Kimbunga kutoka ziwa Victoria chaleta madhara Geita

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,323
24,230
10 September 2023
Geita, Tanzania

Wakaazi hao wa mwambao katika kijiji pwani ya ziwa Victoria wilayani Geita wanasema waliamshwa asubuhi mapema sana na watoto walioamka asubuhi na kukutana na kitu cha kutisha mithili ya ruhani kikionekana kuja taratibu kijijini kwao kutoka ziwa Victoria
1694477419604.png

Baada ya muda kitu hicho kikafikia kijiji na Nyumba kadhaa mapaa yake yachukuliwa na kimbunga cha chamchele kutoka ziwa Victoria wakaazi wasimulia katika video hii hapa chini kitu cha kuogofya kilivyomelea kijiji chao huku mbingu ikigeuka kuwa giza na kusababisha maafa


View: https://m.youtube.com/watch?v=CW3l1VsJ4HE


Watoto wanakijiji wakapiga kelele wazee wakatoka nje na kuona wingu zito likijifungafunga / kujinyonga nyonga mithili ya joka kubwa lililoamka toka ziwani kisha kuanza kusimama kama joka la cobra lililiweza kufika hadi mawinguni kutoka majini na kuanza kuja taratibu kuelekea pwani ya ziwa Victoria ktk kijijini kimoja cha Geita.

Wenyeji wa kandokando ya ziwa Victoria huamini kuwa wakijitokeza watu wengi na kupiga mayowe pamoja na kugonga chochote iwe ngoma mabati kwa wingi wa umoja wao kimbunga kama hicho hakitafika katika makaazi yao, wazee wa maeneo hayo wanasimulizi hizo.

Katika video hii hapa chini Hali kama hiyo ya kimbunga cha chamchele cha maji ziwani imewahi kutokea nchini Kenya tarehe 20 July 2023 na bahati wenyeji walibahatika kuweza kupiga picha za video na kupata uhalisia kinachosimuliwa na kutokea wilaya ya Geita Tanzania na kuchukua hatua za 'kimila' kuepusha madhara.


View: https://m.youtube.com/watch?v=7AfWdI1KGT4


Kimbunga cha Chamchele cha ziwani kitaalamu ni safu ya Maji inayonyonywa na anga inayofanana na kimbunga ya hewa inayozunguka na ukungu unaotokea juu ya maji.

Kinyume na imani maarufu ya wenyeji, mizuka au maruhani ya mababu wa kale huzuka kuwatembelea au kuja kwa kunyanyuka kama joka kuu kudai kafara . Hiki ni kimbunga halisi kisayansi cha chamchele dhaifu (waterspouts) kuliko vimbunga vingine lakini mwingine kinaweza kusababisha vimbunga na dhoruba kali ziwani hadi nchi kavu. Source:30a.com
 
Uliona wapi hayo maono chief?
Nilikuwa nikisikiza u tube channel kuhusu ujumbe wa nabii Boniface victor U-Tube, kuhusu Mafuriko DSM.

Nilipitiwa na USINGIZI wa ghafula,

Ghafula niliona nipo kwetu, ndani ya nyumba, lakini nikiwa ndani ya nyumba, niliweza kuona yaliyokuwa yakiendelea nje,

Niliona Mbinguni juu kitu kikizunguka mithili ya sahani, kitu hicho kulikuwa na RANGI ya birauli,

Ghafula kitu hicho kilifunguka na kumimina maji na kujifunga tena.

Nilipohisi hatari inakuja, nikataka kugeuka Ili niwambie niliokuwanao ndani juu ya yanayoenda Kutokea,

Ghafula, kufumba na kufumbua, nilijikuta naelea juu ya maji na hakikuonekana chochote zaidi ya anga, vyote vilifuniikwa ndani ya maji.

Ndipo nikarudia Hali ya kawaida.

Yajayo mbeleni Si mazuri, tumrudie Muumba na tuache UOVU.
 
Nilikuwa nikisikiza u tube channel kuhusu ujumbe wa nabii Boniface victor U-Tube, kuhusu Mafuriko DSM.

Nilipitiwa na USINGIZI wa ghafula,

Ghafula niliona nipo kwetu, ndani ya nyumba, lakini nikiwa ndani ya nyumba, niliweza kuona yaliyokuwa yakiendelea nje,

Niliona Mbinguni juu kitu kikizunguka mithili ya sahani, kitu hicho kulikuwa na RANGI ya birauli,

Ghafula kitu hicho kilifunguka na kumimina maji na kujifunga tena.

Nilipohisi hatari inakuja, nikataka kugeuka Ili niwambie niliokuwanao ndani juu ya yanayoenda Kutokea,

Ghafula, kufumba na kufumbua, nilijikuta naelea juu ya maji na hakikuonekana chochote zaidi ya anga, vyote vilifuniikwa ndani ya maji.

Ndipo nikarudia Hali ya kawaida.

Yajayo mbeleni Si mazuri, tumrudie Muumba na tuache UOVU.
Kapime Malaria. Sitanii. Kuona maruweruwe ni dalili ya malaria kali kupanda kichwani.
 
10 September 2023
Geita, Tanzania

Wakaazi hao wa mwambao katika kijiji pwani ya ziwa Victoria wilayani Geita wanasema waliamshwa asubuhi mapema sana na watoto walioamka asubuhi na kukutana na kitu cha kutisha mithili ya ruhani kikionekana kuja taratibu kijijini kwao kutoka ziwa Victoria
View attachment 2746420
Baada ya muda kitu hicho kikafikia kijiji na Nyumba kadhaa mapaa yake yachukuliwa na kimbunga cha chamchele kutoka ziwa Victoria wakaazi wasimulia katika video hii hapa chini kitu cha kuogofya kilivyomelea kijiji chao huku mbingu ikigeuka kuwa giza na kusababisha maafa


View: https://m.youtube.com/watch?v=CW3l1VsJ4HE


Watoto wanakijiji wakapiga kelele wazee wakatoka nje na kuona wingu zito likijifungafunga / kujinyonga nyonga mithili ya joka kubwa lililoamka toka ziwani kisha kuanza kusimama kama joka la cobra lililiweza kufika hadi mawinguni kutoka majini na kuanza kuja taratibu kuelekea pwani ya ziwa Victoria ktk kijijini kimoja cha Geita.

Wenyeji wa kandokando ya ziwa Victoria huamini kuwa wakijitokeza watu wengi na kupiga mayowe pamoja na kugonga chochote iwe ngoma mabati kwa wingi wa umoja wao kimbunga kama hicho hakitafika katika makaazi yao, wazee wa maeneo hayo wanasimulizi hizo.

Katika video hii hapa chini Hali kama hiyo ya kimbunga cha chamchele cha maji ziwani imewahi kutokea nchini Kenya tarehe 20 July 2023 na bahati wenyeji walibahatika kuweza kupiga picha za video na kupata uhalisia kinachosimuliwa na kutokea wilaya ya Geita Tanzania na kuchukua hatua za 'kimila' kuepusha madhara.


View: https://m.youtube.com/watch?v=7AfWdI1KGT4


Kimbunga cha Chamchele cha ziwani kitaalamu ni safu ya Maji inayonyonywa na anga inayofanana na kimbunga ya hewa inayozunguka na ukungu unaotokea juu ya maji.

Kinyume na imani maarufu ya wenyeji, mizuka au maruhani ya mababu wa kale huzuka kuwatembelea au kuja kwa kunyanyuka kama joka kuu kudai kafara . Hiki ni kimbunga halisi kisayansi cha chamchele dhaifu (waterspouts) kuliko vimbunga vingine lakini mwingine kinaweza kusababisha vimbunga na dhoruba kali ziwani hadi nchi kavu. Source:30a.com

Yule mtabiri wa Dar kuhusu April na May 2024 anaweza kuanza kuvuna waumini
 
Nilikuwa nikisikiza u tube channel kuhusu ujumbe wa nabii Boniface victor U-Tube, kuhusu Mafuriko DSM.

Nilipitiwa na USINGIZI wa ghafula,

Ghafula niliona nipo kwetu, ndani ya nyumba, lakini nikiwa ndani ya nyumba, niliweza kuona yaliyokuwa yakiendelea nje,

Niliona Mbinguni juu kitu kikizunguka mithili ya sahani, kitu hicho kulikuwa na RANGI ya birauli,

Ghafula kitu hicho kilifunguka na kumimina maji na kujifunga tena.

Nilipohisi hatari inakuja, nikataka kugeuka Ili niwambie niliokuwanao ndani juu ya yanayoenda Kutokea,

Ghafula, kufumba na kufumbua, nilijikuta naelea juu ya maji na hakikuonekana chochote zaidi ya anga, vyote vilifuniikwa ndani ya maji.

Ndipo nikarudia Hali ya kawaida.

Yajayo mbeleni Si mazuri, tumrudie Muumba na tuache UOVU.
Tumrudie kivp bruh
Ww kama ulimuacha shaur lako sisi bado tuko naee
 
Hii kisayansi inaitwaje na kwanini inakuwa hivyo au malaika wa mbingun alikua anakunywa majii? em wajuvi mje mseme
 
Kwa majibu mepesi hicho ni kimbunga na kinatokea ziwani au baharini.
Kiingereza wanaita cyclone

Upepo mkali unaojongea kutokana na mgandamizo wa hewa na joto. Na matokea yake ni mvua kunyesha.

Pepo mbili zinapo kutana ziwani hutengeneza mzunguko ( mduara). Kasi yake itasababisha maji kuvutwa kwenda juu yakiwa yanazungushwa na upepo.

Matokeo yake.
Ni upepo hatari kwenye vyombo vya usafri wa majini. Huwezi kupona ukikutana na huo msoke( kimbuga)

Ni hatari kwa viumbe wa majini kama samaki n.k nao wanapoteza maisha.

Mvua yake ni kubwa inayoweza kusababisha mafuriko na uharibifu wa makazi na miundombinu. Mvua yake sio ya kitoto kutokana na kuwa kiwango kikubwa cha maji kimechukuliwa ziwani.

kimbuga( msoke) kinaweza kuleta upepo mkali sana.

Lakini kuna nadharia ya kiimani.
Upepo wa kimbunga( Msoke) unaweza kuzuiliwa na mtoto wa Mwisho kwenye familia kwa
A. Kujikata sehemu ya kidole na matokeo ta damu yake kudondokea ziwani.

B. Kuchukua panga na kukata hewani. Yakifuatia na manuizo.hii kama upo pembezoni mwa ziwa.

C. Kukata hewani kwa kutumia kasia( kifaa cha wavuvi kusogezea mtumbwi)

D. SALA NA TOBA KWA Mungu Mwenyezi.


Nimeandika haya kutokana na utafiti wangu nilioufanya.

mara yakwanza nilikiona kimbuga kama hicho kakukuru-ukerewe mwaka 2000.

mara ya pili 2005 kahunda- Buchosa.
Mara ya tatu 2008 kasenda- Muganza-chato
 
Kimbunga cha Mbeya unaona mabati hayo hewani yanazunguruka.
Sasa we shangaa tu km hayajapita na shingo yako.
 
Back
Top Bottom