mahakama

Mahakama ni chombo kinachotafsiri na kutumia sheria katika kutoa haki. Ni moja wapo ya mihimili mitatu inayounda serikali, ambapo mihimili mingine ni Bunge na Serikali Kuu.
  1. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Nigeria: Mahakama yaanza kusikiliza Kesi ya Kupinga Ushindi wa Urais wa Abola Tinubu

    Kesi ilifunguliwa na waliokuwa Wagombea Urais katika Uchaguzi wa Februari 2023, Peter Obi wa chama cha Labour na Atiku Abubakar (PDP) kwa madai kuwa Tume ya Uchaguzi (INEC) ilishindwa kuweka Matokeo Mtandaoni kwa muda halisi. Madai hayo ikiwemo ya Tume kushindwa kuwa wazi na kukiuka Sheria za...
  2. benzemah

    JamiiForums Tanzania Mahakama yaridhia kunyongwa aliyemuua Dereva Bodaboda

    Mahakama ya Rufani Morogoro, imetupilia mbali rufani ya Justine Chamashine aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kosa la kumuua dereva wa bodaboda, Joseph Frorence 'Msimbe'. Uamuzi huo ulitolewa wiki iliyopita na Jopo la Majaji watatu likiongozwa na Jaji Mkuu Profesa Ibrahimu Juma. Majaji...
  3. J

    JamiiForums Tanzania Prof. Kitila Mkumbo: Ushauri wa Kishujaa umesababisha Tanzania ishtakiwe katika Mahakama za Kimataifa. Wasomi wetu waliwadanganya Viongozi

    Prof. Kitila Mkumbo anadai Tanzania imeshtakiwa na makampuni ya madini, na mashauri hayo yanapelekea serikali kuingia hasara. Prof anadai Wasomi walitoa ushauri ili kuwafurahisha viongozi badala ya kuwaambia ukweli kuhusu madhara ya kuvunja mikataba ya kimataifa.
  4. TheForgotten Genious

    JamiiForums Tanzania SoC03 Rais kuteua Majaji kunaathiri Uhuru wa Mahakama

    UTANGULIZI Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 109, majaji wote wanateuliwa na Rais ambaye ni kiongozi mkuu wa Serikali na kiongozi mkuu wa chama dola, serikali na Mahakama ni miongoni mwa mihimili mitatu ya serikali bila kulisaghau Bunge, mihimili hii kila mmoja...
  5. R

    JamiiForums Tanzania SoC03 Responded Kitambulisho cha Taifa kiboreshwe ili kuendana na ulimwengu wa kidigitali

    Kitambulisho cha taifa hutumika kuthibitisha uraia wa mwananchi kwenye taifa husika. Lakini namna ulimwengu unavyoshuhudia ukuaji wa kasi kwenye sekta ya teknolojia ni vizuri kuboresha kitambulisho cha taifa kwa kukiwezesha kubeba taarifa nyinginezo muhimu pamoja na nyaraka za mhusika. Itasaidia...
  6. R

    JamiiForums Tanzania Je, wewe katika scenario hii utarudi ili ufungwe miaka 30/ Maisha?

    09.12.2019 Mahakama Kuu ilimwachia huru mtuhumiwa wa madawa ya kulevya. Jana 28/4/2023 Mahakama ya Rufaa ikamuona ana makosa ya madawa ya kulevya , ikamtia hatiani na kuamuru arudi /akamatwe afungwe miaka 30/maisha. Je wewe katika hali hiyo utarudi? Mimi sitarudi yote ya kwangu nyumbani...
  7. F

    JamiiForums Tanzania Bernard Membe ukiacha kuchukua stahiki yako kama Mahakama ilivyoagiza, wewe sio rafiki wa Watanzania!

    Ni haki yako! Ulitukanwa sana na ukadhalilishwa mno! Tafadhali timiza hukumu halali ya Mahakama na chukua fidia dhidi ya udhalimu uliotendewa na Cyprian Musiba. Kumbuka kuwa sio wewe peke yako ulidhalilishwa na Musiba, wewe ni muwakilishi tu, tupo wengi tulioshindwa kwenda mahakamani kumshtaki...
  8. Brain Kingdom

    JamiiForums Tanzania Kichaa haachiwi fursa ya kufanya maangamizi-Ndugu Bernard Membe ziba masikioni, Mahakama iheshimiwe stay firm.

    Hello JF readers and family. Wazandiki na wanafiki ni wauaji, wakati hao wahuni na wadhenzi wakiandika mengi sana kuhusu senior na historical figure na more specifically a gallant and long serving stateman B. Membe, we didn't hear and see them trying hard and wisely to advise Magufuli and his...
  9. LorenzoA

    JamiiForums Tanzania Mahakama yaamuru Mali za Maxcom Afrika zipigwe mnada

    Kwa wanaokumbuka kabla ya 2015 hivi. Hii kampuni ilitamba sana bongo na kuwezesha malipo ya Serikali, wakuitwa MaxMalipo... Story yao kwa sasa inasikitisha kidogo, baada ya bank ya Stanbic kuiburuza mahakamani wakidai walipwe malimbikizo ya deni la Bil 12. Mahakamani walijitetea kwamba baada...
  10. lord atkin

    JamiiForums Tanzania Mahakama yadaiwa kuamuru Mwanamitindo Noel na Mpambaji Kelvin Events wapimwe endapo wanafanya mapenzi ya jinsia moja

    Katika kipande cha amri inayodaiwa kutolewa na mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kivukoni iliyopo Kinondoni inaonesha Mwanamitindo Noel Ndale Mushi maarufu kama Noel ambaye ni mbunifu wa mavazi ya wasanii , Kelvin Maliki Ngao maarufu kama Kelvin Events na Mzungu Mmoja anauejulikana kama David...
  11. Samia atosha tukutane2030

    JamiiForums Tanzania Kitendo cha Mahakama zetu kushughulikia kesi za ushoga na kuwaacha mafisadi ya matrilioni mtaani hiyo ni failure ya nchi kwa 100%

    Kila mwaka tunasomewa report na CAG , tunajionea jinsi watu walnavyogawanya mabilioni ya umma kinyume na sheria. Hatuoni mafisadi wakiwa kwenye pingu. Sijawahi kusikia kuwa kuna fisadi kafungwa miaka 30 jela tangu nipate akili. Ushoga ni tatizo ila si kubwa zaidi ya tatizo la ufisadi na wizi wa...
  12. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Kati ya Miili 1,294 iliyofukuliwa ni 52 pekee ilipata idhini ya Mahakama, mingine ilifukuliwa kinyume cha Sheria

    Katika uchunguzi uliofanywa na Jeshi la Polisi pamoja na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Dar es Salaam, unaonesha kuwa tangu mwaka 2015 hadi 2021, kulikuwa na matukio ya kufukua miili 1,294. Kati ya matukio hayo, yaliyoruhusiwa kufukuliwa kwa amri ya mahakama ni 52 pekee. Aidha, Mahakama ya...
  13. Kenyan

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Japhet Koome: Siogopi vitisho vya mahakama ya ICC

    Inspekta Jenerali wa polisi Japheth Koome amesema kuwa hatishiki na barua iliyotumwa kwenda kwa Mahakama ya kimataifa ICC na upinzani. Upinzani kupitia Muungano wa Azimio unaoongozwa na Raila Odinga uliandikia ICC barua ukitaka Mahakama hiyo kufungua jalada la uchunguzi kutokana na nguvu nyingi...
  14. B

    JamiiForums Tanzania Mahakama ya Rufaa yamuachia huru mtuhumiwa aliyedaiwa kukutwa na heroine gramu 200.34, Bangi gramu 2.88 na vigae 3

    6 April 2023 Mahakama ya Rufaa Tanzania Dar es Salaam, Tanzania Jopo la majaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania chini ya jaji J.A Koroso baada ya kusikiliza rufani ya Mussa R. Magae, imetoa hukumu ya kumuachia huru Mussa Ramadhani Magae baada ya Mahakama ya Rufaa Tanzania kushindwa kushawishika...
  15. Zakaria Maseke

    JamiiForums Tanzania Jinsi ya kuomba Mahakama itengue hukumu ya upande mmoja (how to challenge ex parte judgement)

    Issue: Whether ex parte judgment can be appealed against without first attempting to set it aside?. By zakariamaseke@gmail.com Advocate Candidate - LST. Umeshtakiwa alafu hujatokea Mahakamani, kesi imesikilizwa upande mmoja (exparte) na hukumu imetolewa dhidi yako (umeshindwa kesi)...
  16. O

    JamiiForums Tanzania Majaji wastaafu wataka mahakama ichunguze vifo tata Polisi, Gerezani

    Wakati matukio ya watuhumiwa kufia mikononi mwa polisi, gerezani yakiibua sintofahamu, Chama cha Majaji Wastaafu (Tarja), kimependekeza kurudishwa kwa utaratibu wa mahakama kuwa ndio chombo kitakachochunguza vifo vyote vyenye utata. Chama hicho kimesema huko nyuma mtu akifariki gerezani, kituo...
  17. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Sabaya afikishwa tena Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi leo

    Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya amefikishwa kwa mara nyingine tena leo April 5, 2023 katika Mahakama ya Hakimu mkazi Moshi. Juni Mosi, 2022 Sabaya na wenzake wanne walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi wakikabiliwa na mashtaka 7 ikiwemo...
  18. M

    JamiiForums Tanzania Aliyeshtakiwa kuua mke kwa kumchoma moto aomba mahakama imwachie huru

    Mfanyabiashara Khamis Luwonga (38), anayetuhumiwa kumuua mkewe Naomi Marijani na kumchoma moto kwa kutumia magunia mawili ya mkaa, ameiomba Mahakama Kuu imuachie huru kwa sababu hadi sasa hakuna ushahidi wa kutosha wa kumshtaki. Luwonga aliwasilisha ombi hilo jana mbele ya Jaji Obadia Bwegoge...
  19. K

    JamiiForums Tanzania Mahakama na mifumo ya sheria inaturudisha nyuma kwenye maendeleo

    Mahakama zetu zinajaa ukiritimba ambao unachukuwa muda kuisha. Kuna ucheleweshaji mkubwa wa kesi za muhimu kitaifa kuanzia kesi za kisiasa, kesi za kodi, kesi za ufisadi ni mahakama ndiyo inachewesha maamuzi na kurudisha taifa nyuma. Kuna kesi nyingi sana zinapelekwa na takuturu za rushwa...
  20. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Mshtakiwa aliyeiomba Mahakama akutanishwe na mkewe, aruhusiwa

    Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemruhusu mshtakiwa Said Matwiko anayekabiliwa na kesi ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroine zenye uzito wa kilo 34.89 kuonana na mke wake Sarah Joseph ili wajadiliane kuhusu malezi ya watoto wao. Sara na mume wake pamoja na watu wengine watatu...
Back
Top Bottom