Ndugu wana jf, mi maoni yangu kuhusu mbowe kutuhumiwa na baadhi ya viongozi wa CDM,kua anaendesha chama ki dikteta si za kupuuzwa, kwa mfano hata kitendo cha akina zito kutofika bungeni siku ile ya hotuba ya JK,ni ishara tosha kua kuna matatizo ndani ya chama, ingawa akina halima mdee walitoa excuse mbalimbali za kutofika kwao kabisa lakini ukweli wanaujua wenyewe, hivyo basi chadema inapokua ina wachunguza akina shibuda na Zito ni vizuri imchunguze na mbowe,kuna wav wengi na mimi nikiwemo ambao hatuna imani kabisa na vyama vyetu vya siasa, lakini na cdm jinsi ilivyojipanga vizuri na kuzieleza sera zake kwa wananchi,hata sisi tuliona huenda cdm ikawa ndio mkombozi wetu, sasa basi hali ya migogoro kama hiyo mlionayo inatuvunja moyo na kutufanya tuhisi kua na nyie mnatafuta maslahi yenu binafsi. Mi napendekeza mbowe atoke kwenye kiti chake kwa muda then uchunguzi wa tuhuma dhidi yake ufanyike tena kwa misingi ya haki na ukweli na kama ikionekana ni kweli then aondoke halafu aje mwingine ambae atakaeweza kukinusuru chama kwa maslahi ya taifa zima. Mi yangu ni hayo tu.