Wingi Wabunge wa Zanzibar wana umuhimu gani Bunge la Muungano

Kwa nini nyinyi munaohisi kuwa Zanzibar inapendelewa katika hii ndoa ya Muungano kila wakati munatoa hoja ya idadi ya watu. Kumbukeni kuwa huu Muungano ambao ndio una matokeo mengi ( likiwemo hili la kugawa majimbo ya uchaguzi) ni makubaliano ya zilizokuwa nchi mbili Tanganyika + Zanzibar na sio wingi wa watu kama ni hivyo hamuoni kuwa hakuna haja ya watu milioni 40 kuungana na watu milioni 1. Acheni chokochoko kama unatoa hoja toa kwa kutumia vigezo kamili na ukumbuke kabla ya kufanya haya Zanzibar ilikuwa nchi na Serikali yake. Hakuna thamani ya hilo na tumekubali kuungana na kupoteza vyote hivyo. Jee wachina waombe viti vingapi? huko UN ikilinganishwa na Comoro.
 
Haingii akilini, uwiano wa idadi ya watu na wabunge hao, lakini mkumbuke kuwa wazanzibari walio wengi hawataki (mfumo huu wa muungano), kwa hiyo haya ni matokeo ya udikteta wa Chaka Chua Mapema.
 
Mtabe,

..uki-search kwenye mtandao kuhusu uanachama wa Tanganyika na ule Zanzibar ktk UN bila shaka utakutana na kipande hiki nilichokuwekea hapa chini.



Tanganyika was a Member of the United Nations from 14 December 1961 and Zanzibar was a Member from 16 December 1963.
Following the ratification on 26 April 1964 of Articles of Union between Tanganyika and Zanzibar, the United Republic of Tanganyika and Zanzibar continued as a single Member, changing its name to the United Republic of Tanzania on 1 November 1964.

..tembelea website hii inayoendeshwa na UN na utakutana na habari nyingi sana zinazohusiana na UN, na specifically wanachama wake.

.. "bonyeza hapa kutembelea website"

NB:

..nadhani John Malecelea ndiye balozi wa kwanza wa Tanzania[Tanganyika & Zanzibar] umoja wa mataifa UN.
 
Jamani nauiliza hivi hawa wabunge wa Zanzibar 50+ wa kuchaguliwa na 20+ viti maalumu making a total of 70+ kwenye bunge la jamuhuri lenye wabunge 329 mbona wengi sana na sioni impact yao? Wanakula ruzuku za bure nadhani mbali na kupunguza idadi ya mawaziri tungefikiria kupunguza idadi ya wabunge na hasa wa Zanzibar ambayo unakuta kwa kila watu elfu wana mbunge mmoja?

nadhani umelisahau neno muungano,hebu pitia miungano yooote duniani kisha angalia wanapogawana wenaangalia wingi wa watu au wanangalia haki ya usawa kwa kila upande?nadhani jaribu kusoma kisha ndio uje utoe upuuzi wako hapa,katafute neno muungano kisha uweke upuuzi wako,ni haki yao wazanzibar madhali tumekubali kuungana nao kwa faida yetu wabara maana km kudai nchi yao washadai sana lkn tumewang'ang'ania tu kwa kuwa kuna siri kubwa wewe huijui.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom