mafuriko

  1. Librarian 105

    JamiiForums Tanzania SoC04 Tanzania tuitakayo 2050: Miundombinu ya kukabiliana na mafuriko isanifiwe kiuhandisi kuakisi ongezeko la watu na ukuaji wa makazi nchini

    Utangulizi: Kwa muda mrefu mafuriko yamekuwa yakiharibu miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji nchini, pia kuleta maafa ya vifo kwa raia na mali zao, na kwa ujumla hurejesha nyuma kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Na mara nyingi viongozi wa serikali hutazama majanga ya mafuriko na...
  2. Analogia Malenga

    JamiiForums Tanzania Mabwawa ya Tanzania hayajengwa kukabiliana na mafuriko, bali kuzalisha umeme tu

    Mto Rufiji, unaoishia katika pwani ya kusini-mashariki mwa Tanzania, ulikumbwa na wimbi kubwa la mafuriko Aprili 2024. Mafuriko haya yalisababisha vifo vya kusikitisha na kuathiri watu 88,000. Zaidi ya hekta 28,000 za mazao ziliharibiwa. Tanzania ina historia ndefu ya ujenzi wa mabwawa, kuanzia...
  3. B

    JamiiForums Tanzania Benki ya CDRB yatoa msaada wa mbegu za mahindi kwa waathirika wa mafuriko Rufiji

    Rufiji. Tarehe 29 Mei 2024: Kutokana na mafuriko yaliyotokea katika msimu wa masika mwaka huu, Benki ya CRDB imekabidhi msaada wa mbegu za mahindi zenye thamani ya shilingi milioni 50 kwa wananchi wa Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani. Benki ya CRDB imekabidhi kilo 7,148.857 za mbegu za kisasa za...
  4. Mekim

    JamiiForums Tanzania SoC04 Mafuriko yasiyo na suluhisho la kudumu

    Katika ripoti nyingi za waandishi wa habari na marejeo ya ripoti ya wizara ya makazi, kila mwaka kumekuwa na ongezeko la idadi ya maeneo kupata athari ya mafuriko kwa mvua za vuli na majira ya dharura (kulingana na mabadiliko ya hali ya hewa) na yale yaliozoeleka yakiathiriwa kwa wingi zaidi ya...
  5. B

    JamiiForums Tanzania Video: Mafuriko Manyara, kuaribu vyanzo vya utalii, maji ya funika hoteli ya moja bilionea huyu. Royal tour kupata changamoto

    ROYAL TOUR KUONGEZA IDADI YA WATALII KUPATA CHANGAMOTO https://m.youtube.com/watch?v=Bl1CZq_Uwr4 Mr Chambulo mwenye uzoefu wa industry ya utalii na mwenyekiti wa mawakala wa utalii wa muda mrefu katika mazungumzo exclusive pia anatuonesha mazingira ya maeneo ya utalii. --- Mafuriko...
  6. Roving Journalist

    JamiiForums Tanzania Mbunge Sillo akabidhi magunia 10 ya mahidi wahanga wa Mafuriko Manyara

    Mbunge wa Jimbo la Babati na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo ametoa magunia 10 ya mahindi ya chakula kwa waathirika wa mafuriko waliopo katika Kijiji cha Manyara. Akizungumza mara baada ya kukabidhi chakula hicho Mei 19, 2024 katika Ziara Maalum ya Kikazi ya kutembelea na...
  7. DogoWaNjombe

    JamiiForums Tanzania Katavi: Barabara iliyofungwa kutokana na athari za mafuriko kuanza kutumika

    Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) mkoani Katavi, Mhandisi Martin Mwakabende ameifungua barabara hiyo baada ya kufanyiwa ukaguzi na ukarabati wa Daraja la Stalike kuelekea Mkoani Rukwa. Barabara hiyo ilifungwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko baada ya kujaa maji...
  8. R

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 CCM nilitegemea mtoe shukrani kwa Rais kwa kuleta mafuriko. Maana kila kitu anaupiga mwingi!

    Machawa fanyeni kazi yenu basi ya kusifia. Mvua hizo, mafuriko, mama Anaupiga mwingi. Naomba tumshukuru kwa mafuriko maana maisha yetu yanakuwa determined na Mama. Au nakosea jamani
  9. Ndagullachrles

    JamiiForums Tanzania Profesa Ndakidemi kuipa Milioni 5 familia iliyopoteza watu wanne kwenye mafuriko Moshi

    Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini (ccm),Profesa Patrick Ndakidemi ameahidi kutoa shilingi Milioni tano familia iliyopoteza watu wanne ambao walifari Dunia baada ya nyumba yao kuangukiwa na kifusi baada ya mvua kubwa Iliyonyesha usiku wa April 25 Mwaka huu . Mvua hiyo ambayo ilileta uharibifu...
  10. Msanii

    JamiiForums Tanzania Miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko. Jeshi linaweza kusaidia? Lina wataalam

    Lengo la uzi wangu siyo kumfundisha kazi Mhe. Rais. Bali kumshauri kwa uzingativu wa mamlaka aliyonayo kikatiba. Tunamuona Waziri wa Ujenzi Mhe. Bashungwa akipiga kambi kusini kusimamia urejeshwaji wa mawasiliano ya barabara na madaraja yaliyobomolewa na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha...
  11. Ndagullachrles

    JamiiForums Tanzania Profesa Ndakidemi awakimbilia wahanga wa mafuriko Moshi

    MBUNGE NDAKIDEMI AWAKIMBILIA WAATHIRIKA WA MAFURIKO KATIKA KATA ZA MABOGINI NA ARUSHA CHINI. Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini Profesa Patrick Ndakidemi ametoa pole kwa Wananchi wa Kata za Mabogini na Arusha Chini ambao nyumba na mazao yao yameathirika kwa mafuriko yaliyotokea katika Kata hizo...
  12. Cute Wife

    JamiiForums Tanzania Zoezi la urejeshaji wa Miundombinu Barabara Kuu Lindi-Dar eneo la Somanga laendelea

    Timu ya Wataalamu kutoka Wakala wa Barabara (TANROADS) wanasimamia zoezi hilo ili mawasiliano katika Barabara Kuu ya Lindi - Dar es Salaama kurejea kwa haraka. Waziri wa Ujenzi, Bashungwa alieleza kuwa timu ya watalaamu wa Wakala ya Barabara (TANROADS) na Makandarasi itatumia saa 72 (siku 3)...
  13. S

    JamiiForums Tanzania SoC04 Tanzania itumie takwimu za mifugo kudhibiti mafuriko

    Nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania zimeingia kwenye historia ya kukumbana na athari mbaya za mafuriko ambazo hazijawahi kushuhudiwa kwa miongo mingi iliyopita. 2023 hadi 2024 baadhi za nchi za Afrika hususani kusini mwa jangwa la sahara zimepoteza mamia ya watu, makazi, mifugo na miundombinu...
  14. Ziroseventytwo

    JamiiForums Tanzania Mafuriko makubwa mjini Ifakara leo Mei 5

    Hali ni mbaya. Maji ni mengi mji wa Ifakara kwa 80% upo kwenye maji. Hasara ni kubwa haswa kwa wafanya biashara za hardware. Cement na gipsam zimeharibika kwa kiwango kikubwa. Kuna baadhi ya familia zinahitaji msaada. Mtuombee. Pia soma:Serikali: Watu 33 Wamefariki Kutokana na Mafuriko na...
  15. Roving Journalist

    JamiiForums Tanzania Waathirika 4166 wa Mafuriko Katavi wapewa misaada yenye thamani ya Sh Milioni 113

    Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko amepokea misaada ya waathirika 4166 ambayo imetolewa na Serikali pamoja na Wadau wa maendeleo. Naye, Katibu tawala wa mkoa huo, Albert Msovela amesema misaada hiyo ina gharama ya jumla ya sh milioni 113. Ikumbukwe kuwa mwezi uliopita naadhi ya maeneo...
  16. R

    JamiiForums Tanzania Nabii J. Steven: Dar yapona ghadhabu ya Mungu, mafuriko yasitishwa

    Salaam, Shalom. Hii ni habari njema Kwa wakazi wa Dar es Salaam, Mungu amewaepusha mbali na dhahama ya mafuriko. Iliarifiwa kabla juu ya janga kubwa la Mafuriko kuukumba mji mzima wa Dar na watu kuarifiwa kuhama, Mtumishi mmoja amepata kibali Cha kuomba Kwa HAKI mbele za Mungu na kumsihi...
  17. Lady Whistledown

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Serikali yaahirisha Shule kufunguliwa kwa Mafuriko

    Serikali imeahirisha kufunguliwa kwa Shule kwa Wiki moja kutokana na mafuriko yanayoendelea ambayo hadi sasa yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 80. Taarifa ya Waziri wa Elimu, Ezekiel Machogu imeeleza kutokana na athari za Mafuriko si sawa kuhatarisha maisha ya Wanafunzi na Wafanyakazi, hivyo...
  18. Suley2019

    JamiiForums Tanzania KWELI Watu 155 wafariki kwa Mafuriko Tanzania

    Salaam, Wakuu nimepata wenge baada ya kuona taarifa inaeleza watu 155 wamefafiki kwa Mafuriko Tanzania. Sijakutana na hii habari. Na hata Mtandao wa X (Twitter) wengine wanapata mashaka kama Mimi tu. Je, kuna ukweli kwenye jambo hili? Tunaombeni ufafanuzi
  19. chiembe

    JamiiForums Tanzania Tanzania ina Jeshi la Zimamoto na Uokoaji! Kuna mtu kaliona wakati huu wa mafuriko?

    Mimi ningeteuliwa kuwa kamanda wa kikosi cha zimamoto na uokoaji, jambo la kwanza ningeomba kibali cha kuunda vikosi maalum hata vinne, kwa ajili ya zimamoto na uokoaji wakati nchi inasubiri kuwa na kikosi nchi nzima, Rufiji haupo, Kilosa haupo. Ndio maana hata kwenye gwaride hamkuwepo leo siku...
  20. Meneja Wa Makampuni

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Erick Omondi amua kuingia kwenye maji kuokoa wakenya kwenye mafuriko unaweza toa machozi

    Namwona Eric Omond ni mtu mwenye moyo sana. Namwona kama mtu anayeishi maisha halisia kabisa. Hata komedi zake hazina uongo uongo kabisa. Ukiangalia hii video unaweza toa machozi. Jamaa ana akili sana.
Back
Top Bottom