tcra

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (pia huitwa kwa Kiingereza: Tanzania Communications Regulatory Authority ambapo mara nyingi huitwa kwa kifupi: TCRA) ni taasisi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye majukumu ya kusimamia sekta za mawasiliano na utangazaji.

TCRA Ilianzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya mwaka 2003 kusimamia huduma za kielektroniki na posta na masafa ya mawasiliano nchini Tanzania. Mamlaka ilianza kazi tarehe 1 Novemba 2003 na inafanya shughuli za zilizokuwa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).

Mamlaka ya TCRA ni kusimamia sekta ya posta, mawasiliano ya kielektroniki na utangazaji katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na:
  • Kuzifanya shughuli za TCRA kuwa za kisasa kwa kutumia teknolojia sahihi;kuimarisha tafiti zenye ubora katika huduma zinazodhibitiwa, uwezo na umahiri wa watumishi.
  • Kukuza ufanisi; kuaminika na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya mawasiliano na matumizi yake.
  • Kukuza ufanisi na unafuu wa huduma za Mawasiliano na kuongeza upatikanaji wa huduma za Posta na TEHAMA katika maeneo yasiyohudumiwa ipasavyo na yale yasiyo na huduma kabisa.
  • Kulinda maslahi ya wadau na kukuza uelewa wa haki na wajibu wao.
  • Kufuatilia utendaji wa huduma zinazosimamiwa na kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na Kanuni kwa viwango vinavyostahili.
  • Kuratibu utekelezaji wa ahadi za kisekta kitaifa, kikanda na kimataifa.
  • Kufikia kiwango cha juu ya kuridhisha wateja kama ilivyoainishwa kwenye Mkataba wa Huduma kwa Mteja wa TCRA.
  • Kuendelea kuzingatia matakwa ya kisheria na kiusimamizi.

Sera zinazoathiri utendaji kazi wa TCRA ni pamoja na:
  • Sera ya Taifa ya Mawasiliano ya mwaka 1997
  • Sera ya TEHAMA ya mwaka 2003
  • Sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003
  1. Ponjoro wa Kinondoni

    Lazima Kutakuwa na Wafanyakazi wa TCRA Wanaoendelea Kutumia JamiiForums kwa VPN

    Watu wa namna hiyo wanaitwa WANAFIKI, ni watu wabaya sana. Wewe si umezima, sasa unafuata nini huku? Si uende huko FB?
  2. Isaka James

    JamiiForums Imezuiwa Siku 90? TOR Ndiyo Suluhisho Bila Form ya TCRA!

    Habari za Jumapili wadau wa JamiiForums! Leo nimekujieni na hii thread, haswa baada ya jana kusikia kuwa JamiiForums imepigwa ban ya siku 90 na TCRA kwa kile wanachodai ni maudhui yanayopotosha! (Kulingana na taarifa rasmi za TCRA Septemba 6, 2025, hii suspension inaanza mara moja na...
  3. Common Folk

    Kimahesabu, hakuna tofauti ya kutumia VPN iliyosajiliwa TCRA na kutotumia VPN

    Ikiwa nisipotumia VPN, digital address yangu inakuwa uchi uchi TCRA wananiona eneo niliko na nafanya nini mtandaoni, then TCRA hao hao wakanilazimisha nitumie VPN ili kuzifikia baadhi ya huduma mtandaoni walizozifungia, utaniambiaje tena nijisajili kutumia VPN ili unione nafanya nini mtandaoni...
  4. R

    Coalition on Right to Information (CoRI) yaitaka TCRA kuondoa adhabu dhidi ya JamiiForums

    Muungano wa Asasi Za Kiraia unaotetea Haki ya Upatikanaji wa Taarifa (Coalition on Right to Information - CoRI) umelaani vikali uamuzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuisimamisha kwa siku 90 JamiiForums, jukwaa maarufu la majadiliano na uwazi nchini Tanzania. Uamuzi huo umetangazwa...
  5. Fbn

    JamiiForums, kama TCRA imefungia siku 90 basi habari zinazohusu CCM hapa uchaguzi hatutaki maana serikali ni CCM

    Adui siku zote anajibiwa kwa mambo yake.Hapa wamekufungia forum ila unachotakiwa ndani ya siku 90 hakuna habari yoyote ya CCm inayotakiwa kuwa kwenye uzi kuanzia sasa. JamiiForums hawa watu funga ID zao kwa siku 90 kwanza. Walichofanya mtandao X ambao twitter wanataka kuleta kwenu na hapo...
  6. JamiiForums

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) yatangaza kuifungia JamiiForums

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesitisha Leseni ya Maudhui Mtandaoni ya JamiiForums kwa muda wa siku 90 na kuzuia upatikanaji wa jukwaa hilo, kwa maelezo ya kukiuka Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kuhusu maudhui mtandaoni TCRA imesema uamuzi huu umetokana na JamiiForums...
  7. Ponjoro wa Kinondoni

    TCRA na Jeshi la Polisi Waogopa Kumchukulia Hatua Diamond Platnumz kwa Kutukana Hadharani

    Mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA na Jeshi la Polisi kwapamoja wameogopa kabisa kumchukulia hatua ndugu Naseeb Abdul aka Diamond Platnumz baada ya video yake ya matusi ya nguoni kusambaa. Katika video hiyo, Staa huyo wa muziki amewatukana akina mama wote wa Tanzania ambao vijana wao...
  8. Isaka James

    Jaza Form ya TCRA Usijepatwa na Shida, Serikali Inakufuatilia Vipi? (Watumiaji wa VPN Special Thread)

    Habari wadau wa JamiiForums, Leo nimekuja na kichwa moto kuhusu hili swala la VPN ambalo limekuwa likiwaka kama moto wa gari la maji mitandaoni! Tangu 2023, serikali kupitia TCRA ikawavunja moyo wengi kwa kusema kila mtu anayetumia VPN, iwe mtu binafsi au kampuni, lazima ajaze form rasmi ya...
  9. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 TCRA yawataka Waandishi wa Habari kukemea vurugu Uchaguzi Mkuu 2025

    Meneja wa Huduma za Utangazaji kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mhandisi Andrew Kisaka, amewataka waandishi wa habari kuwa mstari wa mbele kukemea vurugu na migogoro yoyote itakayojitokeza wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2025 badala ya kushiriki kwa njia ya kuripoti au kuchochea...
  10. McLaren

    Andrew Kisaka wa TCRA: Wiki 2 zilizopita tulikaa na Tiktok kujadili kuhusu maudhui yasiyofaa

    Wakuu, Akiwa anazungumza leo kwenye Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Habari Kanda ya Mashariki Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, Meneja wa Kitengo cha Huduma za Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka amesema kwamba mara kwa mara wamejaribu ku-engage na baadhi ya mitandao ya kijamii ili kujadili...
  11. Ponjoro wa Kinondoni

    Anayekata internet anatumia akili gani?

    Anakata internet Polepole akiwa live, live ikiisha anarudisha internet na kutupa fursa ya kuangalia alichokisema polepole, yani hata kama ulikuwa umesahau basi ni lazima utakumbuka maana ukiona tu internet inasumbua, unajua kuna jambo, ikirudi tu unasearch. Huyu anamhujumu mama yetu kipenzi wa...
  12. Teknolojia ni Yetu sote

    Tanzania kutumia satellite badala ya minara ya simu kufanya mawasiliano

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (Tcra) imetoa mwongozo mpya itakayoweza kubadilisha namna ambavyo Watanzania wanavyopata huduma za simu. 🗯️ Mwongozo mpya utoaji wa mawasiliano ya moja kwa moja toka kwenye simu kwenda kwenye satellite, iliyotolewa julai 2025, huruhusu simu za mkononi...
  13. W

    TCRA yatoa onyo kali kwa wanaokiuka sheria na kanuni za huduma za utangazaji

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), chini ya mamlaka iliyopewa kwa mujibu wa Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, Sura ya 306, na Kanuni zake ina wajibu wa kusimamia huduma za mawasiliano ya Simu na Intaneti, Posta, na Utangazaji wa Redio, Televisheni na Maudhui Mtandaoni. Hivi...
  14. R

    GE2025 TCRA:Wanahabari msibebe umbea, hojini sera za vyama

    Meneja wa Huduma za Utangazaji katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mhandisi Andrew Kisaka, amewataka waandishi wa habari na watangazaji nchini kuzingatia sera za vyama vya siasa katika uripoti na mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa 2025, badala ya kuendesha mahojiano kwa misingi ya mambo...
  15. M

    GE2025 TCRA: Masuala ya uchaguzi siyo kama kutangaza mpira, waandishi hakikisha hujatia chumvi au kusisitiza vitu ambavyo havipo

    Meneja wa Huduma za Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mhandisi Andrew Kisaka, amewataka watangazaji na waandishi wa habari nchini kuepuka kuonesha mitazamo yao binafsi au kuongeza “chumvi” wakati wa kuripoti Uchaguzi Mkuu wa 2025. Akizungumza tarehe 16 Agosti 2025 katika...
  16. W

    TCRA: Ukipokea Ujumbe wenye Chuki "Futa Delete Kabisa"

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kupitia kampeni ya kitaifa ya Futa Delete Kabisa inaendelea kusisitiza endapo utapokea ujumbe wenye matusi, uongo au unaoeneza chuki na kuvunja amani katika jamii basi futa na delete kabisa ujumbe huo. Aidha, inasisitiza kujenga tabia ya kuhakiki taarifa...
  17. Mkalukungone Mwamba

    TCRA imezindua tena kampeni ya elimu kwa umma iitwayo "Futa delete kabisa"

    Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Rolf Kibaja, ametoa wito kwa umma kutumia huduma za mawasiliano kwa njia sahihi na salama. TCRA imezindua tena kampeni ya elimu kwa umma iitwayo “FUTA DELETE KABISA”, ikilenga kuendelea...
  18. Youbettersleep

    Mitandao wa FACEBOOK na YOUTUBE ina shida muda huu. Hii ni sababu ya SIASA au ni nini?

    Kama ni SIASA basi nchi yetu inaongozwa kwa mihemko sana au tuliowapa uongozi hawafikirii vyema kuhusu wananchi. Kama ni Inshu critical kumtandao au shida basi wanapaswa kuitatua haraka sana kwani wengi ndio huingiza pesa kupitia platforms hizi. Mtandao wa FACEBOOK na YOUTUBE hazifanyi kazi...
  19. P

    Ifike mahali serikali ya Tanzania na hasa TCRA iwaheshimu watanzania

    Wakuu habari za muda huu? Naandika hapa nikiwa nimefura kupitiliza. Imetosha sasa, hii serikali inabidi ifike mahali iheshimu raia. Haiwezekani watu wawe wanajizimia zimia tu mitandao wanapojisikia. Watu tumejiajiri huko YouTube, na leo jioni hii nilikuwa na darasa (huwa natrain watu mbali...
  20. tonicimmobility

    GE2025 TCRA: Vyombo vya Habari vizingatie Miongozo na Kanuni za Uandishi wa Habari kuelekea Uchaguzi Mkuu

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesisitiza umuhimu wa vyombo vya habari, hususan vya mtandaoni, kuzingatia miongozo na kanuni za uandishi wa habari kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Soma pia: Hali ya Vyombo vya Habari kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025: Kuna...
Back
Top Bottom