Kumekuwepo na machapisho kadhaa kwenye mitandao ya kijamii, hususan Facebook, yakimuonesha aliyekuwa mgombea wa urais nchini Uganda, Bobi Wine, akidaiwa kukutana na Rais wa Marekani, Donald Trump. Hata hivyo, ukweli ni kwamba picha hizo zinazosambaa mitandaoni zimetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya akili unde, na si halisi.
Licha ya kwamba mgombea huyo wa urais alikimbilia Marekani baada ya kuhofia usalama wa maisha yake kufuatia matukio yaliyojitokeza wakati wa uchaguzi mkuu nchini Uganda, hakuna ushahidi unaothibitisha kuwa amekutana na Donald Trump kwa mazungumzo rasmi.
Ufuatiliaji uliofanywa kupitia tovuti rasmi za Ikulu ya Marekani haujaonesha taarifa yoyote kuhusu mkutano kati ya viongozi hao wawili.
taarifa hizo za kukutana...