Serikali ya Cambodia imetoa tangazo linalowaagiza raia wote wa Afrika, wakiwemo kutoka Kenya, Ghana, Cameroon na Uganda kuondoka nchini humo kabla ya Mei 31, 2026, la sivyo watakamatwa na kushtakiwa kwa mujibu wa sheria za uhamiaji.
Katika taarifa rasmi iliyotolewa na Idara Kuu ya Uhamiaji, mamlaka zilisema kuwa msamaha uliokuwa umetolewa awali kwa Waafrika utaisha rasmi mwishoni mwa Mei.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa wageni wote walioathirika ambao wamemaliza kulipa faini zao za uhamiaji wanapaswa kuondoka Cambodia kabla au ifikapo Mei 31, 2026.
“ Juni 1, 2026, raia yeyote wa kigeni atakayekutwa akiwa nchini Cambodia atakamatwa iwe uwanja wa ndege au eneo lolote,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Kwa mujibu wa agizo hilo...