali kuwa kuongozwa na watu wengine akishindwa kupata urais?

4. Malengo ya Lowassa kuja CDM ni nini hasa? Lowassa anakuja na CDM kama kituo cha muda. Ana watu wake na washauri wake nje ya CDM, hao ndo atakamilisha mission zake. Ndani ya muda mfupi, ataamua kwenda alikotarajia. Na hili liko wazi. Hiyo 38% kama mtaji wake ndani ya CDM naonekana kama fiction tu. Hakika hautadumu ndani ya CDM.


Ukimsikiliza Lowassa kwa undani ni mtu mwenye kujiamini kupitiliza. Alianza na hayo akiwa ndani ya CCM katika harakati zake za kuwania urais. Hata majuzi ndani ya CDM ukiangalia kiundani ana maneo ya kijeuri sana na kejeli furani ambazo naziona si rahisi kukaa ndani ya CDM na kujenga chama.

Ninavyoona mimi, hao waliopo ni wa thamani sanaaaaa. CDM ijiangalie sana, hasa mfumo wao wa kiuongozi na kimaamuzi. Wasipo ruhusu demokrasia ndani yake, itarudi makumbusho si muda mrefu.


Mkuu
The Boss, asante kwa kulizungumzia hili la double standard ya Chadema na wafuasi-waabudu wao!, na kiukweli siku zote huwa naikubali objectivity yako!.

Mimi nimepigia sana kelele suala la kufuatwa kwa sheria, taratibu na kanuni huku baadhi yetu wanajidai kupigania haki, wakinyamaza kimya wakati Chadema ikifanya madudu ya wazi!, lakini sasa inapotokea payback time ya 'karma', what goes around, comes around, eti ndio watu wanasusa!, na kuja na hoja kibao za kutokubaliana na kilichofanyka!, what a double standards!.

Kuna tatizo kwa baadhi ya wapenzi wa Chadema, kuwaabudia baadhi ya viongozi wao na kuwaona kama ni miungu watu!, sasa hii miungu watu wa Chadema, inapopuuzwa, waabudu wao wanaiona hii kama ni blasphemy!, mungu wao amekashifiwa!.

Kuna wakati shetani huwa una disguise as god!, na kuna wakati hata shetani mwenyewe kabla ya kuwa shetani, alikuwa malaika!, hadithi ya Paulo na Sauli ni funzo tosha kwa ujio wa Lowassa ndani ya Chadema!, kama Mungu ndio alipepanga mpango huu, hawa wote wanaoupinga ni mashetani disguised as malaika!.

Ningekuwa mimi ni sehemu ya Chadema, wote hawa ningefukuzia mbali na sio kubembeleza!. Utafiti umeishafanya kuwa kuna watu asilimia 10%, ndani ya Chadema watapinga ujio wa Lowassa, lakini gaini itakuwa ni asilimia 38%, nashauri timulia mbali hii asilimia 10% the sooner the better, gain the 38% safari ya matumaini iendelee!.

Kikukweli Magufuli ni mzuri kuliko Lowassa, na CCM is still stronger than UKAWA kwa ujumla wake wote, ila ushindi kwa UKAWA kupitia kwa Lowassa lies on the "positive will power" kwa wanaotaka mabadiliko ya kweli, sasa hawa kenge kwenye msafara wa mamba, wanatuwekea kiwingu cha "negative will power" ambayo itapunguza margin ya ushindi kwa sababu hata hao nao hizo negative will zao nazo zina power kama alivyo devil or satan mwenyewe!.

NB, pia inawezekana na mimi ndio nikawa wrong kuwa CCM ndio malaika na ndio mpango wa Mungu CCM iendelee kuitawala Tanzania, halafu Lowassa ndio mpango wa shetani, hivyo sisi wote tunaosupport ujio wa Lawassa ndio tunaomtumikia shetani, na wote wanaopinga ujio wa Lowassa Chadema, ndio wanaofanya kazi ya Mungu!, that being the case, naomba kuwaomba radhi hao niliowaita mashetani!, kumbe mashetani ni sisi!.

Pasco.
 
Nimeamini kweli CCM kiboko! Wameshindwa kumnunua Dr Slaa lakini wameweza kukinunua chama kizima na kuweka mgombea wao!!!
Mkakati wao bab kubwa da!
Sijui nimuamini nani tena kwa kweli
 
Namuelewa Dr. Slaa; namuelewa Mbowe pia. Mbowe kadharau madhara ya uamuzi wake kama mwenyekiti kumualika mtu ambaye alikuwa na sifa inayopingana na "brand"/jina la chama pasipo kutoa majibu yenye mantiki na mashiko kwa wanachama na wananchi wasioelewa "move" yake na waliohatarisha uhai wao kutetea "brand" ya chama. Ikumbukwe kwamba "brand" ya Chadema ilikuwa ni chuki na vita dhidi ya ufisadi. Na hii "brand" ilijengwa kwa wanachama wa Chadema kama Josephine Mshumbusi kupigwa na serikali ya CCM mpaka kuvuja damu huku akiwa mjamzito.

Kwa upande wa Slaa, ameshikilia msimamo mkali bila kujua kwamba lengo kuu la chama chochote cha siasa na ambalo ni la muhimu zaidi ni kushika dola. Wazo la muhimu katika kushika dola ni kwamba ukishika dola una nafasi kubwa ya kueneza itikadi na sera zako kwenye maisha ya kilasiku ya wale unaowaongoza. Mbowe anaonekana kujali Chadema kushika dola zaidi, kuliko mchakato wake.

Wote, Mbowe na Slaa wapo sahihi. Anachosimamia Mbowe kina umuhimu sawa na kile anachosimamia Slaa, kwani huwezi kuwa na lengo bila kuwa na njia madhubuti ya kufikia hilo lengo. Katika huu mtafaruku, unaweza kusema kwamba Slaa ni njia, na Mbowe ni lengo la kufikia hiyo njia. Kinachotakiwa ni kwamba mawazo ya hawa watu wawili yaheshimiwe kwa uwiano sawa. Chukulia mfano wa uwanja wa mpira wa miguu; hapa kila mmoja atoke kwenye goli lake wakutane katikati ya uwanja, kimawazo. Wasipoweza kufanya hivyo chadema imekufa - haijalishi kwamba itashinda urais au haitashinda.

Mwana kijiji katika ubora wake
 
Mambo haya si ya leo. Kila wakati watu wengi wamelalamikia mfumo wa kifamilia ndani ya CDM. Wanachama wanaona ni mipango ya CCM kuvuruga chama. Sasa ni kweupe, tumechaguliwa anayetakiwa na familia, tusibaki kulalamika.

Usikate TAMAA bado tunaweza,hii changamoto ndiyo itakayotuelekeza kwenda tunakotaka.MM ametupatia ufumbuzi wa nini kifanyike,tukifanye ili twende mbele.

Askari akijeruhiwa halali hapo lazima atajisukuma na kujikaza sana atoke hapo aende mahali salama.
 
Pasco,

Sure!! Lakini kuna vitu ambavyo ni vya msingi sana kuvijuwa juu yake. Wasiwasi wa wengi umejikita katika mambo mengi sana na si kushinda tu.

1. Kikubwa ni sustainability of the project. Umekiri kuwa Lowassa hana uwezo kama Magufuli na UKAWA hawana uwezo kama CCM. Je Lowassa akishindwa atakuwa na uwezo wa kukaa ndani ya CDM na kukitangaza kwa mapambano kama akina Slaa na wengine walivyojitolea?

2. Ndani ya CDM nani anao uwezo wa kumkanya au kumuongoza Lowassa?

3. Lowassa atakubali kuwa kuongozwa na watu wengine akishindwa kupata urais?

4. Malengo ya Lowassa kuja CDM ni nini hasa? Lowassa anakuja na CDM kama kituo cha muda. Ana watu wake na washauri wake nje ya CDM, hao ndo atakamilisha mission zake. Ndani ya muda mfupi, ataamua kwenda alikotarajia. Na hili liko wazi. Hiyo 38% kama mtaji wake ndani ya CDM naonekana kama fiction tu. Hakika hautadumu ndani ya CDM.


Ukimsikiliza Lowassa kwa undani ni mtu mwenye kujiamini kupitiliza. Alianza na hayo akiwa ndani ya CCM katika harakati zake za kuwania urais. Hata majuzi ndani ya CDM ukiangalia kiundani ana maneo ya kijeuri sana na kejeli furani ambazo naziona si rahisi kukaa ndani ya CDM na kujenga chama.

Ninavyoona mimi, hao waliopo ni wa thamani sanaaaaa. CDM ijiangalie sana, hasa mfumo wao wa kiuongozi na kimaamuzi. Wasipo ruhusu demokrasia ndani yake, itarudi makumbusho si muda mrefu.

Achana na Pasco,shemeji yangu huyu ni kipenzi cha Lowassa na ndiyo maana ameweza kuja na jeuri eti hawa 10% fukuzia mbali,je anajua impact ya 10% ya chama cha upinzani?

Je.ni lini Pasco aliweza kupigania upinzani zaidi ya Lowassa?

Pasco yawezekana unamapenzi makubwa na Lowassa,je unafahamu utendaji wake wa kazi kwa undani?Unatuambiaje sisi tuliokuwa tunafanya naye kazi kwenye sekta za binafsi za kupeleka maendeleo kwa wananchi alikuwa anataka nini?

Je ,si huyu ambaye MIRADI ikienda kwake anauliza atafaidikaje nayo?Akiwa mbunge alidai hivyo akiwa RAIS atadai vipi?Muwekezaji akija lazima apewe kiasi gani atafaidika nacho,akija donor lazima aweke kiasi cha Rais kufaidika nacho.Pasco wapo tunaomjua Lowassa ambao ni watu wa kawaida sana tuliokuwa tunatekeleza miradi ya maendeleo.

Kwa uhakika kwabisa jeuri ya kusema eti afukuzwe tu,jamani Pasco hata wewe haujaona mchango wa Dr.Slaa kwenye medani za UPINZANI?

Kwa uhakika kwa kumfukuza huyo CDM mmeimaliza maana wala hakuna haja ya BAO LA MKONO mtakuwa mmeshajifunga wenyewe! Na CCM kila siku wanaota usiku na mchana Dr.Slaa aondoke hapo ili UPINZANI usahaulike.

Kwa Pasco waswahili wanasema "UKIPENDA BOGA PENDA NA MAUA YAKE"Sisi ndiyo maua na majani yake, na kule kwenu Pasco Mboga ya Maboga bila maua haijapikwa bado!
 
Back
Top Bottom