Ugonjwa waliokuwa nao CUF sasa umerithiwa na CHADEMA. Maalim Seif kwa CUF hakosei na kwa CHADEMA ni hivyo hivyo Mbowe ni malaika hana kosa. Tujitahidi kuchanganua mambo bila hivyo tutamalizana.
Ingawa niliusikiliza mdahalo huu mwishoni nakubaliana na wewe kuwa Mbowe alikuwa kama Kasuku anayesema yale aliyoyasikia tu wakati mwenzake (Hamad Rashid) alionyesha upeo wa hali ya juu ya uelewa wa mambo.
Kama ingalifananishwa na mechi ya Mpira basi matokeo yake ni kama ya juzi baina ya Man U...
Kukukua kisiasa kwa CUF ndio kulikowafanya waweze kuinunua Amani kwa gharama ya kusamehe ushindi Zanzibar. Kama wasingalifikiria maisha na roho za watu zitazopotea basi wasingalikuwa tafauti na CCM.
Kama unaona kinyaa tapika au nenda haja kubwa. Kama wingi wa watu basi Wahindi na Wachina wangalikuwa na viti mara laki moja UN ukilinganisha na baadhi ya nchi. Ikiwa hamridhiki na ugawaji wa majimbo ya Bunge basi njia ni rahisi jitoeni katika huu Muungano kwani hata Wazanzibari umeshawachosha.
Kwa nini nyinyi munaohisi kuwa Zanzibar inapendelewa katika hii ndoa ya Muungano kila wakati munatoa hoja ya idadi ya watu. Kumbukeni kuwa huu Muungano ambao ndio una matokeo mengi ( likiwemo hili la kugawa majimbo ya uchaguzi) ni makubaliano ya zilizokuwa nchi mbili Tanganyika + Zanzibar na...
Kilichotokea Zanzibar ni uelewa kuwa maslahi ya Taifa ni lazima yaekwe mbele, ni kukaa na kupima between two side of coin. Kama Maalim Seif angeyakataa matokeo Dkt. Shein angelitangazwa tu na ndio ungelikuwa mwisho wa Serikali ya Kitaifa na kwa vyovyote vile roho za wananchi wasio na hatia...
Kama nimewakosea nawaomba radhi lakini msimamo wangu uko pale pale na nakusikitia sana Mkuu kama bado una mawazo kuwa Wazanzibari hawajui kuwaza wenyewe na kujua lipi zuri na baya bila ya kuwashirikisha waarabu. Kwa taarifa yako waarabu waliondoka Zanzibar baada ya Mapinduzi matukufu ya 1964...
Kama ulisoma maelezo yangu ni kuwa biashara sio lazima kuwa na muungano ni nchi ngapi zinafanya biashara na hazikuungana na hata nyengine si marafiki kwa mfano Marekani na China. Kumbuka kuwa ikiwa nchi ina utaratibu mzuri inaweza kufaidika zaidi na wafanyabiashara walioko nchini kwao na...
Kinachoniishangaza kwa wale wanaoona kuwa Zanzibar inataka kujitutumua kutoka katika katika makucha ya Watanganyika - kutoa hoja zisizo msingi, kwa mfano kusema wazanzibari wanalishwa na kusomeshwa na Tanganyika ni hoja ya kitoto kwani yale ni mashirikiano ambayo yanafanywa na nchi mbali mbali...
Wakati uandikishaji wa wapiga kura nchini umemaliza katika sehemu zote mbili za nchi yetu yaani Bara na visiwani kuna kitu ambacho bado sijapata ufumbuzi wake.Kwa kawaida katika uandikishaji wa kura huku visiwani kuna uandikishaji wa aina mbili; wa kwanza ni wa Rais wa Zanzibar, wajumbe wa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.