13 wahofiwa kupoteza maisha mitumbwi miwili ikizama Ziwa Victoria

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,555
Watu 13 wanahofiwa kufariki dunia huku wengine 14 wakiokolewa baada ya mitumbwi miwili kuzama ndani ya Ziwa Victoria wakati wakitoka kusali ibada ya Jumapili Kijiji cha Ichigondo Wilaya ya Bunda mkoani Mara.

Akizungumza kwa simu na Mwananchi leo Jumatatu Julai 31, 2023, Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dk Vicent Naano amesema tukio hilo lilitokea jana saa 12:30 jioni na tayari mwili wa mtoto anayekadiriwa kuwa na mwaka mmoja umeopolewa.

“Hapa Kijiji cha Igundu kuna kama ras sasa watu walikuwa wakitoka kusali katika kanisa la KTMK ndipo mtumbwi mmoja ukapigwa na dhoruba na kuanza kuzama, ukaja mtumbwi wa pili kwaajili ya kuokoa nao ukapigwa na dhoruba mitumbwi yote miwili ikazama,"amesema Dk Naano

Dk Naano amesema jitihada za kuwatafuta watu hao 13 zinaendelea akidai jana baada ya giza kuingia zoezi la kuwatafuta lilisitishwa.

"Tupo hapa na timu ya usalama ya wilaya tunaendelea kuwatafuta maana jana baada ya giza kuingia hakuna ambacho kingeweza kufanyika ila tu hadi sasa ni mwili mmoja ndio umeopolewa,” amesema.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara, Agostino Magere amekiri kutokea kwa tukio hilo na kuahidi kutoa taarifa zaidi baadaye.

“Ndio nimepokea hizo taarifa na hapa ninajiandaa nielekee huko nadhani nitakuwa kwenye nafasi nzuri kulizungmzia nikishafika eneo la tukio,”amesema Magere

Chanzo: Mwananchi

===

UPDATE
AGOSTI 2, 2023

Mili 12 kati ya 13 iliyokuwa majini, baada ya mitumbwi miwili kuzama, katika Ziwa Victoria, katika Kijiji cha Mchigondo kilichopo wilayani Bunda, mkoani Mara, siku ya Jumapili ya Juni 30, 2023, ikiwa na watu 28, imeopolewa majira ya Saa 3 hadi saa 6 usiku na alfairi va leo, Agosti 02, 2023.

Akizungumza na ITV, Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Vokoaji, Mkoa wa Mara, Augustine Magere amesema wanaendelea na juhudi za kutafuta mwili mmoja ambao bado haujapatikana.
 
Mkuu wa wilya ni muongo muongo sanaaa huyo sasa mara yupo na kamati ya ulinzi na Usalama, alafu kamanda wa uokoaji aasema ndo anaenda eneo la tukio
 
Kwa kawaida binadamu akizama na kufa maji Ziwa (sina hakika na maji ya bahari) hubaki ndani ya maji kwa walau saa 72 ndipo anaibuka. Wazee wote wa kando kando mwa ziwa wanajua hili, ni common knowledge.

Ninashauri waokoji wetu wasione aibu kujifunza kwa wenyeji wenye maarifa haya.

====

Miili ya watu 12 ya watu waliozama ndani ya ziwa Victoria baada ya mitumbwi miwili kupigwa na dhoruba kisha kuzama imepatikana kati ya watu 13 waliokuwa wakitafutwa.

Idadi hiyo inafikisha jumla miili 13 kuopolewa kutokana na tukio hilo lililotokea wakati watu hao wakitoka katika kijiji cha Mchigondo kwenda Kitongoji cha Bulomba katika Kijiji cha Igundu baada ya mwili wa mtoto wa mwaka mmoja kuopolewa siku ya tukio.

Jana Agosti Mosi 2023 miili miwili ilikuwa imeopolewa ziwani ambapo wote walikuwa ni watoto wa kike.

Miili mingine imeopolewa kati ya usiku hadi leo Agosti Mbili saa moja asubuhi.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara, Agostino Magere amesema vikosi vya uokoaji kwa kushirikiana na wavuvi na wenyeji eneo hilo wanaendelea kuutafuta mwili mmoja ambao umesalia.

Julai 30, 2023 mitumbwi miwili iliyokuwa imebeba waumini 28 wa Kanisa Takatifu la Mungu wa Kiroho (KTMK) ilizama ziwani ambapo watu 14 waliokolewa na kukimbizwa hospitalini.

Katika tukio hilo ambapo wengi walikuwa ni watoto na wanafunzi wa Shule ya Msingi Bulomba wilayani Bunda, watu 13 walizama ambapo shughuli ya kuwatafuta ilianza hadi sasa ambapo bado mwili mmoja.

Mwananchi
 
Kwa kawaida binadamu akizama na kufa maji Ziwa (sina hakika na maji ya bahari) hubaki ndani ya maji kwa walau saa 72 ndipo anaibuka. Wazee wote wa kando kando mwa ziwa wanajua hili, ni common knowledge.

Ninashauri waokoji wetu wasione aibu kujifunza kwa wenyeji wenye maarifa haya.

====

Miili ya watu 12 ya watu waliozama ndani ya ziwa Victoria baada ya mitumbwi miwili kupigwa na dhoruba kisha kuzama imepatikana kati ya watu 13 waliokuwa wakitafutwa.

Idadi hiyo inafikisha jumla miili 13 kuopolewa kutokana na tukio hilo lililotokea wakati watu hao wakitoka katika kijiji cha Mchigondo kwenda Kitongoji cha Bulomba katika Kijiji cha Igundu baada ya mwili wa mtoto wa mwaka mmoja kuopolewa siku ya tukio.

Jana Agosti Mosi 2023 miili miwili ilikuwa imeopolewa ziwani ambapo wote walikuwa ni watoto wa kike.

Miili mingine imeopolewa kati ya usiku hadi leo Agosti Mbili saa moja asubuhi.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara, Agostino Magere amesema vikosi vya uokoaji kwa kushirikiana na wavuvi na wenyeji eneo hilo wanaendelea kuutafuta mwili mmoja ambao umesalia.

Julai 30, 2023 mitumbwi miwili iliyokuwa imebeba waumini 28 wa Kanisa Takatifu la Mungu wa Kiroho (KTMK) ilizama ziwani ambapo watu 14 waliokolewa na kukimbizwa hospitalini.

Katika tukio hilo ambapo wengi walikuwa ni watoto na wanafunzi wa Shule ya Msingi Bulomba wilayani Bunda, watu 13 walizama ambapo shughuli ya kuwatafuta ilianza hadi sasa ambapo bado mwili mmoja.

Mwananchi
Mkuu inafatana kina cha maji walichozamia!!

Kama ni kina kifupi ni kuanzia masaa 24 mpaka 48!

Na kama ni karibu na mwaro harafu kuna wimbi ni masaa 24 tu mnakuta amegoa!!

Na hao wanaosema giza lilipoingia walisitisha zoezi la uokozi wanadanganya!

Kwani mtu akishazama ndani ya dakika tano tu anakuwa ameshakufa!

Kinachofuata baada ya hapo ni kusubiri aibuke mwenyewe!!
 
"Tupo hapa na timu ya usalama ya wilaya tunaendelea kuwatafuta maana jana baada ya giza kuingia hakuna ambacho kingeweza kufanyika ila tu hadi sasa ni mwili mmoja ndio umeopolewa,” amesema.

Mili 12 kati ya 13 iliyokuwa majini, baada ya mitumbwi miwili kuzama, katika Ziwa Victoria, katika Kijiji cha Mchigondo kilichopo wilayani Bunda, mkoani Mara, siku ya Jumapili ya Juni 30, 2023, ikiwa na watu 28, imeopolewa majira ya Saa 3 hadi saa 6 usiku na alfairi va leo, Agosti 02, 2023.

Anayeweza kutufafanulia hiyo mistari myekundu atusaidie kama je ni kazi ilikuwa inafanywa na vikosi viwili tofauti?
 
Anayeweza kutufafanulia hiyo mistari myekundu atusaidie kama je ni kazi ilikuwa inafanywa na vikosi viwili tofauti?
Mkuu nilichoelewa ni kuwa miili ilianza kuibuka kuanzia saa9 usiku mpaka saa12 asubuhi!!
 
Mkuu nilichoelewa ni kuwa miili ilianza kuibuka kuanzia saa9 usiku mpaka saa12 asubuhi!!
Statement ya kwanza inasema hawafanyi kazi giza likiingia, statement ya pili inasema wamepata miili usiku
 
Back
Top Bottom