Kumekuwepo na picha inayosambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii kama Facebook, Instagram na X ikimuonesha Rais wa Burkina Faso, Ibrahim Traoré, akiwa amevalia kofia nyekundu ambayo inaonekana kuunganishwa moja kwa moja na bunduki.
Hata hivyo, uchunguzi wa kidijitali umebaini kuwa picha hiyo imehaririwa kutoka kwenye picha halisi na kufanyiwa maboresho kwa kutumia teknolojia ya akili unde , jambo linaloifanya ionekane tofauti na uhalisia wake wa awali.
Aidha, ufuatiliaji zaidi umeonesha kuwa picha hiyo inayosambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii haijawahi kuchapishwa na vyombo vikubwa vya habari nchini Burkina Faso wala kutolewa kupitia vyanzo rasmi vya serikali, jambo linaloibua mashaka makubwa kuhusu uhalisia wake.
Kutokana...