JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Kumekuwepo na chapisho lililosambazwa kwenye mtandao wa Facebook, kupitia ukurasa wa Nalinga Media, na baadhi ya tovuti za kimatifa likidai kuwa mamlaka za Iran zimegundua fuvu la kichwa cha askari wa Jeshi la Marekani katika eneo la Isfahan, katikati mwa Iran. Chapisho hilo linaeleza kuwa fuvu hilo lilipatikana miongoni mwa mabaki ya ndege ya kijeshi ya Marekani iliyodaiwa kudunguliwa wakati wa mapigano ya hivi karibuni kati ya Marekani na Iran.
Taarifa kutoka ukurasa wa Instagram wa Habari 24 zimechapisha habari yenye ujumbe kwamba John Mrema, ambaye ni kada wa chama cha CHAUMA, ameomba kurejea CHADEMA. Katika chapisho hilo, ujumbe ufuatao umeonekana: “Taarifa ambazo bado hazijathibitishwa zinaeleza kuwa aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje pamoja na Mkurugenzi wa Uenezi wa CHADEMA, na baadaye kuhamia CHAUMA, John Mrema, anapanga kurejea CHADEMA.” je uhalisia wa dai hilo upo vipi?
Kumekuwepo na chapisho linalosambaa kwenye mitandao ya kijamii, hususan Facebook, likidai kuwa Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdoğan, ametoa kauli kali kuhusu Iran. Chapishi hilo limechapishwa katika ukurasa wa Athumani Seiph Amri ambapo Erdoğan anadaiwa kusema kuwa Uturuki haitaruhusu Iran kugawanywa, na kwamba itachukua hatua za kijeshi kama ilivyofanya nchini Syria endapo kutakuwa na jaribio lolote la kuivuruga au kuigawa Iran, ikiwemo kupitia makundi ya Wakurdi au njia nyingine. Chapisho hilo linaeleza zaidi kuwa Erdoğan alitoa onyo kwa Marekani na Israel, akisisitiza kuwa yeyote atakayejaribu kugawa Iran au kuingilia uhuru wake atakabiliwa na majibu makali kutoka kwa Uturuki.
Back
Top Bottom