Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na machapisho mbalimbali yanayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii yakiwa na jumbe zinazodaiwa kutolewa na baadhi ya viongozi, hususan wa nchi za Afrika Mashariki na Afrika ya Kati.
Mojawapo ya machapisho hayo linadai kuwa aliyekuwa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, alisema:"If you want to stop youths from alcohol or playing Aviator, just tell them that it's owned by William Ruto."
Chapisho lingine linadai kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, alisema:
"Mimi naomba Rais ndugu yangu William Ruto anipe mamlaka niongoze Kenya kwa wiki mbili tu, nimalize huo mchakato wa hao viumbe wa ajabu wanaojiita Gen Z. Ninyooshe nchi ya Kenya."
moja ya machapisho yamechapishwa hapa
Je...