Basi asikilizie hadi ikishafikia hiyo hela 80M kuliko kujenga upuuzi kama huo anaotaka
Nyumba inajengwa kwa miaka had mitano.
Kwa vipato vyetu vya kuunga unva ukiwa na mentality ya kusema had uwe na mill 100 ndio ununue kiwanja alaf uanze kujenga chap chap.
Niamin unaweza usijenge.
Maana matatizo yapo na saving inaweza ikavurugika.
Ila ukigawa hii project ya kujenga kwa phase.
Yaan ndan ya miaka 5-7 una nyumba yako nzur tu.
Mwaka 1 - Unanunua kiwanja.
Mwaka 2 - Unajenga msingi na unaanza kupandisha boma.
Mwaka 3 - unamalizia kupandisha na Unapaua.
Mwaka 4 - Unafanya wiring na kupiga plasta, kuvuta umeme.
Mwaka 5 - finishing mdogo mdogo.
Mwaka 6 - Unamalizia finishing, unazungusha ukuta.
Mwaka 7 - unamalizia ukuta, gate na paving.
Nimepitia the same process.
Nilianza nikiwa na 27 yrs Na nilivyofika 33 yrs nikawa na nyumba nzur tu na project ikakamilika.
kama 90+ Mill zimeteketea.