Mkuu sisi wote tunaunga mkono hili kwa sababu linasaidia sana kuongeza uwazi na utii kwenye kulipa kodi. Tatizo hapa ni namna ya utekelezaji wa mabadiliko haya. Ninadhani busara, elimu na “phasing” approach vinahitajika la sivyo kinachoathirika ni uchumi wetu..sidhani kama hii ndiyo njia sahihi...
Wale walioko kwenye sekta za usafirishaji, uchimbaji wa malighafi ujenzi na ujenzi kwa ujumla watakuwa wamegundua kuwepo kwa uhaba wa ghafla wa mchanga unaotumika kujengea hivi Karibuni maeneo ya Dar na sehemu jirani. Kwa kipindi cha kama wiki moja hivi, TRA Pwani imekuwa ikikamata magari yote...
Pamoja na kuwa Makonda anaweza kuwa sahihi kwenye hili, ninaonelea ni vyema rais Magufuli akazuia kutumiwa kufanya maamuzi ya haraka namna hii huko mbele..kuna uwezekano mkubwa sana wa kuaibishwa huko mbele
Mkuu, kisheria wafanyakazi wote walio ndani ya Tanzania, wawe raia wa Tanzania ama sio, wanatakiwa kuwa na bank account hapa Tanzania na mishahara yao hutakiwa kulipwa kwenye hizo account. Ikiwa wanataka kusafirisha fedha hizo kwenda nje watafanya hivyo kwa utaratibu wa kawaida wa kuiridhisha...
Kibaya kuliko vyote hawa mabwana wamefanya hii kuwa ni kawaida kwao..kwa hivyo kila kampuni mpya inayotokea Kenya inakuja na kuanza huu ukwepaji kodi mara moja
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.