tcra

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (pia huitwa kwa Kiingereza: Tanzania Communications Regulatory Authority ambapo mara nyingi huitwa kwa kifupi: TCRA) ni taasisi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye majukumu ya kusimamia sekta za mawasiliano na utangazaji.

TCRA Ilianzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya mwaka 2003 kusimamia huduma za kielektroniki na posta na masafa ya mawasiliano nchini Tanzania. Mamlaka ilianza kazi tarehe 1 Novemba 2003 na inafanya shughuli za zilizokuwa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).

Mamlaka ya TCRA ni kusimamia sekta ya posta, mawasiliano ya kielektroniki na utangazaji katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na:
  • Kuzifanya shughuli za TCRA kuwa za kisasa kwa kutumia teknolojia sahihi;kuimarisha tafiti zenye ubora katika huduma zinazodhibitiwa, uwezo na umahiri wa watumishi.
  • Kukuza ufanisi; kuaminika na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya mawasiliano na matumizi yake.
  • Kukuza ufanisi na unafuu wa huduma za Mawasiliano na kuongeza upatikanaji wa huduma za Posta na TEHAMA katika maeneo yasiyohudumiwa ipasavyo na yale yasiyo na huduma kabisa.
  • Kulinda maslahi ya wadau na kukuza uelewa wa haki na wajibu wao.
  • Kufuatilia utendaji wa huduma zinazosimamiwa na kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na Kanuni kwa viwango vinavyostahili.
  • Kuratibu utekelezaji wa ahadi za kisekta kitaifa, kikanda na kimataifa.
  • Kufikia kiwango cha juu ya kuridhisha wateja kama ilivyoainishwa kwenye Mkataba wa Huduma kwa Mteja wa TCRA.
  • Kuendelea kuzingatia matakwa ya kisheria na kiusimamizi.

Sera zinazoathiri utendaji kazi wa TCRA ni pamoja na:
  • Sera ya Taifa ya Mawasiliano ya mwaka 1997
  • Sera ya TEHAMA ya mwaka 2003
  • Sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003
  1. Idugunde

    Mwigulu Nchemba: Tunawafuatilia wanaopotosha na kuzushia viongozi vifo

    Waziri wa Katiba na Sheria amesema wanawafuatilia wote wanaozushia watu vifo. Na hatua kali zitachukuliwa dhidi yao. Mpaka sasa kuna baadhi wameanza kushughulikiwa. Mh waziri hata watoto wa vigogo utawachukulia hatua?
  2. J

    TCRA wakomesha wizi wa kwenye mitandao tuma ujumbe kwenda namba 15040

    Endapo umetapeliwa au umetumiwa ujumbe wa utapeli, tuma ujumbe husika na namba ya aliyekutapeli au kukutumia ujumbe wa utapeli kwenda 15040. Huduma hii ni bure. Tushirikiane kutokomeza utapeli kupitia simu za mikononi. Sambaza ujumbe huu cc @TCRA_Tz @ConsumerCcc
  3. beth

    TCRA kudhibiti utoaji huduma za vifurushi kwa kampuni za simu

    Katika kukabiliana na malalamiko juu ya huduma ya vifurushi zinazotolewa na kampuni mbalimbali za simu nchini, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetengeneza kanuni ndogo zitakazoratibu utoaji wa huduma hizo. Kuandaliwa kwa kanuni hizo kumekuja kufuatia maoni 3278 yaliyotolewa na...
  4. Cpp

    TCRA rungu lao lingekuwa linafika Kenya, wangeifungia Citizen maisha

    Hawa ndugu zetu Wakenya naona wameamua kuishika Serikali yetu sharubu kwa kutuita “Hamnazo”
  5. Saa 7 mchana

    TCRA: Laini zote za simu zitakazotolewa kuanzia Julai 1 zitakuwa na Neno la siri, Mteja atatakiwa kulibadili ili kutumia laini mpya yenye usalama

    Ndugu Mteja, laini zote za simu zitakazotolewa kuanzia Julai 1 zitakuwa na Neno la siri ambalo Mteja atatakiwa kulibadili ili kutumia laini mpya yenye usalama. I smell a fish juu ya laini hizi. Nitahakikisha sipotezi laini ilikuepuka kurenew laini nakuingia huku. -- MAMLAKA ya Mawasiliano...
  6. Analogia Malenga

    TCRA: Utoaji wa Leseni za Maudhui Mtandaoni umesitishwa hadi Juni 30, 2021

    Mkuu wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Mihayo akizungumza kwenye Usiku wa Waandishi wa Habari na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa katika ukumbi wa Gold Crest Hotel Jijini Mwanza. Mamlaka ya Mawasiliano ya Tanzania (TCRA) imetangaza kusitisha utoaji wa leseni za Maudhui Mtandaoni kwa muda kuanzia...
  7. Replica

    TCRA wajifunze kwa Waingereza, kampuni ya simu yalambwa bilioni 33 kwa kuwaongezea gharama wateja

    Pamoja na agizo la waziri mwenye dhamana ya mawasiliano kuitaka mamlaka ya udhibiti wa mawasiliano nchini(TCRA) kudhibiti gharama za mawasiliano bado wameonekana kugonga mwamba huku kampuni za simu zikiweka pamba masikioni. Uingereza sehemu kubwa ya gharama ya mawasiliano ni kwa bili na moja ya...
  8. Granite

    Vodacom Kulikoni? TCRA hebu tuokoeni na hizi gharama za Data

    Nilizoea kujiunga Vifurushi vya aina mbili vya wiki 2Gb kwa Tsh.3,000/= au 4Gb kwa Tsh.5,000/= Leo nimekutana na hali tofauti, 1Gb kwa 3,000/= na 2GB kwa 5,000/= kwa kweli nimechanganyikiwa kidogo hasa ukiangalia hali tunayoipitia mtaani. Mbona hii mitandao imekuwa na upandishaji wa gharama...
  9. Elius W Ndabila

    Hawa wanaofanya uhalifu mitandaoni wako juu ya TCRA?

    HAWA WATU WAKO JUU YA TCRA? NITUMIE KWENYE NAMBA HII 0657523389 Na Elius Ndabila 0768239284 Itakumbukwa kuwa tuliambiwa kuwa watu wamekuwa wanatumia simu kufanya uhalifu kwa kuwa hakukuwa na namna nzuri ya usajili wa laini zetu. Kwa kutambua hilo serikali iliweka mkazo kwa kila Mtanzania...
  10. B

    Naibu Waziri wa TEHAMA, Kundo Andrea ashauri TCRA kuanzisha mitandao yetu ya kijamii tuachane na Twitter, FB, YouTube n.k

    Kuelekea uchumi wa kidigitali Serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imeitaka mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA kufikiri namna ya kutoa fursa kwa waTanzania wenye uwezo wa kuanzisha mitandao ya kijamii ya ndani ya nchi ili kukuza uchumi na usalama wa nchi. Naibu...
  11. DELETED ACCOUNT

    Ni kituo gani cha Television kilipigwa faini na TCRA wakati wa uchaguzi?

    Kuna taarifa naifanyia kazi sasa nahitaji baadhi ya information muhimu. Ningependa kujua, wakati wa kampeni kuna kituo cha television kilirusha matangazo ya BBC yaliyojumuisha taarifa fulani nadhani kuhusu Tundu Lissu. Kile kituo kilipigwa faini nadhani ya milioni 20. Ningependa kujua kituo...
  12. Kelela

    Naomba Ufafanuzi Online Content Regulations za TCRA

    Habari wa taalamu, Regulation iliyotolewa na TCRA kuhusu uhitaji wa leseni ya maudhui mtandaoni imesema ni kwa wale wanaotoa Predominant Content, ambayo si chini ya 85% kwa wiki. Hii ina maana gani? Naomba ufafanuzi zaidi kutoka kwa Wanasheria. Nimeambatanisha na sehemu inayotaja hiyo...
  13. D

    Vipindi vya Mashamsham, Mgahawa na SportsArena vimesheheni Waropokaji; TCRA ni waungwana sana vinginevyo wangeshavifutilia mbali

    Tunapozungumzia uthubutu; Tusisahau kuthubutu bila kuzingatia kanuni (Ethic's) katika kazi husika! Wamiliki wa Wasafi wamethubutu na wanania njema ya kuleta mabadiliko kwenye media lakini malengo yao yataendelea kuwa butu kutokana na aina ya baadhi watangazaji wanaowaajili kushindana kuropoka...
  14. W

    Gigy Money kafanya nini huko kwenye ziara ya Tumewasha na Tigo?

    Habari, Kuna clip moja nimeiona kwenye mtandao wa Instagram ikimuonesha mtu mmoja ambaye bila shaka alikuwa ni kiongozi wa tour ya jana ya WCB ya tumewasha na tigo waliofanya jijini Dododma akiomba radhi ya jambo linaloonesha sio la kiungwana na lisilokuwa na stahala lililofanya na "Msanii"...
  15. Elius W Ndabila

    TCRA, nawaombea msamaha Wasafi TV

    TCRA NINAUNGANA KUWAOMBEA RADHI WASAFI TV. Na Elius Ndabila 0768239284 Leo TCRA wametoa mvua ya miezi sita kwa Wasafi TV kwa kile kinachosemekana ni kurusha maudhui kinyume cha sheria. Niwapongeze TCRA kwa kusimamia sheria hizi kwa uangalifu na nidhamu kubwa. Tunajua kuwa sheria ni msumeno...
  16. Replica

    RUNGU: TCRA imeitaka Wasafi TV kusitisha matangazo kwa Miezi Sita (6) kuanzia leo kwa kurusha Maudhui ya utupu

    TCRA imeitaka Wasafi TV kusitisha kurusha matangazo kwa miezi sita kuanzia leo kutokana kwa kukiuka kanuni za utangazaji kwa kurusha maudhui ya utupu. Maamuzi hayo yanakuja kufuatia maudhui ya picha jongefu yaliyomwonesha msanii wa bongo Fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money akicheza...
  17. mgt software

    Nikusaidie Waziri Faustin Ndugulile kudhibiti TCRA, TRA na TBS juu ya vifaa vya telecom feki

    Jf oyee Kwako Dkt. Ndugulile, vyombo hivyo Hapo juu vimekuwa vikilalamikiwa kwa kutokuwa makini, kweli vyombo hivi vinatumia gharama Kubwa kuwepo huku ufanisi Wa kazi upo chini sana. Nikianza na TRA, hawa wanaruhusu kuingia kwa vifaa ambavyo havina certificate of compliance. Hi yo kuruhusu...
  18. Miss Zomboko

    TCRA yapewa miezi mitatu kumaliza changamoto za bando na vifurushi zinazotolewa na kampuni za simu za mkononi kwa wananchi

    Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk. Faustine Ndugulile ametembelea TCRA na kuipa miezi mitatu kumaliza changamoto za bando na vifurushi zinazotolewa na kampuni za simu za mkononi kwa wananchi kwani hawana imani na vifurushi vya intaneti. Pia, Waziri Ndugulile ameiagiza TCRA...
  19. robinson crusoe

    TCRA achieni Twitter yetu! Tunaojitambua tunaihitaji kwa elimu yetu

    Tuko mikoani tukilamba x-mas yetu lakini tunataka kuwa connected na dunia. Tangu iliposikika kwamba kuna video ya ngono ya wanasiasa wawili, twitter haiko hewani. Tunahangaika kupitia njia za panya ili kuwasiliana na kusoma mambo ya muhimu. Hii kufunga funga itaendelea hadi lini wakati kuna...
  20. Z

    Mtandao wa Smile ni kweli na nyie mmeanza wizi?

    Ukatikaji wa mawasiliano katika mtandao wa smile kwa sasa limeanza kuwa jambo la kawaida sana. Kila wakati mtandao wao unapotea hewani na hawatoagi feedback yoyote unaporudi kwa wateja wao. Ila pia kinachokwaza ni wizi unaoendelea kwa hivi sasa. Kwa mara kadhaa umeshawahi kupotea na bundle za...
Back
Top Bottom