Kuna video inayosambaa kwa kasi kwenye mtandao wa TikTok na majukwaa mengine, ikidai kuonesha dakika za mwisho za msemaji wa kundi la M23, Willy Ngoma, akishambuliwa na kuuawa na ndege zisizo na rubani (drones). Video hiyo inahusishwa na mashambulizi yanayodaiwa kufanywa na jeshi la serikali ya DRC (FARDC) katika eneo la Rubaya, Kivu Kaskazini.