2015-uchaguzi mkuu na hatma ya nchi

Mkuu Tujitegemee
Huko nyuma tumeeleza kwa uchache jinsi Da'Amina alivyopenya hadi 3 .

Hilo ni moja ya tatizo linalotukabili nchini. Hatuchagui viongozi kwa merits, bali kuongozwa na eneo au jinsia.

CCM wanaongozwa na hofu ya kukutana na KANU na UNIP kama watu wataamua kubadilika.

Karata inayochezwa ni jinsia


Mkuu, kuelimika ni zaidi ya vyeti mtu anavyopata. Hatunad hamira ya ku criticize elimu yake, tunachosema ni kuwa elimu ni pamoja naweledi na exposure

Inaonekana Da, amepata nafasi nyingi za kumwezesha kuwa na weledi na exposure.
Swali, je alitumia fursa hizo kupata maarifa zaidi?


Nafasi aliyokuwa anawania inahitaji weledi, hatudhani yeye kama yeye alikuwa tayari kwa ‘prime time'.

Kilichotokea aliandikiwa hotuba na washauri wake kwa lengo la kupata nafasi.

Ndio maana alimshirikisha Edo bila kutambua alikuwa anatia nyongo katika kitumbua.
Hakujua kuwa hadi wakati ule kambi ya Edo ilikuwa namaruwe ruwe
'Delirium'

Waliomwandikia hatujui uelewa wao katika mambo ya siasa.

Siasa za siku hizi ni za kisayansi si za kukota wapiga debe.


Nadhani washauri wake walikuwa dhaifu, ukichanganya na udhaifu wake, unaishia kupata suala la middle class kuelekea first world

Ilikuwa ni rahisi kubaini. Wiki iliyopita UN imetangaza nchi zilizoingia uchumi wa kati.

Jirani zetu kenya walikuwa kundi moja vi nchi masikini sana. Hatujui kama alioma habari hizo


Tuna tatizo, sasa huyo ndiye alikuwa awe mgombea!

Kuna baadhi ya watu wakupata wadhifa wanautumia kutanua. Lakini kuna watu wanautumia zaidi ya matanuzi. DaAmina alikaa kwenye kiti cha kuzunguka, alikuwa anazunguka kwa hiyo siwezi kumlaumu. kama kweli yeye na Dr Migoro wangekuwa rais ingekuwa hatari sana kwa nchi.
If the two had realistic chances, naweza kusema ni hatari sana. Lakini kama walikwekwa as symbol of unity, symbol of solidarity, symbol of proving that they got close to top job, lakini Pombe alikuwa ameandaliwa, si jambo baya. Lakini ukiangalia upigaji kura unaweza kuona kuwa kura za watu kutoka visiwani zote zilienda kwa da Amina.
 
Wakuu zangu,

Nimewasoma kwa kituo na kugundua kwamba bado mnajaribu kufikiria kwa MATUMAINI pasipo kutazama UHALISIA. Mkumbuke kwamba sisi Wadanganyika sote tunaishi kwa mazoea na sii kujifunza! hivyo hurudia makosa yale yale na kuendelea kuweka tumaini katika siasa ambazo wenyeji wake ni WANAFIKI (Uhalisia) wanaoishi kwa mazoea vile vile. Hivyo mnapoteza pumzi na nguvu zenu bure kwa sababu huu unakuwa kama Utabiri badala ya uhalisia wa kisayansi.

Nini UHALISIA basi, Umoja wa UKAWA walitumia mbinu babu kubwa kuitumia KATIBA MPYA kama mmbegu ya kuipnada kisiasa vichwani mwa wananchi dhidi ya chama tawala na nasema kwa mara ya kwanza UKAWA walikuwa na zao bora la kuishnda CCM kupitia Katiba mpya. Lakini UKAWA hawakujiandaa kuchukua NCHI kwa sababu waliweka uroho na tamaa mbele (mali) kabla hawajapanda mbegu hizo na hii ndio tatizo la UMASKINI.

Kujitokeza kwa Katiba kuu kuliwachanganya UKAWA wakajiona tayari wameisha chukua nchi wakati hawakujipima nafsi zao kama wanaweza kuwa kitu kimoja kweli wakalima na kuvuna shmaba moja! UKAWA ni sawa na Ndugu waloambiwa kuna mirathi imeachwa na mzee...Hapo fikiria vichwani mwao kuna kitu gani kitakuwa kinatembea na ndivyo vyama vya UKAWA waliona mwanya wa Kuchukua Chako Mapema. Katiba mpya ndio ikawa curse ya UKAWA maana hawakuungana kwa jingine. Kwa hiyo mahesabu ya UKAWA walianza kuvuna kichwani hata kabla hawajapanda mbegu za zao la Katiba Mpya..

Ukweli wa mambo ni kwamba Tanzania bado hatujapata chama Mbadala wa CCM kwa sababu wanasiasa wa Upinzani wanapingana na fursa zinazojitekeza. wanasiasa wetu huchangamikia FURSA kama wananchi wenyewe ktk maisha yao na hadi leo hatuna chama wala mwanasiasa anayepingana na mwongozo, Ilani wala sera za CCM hakuna isipokuwa vyama vinapingana na vipaumbele vya CCM. Siasa zetu bado kabisa hazijafika mahala pa kutangaza na kusimamia Mrengo, kila chama kina katiba zinazofanana.

Hivyo, tusiwalaumu wananchi hata kidogo maana wao wanalishwa tu siasa za maneno matamu na maadam Upinzani wetu haukutokana na kutokubaliana na mwongozo wa Chama tawala isipokuwa kuweka utaratibu wa Kidemokrasia ili nasi tukubalike na nchi za Kimataifa. Demokrasia yetu sii ya vyama wala mrengo bali upinzani wa WATU kutokana na kwamba vyama vya Upinzani havikuanzishwa kwa sababu walipingana na Mrengo wa CCM. Vyama vyetu vilianzishwa kama vilabu vya mpira kushiriki ligi kuu..

Mzee Mtei mwenyewe alianzisha Chadema wakati CCM yenyewe imeshageuka na kuwa Mabepari toka mwaka 1984 na kuchukua mikakati ya IMF (SAP) ambayo Mtei alikuwa mshauri mkuu toka nyuma, CCM ile (1993) ilikuwa exactly kile Mtei alichokitaka mwaka 1982. CUF na Kina Mrema walienda kutana mna mwalimu kuomba ridhaa yake wajitoe CCM hivyo utaona kwamba vyama vyetu vya Upinzani ni mazao ya CCM wanaopingana ni wafuasi wake tu. Vyama vyetu ni sawa na zao la FIFA kuunda vilabu vya Mpira. Na hivyo kuzaa Ushabiki na uadui baina ya Yanga na Simba usokuwa na sababu zaidi ya Ushindani na hawawezi wote kuwa timu moja!

Leo tumeletewa John Pombe Magufuli, tunaanza kazi mpya ya kutafuta mabaya yake na sii ya CCM kwa sababu masikni siku zote huweka tumaini mbele. Pengine Mafuguli atakuwa mzuri kuliko Kikwete..Tulisema hivo hivo pengine Mkapa atakuwa, Pengine Kikwete atakuwa na upande wa pili wa Upinzani nani mbadala wake ni mfululizo ule ule wa siasa za watu kuzidiana kete. Upinzani hawawezi kuwa wamoja kwa sababu tofauti zao sii za Kiitikadi bali ni za kibinafsi.

Pengine nishauri nyie mlokuwa na fikra pevu, wenye kuitazama CCM kwa ahadi zake za ilani na sera. Wenye kutambua CCM inatupeleka wapi ndoio mnaotakiwa kujiingiza katika siasa na mkaleta mageuzi lakini tusiwalaumu wananchi ambao kwao huishi kwa mazoea. MATUMANI ndio pekee huwawewa hai na huru na hivyo hawataweza kupoteza nguvu zao mahala pasipo kuwa na matumaini. Mshabiki wa Arsenal atamtazama Wenger kujenga tumaini la mwaka ujao vile vile wa yanga na Simba hizi ndio siasa zetu. Njia ilokuwepo pekee ni vyama hivi (UKAWA) kuunda TAIFA STARS na mwanzo mpya na maadam imeshindikana mtaendelea kuwalaumu wananchi bure wakati ilikuwa jukumu la management na Kocha kuchagua wachezaji wa TAIFA STARS..
 
Naufatilia kwa karibu mjadala huu, na ahsanteni nyote kwa michango yenu.

Haikuwa nia yangu kusimamisha muendelezo wa mjadala huu na kuwarudisha nyuma juu ya sifa za watia nia kugombea urais kupitia CCM ambao walifika tatu bora (nadhani twaweza kusema bora tatu). Lakini nimelazimika kuwarudisha nyuma ili niweze kupata maoni yenu juu ya jambo hili ambalo kila ninavyojaribu kulipuuzia kutolileta jamvini linazidi kunikereketa kichwani.

Jambo lenyewe ni kuhusu hotuba walizozitoa watia nia hao wa 'bora tatu' wakati wakiomba kura kwenye mkutano mkuu wa CCM. Niliwasikiliza wote watatu (John, Amina na Asha-Rose) kupitia redio. Amina na Asha-Rose inaonekana walijiandaa, kutokana na namna walivyojieleza lakini John kwa jinsi alivyoomba kura ni dhahiri shairi hakujiandaa kwa tukio lile. Alishtukizwa. Hotuba iliyonistua ni ile ya Amina Salum Ali; hasa aliposema kuwa " ...sasa Tanzania ipo kwenye uchumi wa kati na inaelekea uchumi wa kwanza/juu..." hivyo atasaidia Tanzania kuingiiza kwenye uchumi wa juu akiwa rais wa nchi hii. Nimejaribu kulifuatilia hili kuona kama mimi ndiye 'niliyepitwa na wakati' kiasi kwamba sijui hata uchumi wa nchi yangu uko kiwango gani (kwani nilikuwa najua Tanzania uchumi wetu ni wa kiwango cha chini-low income economy country).

Nilivyotembelea tovuti ya Benki ya Dunia nikakuta kumbe bado Tanzania ni nchi yenye uchumi wa chini ( Tanzania | Data ). Nilivyododosa zaidi juu ya Mama Amina S.A nikagundua alisomoea masuala hayo ya biashara, masoko na uchumi huko India na kwingineko. Na masuala hayo ya Uchumi, masoko na biashara ni masuala ambayo yanahusisha sana takwimu sahihi ili kufikia maamuzi. Pia nikagundua Mama A.S.A ni:

" Mwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Afrika (AU) Marekani (United States) akiwa kama ni Muwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika. (i) Mshauri wa Kamisheni Umoja wa Afrika kuhusiana mambo ya Afrika huko Marekani. (ii) Kufuatilia mambo ya Maendeleo ya Afrika huko Marekani kwa kuwajuilisha kuhusu sera mbali mbali za bara la Afrika zinazoendelea na mpya. (iii). Kuwashajiisha wawekezaji wa Marekani na pia Diaspora wa jamii ya Kiafrika huko Marekani kuwekeza Afrika. (iv) Kuimarisha uhusiano baina ya Marekani na vyombo vya Serikali, Mabunge na Taasisi za kijamii za Afrika . (v) Kusaidia kupatikana kwa Fedha za Maendeleo ya Afrika kwa kuzieleza Sera za Maendeleo za Afrika, na kuwashawishi waziunge mkono. (vi) Kushirikiana na vyombo vya fedha vya Bretton Woods (World Bank na IMF) kwa Maendeleo ya Afrika.
.........................
. (Rejea>>>https://www.jamiiforums.com/uchaguz...tegemewa-kuwa-makamu-wa-rais-kupitia-ccm.html)

Sasa ninajiuliza kama huyu Mwakilishi wetu wa waafrika huko US mwenye majukumu mazito namna hiyo anashindwa kujua nchi ipo kiwango gani kiuchumi (kama takwimu za world bank zitakuwa sahihi):

1. Je. Kamati ya usalama na maadili ya CCM, baraza la ushauri la Wazee wa CCM, Kamati kuu ya CCM (CC), na halmashauri kuu ya CCM (NEC) hawaoni kuwa sasa ni muda muafaka kuwaomba radhi wanachama wa CCM kwa kushindwa kutekeleza jukumu lao sawa sawa kiasi cha kumpitisha mtia nia ambaye hajui anataka kuongoza nchi ya namna ki-uchumi ?

2. Je. hivi kwa kiwango chake (hadhi na kitaaluma) huyu Mama Amina S.A tunaweza kusema 'aliteleza kutoa kauli ile' hivyo tumuache aendelee kutuwakilisha huko US bila bughudha?

Tusemezane juu ya hili kisha tuendelea na mada.
Mkuu kwanza shukran sana kwa mchango wako na nadhani watu hawafahamu ya kwamba URAIS ni mpango wa muda mrefu kwa vyama haswa kwa nchi za Kiafrika (maskini) kwa sababu bado ni mataifa tegemezi. Kwa hiyo hotuba ya Bi. Amina haikuwa na malengo ya kupotosha bali kuwapa wajumbe na wananchi tumaini zaidi ya kwamba UCHUMI wetu ulikuwa katika hali nzuri kulingana na malengo yalotakiwa kufikiwa. Ukati wake unategemea na ujazo wa chupa tulobeba...

Kumbuka tu kwamba Bi. Amina ndiye aliyepangwa kuwa RAIS wa JMT 2015, mimi na wewe ndio hatukufahamu na sifa ulizoziweka hapo juu ndizo zilizompa nafasi kubwa ya kupokea Kijiti kati ya wagombea wote ambao ni ktk mwendelezo wa Milleniunum 2000 to 2025 ya Mkapa. Mpango mzima wa maendeleo ya Tanzania upo mikononi mwa IMF na nchi za Magharibi kama Ugiriki vile na lazima wafadhili watuchagulie chama na pengine hata kiongozi. Hii wekeni akilini mapema kabisa.

Kosa kubwa alolifanya Bi. Amina ni kumhusisha Lowassa. Na kama utakumbuka JK alisema neno baada ya Amina kujitambulisha akimwambia "CCM pagumu" au kitu kama hicho!. Ukumbi kimyaaa na baada ya hapo kazi ya kuhesabu kura ikaahirishwa, ina maana walienda kutazama isije kuwa huyu Bibie kapata kura nyingi baada ya kughiribiwa na kundi la Lowassa ama kafikiri siasa za Ulaya angeweza kuzitumia Tanzania kupata wajumbe wa Lowassa.

Hivyo Usiku mzima wakakaa kuchambua matokeo na hivyo kumpa Magufuli, lakini haikuwa lengo maana huyu mama nasikia alipitishwa toka nitoke, ilikuwa ni wakati wa mwanamke na kuulinda muungano. Aidha yeye au AshaRose lakini imani ikawatoka pale Amina alipojikanyaga na Lowassa!. Magufuli akawa jembe, AshaRose japo aliweza kujieleza vizuri kuliko wote lakini ndiye hakupata kura za kutosha kabisa. Urais wetu unatokana na maridhiano baina ya wafadhali na chama tawala..
 
Mkuu Mkandara

Ni tofautiane nawe kuhusu kuwalaumu wananchi kwa yanayotokea. Ninaamini kabisa, badala ya kuwalaumu wanasiasa na vyama vya upinzani, wananachi wanapaswa kuchukua lawama hizo.

Hakuna mahali katika dunia hii nguvu ya dola iliwahi kushinda umma. Dola ni zao la nguvu ya umma na si kinyume chake
Kwa dunia ya wenzetu, wanasiasa huwatumikia wananchi na si wananchi kuwatumikia wao.
Mambo yekienda kombo, jukumu la kuweka sawa ni la wananchi si la vyama vya siasa.

Vyama vya siasa hubeba agenda ya wananchi kwavile wana platform. Hufanya hivyo wakijua agenda ya wananchi ndio muongozo na si kinyume chake

Kama tutakubaliana wananchi hawana sababu ya kubeba lawama, tukubaliane hawana sababu za kulaumu wanasiasa

Muhimbili wananchi wakilala sakafuni, akina mama wakipanga foleni ya kwenda kwenye chumba cha kujifungulia hilo si tatizo la wanasiasa wanaotibiwa chunusi Appolo au Joberg. Na wala hakuna mwanasiasa atakayesimama kuzungumzia matatizo hayo kwasababu hayamhusu.

Kwa nchi za wenzetu, wananchi wanachukua jukumu mikononi mwao, iwe kwa njia ya sanduku la kura au nyingine

Ni makosa kuwapumbuza wananchi tukitumaini kuwa ipo siku malaika watataremka kulinusuru taifa. Tumejaribu miaka 50, je tusubiri hadi karne nyingine? Wale wenzetu wanaochukua hatua dhidi ya 'malaika' wamepungukiwa nini ?

Ni wananchi wa Tanzania peke yao wanaosubiri miujiza na si wao kuchukua hatma ya taifa lao

Wanasiasa wamefikia mahali wanadhani wao ndio nchi. Sababu kubwa ni wananchi walioshindwa kuwaambia wao ni waajiriwa. Mwajiri anaposhindwa kuchukua hatua dhidi ya mwajiriwa hilo ni tatizo lake, si la mtu au taasisi nyingine
 
Mkuu Mkandara

Ni tofautiane nawe kuhusu kuwalaumu wananchi kwa yanayotokea. Ninaamini kabisa, badala ya kuwalaumu wanasiasa na vyama vya upinzani, wananachi wanapaswa kuchukua lawama hizo.

Hakuna mahali katika dunia hii nguvu ya dola iliwahi kushinda umma. Dola ni zao la nguvu ya umma na si kinyume chake
Kwa dunia ya wenzetu, wanasiasa huwatumikia wananchi na si wananchi kuwatumikia wao.
Mambo yekienda kombo, jukumu la kuweka sawa ni la wananchi si la vyama vya siasa.

Vyama vya siasa hubeba agenda ya wananchi kwavile wana platform. Hufanya hivyo wakijua agenda ya wananchi ndio muongozo na si kinyume chake

Kama tutakubaliana wananchi hawana sababu ya kubeba lawama, tukubaliane hawana sababu za kulaumu wanasiasa

Muhimbili wananchi wakilala sakafuni, akina mama wakipanga foleni ya kwenda kwenye chumba cha kujifungulia hilo si tatizo la wanasiasa wanaotibiwa chunusi Appolo au Joberg. Na wala hakuna mwanasiasa atakayesimama kuzungumzia matatizo hayo kwasababu hayamhusu.

Kwa nchi za wenzetu, wananchi wanachukua jukumu mikononi mwao, iwe kwa njia ya sanduku la kura au nyingine

Ni makosa kuwapumbuza wananchi tukitumaini kuwa ipo siku malaika watataremka kulinusuru taifa. Tumejaribu miaka 50, je tusubiri hadi karne nyingine? Wale wenzetu wanaochukua hatua dhidi ya 'malaika' wamepungukiwa nini ?

Ni wananchi wa Tanzania peke yao wanaosubiri miujiza na si wao kuchukua hatma ya taifa lao

Wanasiasa wamefikia mahali wanadhani wao ndio nchi. Sababu kubwa ni wananchi walioshindwa kuwaambia wao ni waajiriwa. Mwajiri anaposhindwa kuchukua hatua dhidi ya mwajiriwa hilo ni tatizo lake, si la mtu au taasisi nyingine


Nguruvi3:

Kwa sababu ulianzishwa mradi wa demokrasia ya vyama vingi, basi tunaweza kuwalaumu wananchi kwa matatizo yanayotokea Tanzania. Lakini ukichunguza kwa makini demokrasia yenyewe haikuja kumpa mtanzania nafasi ya kuchagua viongozi bora. Ilikuja hili kuonyesha wahisani kuwa Tanzania nayo ina mfumo wa vyama vingi. Hivyo kuwalaumu wananchi wa kawaida ni kutowatendea haki.

Ni kweli wananchi wanatakiwa kuwa chachu ya maendeleo yao. Lakini tusisahau kuwa kundi la intelligensia ndio kioo cha jamii. Na hili kundi ndilo lingeweza kutoa mabadiliko ya kweli ya kijamii. Kwa Tanzania kundi hili bado halijakuwa chachu za maendeleo. Leo hii madaktari, maprofessa, wanafunzi vyuo vikuu na wafanya kazi wa idara za kiserikani wakigoma kudai mabadiliko, mabadiliko hayo yatatokea. Kwanini sasa anasubiriwa mwanakijiji ambaye hana uwezo kufanya uchambuzi.

Nimerudi kutoka Tanzania, wasomi wengi wanaotaka kugombea viti mbalimbali kupitia CCM wanatoa rushwa hili wapate nafasi ya kugombea kupitia chama. Hawa watu ni vioo kwa jamii zao. Kama wao wanaweza kufanya hivyo, kwanini mwananchi wa kawaida asifanye hivyo?
 
Nguruvi3:

Kwa sababu ulianzishwa mradi wa demokrasia ya vyama vingi, basi tunaweza kuwalaumu wananchi kwa matatizo yanayotokea Tanzania. Lakini ukichunguza kwa makini demokrasia yenyewe haikuja kumpa mtanzania nafasi ya kuchagua viongozi bora. Ilikuja hili kuonyesha wahisani kuwa Tanzania nayo ina mfumo wa vyama vingi. Hivyo kuwalaumu wananchi wa kawaida ni kutowatendea haki.

Ni kweli wananchi wanatakiwa kuwa chachu ya maendeleo yao. Lakini tusisahau kuwa kundi la intelligensia ndio kioo cha jamii. Na hili kundi ndilo lingeweza kutoa mabadiliko ya kweli ya kijamii. Kwa Tanzania kundi hili bado halijakuwa chachu za maendeleo. Leo hii madaktari, maprofessa, wanafunzi vyuo vikuu na wafanya kazi wa idara za kiserikani wakigoma kudai mabadiliko, mabadiliko hayo yatatokea. Kwanini sasa anasubiriwa mwanakijiji ambaye hana uwezo kufanya uchambuzi.

Nimerudi kutoka Tanzania, wasomi wengi wanaotaka kugombea viti mbalimbali kupitia CCM wanatoa rushwa hili wapate nafasi ya kugombea kupitia chama. Hawa watu ni vioo kwa jamii zao. Kama wao wanaweza kufanya hivyo, kwanini mwananchi wa kawaida asifanye hivyo?
Mkuu hakuna nchi iliyofanikiwa kupigana na rushwa kama hizi za chaguzi bila kuwashirikisha wadau a.k.a wananchi

Pili, lawama kwa wananchi ni pamoja na hiyo ya kujiunga nao badala ya kupigana nayo.

Mwisho wa siku mwananchi huyo ndiye victim. Mwananchi anapopewa khanga na kofia au 50,000 kuuza shahada, hapo anajikimu kwa siku, kwa muda mrefu atalipa gharama kubwa zaidi.

Kwani umeme wa bei juu wanalipa akina nani? Nani waliokamata mshiko wa Richmond, escrow n.k.

Nchi za wenzetu wameumia sana na rushwa, mwisho wa siku wakasema silaha nzuri na ya amani ni sanduku la kura

Wakaanza kupata watu waadilifu, na waadilifu wakajenga mfumo wa kiadilifu , tukiaaminisha bora ulilinganisha na wetu

Kama mnadhani tunaweza kubadili mfumo kwa maneno, hizo ni njozi za mchana
Ni lazima wananchi watumie 'silaha ya mwisho' ambayo ni uwezo wa kuweka na kuondoa viongozi

Wakishaelewa kuwa hawana nguvu tena dhidi ya wananchi, mengine yatafuata.
 
Sehemu ya I

ANGUKO LA EL NDANI YA CCM

RICHMOND NI SABABU TU, ‘ESCROW' NDILO PIGO LA MWISHO

Wengi wanasema EL ana nguvu za kisiasa, wapo wanaodai anajua mikakati.
Wapo wanaoamini Richmond ndiyo sababu ya kukatwa. Yote yana ukweli,kwamba, nguvu ya kisiasa aliijenga vizuri sana.

Kisiochoeleweka ni kuwa, je,Richmond ndiyo liyohitimisha safari yake? na kwanini alishindwa kuruka kiunzi hicho?

TURUDI NYUMA KIDOGO

Baada ya mkakati wa mtandao kufanikiwa, EL alidhani nafasi aliyopewa ingemsaidia kujijenga kisiasa(Plan A)
Kwa bahati mbaya Richmond ikaingia na kuharibu mipango


KIUNZI CHA KUWAJIBISHWA
Katika kukwepa kiunzi cha kuwajibishwa na Bunge kwa kutokuwa na Imani naye, njia muhimu ilikuwa kujiuzulu.
Kujiuzulu maana kuna maana nyingi, moja ikiwa ni ile inayotumiwa ya kuwajibika kisiasa, nyingine ni kuikoa serikali.

Zote hizo hazimzuii mtu kurudi katika ulingo wa siasa kama ilivyokuwakwa Rais Mwinyi na sakata la Shinyanga


PLAN B
Ili kufaninikisha mkakati ulioshindwa kutokana na kushindwa plan B, time EL ikaanda mkakati wa kuhakikisha inadhibiti vyombo vya chama.Uchaguzi mkuu wa CCM timu ikawekeza katika kupata wajumbe wa kamati kuu na wa halmashauri kuu

Na ili vyombo hivyo viwe na nguvu katika mkakati ilikuwa lazima kulindwa.
Ulinzi ni ule wa kumiliki kamati ya maadili na usalama ya chama ambapo timu ilimweka 'mzee wa vijisenti'

KAMATI YA USALAMA NA MAADILI

Kwa vile ilimilikiwa na timu EL, maamuzi yote ya chama yaliweza kuauziwa. Ndilo chimbuko la watuhumiwa wa kashfa mbali mbali kutoweza kuchukuliwa hatua, au kuvuliwa magamba.

Hii ni kamati ya uslama na maadili yenye uwezo wa kumshughulikia yoyote mwenye kelele.
Hadi hapo timu EL ikawaimefanikiwa


CCM NJIA PANDA

CCM ilifahamu nguvu za kisiasa alizokuwa nazo EL na kwamba kumzuia ilikuwa si jambo rahisi.
Kampeni zilikuwa zimeshakwenda mbali,kilichokuwa kinasubiri ni mhuri wa kamati ya ulinzi na maadili, kamati kuu na halamshauri kuu
.

Escrow ilivyotibua mambo

Inaendelea
...
 
Sehemu ya II

ESCROW ILIVYOTIBUA MAMBO

Timu EL haikuwa na tatizo lolote kuhusiana na Escrow. Shida moja ilijitokeza, baadhi ya wana timu EL walihusishwa na Escow. Hawa ni kama mama ‘pesa za mboga' na mzee wa vijisenti.

Mama wa viji mboga ana ushawishi ndani ya halamashauri kuu,na mzee wa vijisenti anaushawishi humo humo.
Lakini mzee wa vijisenti ndiyealikuwa mwenyekiti wa kamati ya maadili na usalama ambayo pia ilikuwa ‘mlinziwa time EL'


ESCROW YATOA FURSA KWA CCM

CCM ilichokitaka ni mahali laini pa Kamba kukatikia.Waliichukua escrow kama hoja muhimu.
Kilichokuwa kinaendelea ni kuhakikisha wahusika wawili wanapigwa pini. Mama wa mbonga na mzee wa vijisenti

wakazuiwa kuingia katika halmashauri kuu kama wajumbe ili kutumikia adhabu.
Kumbuka,hawakufukuzwa isipokuwa walizuiwa ikiwa ni ‘technical knock out'


Kwa muktadha huo, mzee wa vijisenti akapoteza uenyekiti wakamati muhimu sana ya maadili na usalama.
Hapo ndipo mambo yalipoanza kwenda kombo kwa timu EL.
Hakukuwepo ‘ulinzi wa timu' na mzee Mangul akachukua nafasi


BARAZA LA WAZEE LAITWA

Lengo lilikuwa kupata ushauri kwa kujua kuwa ‘rafiki'asingeweza kukabiliana na nguvu ya EL katika CC na NEC.
Na pia wazee hao hawakuwa na ‘upenzi' na EL.


Kwa kawaida, hoja za CCM huandaliwa na sekretariati husika,na hufikishwa kujadiliwa na CC kwanza kisha NEC.

Safari hii mpira ukarushwa kwakamati ya maadili na usalama , halafu wazee wa baraza la ushauri.


Hilo ndilo lilimpa ‘rafiki' uwezo wa kuzuia hoja za wana CCM kwa kutupia mzigo kwa kamati ya maadili na usalama na wazee wa baraza la ushauri.

Hadi hapo yaliyoendelea ni hadithi

Kwa upande wa pili, yapo makosa ya wazi kabisa yaliyofanywa na timu EL

Tutajadili, itaendelea…
 
MAKOSA YA TIMU EL

Timu iligundua kikwazo cha kamati ya maadili na usalama.Ikatafutwa plan nyingine ya shinikizo ili kamati hizo zikubaliane na EL.Ndivyo ilivyokuwa mwaka 2005 ,shinikizo la makundi ka ma ya akina mama yalilazimisha wana mtandao kupeta

Timu ikatengeneza mkakati
Kwanza, kutafuta makundi yenye ushawishi katika jamii.Tukaona viongozi wa dini wakiandamana kumuunga mkono.
Hilo lilikuwa kosa la kwanza. Kutumia makundi ya dini wazi haikupendeza wahafidhina ndani ya chama.

Pili, timu ikachagua viongozi wasio na ushwawishi ikionekana wazi ilikuwa ni ‘usanii'

Tatu, timu ikatumia bodaboda kuonyesha inaungwa mkono na vijana. Tukaona wakisafiri zaidi ya KM 400 kwa ‘gharama zao''. Haihitaji mtu kuwa genious kubaini kulikuwa na biasharabaina ya timu na bodaboda. Kosa kubwa.

Haiwezekani asiye na sh 20,000 kwa siku , atoe 100,000 za mafuta na muda kwenda kuomba mgombea X. Haiingii akilini

Katika mazingira hayo ya kutaka mass support, timu ikaanda hafla kubwa ya kutangaza nia.
Nalo likaleta hisia mbaya kutokana na ukubwa wa shughuli na gharama. Swali likabaki nani aliye nyuma ya haya yote?


Nne, timu ikaalika watu waliokuwa na madoa kumzunguka EL katika mikutano. Kosa! Kwasababu zilikuwepo hisia za rushwa, wanapoonekana ‘vigogo'hadharani , hakuna shaka ule ni mkakati wa ‘watu fulani' kutaka mtuwao ili waendeleze yao. Kosa kubwa sana.

Timu EL ikaamua kutumia mitandao. Kwa bahati mbaya watuw aliopewa kazi hawakuwa wa kiwango.

Haiwezekani uhubiri uzuri wa mtu ikiwa hujaeleza tuhuma zinazomkabili. Timu ilipaswa kuhakikisha tuhuma inakuwa address halafu agenda nyingine zifuate. Kitendo cha kukimbilia kuzungumzia mazuri ambayo hayakuwa wazi lilikuwa kosa.


Tunaweza kusema, rasilimali zilikuwepo, tatizo ni watu wa kuzifanyia kazi ili zilete tija.

Timu ya EL katika mkakati ilishindwa vibaya .Matumizi ya pesa yalionekana kama nyenzo muhimu.
Walipokamatwa pabaya, ikawa ni technical knock out


TULISEMA

Huko nyuma tulisema bila shaka, CCM haiwezi kuparaganyika kwa sababu ya timu EL

Msukumo naoonekana ni wa wafanyakazi si wakereketwa. Ndivyo inavyoonekana sasa.
Timu nzima imemuacha mzee na wengine kujiunga na timu ‘padlock'


Kwa vyovyote vile CCM ilikuwa na wakati mgumu. Kumkata ELili kukabliana na haya yanayotokea sasa au Kumwacha ingeondoa kundi lisilokubaliana na ‘ufisadi wa wazi wazi'

Tunasema wazi wazi, kwasababu ndani ya CCM nani anaweza kusimama na kusema ni msafi?


Tusemezane
 
Dr.Slaa pengine ndiye mwanasiasa wa upinzani anaeheshimika na kusikilizwa zaidi Tanzania.

Yote hii ni sababu ya misimamo yake kupinga ufisadi, kusimamia na kutetea maslai ya Taifa bila kuogopa.

Amewahi kutaja hadharani listi ya mafisadi 11 Lowasa akiwa namba tisa na Kikwete akiwa namba kumi na moja.

Alienda kule Arumeru alimtuhumu Lowasa waziwazi kwa ufisadi na kukwepesha miradi ya Arumeru na kuipeleka Monduli.

Lakini leo tunaambiwa kuwa Lowasa anakaribishwa ndani ya Chadema na kuungama dhambi na atasamehewa.

Sina tatizo na ujio wa Lowassa ndani ya chama tatizo langu ni heshima na taswira ya Dr. Slaa aliyojijengea kwa muda mrefu kwa kuukemea ufisadi.

Je leo yupo tayari kutangaza hadharani kuwa Lowasa amekuwa msafi sio fisadi tena, yupo tayari kupunguza ile list of shame ya Mwembeyanga kutoka kumi na moja na kubaki kumi.?

Japo siasa hazina adui wa kudumu wala urafiki wa kudumu, kwa hili naona heshima ya Dr.Slaa na Chadema kwa ujumla ikiporomoka.

Maana heshima ya Dr Slaa na Chadema imejengwa kwa kuukemea ufisadi, lakini tunakoelea Hali itabadilika na kuwa Chadema ni chama cha kuwasafisha Mafisadi.

Kuelekea Uchaguzi Mkuu Tutasikia mengi sana Leo hii Chadema wanamlilia Lowassa.

Tusemezane.
 
Dr.Slaa pengine ndiye mwanasiasa wa upinzani anaeheshimika na kusikilizwa zaidi Tanzania.

Yote hii ni sababu ya misimamo yake kupinga ufisadi, kusimamia na kutetea maslai ya Taifa bila kuogopa.

Amewahi kutaja hadharani listi ya mafisadi 11 Lowasa akiwa namba tisa na Kikwete akiwa namba kumi na moja.

Alienda kule Arumeru alimtuhumu Lowasa waziwazi kwa ufisadi na kukwepesha miradi ya Arumeru na kuipeleka Monduli.

Lakini leo tunaambiwa kuwa Lowasa anakaribishwa ndani ya Chadema na kuungama dhambi na atasamehewa.

Sina tatizo na ujio wa Lowassa ndani ya chama tatizo langu ni heshima na taswira ya Dr. Slaa aliyojijengea kwa muda mrefu kwa kuukemea ufisadi.

Je leo yupo tayari kutangaza hadharani kuwa Lowasa amekuwa msafi sio fisadi tena, yupo tayari kupunguza ile list of shame ya Mwembeyanga kutoka kumi na moja na kubaki kumi.?

Japo siasa hazina adui wa kudumu wala urafiki wa kudumu, kwa hili naona heshima ya Dr.Slaa na Chadema kwa ujumla ikiporomoka.

Maana heshima ya Dr Slaa na Chadema imejengwa kwa kuukemea ufisadi, lakini tunakoelea Hali itabadilika na kuwa Chadema ni chama cha kuwasafisha Mafisadi.

Kuelekea Uchaguzi Mkuu Tutasikia mengi sana Leo hii Chadema wanamlilia Lowassa.

Tusemezane.

Umeongea swala la msingi sana, Mtanzania yeyote yule anaruhusiwa kujinga na chama cha siasa na ninafahamu kuwa katika vyama vya siasa kuna wanachama ambao ni wezi, majambazi, wala rushwa, mafisadi na nk.na kwa hili chama hakiwezi kufanya uchunguzi wa kila mwanachama anayejiunga na chama hicho.

Katika swala la Lowassa ninashindwa kuelewa mantiki ya Mh. Mbowe kumkaribisha Lowassa Chadema mtu ambaye tuliaminishwa kwa ni mla rushwa na ni fisadi na waliotuambia hayo si CCM pekee bali hata viongozi wa Chadema akiwemo Dr. Slaa.
Sasa watambie ni lini Lowassa alicha kuwa fisadi? na huyu Lowassa ana muhimu gani ndani ya Chadema maana chadema kama chama kimesimama kwa juhudi na maarifa ya viongozi wake na ya wananchi kwa umjula. Sasa huu muhimu wa Lowassa kwa sasa hivi unatoka wapi? Hivi kweli viongozi wa Chadema wanapenda madaraka kiasi ambacho kwao Lowassa ni muhimu kuliko sera na itikadi za chama?

Ni kweli husiopingika kwa mwaka huu tunahitaji kura ya kila mtu, na hivyo basi tunahitaji hata kura za wafuasi wa Lowassa na kwa hili ni muhimu kutumia ushawishi wa aina yeyote ile ili kuweza kupata kura hizi LAKINI KURA ZA KULAZIMISHA LOWASSA KUJIUNGA NA CHADEMA TENA AKIPAMBWA NA HAO HAO VIONGOZI WALIOTUAMINISHA KUWA LOWASSA NI MLA RUSHWA HIZO HATUZIHITAJI MAANA KWA KUFANYA HIVYO HATUTAKUWA NA TOFAUTI NA CCM. Bora kubaki wapinzani kuliko kumkubali Lowassa kujiunga na Chadema, Maana unapomkubali Lowassa, umemkubali na Chenge, Karamangi, Rostam na nk.Ni lazima tusimamie tuyasemayo majukwaani siasa za kilaghai zikome.

Mbowe kama unataka kwenda Ikulu kwa kutumia mbinu chafu za kunajisi ilani ya Chadema sisi wanachama hatuko tayari kufanya hivyo. Lowassa mlitwambia ni Fisadi na anabaki kuwa Fisadi labda mje mtwambia kuwa mlikuwa mnatulaghai.
 
Sehemu ya I


MBOWE NA CHADEMA 'THIS IS WRONG ON SO MANY LEVELS'

HAMJIFUNZI KUTOKANA NA MAKOSA

HUU SI MUDA WA SINTOFAHAMU, MNAJIMALIZA WENYEWE

Tangu habari za kukatwa kwa mh Lowassa ziwekewe hadharani kumetokea hali inayoonyesha tatizo kubwa

Turudi mabandiko ya nyuma: Tumeahi kuwaasa wapinzani kuwa kipindi cha kuelekea uchaguzi kitakuwa na mazonge zonge.
Hama hama itatamalaki, hujuma zitafanyika na uzalendo utaonekana.
Tuliwaambia wapinzani hii ni make or break. Ndiyo yanayotokea sasa hivi

Msemo maarufu wa wapinzani na CCM ni chama kwanza watu baadaye.
Anayetamka maneno hayo awe tayari kuyasimamia, ikiitwa 'walk the talk'

Huko nyuma tulisema, vyama lazima vijengwe kama taasisi na si magenge au makundi ya watu.
Taasisi ni chombo kinachosimama bila kuegeme mtu au watu.

Vyama vya upinzani vimepita vipindi tofauti. Wameondoka watu na Wamekuja watu vikaendelea.

Hivyo ndivyo taasisi zinapaswa kujengwa, tena kuanzia chini kwenda juu 'bottom-top' wakimaanisha umiliki wa taasisi ni wa watu wenyewe. Watu wale wanaotoa nyoyo na rasilimali zao kupigania chama chao si wale wanaopigania masilahi yao

Ukombozi wa nchi hauji kama mvua. Kuna vipindi vya mpito na vingine vikikatisha tamaa.
Muhimu si kurudi nyuma ni kupigana na kwenda mbele. Miaka 20 ya vyama vya upinzani inatosha kuwaelewa na kuwafunza


CCM INAJIPANGA

CCM imemaliza mchakato wake uliokuwa mgumu sana. Kwasasa mgombea wao anapita kujitambulisha ikiwa ni sehemu ya kampeni.

CCM wana rasilimali za dola na mtandao wao si wa kichama ni wa serikali.
Hata hivyo, kwa kuzingatia ugumu wa uchaguzi ujao, kazi yao imeanza mapema.
Wanaponya makovu na kutafuta udhaifu wa wapinzani

Wapinzani chini ya UKAWA hawana rasilimali za kutosha. Ilitakiwa wawe mbele ya CCM kwasababu, CCM wanatumia gari wao basikeli na hivyo kudamka si suala la hiyari bali ni lazima. Hadi sasa tunasikia vikao visivyoisha vikiendelea.
Kuna suala la CUF ambalo lilitakiwa liwe la dharura. CUF wameshikilia nafasi ya vyama vya upinzani kusonga mbele

Tulidhani viongozi wa upinzani wangekuwa wanahangika kukwamua gari ili safari iendelee.

Haionekan hivyo, kinyume chake wanaingia katika mambo yasiyo na umuhimu wa aina yoyote kwao , upinzani na taifa.

MJADALA WA LOWASSA

Lowassa ameacha na CCM kwasababu zao. Kuhamia kwake chama chochote ni haki ya kikatiba kama wanavyofanya watu wengine. Lowassa ana kundi la wafuasi nyuma yake.

Ikumbukwe tuliandika katika mabandiko ya nyuma kuwa, wafuasi wa Lowassa si wa itikadi za kisiasa,ni wafanyakazi

Wengine tumeona wakimwacha na sasa wamejiunga tena na CCM , chama kile kile walichosema hakikutenda haki kwa mtu wao. Maana yake kazi imekwisha na sasa wanatfuta ajira nyingine

WAPINZANI WANAPOPOTEZA DIRA KWA SABABU YA MTU NA SI TAASISI

Inaendelea sehemu ya II
 
Sehemu ya II


WAPINZANI WANAPOPOTEZA DIRA KWA SABABU YA MTU NA SI TAASISI

matatizo yanayotokea CCM yasichukuliwe kama faraja kwa wqpinzani.
CCM ina watu wa aina nyingi, wa masilahi''waliokufa kifikra'', wanaoona mambo hayapo sawa 'wamevia kiakili' wanaotaka uluwaa 'hawa ni CCM masilahi''

CCM waliokataa kuburuzwa waliondoka bila masharti. Mfano ni Mpendazoe hakusubiri bunge, akajiondokea zake

Hawa wanaoondoka sasa wana malengo mengine, wengi wakiongozwa na masilahi ya viibaru. Huo ndio ukweli hata kama hatuutaki

Hakuna tatizowanachama kujitokeza kuunga mkono chama kingine. Mwenendo uliopo ni wanachama kutimkia Chadema.

Hilo ni jema likitumiwa vema. Lazima tahadhari ichukuliwe, si wote wanaondoka au wanakuja na nia njema

Kukimbilia CDM kuna maana ndicho chama mbadala. Hili linawapa CDM 'vote of confidence' kwamba kuna mbadala.

CDM lazima walichukulie kama changamoto, na ni ishara ya kukua kwao na pengine kukubalika

Shibuda alihamia CDM na kugombea ubunge. CDM walikuwa na furaha ya viti bungeni.Shibuda hakuwa msaada kwa miaka 5.

Maana yake nini! Ni kuwa hata kama CDM wasingepata kiti hicho hakuna ambacho wangepoteza

Pengine nafasi ya Shibuda angeweza kugombea mtu mwingine ashinde pia, au apate uzoefu kwa mwaka huu.

Nafasi hiyo ikapotea kwa kutaka tu kuwa na wingi wa wabunge na si ubora wao.

TETESI ZA LOWASSA

Hizi zimetanda siku nyingi. Katika hali isiyokuwa ya kawaida chama cha ACT kikampa masharti.

Si kuwa walifanya hivyo kwa dhamira njema, ilikuwa kuua hoja ya UCCM-B.

Ni haki kusema, vyovyote iwavyo, msimamo wa ACT kuhusu Lowassa ulitolewa kwa wakati

Ghafla tunasikia anataka kuingia UKAWA na kuna majadiliano. Hatuwezi kuzungumzia hilo kwa kukosa uhakika.

Tunachoweza kusema, tumewaonya UKAWA kuwa huyo si mtu pekee nchi hii.
Ukawa wana wachama madhubuti waliotayari kuifia nchi hii na hao ndio wenye kauli

VIONGOZI NA KAULI ZA KUMKARIBISHA LOWASSA

Viongozi wa upinzani wamezungumzia suala la EL kwa njia za tofauti. Kauli zao haziwezi kubeba uzito kama kauli za viongozi wao

Viongozi ni wasemaji wa vyama, hakuna namna kauli zao zinaweza kuchukuliwa kirahisi rahis

Kuelekea uchaguzi kauli za viongozi zinaweza kujenga au kubomoa, na ni muhimu kuzipima

Inaendelea III
 
Sehemu ya III

MBOWE NA KAULI TATA

Kama alivyonukuliwa ndivyo na tunadhani ndivyo kwasababu haijakanushwa, kauli ya Mbowe kumkaribisha Lowassa inatia huzuni, ukakasi na inasikitisha.

Moja ya sifa ya vyama vya upinzani ni kukabliana na maovu na waovu.

Haijalishi itachukua muda gani, lazima hayo yawe mapambano endelevu ili kuinusuru nchi

Imani wanayoonyesha wananchi si suala la kubahatisha. Ni jambo la kutilia maanani kwa kuzingatia mwelekeo wa nchi yetu.
Hakuna jambo llitakalowavunja moyo kama kusikia waovu au uovu unapewa ''second chance''

Mbowe alipaswa kuwakaribisha wanachama na wananchi wote bila kutoa kipaumbele.

Kauli ya kumtaja mtu haina manTiki na ni butu. Wangapi wamehamia CDM na hatusikii wakitajwa?

Lengo la Mbowe ni kuvuta watu wa EL. Huu ni mkakati wa ajabu sana.

Hawa wanapaswa kujiunga na chama chake na kufuata misingi ya chama si kubadilisha dira na mwlekeo.

Leo mwenyekiti anasahau chama chake kinasimamia nini, hadi anamkaribisha mtu mmoja kama muhimu sana

Mh Mbowe, muhimu ni wanachama walikomaa nawe kwa miaka yote, wakipigwa mabomu, wakinyanayaswa n.k.

Hakuna mtu anaweza kusema ni mkubwa na muhimu sana ndani ya chama chako. Kwani si ni nyie mnaosema hakuna mtu zaidi ya chama? Huku kuweweseka kwa EL kunatoka wapi?

Kauli yako inaleta utata na ukakasi na kuelekea uchaguzi ni kauli ya hatari sana.

Ni bora kuwa na wanachama '10 bora' kuliko kuwa na 1000 usiowajua

Tunayasema haya kwa dhati kabisa, kwa kutambua kuwa mbowe hukupaswa kutoa kauli hiyo kwa wakati huu

Ilipaswa asimame uwaeleze wanachama wa chama wke, nini na hatua gani mumefikia katika mgombea wa Urais.

Nini mkakati wenu kuhusu changamoto nyingi zinazowakabili tukijua CCM ina dola na magoli ya mkono yapo

Ni kwanini suala la Lowassa liwashughulishe viongozi wa upinzani? Huyu ni nani kiasi cha kuopoteza focus kiasi hicho?

Mwisho wa siku akiacha siasa, mtakuwa mumevuna nini? Je, akiamua kwenda UDP mtasemaje?

Matawaeleza nini wananchi wenu kuhusu mapambano yenu dhidi ya ufisadi , wizi na uhujumu uliotamalaki
Mtawanyooshea CCM kidole gani ikiwa nini mumefumbata 5 mkmsuburi masiah?

Miaka 5 mlikuwa mnajaenga nini ambacho mnadhani ujio wa mtu unaweza kubadili upepo?

Huu ni mkakati wa ajabu sana na hapa tunajiuliza, kulikuwa na mashauriano kabla ya kauli kutolewa?

Inaendelea sehemu IV na V
 
Mkuu Mkandara

Ni tofautiane nawe kuhusu kuwalaumu wananchi kwa yanayotokea. Ninaamini kabisa, badala ya kuwalaumu wanasiasa na vyama vya upinzani, wananachi wanapaswa kuchukua lawama hizo.

Hakuna mahali katika dunia hii nguvu ya dola iliwahi kushinda umma. Dola ni zao la nguvu ya umma na si kinyume chake
Kwa dunia ya wenzetu, wanasiasa huwatumikia wananchi na si wananchi kuwatumikia wao.
Mambo yekienda kombo, jukumu la kuweka sawa ni la wananchi si la vyama vya siasa.

Vyama vya siasa hubeba agenda ya wananchi kwavile wana platform. Hufanya hivyo wakijua agenda ya wananchi ndio muongozo na si kinyume chake

Kama tutakubaliana wananchi hawana sababu ya kubeba lawama, tukubaliane hawana sababu za kulaumu wanasiasa

Muhimbili wananchi wakilala sakafuni, akina mama wakipanga foleni ya kwenda kwenye chumba cha kujifungulia hilo si tatizo la wanasiasa wanaotibiwa chunusi Appolo au Joberg. Na wala hakuna mwanasiasa atakayesimama kuzungumzia matatizo hayo kwasababu hayamhusu.

Kwa nchi za wenzetu, wananchi wanachukua jukumu mikononi mwao, iwe kwa njia ya sanduku la kura au nyingine

Ni makosa kuwapumbuza wananchi tukitumaini kuwa ipo siku malaika watataremka kulinusuru taifa. Tumejaribu miaka 50, je tusubiri hadi karne nyingine? Wale wenzetu wanaochukua hatua dhidi ya 'malaika' wamepungukiwa nini ?

Ni wananchi wa Tanzania peke yao wanaosubiri miujiza na si wao kuchukua hatma ya taifa lao

Wanasiasa wamefikia mahali wanadhani wao ndio nchi. Sababu kubwa ni wananchi walioshindwa kuwaambia wao ni waajiriwa. Mwajiri anaposhindwa kuchukua hatua dhidi ya mwajiriwa hilo ni tatizo lake, si la mtu au taasisi nyingine
Mkuu wangu tuendelee kutokubaliana katika hoja hizi maana mitazamo ipo mingi na tutafikia mahala tutaelewana kwa kutokubaliana..

Unajua kwamba wananchi sio wanaochagua viongozi bali huletewa majina na kuchagua kati yao. Unakumbuka ule ubishi wa Dr.Slaa kupata kura za wananchi wa karatu? haikuwa hivyo, na umeona ya CCM majuzi na ndivyo tunavyoendelea kuletewa wagombea au watia nia!. Sio wananchi wanaowaambia wagombea wachukue fomu bali wagombea huamua wenyewe na kwa sababu zao binafsi na hivyo wanapojitangaza ama kutangazwa ni mwanzo mpya wa wananchi wenyewe kumfahamu mgombea.

Licha ya hapo Mfumo wa nchi yetu ulivyo, mwananchi hana nafasi kabisa ya kudai ama kusema jambo na likawa. Kama wazazi wanalala chini Muhimbili unadhani wanannchi wafanye lipi tofauti? kuchagua chama kingine? Hivyo vyama vyenyewe umeona wanashindania nafasi za Uongozi hadi kutoana macho, na sii wamekubaliana nini juu ya maslahi ya wananchi!.

Ebu fikiria kidogo hapo, kwa nini vyama vyote nchini ugonvi wao mkubwa ni madaraka ndani ya vyama! Kuna nini haswa ukiwa kiongozi kiasi kwamba uko radhi kupoteza wanachama ubakie pake yako..Watu ndani ya vyama hawazidiani hoja zao kwa sera, dira ama idea mpya isipokuwa nani awe nani na roho ya KWA NINI..Na ukija kwenye uongozi wa Kitaifa jambo lolote linalowanufaisha wao hufukia vichwa vyao mchangani kama mbuni. Chukulia mfano wa mishahara ya wabunge, posho VX na hivi viiunua mgongo na nkadhalika, hao wananchi wafanye nini ikiwa hawakubaliani na miwang vilivyowekwa?

Mbunge mmoja anakula mshahara wa millioni 11 kwa mwenzi au Mil. 132 kwa mwaka na anaruhusiw akuwa na biashara zake, wapo wabunge 340 ni ngapi hizo - Tril. 44,880 kwa mwaka je miaka mitano?. Wanakula Posho at least mil 50 kila mmoja kwa mwaka mara 340, tril. 17 kwa haraka haraka kuna trillioni 61 kwa mwaka zinachezewa na hao hao unaosema tuwachague watatuletea maendeleo kumbe ndicho kinacho walepeleka Dodoma. Hapo hatujui Mishahara ya rais na ofisi zake, Makamu na ofisi zake, waziri mkuu na ofisi zake! taasisi za seirkali na kadhalika. Unafiiri ni kiasi gani tunachoma kwa matumizi ya kawaida tu..

Unataka mwananchi afanye nini kwenye sanduku la kura kupinga matumizi haya yasokuwa na huruma, ikiwa wagonjwa wanalala chini! Unapojiandikisha Ubunge unaondoa Huruma yote kwa sababu unajua unaenda chuma sio kumhudumia mwananchi. Uzalendo mgumo kaka sii swala la wananchi tena. Hakuna mgombea hata mmoja anayeingia Chimwaga atayezungumzia kuwa haya ni matumizi mabaya ya serikali ndani ya bunge hakuna..

Akitokea mgombea kesho akitangaza nia ya kukata matumizi ya kawaida ya serikali KUBWA na akaweka mfumo bora zaidi wa utekelezaji na uwajibikaji basi ndio nitaweza wapima wananchi kwa sababu adui wa maskini ni Umaskini wenyewe. tazama maskini wa watu wanavyosumbuka na Lowassa, wanamlilia kwa sababu kawaahidi pepo (kuondosha Umaskini) yale yale ya Mtikila 1995, wakidhani kwamba maadam Lowassa ni tajiri basi atakuwa na njia za kutajirisha watu wote wakati Lowassa huyo huyo ana ndugu zake wa damu na maskini..

Haya leo tunaambia tujiandikishe tupige kura ni haki yetu lakini tuloletewa ni Magufuli, Lipumba na Lowassa ambao wote wataahidi mambo yale yale isipokuwa wewe mwananchi unamuona nani zimwi likujualo! Kwa mfano CCM imeshatoa ILANI yake je umesikia Ilani ya UKAWA ama niseme CUF, NCCR au Chadema? hakuna zaidi ya ahadi ahadi ahadi za mgombea.

Haya wananchi wakifanya mgomo wanapigwa tena wanaitwa waleta fujo na kupoteza AMANI, huu ni mtazamoa wa viongozi na nguvu ya dola sio wananchi weloshika mpini. Kuna habari za mujini zinasema kwamba TISS wote wamerudi kambini hawatagombea Uchaguzi huu kwa sababu kuna hali ya hatari Kiusalama, na watu wote wanaoendesha vijimambo vya kuvuruga AMANI na UTULIVU watashughulikiwa! hapo sii swala la demokrasia tena, ila Usalama wa Taifa, sasa wewe na mimi ukishasikia hayo utaweza hata kuhema!..

Kifupi sisi tukubali KUTAWALIWA na hawa ndugu na jamaa zetu rangi moja, lugha moja.. Kufa hatufi, lakini cha moto twakiona!
 
Mkandara.nimekusoma vizuri wewe pamoja na Nguruvi3. hoja zenu.

Ni kipi wananchi wanatakiwa kukifanya kwa sasa maaana walikuwa wanategemea upinzani kama kimbilio lao upinzani nao kimbilio lao kwa hawa mafisadi ambao kila siku wamekuwa wakiwambia wananchi ndiyo wanaoliangamiza taifa letu kwa ufisadi.

Kwa mtazamo huu wananchi wanaotaka mabadiliko wamebakia njia panda hawajui wapi wakimbilie.
 
Last edited by a moderator:
Wanasiasa wamefikia mahali wanadhani wao ndio nchi. Sababu kubwa ni wananchi walioshindwa kuwaambia wao ni waajiriwa. Mwajiri anaposhindwa kuchukua hatua dhidi ya mwajiriwa hilo ni tatizo lake, si la mtu au taasisi nyingine

Lakini Nguruvi3 nadhani ukweli ni kuwa mpiga kura ndio mwajiri. lakini nadhani unakubali kuwa hali halisi hapa tanzania ni tofauti. Mwanasiasa ndio mwajiri mwa mwananchi, ndiye anatoa ujira na ndiye anayeamua kila kitu. Na hii imetokana na kujenga imani kwa wanasiasa wakati wa enzi za Nyerere wakati wanasiasa walikuwa wakweli.
 
Mkuu Nguruvi3, ni kweli EL kawashughulisha sana upinzani, na kwa hakika mtu wa aina yake kuhamia upinzani na kupewa cheo chochote kwa sasa hasa kugombea uraisi its a disgrace to upinzani na watanzania wote, ni kujichafua na kuharibu taswira ya kile ambacho wanakipigabia kila siku.

Wapinzani walipigiwa ngoma wacheze nao wakacheza bila kujua wao wanapoteza muda na kuwapa nafasi wenzao kujipanga na kujisahihisha pale walipoosea, nikosa kubwa sana wanafanya.

Niwapongeze CCM wanajua sana kujipanga nakuju madhaifu ya wapinzani wao na kuwachezesha shere wapendavyo na bahati mbaya wapinzani nao hawajifunzi kwa makosa yao hucheza ngoma ya CCM na kupoteza fursa njema za wao kusogea, sioni mantiki yakumpapatikia mtu ambae kila siku anaonekana kama nembo ya ufisadi. Wapinzani wajifunze kwa hili, kutopotezwa na kutopoteza fursa.

Bado ninaamini sana vyombo vya habari ndio vinashabikia EL kuhamia upinzani na kuwavuruga, bt sidhani kama yeye mwenyewe anaweza kutoka ndani ya CCM na kupoteza legacy yake, wht i belive yeye ni kama samaki nje nye ya maji kama akitoka huko, na pia sidhani kama wapinzani wanaweza kuwa na upungufu mkubwa wa maarifa kufanya maamuzi ya kijinga na kuwaharm katika kipindi hiki muhimu kwao.
 
Mkandara.nimekusoma vizuri wewe pamoja na Nguruvi3. hoja zenu.

Ni kipi wananchi wanatakiwa kukifanya kwa sasa maaana walikuwa wanategemea upinzani kama kimbilio lao upinzani nao kimbilio lao kwa hawa mafisadi ambao kila siku wamekuwa wakiwambia wananchi ndiyo wanaoliangamiza taifa letu kwa ufisadi.

Kwa mtazamo huu wananchi wanaotaka mabadiliko wamebakia njia panda hawajui wapi wakimbilie.
Wananchi hawawezi fanya lolote ikiwa mfumo wenyewe ni mbaya kiasi kwamba tuna Ushabiki wa vyama na sio Upinzani. Hili ni tatizo kubwa Kidemokrasia nchini na hivyo itachukua miaka pengine 20 mbele kabla ya mageuzi ya fikra ifikie watu kuvitazama vyama kiitikadi badala ya WATU waliomo.

Vyama vyote kwa pamoja huwezi kuta wanapingana juu ya itikadi yeyote ile, ni swala la mtu na mtu maana ndani ya CCM wapo wajamaa na wapo wahafidhina; Chadema; CUF; NCCR kote ni hadith ile ile wamejenga makundi ndani na nje ya ushabiki, kwa hiyo ndio maana mijadala yote humu JF inazungumzia WATU na makundi yao. Huwezi sema CCM pasipo kuwataja wahusika ambao wanakufanya uwe mwana CCM au Chadema na kwa kundi gani. Tumefikia hapo sasa kisiasa na tumetoka nje kabisa ya ulingo wa demokrasia.

Maadam wananchi tunachagua WATU ndio maana vyama vinashawishika kupokea viongozi toka vyama vingine kutokana na umaarufu wao wala sio waumini wa kweli wa chama wala mrengo huo. Kwa hiyo, sio kazi rahisi kabisa kuwabadilisha wananchi kwa sababu mpenzi wa Yanga huwezi kumhamishia Simba wala wa Simba kuja Yanga isipokuwa wanaweza kwenda Azam. Sii rahisi CCM kushindwa uchaguzi huu kwa sababu ya kimfumo ..Wachezaji huwa ndio wanahama hama inategemea na Contract na ndivyo vyama vinavyosajili wanachama wapya kwa Contract wakiahidiwa nyadhifa kana kwamba wao ndio waajiri.

Mtu anataka kujiunga na Chadema lakini anaweka masharti, anafuatwa na kuombwa ajiunge, CCM nako wanatembeza pesa kuahidi viongozi wa Chadema, CUF. NCCR walofanya vizuri mwaka 2010 waingie CCM..Sisi washabiki tunabakia kucheka na kushangilia kwa usajili mpya!. Usajili unafanyika na ndio maana wabunge wanaahidiwa nafasi wakijua kuna mishahara mikubwa utadhani wachezaji wa EPL. Vyama ni club za mchezo wa siasa - They make money out of each MP..

Mkuu Wadanganyika hatuwezi kubadilika hata tuichoke CCM, it's a system had to change. Pengine njia pekee ni kupitia UPINZANI ambako hakuna UTU. Hivyo kama Upinzani wataweza kusajili wachezaji wapya na sio kina Balotelli (Lowassa) ama kina Rooney (Lipumba) walochoka kisiasa inawezekana CCM kuondolewa madarakani lakini the game inabakia pale pale. Wananchi wataendelea kuwa washabiki, kuvaa jezi, kupeperusha bendera wakishangilia timu zao ama timu mpya dhidi ya adui yao! Kwa nchi yetu Ubingwa unatokana na vyama sio wananchi kura zetu ni kujiunga na DSTV...
 
Back
Top Bottom