Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Hakuna binadamu aliyekamikika, hivyo hata Mama Samia hajakamilika. Ila kiuongozi nitakuwa wa mwisho kukosoa na kusema Hana sifa ya kuwa Rais wa Nchi.
Urais wa Nchi unaongozwa na sifa Moja kuu, Rais ni Mzazi Kwa Taifa bila kujali ana umri Gani. Mama anasimama kama mzazi kwetu.
Jambo la pili Rais anapaswa kuwa mtu anayekubali kwamba hajui kila kitu ila anaweza kusimamia kila Jambo linalopaswa kusimamiwa. Mhe. Rais hajui kila kitu ila anaweza akasimamia Yale tuliyomkabidhi asimamie.
Jambo la tatu, akikosea anaweza akarekebisha makosa endapo yanarekebishika. Mhe Rais ni mwepesi kurekebisha pale anapopata fact kwamba Kuna mapungufu, aliwahi kuacha baadhi ya wateule wake baada yakusikia wananchi wakilalamika, Leo amerekebisha utata uliokuwa kwenye hotuba yake. Huu ndio uzazi na Uarais siyo kukomaa ukijitapa kwamba hakuna makosa
Anaweza akasemehe na wakati mwingine akapuuza, amempuuza Ndugai, Polepole n wengine. Hakutaka kushindana nao Wala kuwaonyesha yeye ana ñguvu Gani ameacha mamlaka ziangaike nao.
Anakasirika kama mwanadamu, anakwazika lakini hatoki adharani kuonyesha amekwazika. Kwa kuwa wanaomkwaza ni watu wazima anawaita nakuwakanya au kuwasikiliza ndani majirani wasijue. Tulishaanza kuona Taifa likiongozwa Kwa hasira za papo Kwa papo Leo hasira zinaelekea kwenye kalamu bila kudhalilishana. Pongezi
Mwisho; anaamini kwamba anaweza kupotoshwa na walio chini yake Kwa maslahi Yao na anapobaini anarudi nyuma kuyatizama maamuzi yake nakurekebisha pale alipopotoshwa. Tulimsikia kwenye mkutano wa vyama vya siasa,alikiri kwamba maridhiano ni muhimu na akaagiza waliopo chini yake wamshauri namna nzuri yakuliponya Taifa
Hizi sifa wanazo watu wachache sana, hata huko upinzani hakuna watu wenye sifa hizi sema awajapata madaraka mngejionea rangi zao halisi.
Kuhusu maendeleo; ukiwa na Kiongozi anayetenda haki na anayemcha Mungu ni zaidi ya majengo na mareli. Ukiwa na hofu hata utajiri hauna maana. Ameanza kurejesha confidence yetu soon ataendelea kufungua milango tujiletee maendeleo maana hakuna Rais anayeleta maendeleo, maendeleo yanaletwa na watu Kwa kufanya KAZI. Akiendelea mmoja mmoja kati yetu basi Taifa limesonga mbele.
Hongera Mama Samia, unayo nafasi yakurekebisha machache mabaya yanayokuchafua hasa ya kisiasa then utafanya mazuri mengi. Fungua moyo na tangaza msamaha kwa waliokukosea uanze ukurasa mpaya, samehe uliorithi kutoka kwa utawala uliopita. Ponya taifa manunguniko yakiisha taifa litapata baraka na umoja wetu utaonekana. Nikuombe sana sana usirithi ukatili maana ujazaliwa katili, usiumizwe na wapinzani wanaosema adharani, umizwa na wanaokusema gizani ambao umewateua wewe. Hao wa ndani wanaokwambia funga huyu fungua huyu ni wabaya kuliko wanaokubeza adharani.
Nikutakie mwaka mpya 2022, nipo nawewe bega kwa bega kwenye yale tu yenye maslahi kwa taifa na siyo maslahi ya chama.
Urais wa Nchi unaongozwa na sifa Moja kuu, Rais ni Mzazi Kwa Taifa bila kujali ana umri Gani. Mama anasimama kama mzazi kwetu.
Jambo la pili Rais anapaswa kuwa mtu anayekubali kwamba hajui kila kitu ila anaweza kusimamia kila Jambo linalopaswa kusimamiwa. Mhe. Rais hajui kila kitu ila anaweza akasimamia Yale tuliyomkabidhi asimamie.
Jambo la tatu, akikosea anaweza akarekebisha makosa endapo yanarekebishika. Mhe Rais ni mwepesi kurekebisha pale anapopata fact kwamba Kuna mapungufu, aliwahi kuacha baadhi ya wateule wake baada yakusikia wananchi wakilalamika, Leo amerekebisha utata uliokuwa kwenye hotuba yake. Huu ndio uzazi na Uarais siyo kukomaa ukijitapa kwamba hakuna makosa
Anaweza akasemehe na wakati mwingine akapuuza, amempuuza Ndugai, Polepole n wengine. Hakutaka kushindana nao Wala kuwaonyesha yeye ana ñguvu Gani ameacha mamlaka ziangaike nao.
Anakasirika kama mwanadamu, anakwazika lakini hatoki adharani kuonyesha amekwazika. Kwa kuwa wanaomkwaza ni watu wazima anawaita nakuwakanya au kuwasikiliza ndani majirani wasijue. Tulishaanza kuona Taifa likiongozwa Kwa hasira za papo Kwa papo Leo hasira zinaelekea kwenye kalamu bila kudhalilishana. Pongezi
Mwisho; anaamini kwamba anaweza kupotoshwa na walio chini yake Kwa maslahi Yao na anapobaini anarudi nyuma kuyatizama maamuzi yake nakurekebisha pale alipopotoshwa. Tulimsikia kwenye mkutano wa vyama vya siasa,alikiri kwamba maridhiano ni muhimu na akaagiza waliopo chini yake wamshauri namna nzuri yakuliponya Taifa
Hizi sifa wanazo watu wachache sana, hata huko upinzani hakuna watu wenye sifa hizi sema awajapata madaraka mngejionea rangi zao halisi.
Kuhusu maendeleo; ukiwa na Kiongozi anayetenda haki na anayemcha Mungu ni zaidi ya majengo na mareli. Ukiwa na hofu hata utajiri hauna maana. Ameanza kurejesha confidence yetu soon ataendelea kufungua milango tujiletee maendeleo maana hakuna Rais anayeleta maendeleo, maendeleo yanaletwa na watu Kwa kufanya KAZI. Akiendelea mmoja mmoja kati yetu basi Taifa limesonga mbele.
Hongera Mama Samia, unayo nafasi yakurekebisha machache mabaya yanayokuchafua hasa ya kisiasa then utafanya mazuri mengi. Fungua moyo na tangaza msamaha kwa waliokukosea uanze ukurasa mpaya, samehe uliorithi kutoka kwa utawala uliopita. Ponya taifa manunguniko yakiisha taifa litapata baraka na umoja wetu utaonekana. Nikuombe sana sana usirithi ukatili maana ujazaliwa katili, usiumizwe na wapinzani wanaosema adharani, umizwa na wanaokusema gizani ambao umewateua wewe. Hao wa ndani wanaokwambia funga huyu fungua huyu ni wabaya kuliko wanaokubeza adharani.
Nikutakie mwaka mpya 2022, nipo nawewe bega kwa bega kwenye yale tu yenye maslahi kwa taifa na siyo maslahi ya chama.