2015-uchaguzi mkuu na hatma ya nchi

HALI YA WAPINZANI

Nao kama wananchi wameduwaa wakisikiliza nini kitatokea Dodoma.

Tunasema wameduwaa kwasababu hata kama wana shughuli zandani, bado walitakiwa ‘waibe' au steal the show ya CCM katika kueleza mambo kadha wa kadha

Katika kipindi hiki ,wabunge wao walitakiwa wawafikie wananchi kuwaeleza nini kimetokea.

Hilo lingesaidia sana kwenda mbele.Tunasikia walikuwa katika vikao vya kutafuta mgombea

Mgombea wao alikuwa apatikane katika njia mbili

1 Kuwa mbele ya CCM na kupata coverage na publicity yakutosha

2 Kusubiri mwangi wa CCM upite iliwapate publicity sawa aukubwa

Ukawa wakimtangaza mgombea wao katika kipindi cha siku tatu au nne zijazo, litakuwa kosa a kisiasa.

Mgombea wao kama upinzani atapata coverage ndogo akifunikwa na kivuli cha mgombea wa CCM ‘eclipse'

Hivyo, hawatkiwa kuingia katika vurugu za uchaguzi wa ndani.Wanatikiwa wawe na subra kwanza.

JE, KIONGOZI WAO ATAPATIKANA KUTOKA WAPI?

Ukawa wameshaona mpinzani wao wa CCM ,wana nafasi nzuri ya kupata mtu wa kukabiliana naye.

Kosa kubwa ni kudhani mgombe wao atatoka ndani ya wale viongozi. Ni busara wakajaribu kuangalia nje ya viongozi.

Hii haina maana waache viongozi wao, hapana, maana yake ni kuwa lazima waongeze wigo wa kupata mtu mwenye weledi, anayeweza kujieleza,mwenye maono na mvuto

Kukubalika ni zao la mambo hayo, na hivyo kukubalika ni jambo linalofuata siyo linalotangulia kupata mgombea makini

Tutoe mfano, tunajua Prof Kabudi ni CCM. Lakini pia hatumjui kisiasa. Tunachofahamu ni profesa.

Katika tume ya Warioba,mijadala ilipokuwa mikali, Prof alihudhuria mkutano mmoja tu.

Akazungumziasuala la katiba. Kuanzia hapo alibadilisha mwelekeo wa mjadala kabisa.

Tukasikia watu wakimuongelea licha ya kutokuwa na umaarufu.

Prof Kabudi akisimama ana charisma, ana weledi na ushwawishi wa hoja kiasi cha kukubalika na mkaundi yote

Ukawa waangalie mfano huu na kujiuliza kama ni sahihi kujiwekea uzio wa wagombea wao.

Tumalize kwa kusema, kinachoendelea Dodoma ni kukabidhiana vijiti.

Kama Watanzania wataendelea na usahaulifu walio nao, wakaendelea kubadili mvinyo kwenye chupa mpya wakitegemea matokeo tofauti , ni kujidanganya

Uchaguzi wa ndani wa CCM umeonyesha madhaifu makubwa.Kwamba, wagombe wao wamepatikana kwa njia za kubuni.

Wataletwa kwa Watanzania kwa kelele za huyu amelelewa na CCM.

Hawataweza kufanya jingine tofauti na sasa kubadili mfumo huu wa kifisadi uliotufikisha hapa

Kuna uwezakano wa kubadili nchi na utawala iwe, kwa Rais au bunge

Tatizo na swali ni , je, Watanzania wataacha usahaulifu wao,wataacha kulalama na kutenda?

Watasimama katika ukweli au wataogelea katika udanganyifu?

Tusemezane
 
Update : Ni John Pombe Magufuli

hilo ndilo lililotarajiwa kwa sababu ulizozieleza hapo juu, he was the best candidate among ya wale walioingia top 3, pia ni mnufaika wa mnyukano kati ya team Membe na team Lowassa.

waiting for the last part, udhaifu wa upinzani kutoa ruum kubwa ya coverage kwa mchakato wa Dodoma kwa wao kukaa kutokua na shocking activities na kutegemea mvurugano wa CCM, na wht is the way forward UKAWA wafanyaje kukabiliana na CCM iliyoimarika sio kwa umoja wao bali kulinda interest zao
 
hilo ndilo lililotarajiwa kwa sababu ulizozieleza hapo juu, he was the best candidate among ya wale walioingia top 3, pia ni mnufaika wa mnyukano kati ya team Membe na team Lowassa.

waiting for the last part, udhaifu wa upinzani kutoa ruum kubwa ya coverage kwa mchakato wa Dodoma kwa wao kukaa kutokua na shocking activities na kutegemea mvurugano wa CCM, na wht is the way forward UKAWA wafanyaje kukabiliana na CCM iliyoimarika sio kwa umoja wao bali kulinda interest zao
Mkuu ahsante kwa mchango, hapa turejee nyuma.

Kwamba, CCM itaparaganyika hilo Ukawa wasitegemee

Hata kama litatokea, itakuwa ni makossa Ukawa kutegemea manufaa yoyote kutokana na mtifuano au timbwili la CCM

Hivyo, tungewashauri haya

1 Hit the ground running. Kwamba si wakati wa vikao, muda simshiriki wao mzuri.
Wengine wakiwa katika vikao, waliobaki watawanyike kuwafikia wapiga kura


2 Watilie mkazo suala la kujiandikisha kwa wapiga kura na kuhakikisha mbinu zilizotumika huko nyuma za kununua shahada zinaibuliwa mapema

3 Watangaze watu wao mapema, kwasababu hawana resources kama CCM.
Wagombea wao hawatapata msaada wa wakuu wa mikoa wala wilaya.


4. Wasiingie katika vurugu zinazoendelea. Wasubiri afters chok ili waje na shock yao itakayohamisha mjadala kutoka CCM

5 Wahakikishe wanapata coverage kutokana na resource walizonazo

6 Waepuke vurugu za ndani ndani zinazojitokeza magazetini ambazo zinathibitishwa kuwa na ukweli na viongozi wao

7 Wawe na ilani inayo address matatizo ya wananchi, waeleze wataituamiaje na kwasababu zipi kuwafikia wananchi

8 Wahakikishe wana strategists/pundits wa kukabiliana na CCM, kuwaweka CCM katika kujilinda na siyo kushambulia

9 Wachukue agenda zinazowagusa wananchi, wazianishe ili kuwapa weledi wakati wanakwenda kwenye sanduku la kura

10 Watumie fursa na makosa ya kisiasa kutoka kwa wapinzani wao.
Mfano, inashangaza Nape anasema goli la mkono, hadi leo wapinzani wanaongelea kama jambo la kawaida.

Hilo lingeweza kuwa issue na kuwaweka tume na msajili mguu sawa, wakiwalazimisha CCM kujibu na si kueneza
propaganda. Hilo tu lingeweza kufunika mkutano mzima. Wapinzani wapo wapi?
 
Mkuu Nguruvi3, katika bandiko #162 , nakuabaliana na ww kabisa kwamba CCM wamfanikiwa Dodoma na wameondoka wamoja, na kama nilivyosema hapo juu kuna makosa ya kiufundi UKAWA walifanya katika kuwapa coverge CCM sana, walikua na nafasi nyingi sana kupata media coverage atleast kupunguza media attention kule Dodoma, moja wapo ilikua ni walkout yao kupinga miswaada yamafuta na gesi pia kuwa na mchakato wa kutafuta mgombea.

Kuhusu kuamgalia other options, naungan na ww sana tena sana inawezekana wakapata best candidate sana, waache tu ubinafsi, mfano mzuri ni 2010, no one predicts Dr.Slaa as a Chadema presidential nominee before july, ila alivyochaguliwa alibadilisha momentum kabisa tofauti na Mbowe 2005, sowanaweza kuwashawishi wengine wenye haiba kuwasaidia kupambana, lengo ni kushika dola na kubadili mfumo so nikutafuta best strategy. Kuna watu wengi sana hawakubaliani namfumo wa CCM hata kama wako huko wanaweza kushawishiwa, mtu kama Prof. Kabudi, Jaji Warioba au yyt afaae, hii taondoa makando kando mengi sana na kuwaunganisha.

Kuhusu kuimarika CCM huko Dodoma; mkuu Nguruvi3 umeeleza yote ila kwa kuongeza tu, wapinzani bado wana nafas wala hawatakiwi kuvunjika moyo kwani ninachokiona hapo ni kura za hasira kwabaadhi ya maeneo hasa ukanda wa Kaskazini ambako mtu wao aliyjihakikishiasana ametoswa, wajipange tu kuwa na strategy nzuri za kutozimisha moto kuanzia kipindi hiki mpaka kipindi cha kura,
Niwapongeze CCM wamepambana dakika za mwisho kunusuru chama chao kuvunjika pale Dodoma, ila tu mfumo mzima ninavyona wa kumpata mgombea this time kwao umeacha sana madonda mengi ambayo wapnzani wakikaa vizuri ni advantage kwao.

Mwisho niwashauri UKAWA wasiwe na pupa sana kumtangaza mgombea wao kwa sasa maana all over there isa cloud kwa mgombea wa CCM, watulie kdg nakujipanga vizuri huku wingu la CCM likipotea, wao wakitangaza waje na mshituko wao na utakao amsha ari ya wapiga kura na mashabiki wao, kwa sasa wataonekana wamefollow CCM paths, wakomae na watu vijana kwa wazee wajiandikishe kwa wingi kwamaeno yaliyobaki na pia kwa tume ilikopita ila bado watu hajapata nafasi kujiadikisha,
Knw uwanja sio balanced kwa maana ya tume ya uchaguzi na mazingira yake yote, bt wakikomaa kupata kura za mafuriko, ltaleta maana kwenye Plan A1 na Plan A2 ( sio plan A and B) kama alivyoeleza Nguruvi3 kwenye mabandiko ya mwanzo
 
MGOMBEA MWENZA

'WOMEN FACTOR'


Tulisema,dhahiri ‘women factor' ni karatamuhimu sana kwa CCM. linatokana na ukweli kuwa katika makundi kama ya vijana, CCM ina wakati mgumu.

Samia Suluhu ndiye mgombea mwenza.Watanzaniawakikumbatia hali iliyopo, anaweza kuwa makamu wa Rais.
Ukiangalia kwa undani, Samia amekuwa waziri wa muungano, na pia naibu Spika wa bunge la katiba


Madudu yaliyofanywa na akina Sitta, alikuwa mshiriki.Madudu ya serikali hii ni mshirika kama alivyo Magufuli.
Kama yupo anayetarajia kitu tofauti, huyo ajiulize tena na tena, hivi lini Mchicha uliweza kugeuka kuwa mbuyu?


Women factor ni karata kwa kuangalia population. Ndiko CCM wanakowekeza kwa gharama zozote .
Wapinzani wana advantage ya kundi lenye ushawishi la vijana, kazi waliyo nayo ni kushinda kundi la akina mama


Kwa mtazamo wa kisiasa, mwanaume anapokwenda 'toe to toe' namwanamke hasa katika jamii zetu, mwanaume ana kesi ya kujibu. Hivyo, wanawake wa CCM wanapaswa kujibiwa na wale wa upinzani.
Haionekani kama upinzani uposawa katika eneo hilo. Kuna kudorora kuzuri tu, na hilo lazima liwe wake up call kwa UKAWA


Wanawake wa kundi la upinzani wana agenda juu ya nchi na wanawake wenzao. Kwa miaka 50 wanawake wa CCM wamekuwa madarakani wakipewa kila ushirikiano. Leo wanawake wa Tanzania wanalala wawili vitandani kwa wenye bahati, wengi wao wanajifungulia juu ya matenga ya baiskeli. Vifo vinavyotokana na kuwa neglected na serikali havina unafuu. Matatizo yanayomkabili mtoto wa kike yapo pale pale miaka 50 n.k

Wapinzani wana kesi, kinachotakiwa ni mwendesha mashtaka ili hukumu itolewe na akina mama.
Wana fursa nyingi, ikiwa ni pamoja na mifano halisi. Mfano, UWT wamefanyanini cha kuwaonyesha wanawake wenzao kama mafanikio. Ni agenda ipi ya wanawake wameipeleka mbele ukiachilia mbali kugawana madaraka na kudai vyeo


Katika mazingira halisi wanawake wa upinzani wanahoja, tatizo ni kuwa, je wapo tayari kutengeneza mashtaka na kuyafikisha katika koti ya wanananchi

Hili la women factor ni moja ya karata muhimu sana za CCM kwasasa. Wakibanwa eneo hilo watakuwa na wakati mgumu. Katika hotuba ya JKbungeni kwa wabunge wa CCM, Rais alizungumzia sana fursa za wanawake.

Ile ni makusudi kabisa akielewa CCM imepoteza ushawishi na kundi walilo nalo niwanawake tu.


Je, wapinzani wanaona hii kama opportunity kwaupande wao?

Je, wataweza kutumia fursa hiyo kupata mafanikio chanya? Wako wapi?


Tusemezane
 
Nguruvi3,

Ukawa kama wakiwa smart, wangeweza ku-target vijana na wanawake wa CCM ambao wako marginalized.

January Makamba alitumia muda mrefu kujenga base kupitia vyuo, John Mnyika anatumia muda kupigania maslahi ya jimbo.

Kuna haja ya Chadema, CuF, NCCR kuanza kubadilisha Guards. Mtu kama Himid angekuwa chambo kizuri sana kwa Ukawa kugombea Muungano kama CUF wanaweza kuwa open minded na kuachana kung'ang'ania Zanzibar.

Njaa ya kukimbilia IKulu pekee, ndiyo itakayowaangusha Ukawa. Aidha kutarajia fall out na makombo ya CCM au viporo vya CCM si tija.

I trully hope kutatokea change of guard ndani ya hivi vyama pamoja na kujibadilisha kimfumo na utendaji kuhakikisha kuna balance katika bunge.

Kinana keshatangaza kuwa wanafanya reforms ndani ya chama na kuwavua mawaziri na watendaji wakuu wa Serikali sehemu kuu za maamuzi ya kichama ili kuongeza ufanisi na uwajibikaji.

Ukawa tuliwashauri hili, kuunda timu ya kukaa bungeni pekee kama serikali na timu ingine kichama kutangaza sera na itikadi. Lakini sidhani kama hili lilizingatiwa au kupewa kipaumbele.

Mengi ya kujifunza mwaka huu!
 
Nguruvi3,

Ukawa kama wakiwa smart, wangeweza ku-target vijana na wanawake wa CCM ambao wako marginalized.

January Makamba alitumia muda mrefu kujenga base kupitia vyuo, John Mnyika anatumia muda kupigania maslahi ya jimbo.

Kuna haja ya Chadema, CuF, NCCR kuanza kubadilisha Guards. Mtu kama Himid angekuwa chambo kizuri sana kwa Ukawa kugombea Muungano kama CUF wanaweza kuwa open minded na kuachana kung'ang'ania Zanzibar.

Njaa ya kukimbilia IKulu pekee, ndiyo itakayowaangusha Ukawa. Aidha kutarajia fall out na makombo ya CCM au viporo vya CCM si tija.

I trully hope kutatokea change of guard ndani ya hivi vyama pamoja na kujibadilisha kimfumo na utendaji kuhakikisha kuna balance katika bunge.

Kinana keshatangaza kuwa wanafanya reforms ndani ya chama na kuwavua mawaziri na watendaji wakuu wa Serikali sehemu kuu za maamuzi ya kichama ili kuongeza ufanisi na uwajibikaji.

Ukawa tuliwashauri hili, kuunda timu ya kukaa bungeni pekee kama serikali na timu ingine kichama kutangaza sera na itikadi. Lakini sidhani kama hili lilizingatiwa au kupewa kipaumbele.

Mengi ya kujifunza mwaka huu!
Mkuu Rev. Kishoka

Umeibua hoja nyingi muhimu sana kwa kuzinyambulisha

1 UKAWA wana base ya vijana, CCM wanaelewa. Vijana wameichoka CCM na matumaini yao ni mbadala kama UKAWA.

Mfano wa January ni mzuri sana, alicheza na kundi ailoona lina nguvu na ushawishi

Ndivyo Obama alivyocheza. Ukiangalia ramani, institutions ilikuwa base yake. Hilo liliondoa ‘women factor' ya Hillary na old guard ya Mcain

Ukawa wana advantage, kundi la vijana ni ‘tuned' linasubiri hamasa. Waelekeza nguvu maeneo udhaifu.

Ukawa akina mama lipo tatizo na hapo ndipo watakuwa vulnerable


2 Kutarajia makombo a.k.a fall out ya CCM.
Kama lipo kosa nihilo la kuchukua CCM waliochukizwa na mfumo wa kifisadi kufisadi watu wao ambaoni fisadi

Waliochukizwa na CCM wapo, Mpendazoe ni mfano. Haieleweki ni kwa vipi haonekani katika inner circle? Kuna shaka gani? Kuchukua makombo kutavunja morali ya watu wa kweli, kama hawakumbuki wajiulize wapo wapi akina Amani?

3 Kuhusu reform
Wapinzani wameelezwa siku nyingi, lazima wawe na structure inayo fit mahitaji ya sasa.
Template ya CCM siyo standard. Na kwavile wanafuata template ya CCM, kuna tatizo linawakabili, mgombea mwenza


4. Kuhusu Mansour Himid, hakika ni mjenzi mzuri wa hoja.Naye kama Maalim wamejikita katika siasa za Uzanzibar zaidi kuliko Utanzania.Wangeweza kufanikiwa kama wangepigana ndani ya Tanzania ili mwisho wapate upper hand ya kutaka Uzanzibar. Kisiasa hilo lina waumiza kwasababu wanakosa platform and publicity ya bure

Mfano, CUF wamefanya mkutano ZNZ, wakaamua nani agombee na kila jambo likaishia huko.

Laiti wangefanya Dar kungekuwa na publicity si ya kule visiwani tu bali ndani ya Ukawa bara.


Yote hayo yanatokana na Ukawa kuanzishwa kutokea top to bottom. Haikuwa jambo baya, tatizo ni kuwa hakuna aliyeshughulika kuichukua kutoka top kuipeleka bottom.

Pamoja na resource na public support,kuna swali, je wameweza kuunganisha nguvu na hoja zao kwenda kule walikotarajia?


Pamoja na udhaifu unaonekana, Ukawa wakijipanga na kuacha innuendos na endless meetings, wakatoka na ujumbe na kufikia walengwa,wakisoma ramani ya uchaguzi, hoja za wananchi na agenda ya nchi, kama upo mwaka wanaoweza kufanya breakthrough ni huu. CCM ni vulnerable kutokana na udhaifu walio nao sasa hivi

Hofu niionayo kwa ukawa ni , je, wanauona udhaifu wa CCM na wana uwezo wa kutumia udhaifu kwa faida yao?

Tusemezane


cc MJINI CHAI
 
Nguruvi3 na Rev. Kishoka, bandiko # 167 & 168, mmeniacha kidogo kwenye hoja moja ya kuchukua watu toka CCM au vyama vigine.
Kwa mtazamo wangu lengo la chama kushindana ni kupata wanachama wapya including wasiokua na gyama na waliokua kwenye vyama vingine, mm naona hakuna ubaya wowote kuchukua watu waliochoka na mfumo wa CCM au vyama vingine na kujinga na upinzani ( UKAWA), I wapo tu watu hao sio mamluki wameondoka kwa moyo mmoja.

Kosa ninalo liona ni kitendo cha hao wanohamia kuwapa vyeo kwenye chama na kuwaacha wenyeji na waliokipigania chama muda mrefu, hapo itawavunja moyo, ila kama kuna sehem hao waliohamia wanaweza kusaidia without affecting those who suffers to build the party hapo patakua pana kosa.

Mm naamini wengine huamua kuahama kwa hasira toka kwenye vyama vyao vya awali, na kama walikua ni viongozi au wenye influence huondoka na kundi kubwa sana, sasa hili kundi kubwa ndio lenye shida na more critical ambalo sasa ni jukumu la strategist wa chama kukomaa kuwaelimisha kuelewa falsafa na muono wa chama na kuwashawishi kwamba ni chama Bora na wakiamini, sijajua mipango yao kwenye hilo.

Mm naona UKAWA wawapokee hao waliokimbia vyama vyao either kwa hasira, sera za chama au kuumizwa walikotoka, ila tu asiwape madaraka mapema mpaka kwanza wajiridhishe kuwa ni wanachama waaminifu, na kwa maana hiyo ni next uchaguzi not nw, kwa sasa waendelee na watu wao waliojipanga muda mrefu, kama hao wamehamia kwa mema hawatang'ang'ania vyeo.

Huo ndio mchango wangu kuhusu wanohamia kutoka CCM na vyama vingine, naomba ufafanuzi zaidi wakuu kama nimeelewa vibaya.
 
King Suleiman

Hoja siyo wapinzani kukataa wanachama wapya waliohama kutoka mahali pengine.
Kila mwanachama ana haki ya kujiunga na chama cha siasa kwa kadri anavyoweza na ni kumnyima 'haki' yake kisiasa akikataliwa

Hoja hapa ni kuwa wapo wenye hasira ndani ya CCM, na wenye kuvizia madaraka wanaoona kauzibe

Hawa watatafuta mahali ili kwenda kupata ticket tu ya udiwani au ubunge.
Pengine hawajui hata mstari mmoja wa sera za chama wanachohamia

Hawa ni hatari sana hawana uchungu na wanachosimamia. Yaani wanajiuliza vyama vitawafanyia nini badala watafanyia nini vyama.

Mfano mzuri ni Shibuda. Baada ya kupata Ubunge akarudi kueneza sera za CCM ile ile iliyomkataa.
Maana yake ni kuwa anaamini katika CCM na anaamini katika Upinzani katika kupata tiketi. Angalia alivyowavuruga Chadema, badala ya kuwa assest amekuwa liability.

Hatari nyingine ni kuua moyo wa watu wenye mapenzi ya dhati ya vyama vyao.

Utakumbuka Iringa alipouawa Mwandosi, kuna mwananchi alitoa eneo ijengwe ofisi ya chama, wapo waliotoa senti ofisi zisimame.

Hawa ndio wenye vyama, leo ukiwapelekea makapi ya CCM kwasababu tu yana jina, tayari unaua morali na chama

Suala si kuzuia mtu au watu kujiunga, hoja ni kuzuia kujiunga kwa manufaa yao binafsi. Hilo ni baya sana katika politics

Ima kuna eneo wanaweza kusaidia bila kuathiri hali iliyopo, sioni kama kuna tatizo kubwa.
 
YA DODOMA KWA UFUPI

Mkutano mkuu ulipooza, sababu kubwa ni uwepo kwa makundi.
Wajumbe walifika Dodoma wakiwa na maamuzi Kilichopoozesha zaidi ni uwepo wa kundi kubwa la EL


Baada ya mgombea wako kutopata nafasi, lilivuruga uchaguzi kwa njia moja au nyingine.
Wajumbe wakagawanyika kuunga mkono kambi zingine, wengine wakisusia kabisa


KILICHOTOKEA
Hakukuwepo na ushindani wa hoja. Wagombea hawakuulizwa maswali wajumbe walishakuwa na maamumzi.

Katika chama kikongwe chenye demokrasia hakikuonyesha ukomavu bali udumavu.
Hii si mikutano mikuu tuliyoona nyuma. Ilikuwa ushindani wa ‘mtu wetu'


Hali hiyo ikaleta hoja nyingine ‘Udhaifu wa kujieleza wa wagombea''

Walilenga kuvuta makundi ili kupata ushindi si kuongea viongozi watarajiwa wa kitaifa. Maana nzima ya kuchagua ikaingia doa.

Amina S Ali

Kambi yake ilijua ni dhaifu, asingeweza kukabiliana na hoja au maswali. Akakimbilia kuungwa mkono na Kambi ya Lowassa.

Alifahamu uzoefu wa kazi na taaluma zake na ugeni katika siasa za muungano usingempa nafasi hata kidogo.

Alijua anaungwa mkono na Wazanzibar, pengine angepata za watu wa kambi ya Lowassa angefanikiwa.
Ni kosa la kutosoma mazingira. Kambi ya Lowassa ilishavurugika na hakukuwa na msimamo tena


Masimamo wao uliisha baada ya kuwashughulikia Jan na Bern katika NEC

Asha Rose Migiro

Aliingia kwa kete ya usomi na uzoefu katika taifa na kimataifa.
Akatafuta kuungwa mkono kwa kusema alizaliwa ‘Ruvuma' Inaweza kuwa kweli alizaliwa huko, je, ni mwenyeji wa Ruvuma?

Kuzaliwa sehemu hakuondoi asili tukijua wazazi husafiri kutafuta maisha.
Neno Ruvuma lilikuwana maana katika kutafuta ‘neutral position'


Mbele ya safari kauli ya kuzaliwa ingemsumbua,Asha ni mwenyeji wa mkoa mwingine hata kama amezaliwa Ruvuma.
Siyo mngoni


Kosa lake kisiasa ni kujifungaminisha na viongozi wa juu na kusahau kundi la akina mama.
Alionekana siyo mwenzao na anabebwa. Ndicho chanzo cha kura 59


Magufuli Pombe

Aliingia na gia ya ujenzi wa miundombinu .akilenga kuvuta watu kwa utendaji unaosifiwa hasa kumbu kumbu za takwimu.

Ushindi wake ulitokana na udhaifu wa wapinzani wake wawili.
Bahati aliyokuwanayo ni kutoshambulia kambi kubwa ya EL.

Akaungwa mkono na masalia ya Edo,kambi za wasomi kama Mwandosy,na kambi ya Bern na Jan


Kimya chake wakati wa kutia nia, kuchukua fomu na kurudish ailikuwa kete muhimu sana

Tusemezane
 
SAMIA SULUHU
‘MACHALE' YAMSADIA KUPATA UGOMBEA WENZA
Katika mazingira ya kawaida, Amina Salum angekuwa mgombea mwenza wa Magufuli.

Kinyume chake, Samia suluhu akachukua nafasi hiyo. Zipo sababu za hayo kutokea

Kwa vile CCM inacheza na karata ya jinsia, wanachama wa kiume hawakufikiriwa katika nafasi hiyo.

Kete ya jinsia ilimsaidia sana JK kipindi cha pili, vinginevyo angeweza kushinda kwa 0.1 ya jumla

Kwa ufupi, wazanzibar wanaume waliofikiriwa kwa uchache ni hawa

Shamsa Nhodha
Huyu alikuwa waziri kiongozi, akawa waziri wa ulinzia. Ni muumini wa muungano wa serikali mbili.
Ni mtu anayetaka kulinda mapinduzi, akiongozwa na ''hisia na woga'' zaidi za lengo la mapinduzi
Ni mwiba mkali na mhafidhina,. Uwepo wake ungejenga ufa na kuimarisha kambi ya wapinzani CUF

Seif Idd
Ni mwiba mkali sana wa upinzani. Hana masihara na mapinduzi na muungano wa serikali mbili.
Ni mgumu wa kutafuta kati na kati. Hupiga kwa maneno bila kuangalia kulia au kushoto.
Uwepo wake ungesumbua serikali ya umoja wa kitaifa

Shamhuna na Vuai Ali
Nao kama wengine ni waumini wa muungano wa S2. Ni wahafidhina wakubwa , wasiotaka kusikia zaidi ya wanachokiamini.

Samia Suluhu
Alikuwa makamu mwenyekiti wa Bunge la katiba. Alishiriki katika madudu ya katiba kama bosi wake mzee wa viwango.

Alionyesha uwezo wa kusimama katika chombo kikubwa kama bunge.

Ni mcheshi anayeonekana kuwa mtu wa kati na kati. Msimamo wake katika BMLK uliongozwa na shinikizo

Alitambua madudu ya BML yamevuruga sana sifa yake. Akasita kuchukua fomu

Ugombea mwenza
Udhaifu wa Amina ulionekana bila kificho. Pepesa pepesa wa kutafuta kete ya jinsia kutoka Zanzibar ikamuona Samia.

Uzoefu wake katika mambo ya muungano kama waziri na ule wa BMLK ulionekana kuwa muhimu kuliko wa Amina.

Kwavile hakuingia katika kinyang'iro, ‘CV' yake ikabaki juu. Mzigo wa madudu ya BMLK akabaki nao mzee 'Sittah'

Karata ya jinsia na Uzanzibar ilimtoa kimaso maso dhidi ya dhaifu Da'Amina

Machale yake yamemsaidia kupata nafasi ya ugombea wenza. CCM ikapata si kwa ubora bali bora kiongozi

Swali la kujiuliza, hivi taifa linahitaji nini? Viongozi wenye maono, weledi na sifa au viongozi wa jinsia na maeneo wanayotoka?

Je, hilo haliwezi kuwa tatizo la kutupatia watu kwa vigezo visivyolingana na mahitaji yetu?

CCM ni dhaifu na imechoka. Viongozi wanapopatikana kwa kete za jinsia /maeneo ni dalili za kuishiwa ushawishi.

Wapinzani wakijipanga, CCM ina wakati mgumu na CCM ikeiendelea kutawala, tutashuhudia madudu yaliyopo yakitamalaki

Tusemezane
 
''WHAT GOES AROUND COMES AROUND''

UCHAGUZI NA FUNZO KWA WANASIASA

Uchaguzi wa awali wa CCM umetoa mafunzo kwa wanasiasa wanaodhani madaraka ni haki yao na kwamba wataishi katika maisha hayo kwa muda wote

Mgombea aliye engulia analalamika kuhusu utaratibu uliotumika, kukiukwa

Kwanza, CCM ilitumia kamati ya maadili, kamati ya wazee,kamati kuu, NEC na mkutano mkuu.
Hakuna anayeweza kusema utaratibu ulikikuka taratibu isipokuwa wanachama .

Inashangaza , wale waliolalamika kiongozi mmoja kutimuliwa chama cha upinzani kwa kukiukwa taratibu za vikao,wamegeuka kulalamikia taratibu zile zile walizotaka zitumike kwa upinzani. What goes around….


Pili, kwa muda, Watanzania wametaka uwepo wa mgombea binafsi.

CCM imekataa ikijua matatizo mbele ya safari. Laiti sheria ingeruhusu mgombea binafasi, EL angepata nafasi hiyo badala ya kufikiria namna ya kujijenga tena kama ipo kwa upande wake. Ingetokea, maafa yangeikumba CCM.

Kundi kubwa lingemeguka kutoka CCM nakupunguza kura.Uwezekano wao wa kushinda ungetegemea ‘goli la mkono' la kulazimisha katika 50.1% ambayo waliiona tatizo hilo mapema na kuondoa2/3. CCM wana maono


Tunaona kuwa kujipendekeza ndani ya chama ni suala la muda.Kujipendekeza katika taifa ni suala la kudumu.

Mzee wa viwango na spidi alijizolea heshima bungeni, akaamua kuivuruga katika BMLK.

Mzee wa Arusha alijizolea umaarufu serikali, akavuruga kwa kuheshimu chama.
Leo wote wawili ni waathirika wa taratibu walizozipinga huko nyuma. Huenda wangeweza kuwa pamoja kama wagombea binafsi kama wangekubali kuwa upande wawananchi.

Hawakufanya hivyo, mfumo waliosimamia umegeuza kibao, ni waathirika. What goes around…….


Ndiyo maana tunasema, watulie kama maji mtunguni,walichokisimamia ndicho kinawatafuna.

Na wala si wao, ni funzo kwa wanasiasa. Ni vema kusimama na umma kuliko kundi



Tusemezane
 
Tanzania hatuna upinzani wa kuweza kuwasaidia watanzania kuwatoa sehemu moja kwenda nyingine. Wapinzani wangekuwa na nia ya dhati wangejiunga na umoja wao kama vyama vilivyounda UKAWA na kuhakikisha wanaisimamia serikali kuandikisha watu wote wenye vigezo vya kupiga kura. Hii ingewasaidia sana kuitoa CCM madarakani. Wasimamie zoezi zima la kupiga kura, kuhesabu na kutangaza matokeo.

Nguvu ya umma.
Watanzania ni waoga na wasahaulifu sana. Ukiangalia toka JKikwete aingie madarakani hadi leo madudu mengi yamefanyika, kuna ufisadi wa wazi sana na hadi waziri mkuu kujiuzulu. Lakini sisi tumesahau kiasi kwamba huyo waziri mkuu tunamuona amegeuka lulu.

Maswala nyeti yanayohusu maslahi ya taifa tunayasahau sana. Watu wanaendelea na shughuli zao kana kwamba hayawahusu kumbe wao ndo wahanga wakuu wakubwa.

Binafsi naona dhahiri kuwa ukombozi tunaoudhania utatokea 2015 hautatokea kwasababu wananchi hatujatambua nguvu tulionayo.

Mkuu inawezekana kuwa Tanzania imefika mahali tulipokuwa tunapasubiri. Inawezekana uchaguzi wa safari hii ukaleta mabadiliko makubwa ya kuifanya Tanzania ivuke kutoka kwenye lindi za siasa za chama kimoja kivitendo na kuwa za chama zaidi ya kimoja. Tukiweza kuwa na makubndi mawili yenye nguvu ndani ya bunge, kuna uwezekano kuwa Tanzania ikawa ya maana zaidi kuliko vyama. naweza kukubaliana na wewe kuwa vyama vyetu vya kisiasa bado haviko tayari, na hata wananchi hawako tayari kuleta mabadiliko kivitendo...lakini hali ya hewa kisiasa, kiuchumi na kijamii inaweza kuwa msukomo.

By the way, tukiangalia wanasiasa wetu. Kama sijakosea nakumbuka mh Membe alisema hatagombea tena ubunge, sina uhakika sana. Ningependa kujua kama ni kweli atafanya hivyo, au alikuwa anadanganya tu, na kama kuna utaratbu wowote wa kuwachukulia hatua wanasiasa wanaodanganya.
 
Mkuu inawezekana kuwa Tanzania imefika mahali tulipokuwa tunapasubiri.

Inawezekana uchaguzi wa safari hii ukaleta mabadiliko makubwa ya kuifanya Tanzania ivuke kutoka kwenye lindi za siasa za chama kimoja kivitendo na kuwa za chama zaidi ya kimoja.

Tukiweza kuwa na makubndi mawili yenye nguvu ndani ya bunge, kuna uwezekano kuwa Tanzania ikawa ya maana zaidi kuliko vyama. naweza kukubaliana na wewe kuwa vyama vyetu vya kisiasa bado haviko tayari, na hata wananchi hawako tayari kuleta mabadiliko kivitendo...lakini hali ya hewa kisiasa, kiuchumi na kijamii inaweza kuwa msukomo.
Mkuu Msukumo wa hali ya hewa ya kisiasa, kijamii na kiuchumiupo. Kuna matatizo yanayojitokeza


1 Vyama vya siasa haziwezi kuwa tayari kama wananchi hawapotayari.
Utayari wa wananchi ni kukubali kuwa wakati umefika,mabadiliko ni lazima

Wananchi wamegawanyika katika sehemu kuu mbili

Wananchi wa vijijini ambao CCM ni mazoea na mbadiliko ni jambo la hatari kwa fikra zao.
Hutishwa kiurahisi, hudanganywakirahisi na hudanganyika kirahisi


Wananchi wa mjini: Hawa wamegwanyika katikamakundi mawili

i)Wapiganaji wanaotaka mabadiliko haswa,wengi ni vijana na wasomi

ii)Wachumia tumbo, ni wale wanaoishi kwamfumo huu wakifaidika kiaina.Wengi ni wasomi waajiriwa wanaoishi kwa madili

iii)Wakazi wa mijini wanaosombwa kwa mkumbo tu. Hawajui kwanini wanataka mabadiliko, wanachotaka ni mtu wa kuwaahidi ulaini wa shughuli zao hata kama ni kinyume cha taratibu na sharia

Tatizo si wale wa kijijini, kwani huangalia upepo wa mjinina ni rahisi kubadilika. Wakipatamsukumo kidogo tunaona ya Tarime, Karatu, Kigoma n.k.


Shida ipo hapo juu2(b)(ii)(iii)

 
By the way, tukiangalia wanasiasa wetu. Kama sijakosea nakumbuka mh Membe alisema hatagombea tena ubunge, sina uhakika sana. Ningependa kujua kama ni kweli atafanya hivyo, au alikuwa anadanganya tu, na kama kuna utaratbu wowote wa kuwachukulia hatua wanasiasa wanaodanganya.
Membe aliaga kamawengine. Hakuna utaratibu wa kuadhibu wanaoongopa. Mfumo umejengwa kuleana nakuvumiliana.
 
Mkuu Nguruvi3 uliongea ni kweli kuhusu wananchi wa vijijini kuamini kuwa bila CCM maisha yao hayaendi.. Matatizo kwao imekuwa ni sehemu ya maisha yao hivyo hawaoni kero, kwao muhimu ni mvua zinyeshe walime, wavune, washerekea mavuno basi kwao wanakuwa wameridhika.

Hawa watu hawaelewi kuwa ni haki yao kupata maji, umeme, mashule, kujenga barabara, serikali kutengeneza vyanzo vya ajira kwa ajiri ya watoto wao, ni wajibu wa serikali kuhakikisha hakuna mtu anayekosa matibabu na nk. Hawa watu wanaamini kabisa kuwa kukosa dawa hospitali ni kawaida, watoto kurundikwa madarasani ni kawaida, shule kukosa waalimu ni kosa la waalimu, kukosa maji ni adhabu kutoka kwa mwenyezi Mungu na nk.

Hawa watu wanahitaji elimu ya uraia hii elimu kwa bahati mbaya au nzuri hawezi kutolewa na serikali maana serikali kuwapa elimu ya haki zao ni kama kujichongea.. Elimu hii inabidi itolewa na vyama vya siasa, wapenda mabadiliko, wanaharakati na nk.Lakini kwa bahati mbaya kutokana na ukosefu wa pesa, vikwazo mbali mbali kutoka serikalini inakuwa ni vigumu kutoa elimu hii. Hivyo basi kujikuta watu wengi waishio vijijini kuendelea kuichagua ccm pamoja na umasikini mkubwa walionao.

Tatizo lingine linalokumba siasa yetu za Tanzania au za Afrika kwa ujumla ni ubinafsi wa viongozi, viongozi wetu wa vyama vya siasa ni wabinafsi anapokuwa kiongozi malengo yake si kukuza hicho chama bali malengo yake ni yeye kama yeye kufaidka kwa namna moja au nyingine na uongozi wa hicho chama.

Tukiangalia baadhi ya vyama vya siasa vimekuwa vikifanya vibaya mwaka hadi mwaka lakini huoni uwajibikaji wa uongozi pale wanapopoteza kura/wanapopata kura chache kulingana na chaguzi zilizopita. Utakuta kiongozi tena msomi kabisa chama chake kinadidimia kila mwaka lakini hashutuki na kuachia ngazi bali atang´angánia mpaka chama kife au kisahaulke kabisa, sasa mtu unajiuliza hivi hawa viongozi akili zao huwa ziko sawa kweli? huyu mtu anaweza ana mapenzi mema na chama chake kweli?
 
....

3. Amina Ali-akiwakilisha kundi la muungano

....…
Naufatilia kwa karibu mjadala huu, na ahsanteni nyote kwa michango yenu.

Haikuwa nia yangu kusimamisha muendelezo wa mjadala huu na kuwarudisha nyuma juu ya sifa za watia nia kugombea urais kupitia CCM ambao walifika tatu bora (nadhani twaweza kusema bora tatu). Lakini nimelazimika kuwarudisha nyuma ili niweze kupata maoni yenu juu ya jambo hili ambalo kila ninavyojaribu kulipuuzia kutolileta jamvini linazidi kunikereketa kichwani.

Jambo lenyewe ni kuhusu hotuba walizozitoa watia nia hao wa 'bora tatu' wakati wakiomba kura kwenye mkutano mkuu wa CCM. Niliwasikiliza wote watatu (John, Amina na Asha-Rose) kupitia redio. Amina na Asha-Rose inaonekana walijiandaa, kutokana na namna walivyojieleza lakini John kwa jinsi alivyoomba kura ni dhahiri shairi hakujiandaa kwa tukio lile. Alishtukizwa. Hotuba iliyonistua ni ile ya Amina Salum Ali; hasa aliposema kuwa " ...sasa Tanzania ipo kwenye uchumi wa kati na inaelekea uchumi wa kwanza/juu..." hivyo atasaidia Tanzania kuingiiza kwenye uchumi wa juu akiwa rais wa nchi hii. Nimejaribu kulifuatilia hili kuona kama mimi ndiye 'niliyepitwa na wakati' kiasi kwamba sijui hata uchumi wa nchi yangu uko kiwango gani (kwani nilikuwa najua Tanzania uchumi wetu ni wa kiwango cha chini-low income economy country).

Nilivyotembelea tovuti ya Benki ya Dunia nikakuta kumbe bado Tanzania ni nchi yenye uchumi wa chini ( Tanzania | Data ). Nilivyododosa zaidi juu ya Mama Amina S.A nikagundua alisomoea masuala hayo ya biashara, masoko na uchumi huko India na kwingineko. Na masuala hayo ya Uchumi, masoko na biashara ni masuala ambayo yanahusisha sana takwimu sahihi ili kufikia maamuzi. Pia nikagundua Mama A.S.A ni:

" Mwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Afrika (AU) Marekani (United States) akiwa kama ni Muwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika. (i) Mshauri wa Kamisheni Umoja wa Afrika kuhusiana mambo ya Afrika huko Marekani. (ii) Kufuatilia mambo ya Maendeleo ya Afrika huko Marekani kwa kuwajuilisha kuhusu sera mbali mbali za bara la Afrika zinazoendelea na mpya. (iii). Kuwashajiisha wawekezaji wa Marekani na pia Diaspora wa jamii ya Kiafrika huko Marekani kuwekeza Afrika. (iv) Kuimarisha uhusiano baina ya Marekani na vyombo vya Serikali, Mabunge na Taasisi za kijamii za Afrika . (v) Kusaidia kupatikana kwa Fedha za Maendeleo ya Afrika kwa kuzieleza Sera za Maendeleo za Afrika, na kuwashawishi waziunge mkono. (vi) Kushirikiana na vyombo vya fedha vya Bretton Woods (World Bank na IMF) kwa Maendeleo ya Afrika.
.........................
. (Rejea>>>https://www.jamiiforums.com/uchaguz...tegemewa-kuwa-makamu-wa-rais-kupitia-ccm.html)

Sasa ninajiuliza kama huyu Mwakilishi wetu wa waafrika huko US mwenye majukumu mazito namna hiyo anashindwa kujua nchi ipo kiwango gani kiuchumi (kama takwimu za world bank zitakuwa sahihi):

1. Je. Kamati ya usalama na maadili ya CCM, baraza la ushauri la Wazee wa CCM, Kamati kuu ya CCM (CC), na halmashauri kuu ya CCM (NEC) hawaoni kuwa sasa ni muda muafaka kuwaomba radhi wanachama wa CCM kwa kushindwa kutekeleza jukumu lao sawa sawa kiasi cha kumpitisha mtia nia ambaye hajui anataka kuongoza nchi ya namna ki-uchumi ?

2. Je. hivi kwa kiwango chake (hadhi na kitaaluma) huyu Mama Amina S.A tunaweza kusema 'aliteleza kutoa kauli ile' hivyo tumuache aendelee kutuwakilisha huko US bila bughudha?

Tusemezane juu ya hili kisha tuendelea na mada.
 
Mkuu Nguruvi3 uliongea ni kweli kuhusu wananchi wa vijijini kuamini kuwa bila CCM maisha yao hayaendi.. Matatizo kwao imekuwa ni sehemu ya maisha yao hivyo hawaoni kero, kwao muhimu ni mvua zinyeshe walime, wavune, washerekea mavuno basi kwao wanakuwa wameridhika.

Hawa watu hawaelewi kuwa ni haki yao kupata maji, umeme, mashule, kujenga barabara, serikali kutengeneza vyanzo vya ajira kwa ajiri ya watoto wao, ni wajibu wa serikali kuhakikisha hakuna mtu anayekosa matibabu na nk. Hawa watu wanaamini kabisa kuwa kukosa dawa hospitali ni kawaida, watoto kurundikwa madarasani ni kawaida, shule kukosa waalimu ni kosa la waalimu, kukosa maji ni adhabu kutoka kwa mwenyezi Mungu na nk.

Hawa watu wanahitaji elimu ya uraia hii elimu kwa bahati mbaya au nzuri hawezi kutolewa na serikali maana serikali kuwapa elimu ya haki zao ni kama kujichongea.. Elimu hii inabidi itolewa na vyama vya siasa, wapenda mabadiliko, wanaharakati na nk.Lakini kwa bahati mbaya kutokana na ukosefu wa pesa, vikwazo mbali mbali kutoka serikalini inakuwa ni vigumu kutoa elimu hii. Hivyo basi kujikuta watu wengi waishio vijijini kuendelea kuichagua ccm pamoja na umasikini mkubwa walionao.

Tatizo lingine linalokumba siasa yetu za Tanzania au za Afrika kwa ujumla ni ubinafsi wa viongozi, viongozi wetu wa vyama vya siasa ni wabinafsi anapokuwa kiongozi malengo yake si kukuza hicho chama bali malengo yake ni yeye kama yeye kufaidka kwa namna moja au nyingine na uongozi wa hicho chama.

Tukiangalia baadhi ya vyama vya siasa vimekuwa vikifanya vibaya mwaka hadi mwaka lakini huoni uwajibikaji wa uongozi pale wanapopoteza kura/wanapopata kura chache kulingana na chaguzi zilizopita. Utakuta kiongozi tena msomi kabisa chama chake kinadidimia kila mwaka lakini hashutuki na kuachia ngazi bali atang´angánia mpaka chama kife au kisahaulke kabisa, sasa mtu unajiuliza hivi hawa viongozi akili zao huwa ziko sawa kweli? huyu mtu anaweza ana mapenzi mema na chama chake kweli?
Alinda , CCM haiwezi kutoa elimu ya Uraia. Wanafahamu huo unaweza kuwa ndio mwisho wao. Wanachokifanya ni kwenda kula na wananchi au kubeba matofali mawili ili wananchi waone hiyo ndiyo haki zao.
Wanabeba matofali mawili kujenga zahanati, wakati gharama za matibabu kwa mmoja tu ni sawa na gharama za zahanati tatu au nne. Kuna waziri mmoja alipelekwa India na kukaa miezi 6 huko akitibiwa.
Tunamsikia akisema CCM imeleta maendeleo, wananchi hawajiulizi yapi hayo? Ya yeye kuishi hotelini India au

Tatizo la vijijini si kukosa pesa za kuwafikia wananchi tu, ni kubwa zaidi ya hapo. Kuna watu muhimu sana katika jamii wanaoishi huko( Walimu). Sasa kama wao wameridhika kupata mafao kila miaka 10 kama walivyoahidiwa Ngurufoto, tutegemee wanakijiji wachote wapi elimu?

Kundi lingine ni la vijana na hasa wasomi. Wakirudi vijijini hakuna anyewasaidia wananchi kutambua kuwa huduma ya afya, maji na elimu ni haki yake. Kazi yao ni kutafuta kazi za upambe. Mwisho wa siku kazi ya upambe inakwisha wanarudi mjini kulalamika mambo si mazuri

Nasi huku mitandaoni tuna 'share' yetu. Tunajadili mambo yasisyowagusa wananchi kabisa. Mfano, topic inayohusu gari la Obama kuwasili Nairobi. Nyuzi hiyo inachangiwa vema sana na hata kujiuliza, gari hilo ujio wake unamsaidiaje mwananchi wa kawaida wa Kenya au Tanzania?

Pengine tubadilike na kujadili matatizo yao, si wote lakini wachache wanaweza kukota kitu na muda unavyosonga mbele kasi ikashika.

Kuhusu viongozi kutowajibika, hili nalo neno. Ni tatizo linalotokana na sisi wananchi kuacha mambo yakielewa. Uchaguzi unapokwisha mwingine unaanza. Ni lazima kuwe na post mortem ya kujua kwanini imetokea hivi na si vile
Tatizo ni sisi tusio wawajibisha, si wao wanaotaka kutowajibishwa

Tatizo la watanzania ni ile hali ya ' baasi waache tu au tutafanyaje au kazi ya mungu hiyo'
Ndio maana unakutana nao wakienda muhimbili, ukiwauliza , mambo? Utasikia poa tu. Yaania anakwenda Muhimu kwenye hukumu ya maisha yake, akijua hakuna dawa, atalala chini na pengine asimuone Dr bado anasema mambo poa tu!

Akitoka muhimbili na kusawajika kwa maradhi anasima na kusema CCM itamleta nani kugombea? Tunataka mtu wa kutuletea maendeleo.

Lazima tubadilike, tuangalie taifa kwanza. Tuache mambo ya vyama, kama kiongozi kacheza fyongo anaambiwa kaa pembeni. Hatuna upungufu wa viongozi, tuna upungufu wa maadili na wingi wa ubinafsi.
Tusiwaonee haya, tuwaambie sasa inatosha
 
Mkuu Tujitegemee
Huko nyuma tumeeleza kwa uchache jinsi Da'Amina alivyopenya hadi 3 .

Hilo ni moja ya tatizo linalotukabili nchini. Hatuchagui viongozi kwa merits, bali kuongozwa na eneo au jinsia.

CCM wanaongozwa na hofu ya kukutana na KANU na UNIP kama watu wataamua kubadilika.

Karata inayochezwa ni jinsia


Mkuu, kuelimika ni zaidi ya vyeti mtu anavyopata. Hatunad hamira ya ku criticize elimu yake, tunachosema ni kuwa elimu ni pamoja naweledi na exposure

Inaonekana Da, amepata nafasi nyingi za kumwezesha kuwa na weledi na exposure.
Swali, je alitumia fursa hizo kupata maarifa zaidi?


Nafasi aliyokuwa anawania inahitaji weledi, hatudhani yeye kama yeye alikuwa tayari kwa ‘prime time'.

Kilichotokea aliandikiwa hotuba na washauri wake kwa lengo la kupata nafasi.

Ndio maana alimshirikisha Edo bila kutambua alikuwa anatia nyongo katika kitumbua.
Hakujua kuwa hadi wakati ule kambi ya Edo ilikuwa namaruwe ruwe
'Delirium'

Waliomwandikia hatujui uelewa wao katika mambo ya siasa.

Siasa za siku hizi ni za kisayansi si za kukota wapiga debe.


Nadhani washauri wake walikuwa dhaifu, ukichanganya na udhaifu wake, unaishia kupata suala la middle class kuelekea first world

Ilikuwa ni rahisi kubaini. Wiki iliyopita UN imetangaza nchi zilizoingia uchumi wa kati.

Jirani zetu kenya walikuwa kundi moja vi nchi masikini sana. Hatujui kama alioma habari hizo


Tuna tatizo, sasa huyo ndiye alikuwa awe mgombea!
 
Back
Top Bottom