Katika siku za hivi karibuni, kumekuwepo na picha (graphic) inayosambazwa kwenye vikundi vya Facebook ikimnukuu Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS). Boniface Anyisile Mwabukusi Picha hiyo inadai kuwa Rais huyo amesema matamshi ya Tundu Lissu yana viashiria vya "uhaini" na kwamba yanapaswa kuzungumzwa mezani .kama yanavyonukuliwa Matamushi ya Lissu yalikuwa na Uhaini ndani yake turudi mezani yanazunguzika..
Ufuatiliaji wa kina uliofanywa kupitia mbinu ya utafutaji wa maneno muhimu (Keyword Search) umebaini yafuatayo:
Ufuatiliaji umebainisha kuwa Ukurasa wa Chanzo TV, ambao nembo yake imetumika kwenye picha hiyo, haujachapisha taarifa yoyote ya aina hiyo katika akaunti zao za Facebook, X (zamani Twitter), wala Instagram.
Rais...