Kumekuwepo na chapisho lililosambazwa kwenye ukurasa wa Facebook likimnukuu mfugaji mmoja nchini Kenya akilalamikia uwepo wa zebra katika eneo lake. Mfugaji huyo anadai kuwa zebra hao wanazaliana na ng’ombe pamoja na punda wake, hali inayosababisha kuzaliwa kwa wanyama wenye madoa yanayofanana na ya zebra.
pia kupitia chapisho ambalo limechapishwa na ukurasa wa instagram wa safari podcast lina nukuu kuwa “Ninaiomba Mamlaka ya Wanyamapori ya Kenya (KWS) waje kuwachukua zebra hawa. Wamekuwa wakizaliana na ng’ombe wangu, na tayari kuna ndama aliyezaliwa akiwa na madoa kama ya zebra. Endapo hamtachukua hatua mapema, nitalazimika kuwaua zebra hao. Nawasisitiza mfike haraka kuwaondoa, kwani pia wamezaliana na punda wangu, na kusababisha...