Hili ni vunzo kwa vijana wengine,hakika ni wengi wajutao kama Nakaya ila wanaona aibu kusema,sasa Nakaya kawafungulia njia wawahi mapema kuja CHADEMA pakiwa angali mchana peupe
Mzee magula amechoka kifikra na pia uwezo wake wa kufanya kazi amekwisha sasa ni wakati wa yeye kuendelea kufanya kitu anachoweza kufanya nacho ni ukulima wa nyanya.
Anayosema kibonde namuunga mkono ni jimbo lililo wazi kabisa waliofanya jambo hili wachukuliwe hatua kali sana,pia ningemshauri Kibonde asiishie hapo yapo madudu mengi yanafnywa na serikali ya CCM yeye hujaribu kuyakanusha kama vile yeye ni msemaji ya Ikulu, aache kujipendekeza awe mkweli.
Roma kama msanii wa hip hop anayo haki ya kuimba na kutoa mawazo yake na kufikisha ujumbe kwa wanaomsikiliza,tukikumbuka tungo za mwanamuziki galacha la muziki wa regge Hayati Bob Marley alikuwa akiimba nyimbo zenye ujumbe mbali mbali bila kutumwa na mtu bali nafsi yake na nyakati zilimuongoza...
Msitu wa pande ni chaka kubwa la kihalifu na watu wetu wengi wamepotelea mule,sasa ni wajibu wa serikali kubadilisha matumizi ya huo msitu, :A S cry: kama serikali wamekataza mashamba pori mjini kwa nini waache huo msitu.
Tufike mahali watanzania tukatae kwa nguvu moja wimbi jipya la kutekana na ikiwezekana kuuwana,tukikumbuka mbunge wa ilemela ndg kiwia alinusurika kutolewa uhai,usariva arusha yule mwanachadema mbwambo alichinjwa kama mbuzi,kwa hali hii inaonyesha ni jinsi gani watawala wanaogopa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.