JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Julai 12, 2023, Balozi mstaafu wa Tanzania Nchini Sweden, Dkt. Wilbroad Slaa akiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari alitoa kauli inayotuhumu waandishi wa habari kwa kufanya upotoshaji wa matamshi yake kwenye sakata la uwekezaji wa Bandari. Baada ya kauli hii, wadau mbalimbali walianza kutoa maoni yao ambapo jioni ya siku hiyo ilianza kusambaa barua inayodaiwa kutolewa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) ikionesha masikitiko na kulaani kauli za Dkt. Slaa. Barua hiyo ilienda mbali zaidi kwa kumtaka Dkt. Slaa kumba radhi kwa matamshi yake.
Wakuu, Nimekutana na ujumbe unasambaa kwenye mitandao ya kijamii Twitter, Instagram na hata humu JF nimeona mtu kaweka uzi kuwa wanafunzi tena wakike kutoka shule ya wasichana ya Lucas Malia walifungiwa mlango na hivyo kulazimika kulala nje sababu eti walichelewa kufika siku waliyotakiwa kuripoti shuleni. Tukio hilo limetokea Julai 9 na mpaka sasa hawajapolewa wako wanaranda tu mtaani. Wakuu taarifa hii ni ya kweli?
Mdau wa JamiiForums ameweka Chapisho lenye kichwa cha habari "CCM kimeanza kuumana" akimaanisha kuwa hali imeanza kubadilika kwenye Chama cha Mapinduzi baada ya Serikali inayoongozwa na Chama hicho kusaini Mkataba na kampuni ya DP World kuhusu uwekezaji kwenye Bandari ya Dar es Salaam. Hali hii imesababisha kuvunjwa kwa mojawapo ya Ofisi za Chama hicho iliyopo Kinondoni. Ukweli wa suala hili upoje?
Nimekuwa nikisikia kutoka kwa watu mbalimbali kuwa pindi hutumiapo dawa zozote basi itakupaswa usitumie maziwa aina yoyote kwasababu matumizi ya maziwa hupunguza au kuondoa kabisa ufanisi wa dawa hizo hivyo kupelekea kutotibu ugonjwa uliokusudiwa. Kwa uelewa wangu ni dawa mbili tu ambazo hushauriwi kutumia maziwa pindi ukiwa unazitumia ambazo ni Tetracycline Antacids Je, upi ukweli kuhusu jambo hili? Nawasilisha.
Kijana mmoja aliejulikana kwa jina la Israel Daudi, amefariki dunia baada ya kupigwa risasi 3 na askari Polisi kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuachia ng'ombe kuingia shambani. Tukio hilo limetokea katika Mtaa wa Olaresho, Kata ya Olasiti katika Halmashauri ya Jiji la Arusha. Akizungumzia tukio hilo Diwani wa Kata ya Olasiti, Alex Martin amesema hilo ni tukio la pili kwa askari huyo kufanya mauaji katika Kata hiyo ya Olasiti kwani huko nyuma alishafanya mauaji na Wananchi walitaka kumuua askari huyo lakini diwani aliingilia kati kwa kumuepusha askari huyo kuuliwa na Wananchi. Lakini cha kushangaza askari huyo amerudia tena kufanya mauaji katika kata hiyohiyo. Diwani Alex ametoa wito kwa Jeshi la Polisi kutotumia nguvu na mabavu kwa...
Nimepokea hivi karibuni voice note kutoka kwa Mtanzania anayeishi Afrika Kusini. Sauti hiyo ya Dudula Master ambaye ni mhamasishaji mkubwa wa Xhenophobia ametoa onyo dhidi ya wageni wote kuondoka Afrika ya Kusini kuanzia tarehe 02 Septemba 2022 hadi Machi 2023. Nchi zetu hususan Tanzania zinapaswa kuhakikisha usalama kwa raia wao wanaoishi kule kihalali na ikiwezekana kuweka utaratibu wa kuwaondoa raia wake Afrika ya Kusini. Matishio haya yamekuwa yakifanyika bila hatua zozote kuchukuliwa, hivyo inawezekana baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola vya Afrika ya Kusini ni wahusika wa hizi operesheni dhidi ya wageni. Hatulipi ubaya kwa ubaya bali kumtenga mtu mbaya ni sehemu ya kumpa fundisho dhidi ya mtenda ubaya. Ni wakati sasa wa Nchi...
Mtumiaji wa Mtandao wa TikTok anayetumia jina la Leonard Clasic (User4692412178624), Julai 3, 2023 mchana, aliweka video moja kwenye ukurasa wake pasipo kufafanua chochote. Video hiyo inamuonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akikemea baadhi ya watendaji wa Serikali wanaoingia mikataba mibovu na kusababisha hasara kubwa kwa taifa. Video hii inahusianishwa na Sakata la uwekezaji wa Bandari unaotarajiwa kufanywa na Kampuni ya DP World ya Dubai, imeendelea kusambaa sehemu mbalimbali huku baadhi ya watu wakimpongeza Rais Samia kwa kutoa kauli hiyo.
Juni 15, 2023, Mdau wa JamiiForums aliweka chapisho linaloelezea jinsi alivyokwenda kupata chanjo ya COVID-19 na kupatiwa cheti ya chanjo husika. Mdau huyu anaeleza kuwa alitishwa sana kabla ya kupata chanjo hiyo na wengine walimuomba alipie tu pesa ili apatiwe cheti kama sehemu ya uthibitisho wa kuchanjwa. Katika Mjadala huo, mchangiaji mmoja alisema kuwa Taasisi ya Msalaba Mwekundu (Red Cross) ilikuwa imetoa taarifa inayokataza watu waliochanja kuchangia damu kwa wahitaji. Taarifa hii ni sahihi?
Kumekuwa na debate kubwa kuhusu uchezaji wa Michael Jackson kwenye wimbo wa Smooth Criminal, kuna ile dance aliinama digrii 45 akiwa sakafuni mgongo ukiwa umenyooka, alikaa sekunde kadhaa kabla ya kurudi wima. Wataalamu wa uti wa mgongo wanaonya wengine dhidi ya kujaribu hatua inayoweza kuwadhuru. Wanadai uchezaji wa vile hauwezekani kabisa kwa binadamu yeyote. Wengine wanasema Mfalme huyo wa Pop alikuwa na kipaji kikubwa cha uchezaji hivyo suala lile lilikuwa jambo la kawaida. Wengine wanadai kuwa alivaa viatu vilivyoshikilia sakafu ili kumwezesha kuinama mbele digrii 45. Ukweli ni upi kuhusu 'Smooth Criminal Lean Dance'? VIDEO: Smooth criminal Lean Dance
Salaam Wandugu, Nimepata taarifa mtandaoni kuwa ndege ya Malaysia iliyopotea miaka tisa iliyopita imekutwa kwenye maji ikiwa haina abiria. Habari hiyo ilichapishwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwamo Twitter linaonesha picha ya mbele ya ndege yenye kutu inayosomeka: “Ndege ya Malaysia MH370 iliyotoweka miaka 9 iliyopita imepatikana chini ikiwa haina abiria. Ndege hiyo ilikuwa na abiria 239.” Je, kuna ukweli wowote? Picha inayoenea kwenye mitandao Picha ya ndege ya Lockheed Martin L1011 Tristar kwa upande wa pembeni Source: Deepbluedivecenter Video credit: Deepbluedivecenter
Ulaji wa viazi vitamu kwa kipindi kirefu unadaiwa kusaidia uzalishwaji wa mayai mengi kwa Mwanamke na hivyo kupelekea kupata watoto mapacha. Jiji la Igbo-Ora lililopo nchini Nigeria ni jiji lenye mapacha wengi na Nigeria imepewa jina la mji mkuu wa Mapacha Duniani kwa kuwa na watoto mapacha wengi zaidi kuliko eneo lolote duniani huku viazi vitamu vikiliwa zaidi nchini humo. Ni kweli kuwa Viazi vitamu huongeza homoni aina ya ‘phytoestrogen’ ambayo huchangia kwenye kupevusha yai zaidi ya moja kwa wakati mmoja hivyo kusababisha kuzaliwa kwa watoto mapacha?
Back
Top Bottom