Kumekuwepo na mijadala inayoendelea kwenye mitandao ya kijamii ikizungumzia uondolewaji wa tozo kwenye miamala ya kielekroniki.
Baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa tozo hizi zimefutwa kila sehemu huku wengine wakidai kuwa zimeongezeka tofauti na awali.
Ukweli wa suala hili upoje?
Kuna wakati upotoshaji huweza kutokea kwa kutumia picha ya zamani au picha isiyo mahali pake kuwaaminisha watu kuwa picha hiyo inahusiana na tukio au taarifa husika.
Watumiaji wa picha hii hukusudia kuibua taharuki au kutaka kukupa nguvu upotoshaji wao kuufanya uaminika kirahisi.
Zifuatazo ni baadhi ya mbinu za kubaini kama picha ya kwenye habari imeshawahi kutumika sehemu nyingine:
1. Kutumia Google Image Search
Ingia kwenye browser na andika "Google Image Search."
Apload au paste picha unayotaka kuchunguza.
Ruhusu Google kuitafuta na angalia matokeo kama picha hiyo inapatikana kwenye vyanzo vingine.
2. TinEye
Nenda kwenye tovuti ya TinyEye.
Apload au paste URL ya picha unayotaka kuchunguza.
TinyEye itatafuta picha hiyo au...
Uhakiki wa Taarifa hudumisha uwazi, kujenga imani kwa jamii, kukomesha upotoshaji pia kuwepo kwa taarifa sahihi katika jamii itaifanya jamii iweze kufanya maamuzi sahihi kwenye jambo sahihi.
Kuchochea uwajibikaji- Uhakiki wa taarifa utachochea makundi mengi kuwajibika kwani watakosa fursa ya kusambaza taarifa potofu kwa manufaa yao.
Mfano, wanasiasa husambaza taarifa au kutoa ahadi nyingi za kweli na za uongo ili kuwaaminisha watu wao ni sahihi kuchukua wadhfa wanaokuwa wanagombea na baada ya kupata nyadhfa huendelea kusambaza taarifa ili aidha kuwapumbaza wananchi juu ya mabaya yao au kupalilia nafasi zao.
Kwa kuhakiki taarifa jamii itaweza kuwawajibisha pale watakapokuwa wanaweza kubaini kuwa taarifa fulani si kweli au kweli...
Magonjwa mbalimbali yametufanya binadamu kubuni tiba aina mbalimbali ambazo zitatusaidia kuondokana na magonjwa hayo. Moja ya tiba iliyobuniwa na binadamu ni pamoja na mkoja wa binadamu kama tiba ya magonjwa mbalimbali.
Tena unaambiwa ukipata mkojo wa asubuhi ndio kiboko ya magonjwa kama anavyosema mdau hapa wa mtandao wa JF kuwa Mkojo wa asubuhi ni dawa murua
Shuhuda ni nyingi sana, moja ikiwa ni ya mdau huyu wa JF kutibu maumivu ya meno kwa kunywa mkojo wa asubuhi
Miaka ya 2013-2016 nchini Tanzania kulitokea kundi la wanunuaji wa mkojo wa binadamu kwa madai kuwa unaenda kutumika kama dawa.
Katika ukuaji wangu, mimi ni mmoja wa walioshawishika kutumia mkojo kwa kunywa au kupaka. Kwa kutokuzingatia suala la afya, nimewahi pia kunywa...
Wakuu nimekutana na makala moja CNN kuhusu utafiti ulioonesha kuwa Watu wanaotumia Bangi wako hatarini kupatwa na matatizo ya Shambulio la Moyo au Moyo kushindwa kufanya kazi (Heart Failure). Hii imakaaje wakati hivi karibu kumekuwa na maelezo kuwa Bangi husaidia kutibu baadhi ya Seli za Saratani?
Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia kumeibuka Application nyingi za kutengeneza picha, ambazo zinaweka kubadili muonekano wa picha kwa namna nyingi na hata kuleta sintofahamu baadaye
Upotoshaji katika picha ni kitendo Cha kuhariri (edit) picha kwa kuongeza kitu, kupunguza kitu kuwaaminisha watu kuhusu jambo fulani kutokana na muonekano mpya ulioutengeneza katika picha hiyo.
Upotoshaji wa picha huweza kufanywa kwa namna mbalimbali, zifuatazo ni namna chache kati ya nyingi:
1. Kuhariri au kutengeneza
Huu ni upotoshaji katika picha ambapo mpotoshaji hutumia utaalamu kuhariri au kutengeneza picha fulani kwa lengo la kuitoa uhalisia wake na kuifanya iwe kwa namna inayoendana na lengo lake. Picha huweza kuhaririwa kwa kubadili...
Deepfake ni aina ya ubunifu wa kidigitali unaotumia teknolojia ya Akili Bandia (AI) kubadilisha au kuunda picha, sauti na video ambazo huonekana kama ni za kweli, lakini zimeundwa kwa njia bandia. Jina "deepfake" linatokana na maneno mawili: "Deep learning" (kujifunza kwa kina), ambayo ni aina ya teknolojia ya AI inayotumika kufanya mabadiliko haya, na "Fake" (bandia).
Teknolojia hii hutumia seti kubwa ya data kuunda maudhui mapya yayofanana sana na yale yanayopatikana kwenye data za awali. Hii inaweza kumaanisha kubadilisha sura za watu kwenye video, kuingiza watu kwenye matukio ambayo hawakuhudhuria, au hata kuunda mazungumzo ya video na sauti za watu ambao hawajasema mambo hayo.
Deepfake imeleta wasiwasi mkubwa kuhusu matumizi yake...
Beki wa Simba Che Malome,siku ya tarehe 05.11.2023 wakati wanakandwa kichapo cha mbwa mwizi kutoka kwaa watani zao Yanga, alionyeshwa kadi mbili za manjano.
Kitu ambacho kilipaswa kupewa card nyekundu, lakini refa na wasaidizi wake hawakuliona hili sijui hawakuwa na kumbukumbu vizuri, Che Malome hakutoka nje kwa adhabu ile, alicheza tu.
Juzi kati, kati ya Mechi ya Simba na Namungo,Che Malome alicheza tena, Simba walimchezesha mchezaji mwenye card nyekundu kwa sababu zipi?
Bodi ya Ligi mko wapi? TFF mko wapi? Wapeni Namungo ushindi wa point tatu na magoli mawili kama kanuni inavyotamka.
Baada ya kukutana na taarifa yoyote unayoitilia shaka, kuna hatua kadhaa unaweza kuchukua ili kujiridhisha uhalali wa taarifa hiyo. Kuchukua hatua za haraka na kutoa habari sahihi ni muhimu ili kuzuia kuenea kwa habari feki au gushi.
Hizi ni baadhi ya hatua za kuchukua unapokutana na taarifa au habari unayohisi ni gushi au feki:
1. Usieneze Taarifa hiyo mpaka upate uhakika: Usiisambaze au kueneza taarifa hiyo kwa wengine kabla ya kuithibitisha kuwa ni taarifa sahihi ili kuzuia kusambaa kwa taarifa feki. Kusambaza taarifa/ habari unayoitilia shaka kunaweza kuchangia kusambaa kwa habari potofu
2. Tafuta Ukurasa wa Kukosoa au kuhakiki taarifa/habari: Kuna mashirika na tovuti zinazochambua na kukosoa habari feki, moja ya kurasa hizo ni...
Huu Muungano ni chenga kabisa una kero nyingi mno, naona kwa Zanzibar wao ni raha kwenda mbele.
Sisi wote ni Watanzania lakini ajabu Mtanganyika akienda Zanzibar endapo atahitaji kuendesha gari basi atatakiwa kuomba kibali maalum kinachotolewa na mamlaka za huko, vinginevyo utakuwa unavunja sheria.
Hili suala halijakaa sawa kabisa, sawa na lile la kulipia kodi electronics kutoka Zanzibar, au Mzanzibar kumiliki ardhi Bara wakati Mtanganyika anawekewa vikwazo mfululu kumiliki ardhi Zanzibar.
Huu Muungano ni wa kishenzi sana.
Habari Potofu ni Taarifa au Maelezo yaliyobuniwa kwa kuiga mtindo fulani ili zionekane zina ukweli au halisi. Taarifa hizi hulenga kuleta Athari fulani, kuzua Taharuki au kudanganya Umma.
Unaweza kubaini taarifa potofu kwa kufuata hatua hizi:
Tathmini (thaminisha) chanzo
Hakikisha kwamba chanzo cha habari ni halali na kinachoaminika. Unaweza kutumia vyanzo vya habari rasmi, kama vile vyombo vya habari vya kuaminika, magazeti, na tovuti za habari zenye sifa nzuri. Epuka kuchukulia kwa uzito habari kutoka kwenye vyanzo visivyojulikana au vyenye sifa ya kuzusha mambo mara kwa mara.
Kagua vyanzo vingine
Tafuta habari hiyo kwenye vyanzo vingine vyenye sifa nzuri ili kuona ikiwa habari hiyo inathibitishwa na vyanzo vingine.
Tathmini lugha...
Usambazaji wa Habari (taarifa) potofu umekuwepo kwa muda mrefu katika historia ya binadamu. Hata kabla ya teknolojia ya kisasa na mitandao ya kijamii, watu wamekuwa wakisambaza taarifa za uongo au potofu kwa njia tofauti, kama vile kupitia vyombo vya habari, mdomo, au vyanzo vingine vya habari.
Hata hivyo, katika nyakati za hivi karibuni, hasa na baada ya kuongezeka kwa matumizi ya mtandao na mitandao ya kijamii, usambazaji wa taarifa potofu umezidi kuwa suala kubwa duniani. Ulianza kuwa suala kubwa zaidi katika miaka ya hivi karibuni, na linaweza kuwa na athari kubwa kwa jamii, siasa, na masuala mengine. Kampeni za kueneza taarifa potofu zinaweza kuwa za kimkakati na kutumika kwa madhumuni mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kujenga hisia...
Tulianza na shopping mall Dodoma, sasa tena ni kiwanda cha Tumbaku. Yasemekama wahusika ni wale wale!
Ukiingia mjini Morogoro, umbali kidogo kutoka mzunguko wa Msamvu kuelekea Iringa, unakutana na daraja la reli na pembeni yake unakuta shughuli za ujenzi wa kiwanda kipya cha Tumbaku.
Eneo hili kwa miaka mingi lilieleweka ni eneo la wazi, na kwa sheria zetu za ardhi, hakuna aliye na madaraka ya kubadili matumizi ya eneo la wazi.
Wakati napitia pitia mitandaoni kutafuta style mpya kwa ajili ya shangazi yenu ndio nikakutana na hili bandiko kuwa aina ya kujamiiana huku mwanamke akiwa amemkalia mwanaume juu ('woman on top' or 'cowgirl' or 'reverse cowgirl'), hatari kwa afya ya mwanaume kwani hupelekea maumivu makali kwani hupekelea fracture ya uume kwa asilimia kubwa wakati wa kushiriki tendo la ndoa.
Inashauriwa mwanaume ndio akae juu ili kupunguza uwezekano wa kupata madhara.
Ikatokea mwanaume amemwaga manii kwenye taulo ambalo muda mchache baadae mwanamke akalitumia kukaushia uke wake.
Kuna uwezekano akapata ujauzito kupitia taulo hilo?
Salaam ndugu zangu,
Nimeona picha inasambaa ikieleza kuwa Kampuni ya Israeli ya PEPSI imebadilisha muundo wake na kuandika Palestina ili kuepuka kufungiwa na Palestina.
Kuna wazandiki huwa nawashangaa wanavyoponda pombe. Pombe haina madhara kama wanafiki wanavyotuaminisha. Pombe ni nzuri ukinywa kistaarabu, ina faida lukuki, ukibisha muulize Albert Chalamila.
Tafiti zinasema kuwa beer zinasaidia kujilinda na magonjwa ya moyo. Kama mnavyojua magonjwa ya moyo yanaondoa watu kimya kimya hivyo mimi nawashauri tunywe beer kujilinda na magonjwa ya moyo.
Hata Biblia inasisitiza tunywe pombe tufurahie, na mkituona tunakunywa pombe msitukwaze.
Too much of anything is bad, but too much good whiskey is barely enough