Utimamu wa kiongozi bora ni kuwa na kichwa chenye ubongo wa hekima, unaowaza, unoainisha, unaochambua, na kuweza kufanya tathimini. Vile vile ukamilifu wa kiongozi ni awe na kinywa chenye ulimi wa ufasaha, unaonena maneno ya staha, unaosema maneno ya uhakika, weledi na wenye kutoa nasaha bora...