Urais 2015 kupitia CCM: Mangula amshukia Samwel Sitta...

Urais 2015 kupitia CCM: Mangula amshukia Samwel Sitta...

babalao 2

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
5,426
Reaction score
3,308
Makamu Mwenyekiti wa CCM ndg. Philip Mangula amekerwa na kauli ya mh. Sitta ya kutangaza NIA yake ya kuutaka Urais.

Mangula alisema kitendo alichofanya Sitta cha kujitangaza hadharani si kizuri na wote wanaojipitisha kuutaka Urais Hakika watakatwa majina yao wakati ukifika wa kuwapata wale watakaoingia kwenye mchakato wa kumpata mteule wa CCM.

Amewaasa ya kwamba muda wa Rais Kikwete bado haujaisha hivyo washirikiane kutekeleza Ilani ya CCM kwanza ili kuepuka kuenguliwa kwa kujitatangazia nia Mapema.

(Ikumbukwe wiki jana mh. Sitta alisema kwa hali ilivyo sasa yeye ndiye anafaa kuwa RAIS wa Tanzania kwani ana sifa ya kuwa Rais na Wananchi Wengi wanamtaka na kumsungumzia yeye kupewa dhamana hiyo).

Haya wataalamu wa demokrasia mnasemaje kwa hili?

Mbona Zitto alipotangaza Nia watu wa chama chake walivyosema si sahihi kwa muda huu CCM WAlisema NI HAKI YAKE KIKATIBA JE KWA CCM SI HAKI YA KIKATIBA KUTANGAZA NIA MAPEMA?

Source: Magazeti ya leo

==================
Kutoka Mwananchi

Mangula: Wanaojinadi kugombea urais CCM wanajiondolea sifa

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Phillip Mangula amesema kada yeyote wa chama hicho anayejinadi sasa kuwa anafaa kuwa Rais ajaye, anajiondolea sifa ya kuwania nafasi hiyo ndani ya chama.

Mangula alitoa kauli hiyo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara kwenye Viwanja vya Mwembetogwa mjini Iringa.

"Siyo urais tu, hata hao wanaopita na kuonyesha nia ya kuwania nafasi za ubunge na udiwani katika majimbo mbalimbali yanayoshikiliwa na wanaCCM, hawatateuliwa na sekretarieti ya chama kuwania nafasi hizo," alisema. "Rais wetu wa sasa ni Jakaya Kikwete, huyu ndiye Rais hadi 2015.

Pia tunao wabunge na madiwani walioapa kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM hadi mwaka 2015. Huyo anayepita sasa na kufanya kampeni kwa lengo la kuwania nafasi hizo anatumia ilani gani? Msimamizi wa Ilani iliyopo sasa yupo na bado hatujaandaa ilani nyingine," alisema Mangula na kuongeza:

Aruhusu kampeni majimbo ya upinzani

Mangula alitoa ruksa kwa wanachama wa CCM kuanza kampeni kwenye majimbo yanayoshikiliwa na upinzani akisema ni sahihi.

"Unapita kwenye jimbo linaloongozwa na Mbunge wa CCM unatumia ilani gani? Lakini kwa majimbo yanayoongozwa na wenzetu huko piteni," alisema Mangula. Alieleza madhara ya wanaCCM kuanza kampeni kwenye majimbo yanayoshikiliwa na makada wenzao kuwa ni pamoja na kuzalisha makundi ndani ya chama hicho tawala. "Makundi ni sumu na yanaleta mgawanyiko wenye madhara makubwa kwenye chama," alisisitiza.

Ashangaa Iringa kuwa upinzani
Katika hatua nyingine, Mangula alieleza kushangazwa na Jimbo la Iringa Mjini kuongozwa na upinzani akihoji ni pepo gani lililotokea. Aliagiza wanachama wa CCM kujipanga kwa ajili ya uchaguzi ujao ili kulirudisha mikononi mwao.

Aondoka uwanjani kiaina
Muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkutano huo Makamu Mwenyekiti huyo wa CCM, aliondolewa uwanjani hapo katika mazingira ya kutatanisha baada ya kuhofiwa kuwapo kwa kundi la watu waliojianda kufanya vurugu.

Mangula alibadilishiwa njia tofauti na msafara wake ulioelekea ofisini mara baada ya mkutano wake kumalizika, baada ya kuwapo taarifa za kuwepo vurugu.


======================

PAMOJA DAIMA.
 
Mangula aliiba fedha za EPA, Zakhia Meghji akajaribu kuCOVER issue ya EPA isiwafikie wananchi, Mwigulu Nchemba alikuwa anafanya kazi BOT wakati fedha za EPA zinaibiwa na KUBWA LA MAADUI KINANA alikuwa busy kwenye mapori akiangamiza Tembo. Hii ndio secretariat ya CCM hakuna msafi wa kusema mwenzie
 
Ccm wananikumbushia hadithi ya Sungura Mjanja
Hadithi inayokuja, ni ya sungura mjanja ...

Kwa kifupi kwao ccm - Chako changu, changu changu!
 
OLe wake Mangula athubutu kulikata JINA la Sitta, kwa kisingizio chochote kile, atakuwa ameisambaratisha CCM.
 
Haya tuwakaribishe wale walioshupalia kuwa CDM hamna demokrasia zaidi yule mdau aliyeanzisha thread ya kwa nini unaipenda CDM..akidai mwenyewe anaipenda CCM kwani kuna Demokrasia tofauti na CDM akatolea na mfano wa Zuberi..haya tunawafungulia jimwageni na demokrasia hiyo,ni wakati wenu kujidai sasa
 
Haya tuwakaribishe wale walioshupalia kuwa CDM hamna demokrasia zaidi yule mdau aliyeanzisha thread ya kwa nini unaipenda CDM..akidai mwenyewe anaipenda CCM kwani kuna Demokrasia tofauti na CDM akatolea na mfano wa Zuberi..haya tunawafungulia jimwageni na demokrasia hiyo,ni wakati wenu kujidai sasa

Ccm wanasahau haraka sana huwa wepesi kulaumu.
 
Mi nawataja wale wakuda wa CCM. waliokuwa wanasema CDM hakuna democrasia waje hapa wampinge makamu wao kwa kumpinga mzee Sita. ZOMBA, RITZ, MWIGULU, NAPE, CHAMA, WEB, na wengine wengi watoe mapovu.
 
Nchi kukumbatia mawazo ya zamani ya wazee kama hawa ndo maana hatutoki.
 
Makubwa,ndio kazi hii ya kusafisha chama ndani ya miezi 6 anayoifanya philip muanguka
 
Mi nawataja wale wakuda wa CCM. waliokuwa wanasema CDM hakuna democrasia waje hapa wampinge makamu wao kwa kumpinga mzee Sita. ZOMBA, RITZ, MWIGULU, NAPE, CHAMA, WEB, na wengine wengi watoe mapovu.

Hao hawapatani na ukweli huwezi waona hapa. Kumbuka kwenye uchaguzi wao uliopita hakukuwa na demokrasia wale waliotaka kumpinga jk waliitwa wana kura za MARUHANI MARA UTASIKIA UKIMPINGA JK UTAKUFA KWA CDM KITENDO CHA ZITTO KUMPISHA MBOWE WALIPIGA KELELE MPAKA BASI.
 
Soma vizuri maada kabla ya kuchangia. Mtoa uzi anatuomba tuchangia kuhusu kujitangaza nia ya kugombea kiti cha urais kabla ya wakati. Wewe unasema mambo ya EPA. Vinahusiana vipi? Jipange ujibu hoja au la kaa pembeni, usome wenzio wenye uelewa kile kinachotakiwa wachangie kwa faida yako pia.
Nionavyo mimi kila mchezouna kanuni zake. Mfano Demokrasia ina hatu kuu mbili: Majadiliano na Maamuzi.Wanademokrasia au wanachama wanaanza kujadiliana juu ya jambo fulani baada ya agenda za mjadala kupitishwa. Baada ya mjadala hupiga kura. Wengi hupewa ushindi wa kukubalika kwa hoja husika.Mwanachama hawezi kuanza kutoa hoja zake kablaya mjadala kuanza. Kufanya hivyo ni kukiuka taratibu, kanuni, na sheria za demokrasia. Ukifanya kosa lolote kwenye mchezo wowote unapewa adhabu.Ukianza kufaidi matunda ya ndoa kabla ya kufunga ndoa wewe ni mzinzi. Ukiotea kwenye mpira wa miguu hata kama utafunga goli, goli ni batili. Ukiomba tenda kabla ya tangazola tenda, tenda yako haipokelewi.
Hapo ndipo anaposimamia Mzee Mangula. Hatuwezi kuwa na demokrasia isiyo na kanuni. Itakuwa vurugu. Kama anataka kugombea kwenye chama kisicho na kanuni 6 atafute chama hicho aende akatangania yake huko. CCM kupitia Makamu wake Mwalimu Philip Mangula wanasema HAPANA! HAPANA! HAPANA! Na kama jina la 6 halikukatwa nitasema Mangula ni mbabaishaji.
Mangula aliiba fedha za EPA, Zakhia Meghji akajaribu kuCOVER issue ya EPA isiwafikie wananchi, Mwigulu Nchemba alikuwa anafanya kazi BOT wakati fedha za EPA zinaibiwa na KUBWA LA MAADUI KINANA alikuwa busy kwenye mapori akiangamiza Tembo. Hii ndio secretariat ya CCM hakuna msafi wa kusema mwenzie
 
Kumbe ndivyo wanavyofanya kukata majina ya watu kwa chuki binafsi. sas sitta amesema wazi tuone kama watalikata jina lake.
 
......
Soma vizuri maada kabla ya kuchangia. Mtoa uzi anatuomba tuchangia kuhusu kujitangaza nia ya kugombea kiti cha urais kabla ya wakati. Wewe unasema mambo ya EPA. Vinahusiana vipi? Jipange ujibu hoja au la kaa pembeni, usome wenzio wenye uelewa kile kinachotakiwa wachangie kwa faida yako pia.<br />

Nionavyo mimi kila mchezouna kanuni zake. Mfano Demokrasia ina hatu kuu mbili: Majadiliano na Maamuzi.Wanademokrasia au wanachama wanaanza kujadiliana juu ya jambo fulani baada ya agenda za mjadala kupitishwa. Baada ya mjadala hupiga kura. Wengi hupewa ushindi wa kukubalika kwa hoja husika.

Mwanachama hawezi kuanza kutoa hoja zake kablaya mjadala kuanza. Kufanya hivyo ni kukiuka taratibu, kanuni, na sheria za demokrasia. Ukifanya kosa lolote kwenye mchezo wowote unapewa adhabu.Ukianza kufaidi matunda ya ndoa kabla ya kufunga ndoa wewe ni mzinzi. Ukiotea kwenye mpira wa miguu hata kama utafunga goli, goli ni batili. Ukiomba tenda kabla ya tangazola tenda, tenda yako haipokelewi.<br />

Hapo ndipo anaposimamia Mzee Mangula. Hatuwezi kuwa na demokrasia isiyo na kanuni. Itakuwa vurugu. Kama anataka kugombea kwenye chama kisicho na kanuni 6 atafute chama hicho aende akatangania yake huko.

CCM kupitia Makamu wake Mwalimu Philip Mangula wanasema HAPANA! HAPANA! HAPANA!

Mkuu nimekupata ila hapo kwa cdm kulalamikiwa kwa kumkataza zitto kujipitisha mapema ilikuwaje? Dadavua wala ucpendelee popote.
 
Makamu Mwenyekiti wa CCM ndg. Philip Mangula amekerwa na kauli ya mh. Sitta ya kutangaza NIA yake ya kuutaka Urais.

Mangula alisema kitendo alichofanya Sitta cha kujitangaza hadharani si kizuri na wote wanaojipitisha kuutaka Urais Hakika watakatwa majina yao wakati ukifika wa kuwapata wale watakaoingia kwenye mchakato wa kumpata mteule wa CCM.

Amewaasa ya kwamba muda wa Rais Kikwete bado haujaisha hivyo washirikiane kutekeleza Ilani ya CCM kwanza ili kuepuka kuenguliwa kwa kujitatangazia nia Mapema.

(Ikumbukwe wiki jana mh. Sitta alisema kwa hali ilivyo sasa yeye ndiye anafaa kuwa RAIS wa Tanzania kwani ana sifa ya kuwa Rais na Wananchi Wengi wanamtaka na kumsungumzia yeye kupewa dhamana hiyo).

Haya wataalamu wa demokrasia mnasemaje kwa hili?

Mbona Zitto alipotangaza Nia watu wa chama chake walivyosema si sahihi kwa muda huu CCM WAlisema NI HAKI YAKE KIKATIBA JE KWA CCM SI HAKI YA KIKATIBA KUTANGAZA NIA MAPEMA?

Source: Magazeti ya leo

==================
Kutoka Mwananchi

Mangula: Wanaojinadi kugombea urais CCM wanajiondolea sifa

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Phillip Mangula amesema kada yeyote wa chama hicho anayejinadi sasa kuwa anafaa kuwa Rais ajaye, anajiondolea sifa ya kuwania nafasi hiyo ndani ya chama.

Mangula alitoa kauli hiyo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara kwenye Viwanja vya Mwembetogwa mjini Iringa.

“Siyo urais tu, hata hao wanaopita na kuonyesha nia ya kuwania nafasi za ubunge na udiwani katika majimbo mbalimbali yanayoshikiliwa na wanaCCM, hawatateuliwa na sekretarieti ya chama kuwania nafasi hizo,” alisema. “Rais wetu wa sasa ni Jakaya Kikwete, huyu ndiye Rais hadi 2015.

Pia tunao wabunge na madiwani walioapa kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM hadi mwaka 2015. Huyo anayepita sasa na kufanya kampeni kwa lengo la kuwania nafasi hizo anatumia ilani gani? Msimamizi wa Ilani iliyopo sasa yupo na bado hatujaandaa ilani nyingine,” alisema Mangula na kuongeza:

Aruhusu kampeni majimbo ya upinzani

Mangula alitoa ruksa kwa wanachama wa CCM kuanza kampeni kwenye majimbo yanayoshikiliwa na upinzani akisema ni sahihi.

“Unapita kwenye jimbo linaloongozwa na Mbunge wa CCM unatumia ilani gani? Lakini kwa majimbo yanayoongozwa na wenzetu huko piteni,” alisema Mangula. Alieleza madhara ya wanaCCM kuanza kampeni kwenye majimbo yanayoshikiliwa na makada wenzao kuwa ni pamoja na kuzalisha makundi ndani ya chama hicho tawala. “Makundi ni sumu na yanaleta mgawanyiko wenye madhara makubwa kwenye chama,” alisisitiza.

Ashangaa Iringa kuwa upinzani
Katika hatua nyingine, Mangula alieleza kushangazwa na Jimbo la Iringa Mjini kuongozwa na upinzani akihoji ni pepo gani lililotokea. Aliagiza wanachama wa CCM kujipanga kwa ajili ya uchaguzi ujao ili kulirudisha mikononi mwao.

Aondoka uwanjani kiaina
Muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkutano huo Makamu Mwenyekiti huyo wa CCM, aliondolewa uwanjani hapo katika mazingira ya kutatanisha baada ya kuhofiwa kuwapo kwa kundi la watu waliojianda kufanya vurugu.

Mangula alibadilishiwa njia tofauti na msafara wake ulioelekea ofisini mara baada ya mkutano wake kumalizika, baada ya kuwapo taarifa za kuwepo vurugu.


======================

PAMOJA DAIMA.
Mzee magula amechoka kifikra na pia uwezo wake wa kufanya kazi amekwisha sasa ni wakati wa yeye kuendelea kufanya kitu anachoweza kufanya nacho ni ukulima wa nyanya.
 
Soma vizuri maada kabla ya kuchangia. Mtoa uzi anatuomba tuchangia kuhusu kujitangaza nia ya kugombea kiti cha urais kabla ya wakati. Wewe unasema mambo ya EPA. Vinahusiana vipi? Jipange ujibu hoja au la kaa pembeni, usome wenzio wenye uelewa kile kinachotakiwa wachangie kwa faida yako pia.
Nionavyo mimi kila mchezouna kanuni zake. Mfano Demokrasia ina hatu kuu mbili: Majadiliano na Maamuzi.Wanademokrasia au wanachama wanaanza kujadiliana juu ya jambo fulani baada ya agenda za mjadala kupitishwa. Baada ya mjadala hupiga kura. Wengi hupewa ushindi wa kukubalika kwa hoja husika.Mwanachama hawezi kuanza kutoa hoja zake kablaya mjadala kuanza. Kufanya hivyo ni kukiuka taratibu, kanuni, na sheria za demokrasia. Ukifanya kosa lolote kwenye mchezo wowote unapewa adhabu.Ukianza kufaidi matunda ya ndoa kabla ya kufunga ndoa wewe ni mzinzi. Ukiotea kwenye mpira wa miguu hata kama utafunga goli, goli ni batili. Ukiomba tenda kabla ya tangazola tenda, tenda yako haipokelewi.
Hapo ndipo anaposimamia Mzee Mangula. Hatuwezi kuwa na demokrasia isiyo na kanuni. Itakuwa vurugu. Kama anataka kugombea kwenye chama kisicho na kanuni 6 atafute chama hicho aende akatangania yake huko. CCM kupitia Makamu wake Mwalimu Philip Mangula wanasema HAPANA! HAPANA! HAPANA! Na kama jina la 6 halikukatwa nitasema Mangula ni mbabaishaji.
Kwa kuwa huwezi kufikiri outside the box huwezi kujua ninamaanisha nini...

Namaanisha kuwa Mangula kwa kuwa ni mwizi kama mwizi mwingine, hana moral authority ya kuwapangia watu lini wajitangaze kugombea au kutogombea kwa vile haaminiki kwenye jamii. Dhamira yake ya wizi inaweza kuwa inamtuma kufanya kazi ya kuweka mgombea wanayemtaka na wezi wenzie ili aje ku COVER wizi wote waliofanya. Mwizi ni mwizi tu mwanawane...
 
Soma vizuri maada kabla ya kuchangia. Mtoa uzi anatuomba tuchangia kuhusu kujitangaza nia ya kugombea kiti cha urais kabla ya wakati. Wewe unasema mambo ya EPA. Vinahusiana vipi? Jipange ujibu hoja au la kaa pembeni, usome wenzio wenye uelewa kile kinachotakiwa wachangie kwa faida yako pia.
Nionavyo mimi kila mchezouna kanuni zake. Mfano Demokrasia ina hatu kuu mbili: Majadiliano na Maamuzi.Wanademokrasia au wanachama wanaanza kujadiliana juu ya jambo fulani baada ya agenda za mjadala kupitishwa. Baada ya mjadala hupiga kura. Wengi hupewa ushindi wa kukubalika kwa hoja husika.Mwanachama hawezi kuanza kutoa hoja zake kablaya mjadala kuanza. Kufanya hivyo ni kukiuka taratibu, kanuni, na sheria za demokrasia. Ukifanya kosa lolote kwenye mchezo wowote unapewa adhabu.Ukianza kufaidi matunda ya ndoa kabla ya kufunga ndoa wewe ni mzinzi. Ukiotea kwenye mpira wa miguu hata kama utafunga goli, goli ni batili. Ukiomba tenda kabla ya tangazola tenda, tenda yako haipokelewi.
Hapo ndipo anaposimamia Mzee Mangula. Hatuwezi kuwa na demokrasia isiyo na kanuni. Itakuwa vurugu. Kama anataka kugombea kwenye chama kisicho na kanuni 6 atafute chama hicho aende akatangania yake huko. CCM kupitia Makamu wake Mwalimu Philip Mangula wanasema HAPANA! HAPANA! HAPANA! Na kama jina la 6 halikukatwa nitasema Mangula ni mbabaishaji.

Mimi naunga mkono wale wote wanaojitangaza mapema kuwania kiti cha uraisi hasa kupitia ccm ukizingatia raisi kikwete anamaliza muda wake. Mtu kutangaza nia ni jambo zuri ili wanachama wa ccm na watz kwa ujumla wawe na nafasi ya kujadili kama kweli huyu mtu anasitahiri kuliongoza taifa hili. Watz lazima watambua kuwa si kila mtu anaweza kuwa raisi. Kuna viongozi uwezo wao wa kuongoza unaishia kuwa waziri na sio raisi. Ukimpa uraisi anachemsha na nchi inaweza kuyumba kama sio kuingia ktk machafuko. Mifano hiko mingi hasa barani Afrika. Kwahiyo pamoja na kanuni na taratibu za vyama kwa wanachama wanaohitaji kugombea uraisi ni muhimu ukatolewa uhuru mkubwa kwa raia kuwajadili mapema wale wote wenye nia ya kugombea uraisi.
 
Kwa kuwa huwezi kufikiri outside the box huwezi kujua ninamaanisha nini...

Namaanisha kuwa Mangula kwa kuwa ni mwizi kama mwizi mwingine, hana moral authority ya kuwapangia watu lini wajitangaze kugombea au kutogombea kwa vile haaminiki kwenye jamii. Dhamira yake ya wizi inaweza kuwa inamtuma kufanya kazi ya kuweka mgombea wanayemtaka na wezi wenzie ili aje ku COVER wizi wote waliofanya. Mwizi ni mwizi tu mwanawane...

Nakubaliana na wewe kabisa. Lazima watz watambue kuwa ingawaje raisi anatokana na chama fulani lkn akisha chaguliwa yeye ni kiongozi wa watu wote bila kujali itikadi zao. Hii ni pamoja na mbunge au diwani. Hawa ni viongozi wa watu ktk eneo husika, kwahiyo ni vema wale wote wanaofikiri wanawiwa kuwa viongozi wetu ktk ngazi mbalimbali wajitokeze mapema ili kwa nia njema kabisa watz ktk vikundi mbalimbali vya jamii yetu waweze kuwawahoji dhamira yao na ni kwa kiasi gani wanaweza kutatua matatizo sugu wanayowakabili watz. Safari hii watz haitaji kiongozi kwa kigezo cha ujana au uzee, mwanamke au mwanaume, watz wanahitaji mtz mwenye nia thabiti na uchungu wa dhati kabisa wa kuwasaidia watz kutatua matatizo lukuki yanayotukabili kwa sasa. Ni bahati mbaya sana kwa watz kuendelea kusikiliza fikra mfu za mtu kama Mangula ambaye ni kati ya viongizi walioshiriki kuharibu taasisi na uchumi wa nchi yetu.
 
Huyu wala hana haja ya kumkata jina lake. Dawa yake ni kusubiri dakika ya mwisho unaweka kigezo cha jinsia kama ilivyofanyika wakati wa uchaguzi wa spika wa bunge.
 
Back
Top Bottom