Wajukuu zangu mimi huwa nawakemea vijana wasiotoa hoja katika kujibu hoja kama wewe. Mbona unakurupuka tu mjukuu. Kwa kuwa hicho kinachosemwa ni chama chako, tumia jukwaa hili kumwaga hoja ili nasi tuchambue ambao si miongoni mwa nyie mnaochuana.
Mjukuu wangu unaonyesha unaupungufu wa elimu kuhusu makubaliano (negotiation technique). Makubaliano hayazuki tu, ni lazima upande mmoja utoe mapendekezo ya nini unakitaka, upande wa pili utaangalia vigezo vingi ili kukubaliana na ombi la mhitaji. Vigezo hivyo ni uwezo wa kumudu hitaji, umuhimu...
Mjukuu wangu, maneno hayo wameyatoa kwenye taarabu ya zamani kidogo. Imejaa tafsida, si rahisi kusema matusi moja kwa moja, lakini wako ni mtazamo. Kuna taarabu nyingi inasema, manahodha wa mashua kwanini wakae nyuma, ukisikia wimbo kwa kina utaona wanakemea tabia fulani katika mahusiano.
The...
Mjukuu wangu, unapotoa hoja wenzako wanaipima ili waitekeleze kwa nia nia ya kuboresha mapungufu yaliyojitokeza. Kwa hoja yako hii unawapa shida wenzako na pia hujamtendea haki aliyekupeleka shule, hoja zako zinaonyesha uwezo wako. Ngoja niachane na wewe.Wajukuu zangu, mtoa habari anaonyesha...
Kijana wangu, mwenzako ametoa hoja, naamini nawe utaleta hoja ili tuzipambanishe. Hapo CV yake ya nini? Tupe yako kwanza kabla hujadai yake ili nasi tujue uwezo wako. Kumbuka, inawezekana umekwenda shule lakini hujaelimika mwanangu.
Maneno yako yapo sahihi binti yangu. Ninafurahi pia kuwa uliyajua haya mapeama baada ya kuelezwa na bibi yako. Kinachonisikitisha mimi ni kuyasema hayo baada ya kuachwa na mume wa mtu. Napata shida kupima busara yako mwanangu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.