Licha ya kufanya makubwa kwa muda mfupi ndani ya Mhula wa Kwanza, Rais wa Zambia Hakainde Hichilema ametangaza hataomba muhula wa pili kwenye uchaguzi mkuu wa baadae 2026.
Hapa Tanzania hakuna chochote kafanya na bado chawa wanataka aongeze muda mpka 2030!
Tamaa na Uroho wa Madaraka. Tazama video hii ujionee mwenyewe.
Video ya Rais Hakainde Hichilema akisema hatagombea tena mwaka 2026.
CAF wamethibitisha kuwa kwenye michuano ya AFRICAN FOOTBALL LEAGUE hakuna kanuni ya goli la ugenini (away goal rule) hivyo mechi ya Simba na Al Ahly ni mpya kabisa kule Cairo, yani lazima timu ishinde kuvuka nusu fainali. - Farhan kihamu jr
Nina swali ndugu zangu hivi inawezekana siku za hatari zikaangukia katika mzunguko kuingiliana na siku za hedhi?
Mfano, siku za hedhi ni tano ile siku ya 4 au 5 ikiwa siku ya hatari?🤔
Inadaiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi, amekitaka Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kusitisha mkutano wake uliopangwa kufanyika kesho Julai 23,huko Buriaga, Temeke jijini Dar es Salaam.
Barua inayodaiwa kuandikwa na Sisty Nyahoza, Naibu Msajili wa vyama.
Habari,
Nimekutana na picha zinazodaiwa kuwa ni kiwanda cha mayai Goba ambacho kinadaiwa kimekaa karibuni. Pia kuna video inasambaa ikionesha mtu akiuza mayai yenye viini viwili.
Video inayosambaa ikihusishwa na kuwapo kwa kiwanda Cha kutengeneza mayai
Kuna ukweli wowote kuhusu picha, video na habari hii?
Kuna imani au tuseme maneno mtaani kwamba ukitoa Damu (kuchangia Damu) mara moja basi itabidi uwe unatoa kila mara ili kudhibiti ongezeko kubwa linalotokea baada ya hapo.
Wengine wanasema usipofanya hivyo utakuwa ukipata maumivu makali ya Kichwa kila wakati.
Ukweli ni upi hapa?
Salaam ndugu zangu,
Leo katika pita zangu mitandaoni nimeona baadhi ya kurasa zinazoweka masula ya burudani na habari za Wasanii zikieleza kuwa kuna sauti ya Keefe D imevunja ikikiri kuhusika na kifo cha 2 Pac.
Upi ukweli kuhusu sauti na sakati hilo?
Baada ya Singida Fountain Gate FC kupoteza mchezo wao wa Ligi ya NBC Premier League wakiwa nyumbani dhidi ya Simba, kupitia mitandao ya kijamii walitoa malalamiko yao wakiituhumu TFF na Ligi ya Bodi kuwapangia refa kwenye michezo wanayokutana na Simba ambaye amekuwa akiibeba timu ya Simba SC baada ya kupewa maelekezo maalum ya kuwabeba Simba.
Singida FG wamedai kuwa katika michezo ambayo refa huyo amekuwa akichezesha dhidi ya Simba basi yeye ndiye huibuka Man Of The Match, hivyo wamezitaka taasisi hizo zinazosimamia ustawi wa mpira wa miguu nchini kutolea ufafanuzi.
Nimeona mjadala kuhusu mihula anayoruhusiwa kugombea makamu aliyeshika madaraka ya Urais kutokana na kuchukua kiti katikati ya muhula baada ya Rais aliyekuwepo madarakani kushindwa kuendelea aidha kwa kufariki akiwa madarakani, kujiudhuru au sababu za kiafya.
Mjadala umechagizwa na kauli ya Sophia Mjema aliyesema Rais Samia ni hadi 2035, huku wanaharakati wakipinga vikali kuwa hana sifa ya kugombea mihula miwili tena.
Je, ukweli ni upi?
Salaaam Wakuu,
Nimeona katika sehemu mbalimbali picha zikisambaa zikionesha nembo inayotumika kwenye Podium ya Rais Samia haina bibi na bwana kama ambayo alikuwa anaitumia Rais Magufuli.
Hili limekaaje Wakuu tunaomba ufafanuzi.
Nembo anayotumia Rais Samia ikiwa haina Bibi na Bwana
Nembo aliyokuwa akiitumia Hayati Magufuli ikiwa na Bibi na Bwana
Aprili 27, 2023, akaunti ya Mtandao wa Twitter inayotumia jina la MainLandAfrica iliweka chapisho linalodai kuwa Bilionea wa Marekani Dan Friedkin amekodisha takriban Ekari 6,000,000 za ardhi nchini Tanzania.
Chapisho hilo lilienda mbali zaidi kwa kudai kuwa Friedkin ni mmiliki wa Ekari zingine 25,000 za ardhi zinazounda pori la Akiba la Mwiba.
Wanaojua kuhusu huyu jamaa watupe details anafanya biashara gani na ardhi kubwa kiasi hicho?
Kiongozi mkuu wa Chama cha EFF amemtaka Raila Odinga kuacha maandamano na kukubali kuwa alishindwa. Amesema pia aache kuvuruga amani nchini Kenya kwani Rais Ruto alipita kwa haki.
Julius Malema akihutubia kwenye maadhimisho ya miaka 10 ya EFF
Tetemeko la aridhi nchini Morroco limeua zaidi ya watu 5000, kuna kijiji kimoja cha mlimani chote kimefutwa na tetemeko isipo kua majengo mawili tu, hayo majengo mawili ni msikiti wa kijiji na nyumba ya huyu alio jenga huo msikiti, hiivi hili lina uhusiano wote na Imani au ni ecological force tu, wenye uelewa mambo theology na geography tuambieni.
Kumekuwepo na madai yanayosambaa mtandaoni kuwa makasha ya dawa za meno huwa na rangi (code) za aina mbalimbali zinazofafanua aina ya kemikali zilizotumika kutengenezea dawa hiyo.
Aidha, madai hayo yanafafanua zaidi kuwa kemikali husika ni hatari kwa afya na husababisha saratani, na kwamba makampuni yanayozalisha dawa hizi hayawezi kukupa siri hii.
Ukweli wake upoje?
Picha hii inasambaa mtandaoni. Inadaiwa kuwa magari haya yapo Bandari ya Dar es Salaam, yameingizwa nchini na kampuni ya DP World tayari kwa kuanza kazi zake.
Chips ni chakula kinachotengenezwa kutoka kwenye viazi. Chakula hiki kimekuwa kinahusishwa na matatizo mengi ya kiafya ikiwemo magonjwa ya moyo.
Wataalam, tusaidieni ni kipi hasa kinachofanya chips iwe mbaya kiasi cha kuhusishwa na mambo mabaya.
Huwa navutiwa sana Historia za wanamke shupavu ambao walifanya mambo ya kuacha alama kwenye jamii zao na kukumbukwa mpaka sasa.
Katika pitapita zangu kwenye machapisho nikavutiwa na historia ya mtawala kutoka katika kabila la Waha wa Jamii ya Kitutsi, ukanda wa Kasulu sehemu za Heru Juu.
Imezoeleka kuwa wanaume ndio huwa machifu katika jamii mbalimbali za Kitanzania kabla na baada ya Uhuru. Sikuwahi kusikia mwanamke yeyote kuwa Chifu wa jamii fulani tofauti na Theresa Ntare. Tukiachana na Chifu Hangaya ambaye ni Chifu wa Heshima wa kabila la Wasukuma, naweza kuhitimisha kwa kusema Chifu Theresa Ntare ni Chifu pekee mwanamke katika historia ya nchi yetu Tanzania.
Mwami Theresa Ntare
Tangu zamani nasikia stori za mwanamke akifanya mapenzi kwa mara ya kwanza (kutolewa bikra kama wanavyoita) lazima atoke damu. Japo kumekuwa na baadhi ya wanawake wanasema hawakuwahi kutokwa damu, hii imekaaje?
Je, ni kweli mwanamke akitolewa bikra lazima atoke damu? Na kama ndiyo hao wanaodai hawajatoka wanakuwa wanadanganya?