JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Picha moja iliyosambaa mtandaoni – ikiwemo hapa JamiiForums – inamuonesha mwanaume mmoja akiwa katika hali mbaya ya kiafya. Maelezo katika picha hiyo yameandikwa kwa lugha ya Kiarabu yakieleza: “Kutoka tetemeko la ardhi la Februari 6, leo ametolewa chini ya vifusi huko Antakya, Uturuki hai na akiwa vizuri. Utukufu ni wa Mungu.” Picha ya sasa ya Ahmed Al-Sousi (Chanzo: An-Nahar)
Kumezuka tabia ya waandishi wa habari mkoani Kilimanjaro kujihusisha na utapeli kwa kuchukua fedha za watu (wadau) wakidai ni gharama za kutuma habari lakini kinachotokea ni wizi mtupu. Juzi mama mmoja wa Uru Mjini wilaya ya Moshi Vijijini ametoa Tsh. laki 4 kwa waandishi wa habari wanne ili waripoti tukio la mtoto wake mwenye Utindio wa ubongo kubakwa na kupewa ujauzito, mpaka sasa waandhi hao watatu wa TV na mmoja wa gazeti wameshindwa kutoa habari yake. Huu ni utapeli wa aina yake, ni jukumu la viongozi wa Press Club kilimanjaro kuchukua hatua dhidi ya waandishi hawa ambao ni wanachama wenu na hata kama si wanachama wenu wanachafua tasnia ya habari. Ni hayo tu kwa leo, wasiporudisha tunawaanika chap ili vyombo vya vichukue...
Miaka ya hivi karibuni, matumizi ya dawa za uzazi wa mpango (Vidonge na Sindano) yameongezeka sana, hali inayozua wasiwasi wa usalama wake miongoni mwa watumiaji. Baadhi wameonesha wasiwasi wao kuwa dawa hizi husababisha kupata watoto wa kiume wenye homoni nyingi za kike, au hata kupata watoto wa kike wenye kiasi kikubwa cha homoni za kike hivyo kuwafanya wakomae mapema kabla ya umri sahihi. Mathalani, mdau mmoja wa JamiiForums.com amekiri kuwahi kusikia kuwa matumizi ya muda mrefu ya dawa hizi yanaweza kusababisha mama kupata binti ambaye akifikisha umri wa miaka 8 matiti yake yanaweza kuwa makubwa, yaliyolala. Ukweli kuhusu athari za dawa hizi ukoje?
Kumekuwepo na taarifa kwenye mitandao ya kijamii lakini pia gazeti la Mwananchi limeandika kuwa Serikali ya Marekani imewawekea vikwazo wanasiasa wanne wa Kenya pamoja na familia zao akiwemo Naibu Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua baada ya kupata taarifa kuwa wanasiasa hao walipanga na kufadhili vurugu wakati wa maandamano ya Jumatatu iliyopita. Wanasiasa wengine katika orodha hiyo ni pamoja na Waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda, Moses Kuria, kiongozi wa walio wengi katika Bunge la Kitaifa, Kimani Ichungwa na Mbunge wa Kiharu, Ndindi Nyoro. Ukweli wa taarifa hii upoje?
Mdau wa JamiiForums amedai kuwa jamii za wafugaji ni warefu kwasababu wanakunywa sana maziwa tofauti na jamii za watu wasiotumia maziwa. Amebainisha baadhi ya sababu ni kutokana na maziwa kuwa na madini ya calcium na vitamini D ambavyo husaidia kutengeza na kuimarisha mifupa. Kinyume chake kwa jamii za wakulima ambazo hazitumii sana maziwa huwa wanakuwa wafupi. Jambo hili lina ukweli kiasi gani?
Ushiriki wa mazoezi ni jambo muhimu kwa afya. Husaidia kuongeza utimamu wa mwili pamoja na kuupa kinga ya kutosha dhidi ya magonjwa, hasa yale yasiyoambukizwa kama kisukari, shinikizo kubwa la damu na viribatumbo. Pamoja na faida hizi, watu wengine hushiriki mazoezi mbalimbali ya Gym kwa lengo la kuboresha muonekano wa miili yao, tunaweza kusema kwa sababu za urembo au utanashati. Miongoni mwa mazoezi yanayofanyika sana siku hizi hasa kwa wanawake ni kupiga vibao sehemu ya chini ya tumbo ili kubana misuli. Je, ni kweli kuwa mazoezi haya husaidia kubana misuli ya tumbo?
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…