2011 UDSM nilinusurika kukamatwa

Ilikua hivi, mwaka wa kwanza 2011, walipangiwa chuo wengi wao wakikosa mikopo. Kwa hiyo baada ya muda wengine wakaanza kuacha masomo kwa ugumu wa maisha na kushindwa kulipa ada.
Wakati huo wote kulikua kikundi cha watu wachache waliokua wanajiita ama kuitwa wanaharakati, muda wote walikua wakifanya jitihada na kuwasiliana na uongozi wa chuo (DARUSO) ili vijana wa mwaka wa kwanza wapewe mikopo wote.

Juhudi hizi zilipogonga mwamba sasa ndio inakuja option ya mwisho ya kuandaa mgomo ambapo vijana wanaanza kuandamana sasa.
Yeah nikweli mkuu, madogo walisuffer sana
 
Uzi tayari?
Huu mwaka sitausahau pale mlimani.

Washikaji zetu ,Christopher mbusule, Lusako ,Ndunguru na wengine wengi tu walipoteza chuo.

Mlimani city ilikuwa jumba la maficho . Tulikimbia tukajificha kwenye maduka. Wale jamaa walikuja na hasira kama za simba wakitutafuta.

Poleni sana washikaji wote mliopoteza chuo kipindi Hicho. Harakati zenu zilifanyika neema kwa wengine.

Mungu bado anatupigania . Siku zimepita na maisha yanaendelea.
 
Kipindi hicho shule nyingi zilikuwa zinakabiliwa na baa la njaa, kama kumbukumbu ziko sawa kipindi hicho wazabuni waligoma kwa sababu serikali ilikuwa haijawalipa kwa muda mrefu, baadhi ya shule zilifikia hatua ya kufungwa kwa ukosefu wa chakula
Kweli kabisa.. nakumbuka mwaka 2008 njaa ilisababisha tukagawiwa chai na maharage Kama dinner kisa shule haikuwa na unga wa kupika ugali...
Ilikuwa shida sana..
 
Kweli kabisa.. nakumbuka mwaka 2008 njaa ilisababisha tukagawiwa chai na maharage Kama dinner kisa shule haikuwa na unga wa kupika ugali...
Ilikuwa shida sana..
Chai na maharage kama dinner bado unasema ilikuwa shida sana?
 
Ndiyo yule pia alimzingua Dr Kawambwa alipokuja pale chini ya shuttle point kusikiliza hoja za wanafunzi,tukaishiwa kupigwa mabomu.......Kumbukumbu kama zipo sawa ni Mwita
Nilichojifunza kwenye wengi poana mengi. Wewe unaweza ukawa unafikiri kua lengo lenu ni moja ila kumbe miongoni mwenu kuna watu wana maelngo tofauti kabisa na maovu. Kusema kweli mgomo wa 2011 ulikua wa mwisho na sidhani kama itakaa kutokea mgomo mwingine tena kwenye vyuo vikuu.
Vijana walifanikiwa kwa asilimia mia moja kwenye mgomo ule japo furaha iligeuka msiba baada ya kusherehekea ushindi kwa kutaka kwenda kutoa kipigo kwa viongozi wa serikali ya wanafunzi (DARUSO) ambapo ilikuja kutafsiriwa kama jaribio la kutaka kupindua serikali ya wanafunzi.

Wakati mwingine najiuliza kama wale wanaosomea uandishi wa habari (Mass communication) matukio kama yale hawawezi hata kuyaandalia habari kwa kina na kuja na kitabu au makala zinazoelezea kwa kina kiini cha tatizo na masimulizi mpaka ilivyoisha na hasara au faida zilizopatikana.

Ila yote kumi tisa yule jamaa aliyejiita alshabab alikua mtu wa tofauti sana (Charismatic leader) kwa waliokuwepo mitaa ya chuo na kufatilia kiundani jamaa alijaliwa uwezo wa kushawishi watu.

jina lake lilikua halifahamiki kwa hiyo hata utawala walipata shida sana kumdhibiti mana hawajui ni nani wala anasoma kozi gani, alisumbua sana.
 
Nilichojifunza kwenye wengi poana mengi. Wewe unaweza ukawa unafikiri kua lengo lenu ni moja ila kumbe miongoni mwenu kuna watu wana maelngo tofauti kabisa na maovu. Kusema kweli mgomo wa 2011 ulikua wa mwisho na sidhani kama itakaa kutokea mgomo mwingine tena kwenye vyuo vikuu.
Vijana walifanikiwa kwa asilimia mia moja kwenye mgomo ule japo furaha iligeuka msiba baada ya kusherehekea ushindi kwa kutaka kwenda kutoa kipigo kwa viongozi wa serikali ya wanafunzi (DARUSO) ambapo ilikuja kutafsiriwa kama jaribio la kutaka kupindua serikali ya wanafunzi.

Wakati mwingine najiuliza kama wale wanaosomea uandishi wa habari (Mass communication) matukio kama yale hawawezi hata kuyaandalia habari kwa kina na kuja na kitabu au makala zinazoelezea kwa kina kiini cha tatizo na masimulizi mpaka ilivyoisha na hasara au faida zilizopatikana.

Ila yote kumi tisa yule jamaa aliyejiita alshabab alikua mtu wa tofauti sana (Charismatic leader) kwa waliokuwepo mitaa ya chuo na kufatilia kiundani jamaa alijaliwa uwezo wa kushawishi watu.

jina lake lilikua halifahamiki kwa hiyo hata utawala walipata shida sana kumdhibiti mana hawajui ni nani wala anasoma kozi gani, alisumbua sana.
Kweli kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom