tcra

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (pia huitwa kwa Kiingereza: Tanzania Communications Regulatory Authority ambapo mara nyingi huitwa kwa kifupi: TCRA) ni taasisi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye majukumu ya kusimamia sekta za mawasiliano na utangazaji.

TCRA Ilianzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya mwaka 2003 kusimamia huduma za kielektroniki na posta na masafa ya mawasiliano nchini Tanzania. Mamlaka ilianza kazi tarehe 1 Novemba 2003 na inafanya shughuli za zilizokuwa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).

Mamlaka ya TCRA ni kusimamia sekta ya posta, mawasiliano ya kielektroniki na utangazaji katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na:
  • Kuzifanya shughuli za TCRA kuwa za kisasa kwa kutumia teknolojia sahihi;kuimarisha tafiti zenye ubora katika huduma zinazodhibitiwa, uwezo na umahiri wa watumishi.
  • Kukuza ufanisi; kuaminika na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya mawasiliano na matumizi yake.
  • Kukuza ufanisi na unafuu wa huduma za Mawasiliano na kuongeza upatikanaji wa huduma za Posta na TEHAMA katika maeneo yasiyohudumiwa ipasavyo na yale yasiyo na huduma kabisa.
  • Kulinda maslahi ya wadau na kukuza uelewa wa haki na wajibu wao.
  • Kufuatilia utendaji wa huduma zinazosimamiwa na kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na Kanuni kwa viwango vinavyostahili.
  • Kuratibu utekelezaji wa ahadi za kisekta kitaifa, kikanda na kimataifa.
  • Kufikia kiwango cha juu ya kuridhisha wateja kama ilivyoainishwa kwenye Mkataba wa Huduma kwa Mteja wa TCRA.
  • Kuendelea kuzingatia matakwa ya kisheria na kiusimamizi.

Sera zinazoathiri utendaji kazi wa TCRA ni pamoja na:
  • Sera ya Taifa ya Mawasiliano ya mwaka 1997
  • Sera ya TEHAMA ya mwaka 2003
  • Sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003
  1. Genius Man

    JamiiForums Tanzania TCRA imeitaka media ya chanzo kushusha video za gwajima kwamba bado hawajatoa ufafanuzi mbona jamiiforums na BBC hawajaambiwa washushe na ufafanuzi ba

    TCRA imeitaka media ya chanzo kushusha video za gwajima kwamba bado hawajatoa ufafanuzi mbona jamiiforums na BBC hawajaambiwa washushe na ufafanuzi bado. Nimesikia heti wanadai kwamba chanzo imeegea tu upande mmoja kwamba maelezo kwenye video ya gwajima hayajatolewa ufafanuzi na serikali, sasa...
  2. Just Pray

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 The Chanzo yaondoa Maudhui ya Askofu Gwajima YouTube Kufuatia wito wa TCRA

    Leo Mei 27, 2025, The Chanzo imepokea wito kutoka kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kuhusu maudhui ya video tuliyochapisha katika chaneli yetu ya Youtube, ambayo ni mkutano na waandishi wa habari mazungumzo aliyoyafanya Askofu Josephat Gwajima, Mbunge wa Kawe (Chama cha Mapinduzi -...
  3. R

    JamiiForums Tanzania TCRA tunaomba ufafanuzi kuhusu kutopatikana kwa tweeter (X) Tanzania

    Tunakwenda wiki ya pili bilaa Tweeter (X). Hakuna taarifa kutoka TCRA nini kimetokea Tweeter kutopatikana. watu wanasema (speculate) kuwa Serikali imeifunga , KWAHIYO TUSEME TWEETER (x) NDIYO BASI TENA IMEFUNGWA INDEFINITELY? TCRA tunaomba ufafanuzi
  4. Replica

    JamiiForums Tanzania Nadharia (Technical): Kilichotokea mpaka akauti nyingi zikadukuliwa

    Jana May 20 ulitokea mshtuko baada ya akaunti nyingi za mitandao ya kijamii kudukuliwa kwa pamoja idadi kubwa ikiwa taasisi za Serikali. Watu hawa wametumia kurasa za mtandao wa X na youtube. 1. Mitandao hii miwili ya X na youtube inarusu third party app kustream. Mfano nataka kuweka tukio...
  5. sanalii

    JamiiForums Tanzania Mtandao wa Tigo/Yas wanakiburi sana cha biashara au wanadharau wateja, TCRA wako wapi?

    Nimetuma pesa kwenye mtandao tofauti, pesa haijafika kwangu wamekata, na wananiambia masaa 72, wanasema tatizo lilitokea jana, chaajabu nimeangalia Instagram, nimeona malalamiko ni mengi sana, na yapo hadi siku za nyuma. Hii inapnesha ni tatizo la muda mrefu. Sasa kwanini hawaweki wazi tatizo...
  6. Mkoba wa Mama

    JamiiForums Tanzania TCRA ifuatilie wizi wa taarifa za nida unaofanywa na mawakala wa kusajili laini

    Hii imenitokea leo, nilienda kubadili laini ya Vodacom ili nipate laini ya 5G, wakala akaniambia niweke finger print, niliweka mara mbili baada ya kusema mara ya kwanza nilikosea. Baada ya kumaliza zoezi hilo na kuondoka pale, nilipokea ujumbe mfupi kutoka Airtel kuwa nimesajili laini mpya ya...
  7. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania Serikali yafungia mitandao na tovuti 80,171 zisizo na "maadili"

    Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imefunga tovuti, akaunti za mitandao ya kijamii, blogu na majukwaa 80,171 yaliyokuwa yakichapisha maudhui yanayokiuka maadili na kuhatarisha afya ya akili ya watoto. Kauli hiyo imetolewa Bungeni jijini Dodoma leo, Jumatatu Mei 5, 2025 na...
  8. R

    JamiiForums Tanzania Je, matumizi ya proxy server (VPS) hapa Tz nayo yamewekewa vikwazo kama ilivyo VPN?

    Wakuu naomba kwa anayejua kama kutumia VPS hapa Tanzania ni lazima nipate kibali TCRA kama ilivyo kwa VPN. Nataka nilipie proxy server huko ughaibuni. Nilishatumia miaka ya zamani sielewi kama sheria ya matumizi imebadilika. Shukran
  9. T

    JamiiForums Tanzania TCRA na Kesho la Polisi (15040)

    Mmekuwa mkitutaarifu kutoa taarifa kwenu kila tunapopokea message za utapeli kupitia namba yenu 15040. Nimekuwa nikiwatumia namba hizo za utapeli nami kuweka kumbukumbu. Tarehe 11 Apr 2025 nililipoti namba 0615656151 kuhusika na utapeli, cha ajabu Leo tena namba hiyo hiyo 0615656151 bado iko...
  10. Fbn

    JamiiForums Tanzania Kero TCRA mfumo SMS za lazima ambazo zinataka ukubari au kukataa huduma

    Kuna shida za SMS ambazo zinakuja kuchagua huduma zozote ambazo sio hitaji lako. Kwa wasio waelewa wanaweza kujikuta wanaingia makubariano bila kujua na ili bado TCRA imekaa kimya.
  11. Damaso

    JamiiForums Tanzania TCRA Yatakiwa Kuchukua Hatua Madhubuti Kudhibiti Utapeli wa Kielektroniki Kupitia Ujumbe wa Simu

    Ni Jumapili juzi nikiwa zangu mitaa ya Arusha natoka zangu kumshukuru Mungu basi nikaona ni vyema nijiandae kutoka out kidogo nikatafuta sehemu kuna wakala wa huduma za kifedha. Nikauliza kama naweza kutoa pesa na alinikubalia kuwa nitoe huku akinipa na namba ya kutolea. Dakika kama tano...
  12. Carlos The Jackal

    JamiiForums Tanzania TCRA mpo kweli Nchi hii? Mnaachaje Watu wanazungumza public Ngono kinyume na maumbile kama jambo linalofaa Ndani ya Jamii namna hii ?

    Kwann mnaacha Hawa watu wenye umaarufu ,wautumie Umaarufu wao kueneza habari zinazomomonyoa Maadili namna hii?. Nini hii?? Kwanini akili zenu na Focus zote zimemtazama LISSU kasema nini mtandaon ?. Kwanini hamlindi watoto ?? Kuna ugumu gani wa kuwalinda watoto dhidi ya unyanyaji wa kiakili...
  13. I

    JamiiForums Tanzania TCRA kweli wana nia ya dhati ya kushughulikia hawa matapeli wa mitandaoni?

    Utapeli kwa njia ya kimtandao ya simu umekuwa ukishika kasi kila siku, kama TCRA wangekuwa kweli wana nia ya kutokomeza ama kupunguza,ingewezekana. Wana namba yao, wanadai ukituma sms ya namba ya tapeli wanaifungia lakini cha ajabu, unaweza kutumia ujumbe na tapeli, ukatuma hizo namba kama...
  14. Mkalukungone Mwamba

    JamiiForums Tanzania TCRA: Utapeli mtandaoni umepungua asilimia 79.3 mkoani Tabora

    Mkoa wa Tabora umeshuhudia upungufu mkubwa wa majaribio ya uhalifu na utapeli kupitia mtandao, kutoka majaribio 590 hadi 122 katika kipindi cha miezi mitatu ya Oktoba hadi Disemba, kwa mwaka wa fedha 2023/2024. Hii ni sawa na upungufu wa asilimia 79.3. Taarifa hiyo imetolewa na Meneja wa...
  15. R

    JamiiForums Tanzania Kwako Dr Jabiri Bakari: TCRA yatoa ufafanuzi kuhusu gharama za vifurushi vya simu...... internet na muda wa maongezi

    Director General Dr Jabiri Bakari malalamiko ya kuibiwa bando/airtime yamekuwepo tangu Nape alipokuwa waziri wa sekita hiyo. Alikuwa anajibu kwa dharau na kiburi na majibu yake yalikuwa hayo hayo kama ulivyosema wewe. HILO NALIACHIA HAPO. LA PILI: Tumelalamikia kuhusu mtu kuweka bando/airtime...
  16. Mkalukungone Mwamba

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 TCRA yataka Vyombo vya Habari kuripotiwa uchaguzi bila upendeleo

    MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imevitaka vyombo vya habari nchini katika kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu kuvipatia vyama vya siasa nafasi sawa katika kuripotiwa habari bila upendeleo ili kuondoa malalamiko. Meneja wa Kitengo cha Utangazaji TCRA...
  17. Just Pray

    JamiiForums Tanzania Ally Kamwe: Habari za kufungiwa sio za kweli TCRA washughulikie taarifa kama hii

    "Na mimi nitumie nafasi hii kuwaomba watu wanashughulikia mitandao ya kijamii (TCRA) washughulikie taarifa kama hii, kwasababu Unapotoa taarifa kama ile huenda una vyanzo, lakini madhara ya taarifa kubwa kama ile ni makubwa kweli kweli, ule usiku wa taarifa imetoka nilienda kukesha hospitali na...
  18. Mzee wa Code

    JamiiForums Tanzania TCRA HESHIMUNI HAKI ZA WAALIKWA MLIWAALIKA MKUTANO MKUU WA DODOMA

    Mamlaka ya Mwasiliano acheni ubabaishaji fanyeni malipo ya washiriki waliofika dodoma kwenye mkutano mkuu wa vyombo vya habari mliufanya Dodoma kitendo cha kutowalipa washiriki mpaka sasa toka siku ya tukio kumalizika ni jambo ajabu sana sio heshima wapo watu walitoka mbali wakatumia gharama zao...
  19. Braza Kede

    JamiiForums Tanzania Hivi TCRA imewashindwa kabisa hawa watu wanaotuma SMS za kitapeli au kuna nini kinachoendelea?

    eti wakuu Kunani hapa? Mbona bado hizi meseji za ajabuajabu zinaendelea kutumwa licha ya mabiti yanayopigwa kila mara na hawa jamaa wa TCRA? Kwanini hawafungiwi hawa watu?
  20. Mr Why

    JamiiForums Tanzania TCRA tunaomba mtusaidie Wananchi wenu, kuna mitandao ya simu kila ukiweka salio la fedha unatafutwa na namba ngeni

    Serikali ya Tanzania kupitia TCRA tunaomba mtusaidie Wananchi wenu, kuna mitandao ya simu (..) kila ukiweka salio la fedha unatafutwa na namba ngeni Kuna mitandao fulani ya simu kila ukiweka salio la fedha katika account yako au ukitumiwa pesa unatafutwa na namba mpya yenye viashiria vya...
Back
Top Bottom