JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Habari wakuu, nimeshangaa sana kuona WASAFI TV ikitumia lugha ya kihuni tena yenye maudhi katika uwasilishaji wa taarifa. Chombo mahili hakiwezi kutumia neno 'usela mavi' katika kufikisha ujumbe wake kwa hadhira,binafsi siyo mtaalamu wa teknolojia labda nyie wajuvi wa mambo hayo tazameni hii video chini kisha mniambie kama ni editing au laa. Kama ni Wasafi kweli lazima tujiulize maswali yafuatayo: Je hii jeuri wanaipata wapi ya kutudhihaki sisi juu ya msiba mkubwa kama huo? Je wao wanatumika katika kuchochea maovu ya utekaji au wao wanajikuta akina nani labda na chombo chao? Je wamezingatia nini katika uwasilishaji wao wa hiyo habari na je wameelewa kweli nini maana ya kupinga na kupaza sauti kwa vitendo juu ya mauaji? Pia soma...
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu, amesema Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe amemzuia kwenda katika ofisi kutokana na yeye kueleza ubadhirifu unaofanywa ndani ya chama. Pia Lissu amesema sababu nyingine ya kuzuiwa kwenda katika ofisi hizo ni kutokana na kutoa siri za vikao ndani ya chama, na kumueleza ukweli kuhusu kitendo cha kuanzisha taasisi nyingine ndani ya CHADEMA. Aidha Mwanahalisi ina nakala rasmi ya barua ya siri ambayo Mbowe amemwandikia Lissu kwa kumpiga zuio la kwenda ofisini.
Katika pita pita yangu ndani ya maktaba moja kubwa hapa nchini nimekutana na jina la huyu mtoto, Momčilo Gavrić na taarifa kuwa ndiye mtoto au mtu mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kuingia vitani mpaka sasa, huku vita ya kwanza ya dunia WWI iliyoanza Julai 28, 1914 na kutamatika mwezi Novemba 11, 1918. Momčilo Gavrić inasemekana aliingia vitani akiwa na umri wa miaka nane tu na kuanza majukumu ya kupambania taifa la Serbia. Nimekuja huku ili nipate kufahamu je ni kweli kuwa Momčilo Gavrić alipata kujiunga na jeshi akiwa na umri huu wa miaka nane?
Back
Top Bottom