Featured content

UDSM yailaani UDASA kwa kukosa “Maadili ya Umma”
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni taasisi ya umma, inayozingatia misingi ya kitaaluma, katiba, sheria za nchi, na maadili ya umma, na kujikita katika mijadala yenye tija kwa maendeleo endelevu na mshikamano wa kitaifa. Tunatoa wito kwa Watanzania wote wenye sifa za kisheria kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025, kwa amani, utulivu na uzalendo, tukizingatia kwamba amani ni msingi wa maendeleo, demokrasia, na ustawi wa Taifa letu. Pia soma: GE2025 - Jumuiya ya...
Japan: Takaichi achaguliwa kuwa Waziri Mkuu wa kwanza mwanamke
Sanae Takaichi kutoka chama cha Liberal Democratic Party (LDP) alishinda katika uchaguzi uliofanyika mapema Oktoba 21, 2025, ikiwa ni jaribio lake la tatu la kuwa Waziri Mkuu. Baada ya kuchaguliwa, Takaichi anatazamwa na wengi ni kwa namna gani atakabiliana na changamoto zinazojumuisha uchumi duni, uhusiano mbaya dhidi ya Marekani na mataifa mengine, lakini pia kuunganisha chama tawala ambacho kimetikiswa na kashfa pamoja na migogoro ya ndani.
Ufaransa: Rais Mstaafu Sarkozy aanza kutumikia kifungo cha miaka 5 jela
Rais wa zamani wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy (2007 – 2012), ameanza kutumikia kifungo chake cha miaka mitano gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kutafuta ufadhili wa kampeni kutoka kwa kiongozi wa zamani wa Libya, Muammar Gaddafi, katika uchaguzi ambao alishinda. Sarkozy anakuwa Rais wa kwanza wa Ufaransa kufungwa jela tangu Rais Philippe Petain ambaye alishirikiana na utawala wa Kinazi. Petain alifungwa jela baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia.
Mnyika: Kuna njama za kuwakamata Viongozi wa CHADEMA kabla ya Oktoba 29, 2025
John Mnyika (Katibu Mkuu CHADEMA) akiwa anatoa taarifa ya kukamatwa kwa John Heche (Makamu Mwenyekiti Bara) alieleza kuwa anafahamu kuna njama za kuwakamata viongozi wa chama hicho kabla ya Oktoba 29, 2025 na kuwaachia baada ya uchaguzi kufanyika kama namna ya kuondoa ushawishi wao katika zoezi la kupiga kura na kutangazwa kwa matokeo.
Wakili Gaston: Heche amepelekwa Tarime baada ya kukamatwa Mahakama Kuu
Wakili Gaston (Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu CHADEMA) amesema kuwa kwa taarifa za polisi, John Heche amesafirishwa Tarime baada ya kukamatwa Mahakama Kuu, kwani sababu za kukamatwa kwake zipo huko. Heche alikamatwa Oktoba 18, 2025 na kuwekwa kuzuizini kwa masaa kadhaa katika mpaka wa Sirari akiwa anaelekea kwenye mazishi ya Odinga, Kenya. Baadaye akiwa ameachiwa, Uhamiaji walitoa taarifa kuwa Heche alivuka mpaka huo kuingia Kenya kinyume cha sheria.
Wimbo wa Roma Mkatoliki, "Teremsha Bunduki" wafungiwa na BASATA
Wimbo wa msanii Roma Mkatoliki, "Teremsha Bunduki" wafungiwa na BASATA kwa madai ya Kupotosha, Kuchochea Ghasia, pamoja na kuwa na maneno ya Uongo na Uchochezi kulingana na Kanuni za Baraza 25 (6) (b),(c),(d). Katika wimbo huu, Roma amewataka polisi waache kupiga na kunyanyasa wananchi, waachie maandamano ya haki, akisisitiza kuwa bunduki si za kulinda mtawala anayeibia na kuteka wananchi.
Sirari: Wananchi wampambania mwenzao asitekwe!
Ni baada ya mwananchi mmoja kudaiwa amechukuliwa na "wasiojulikana" ambapo baada ya wananchi kufunga njia zote watu hao 'wasiojulikana' walikimbilia Polisi
Fahamu jinsi ya kutumia Pressure Cooker kwa usahihi ili kuepuka mlipuko
Pressure cooker ni kifaa muhimu jikoni kinachopunguza muda na kuokoa nishati kwenye baadhi ya mapishi ambayo huchukua muda mrefu kuiva. Siku za hivi karibuni matukio ya kifaa hiki kulipuka yamekuwa yakiongezeka kwa kasi huku sababu mbalimbali zikitajwa kusababisha hilo. Fahamu matumizi sahihi ya Pressure Cooker ili kuwa salama wakati wote unapoandaa mapishi yako.
Mzazi: Nilipigiwa simu kuwa mwanangu amechukuliwa na watu wasiojulikana...
Ashura Simba, mama wa Mickdady (21), anayeishi Tabata Chang'ombe, alieleza kuwa alipigiwa simu kuwa mwanaye amechukuliwa na watu wasiojulikana. Licha ya jitihada zake kumtafuta, hakufanikiwa hadi alipopokea taarifa za kupatikana kwa miili ya vijana hao wanne eneo la Mapinga, mkoani Pwani.
Heche akamatwa na kuzuiliwa Sirari akielekea Kenya kumzika Odinga
Pamoja na kumuweka kizuizini, Mamlaka ya Uhamiaji Tanzania imemnyang'anya hati yake ya kusafiria (Passport) bila kueleza kwanini wamechukua uamuzi huo.
Madagascar: Kanali Randrianirina aapishwa kuwa Rais, awashukuru waandamanaji
Randrianirina, ambaye alikuwa kamanda wa kikosi maalum cha jeshi, aliapishwa katika Ukumbi Mkuu wa Mahakama ya Katiba ya Juu, hatua iliyotamatisha mchakato wa haraka wa kuichukua madaraka ya nchi yenye wakazi takribani milioni 30 iliyoko katika Bahari ya Hindi, upande wa mashariki mwa Afrika
Cameroon: Raia waandamana, wachoma baadhi ya Majengo ya Serikali wakidai hawamtaki Rais
Wananchi wengi wamejitokeza barabarani wakipinga kile wanachokiita “uchaguzi wa wizi” na wakitaka Rais Paul Biya aondoke madarakani, wakimtaka Issa Tchiroma Bakari kutangazwa mshindi halali
Wasira: Kuna maswali kuhusu Polepole, alisema ametelekezwa Cuba halafu ghafla ikawa ametekwa Tanzania!
Wassira: Sitaki kuzungumza sana mambo ya Polepole kwasababu sasa hivi yanachunguzwa na Polisi, lakini yako maswali vilevile juu ya Polepole kwasababu, Polisi haohao walimwandikia wito aende akaandikishe kwao mambo anayo yazungumza kupitia mtandao ili wayachunguze Polepole akawaambia yeye yuko nje ya nchi...ametelekezwa Cuba alafu ghafla ametekwa Tanzania
Wamiliki wa "Online TV" zilizorusha maudhui ya Polepole wakamatwa na Polisi
Wakuu, Watu wanne waliokuwa wanamiliki akaunti za mtandao wa Youtube za Wispoti TV, T.Media Two na Costa Tv wamekamatwa kwa madai ya kuendesha akaunti hizo bila ya kuwa na leseni. Akaunti hizo ni kati ya zile zilikokuwa zikirusha press za Polepole kila alipokuwa akizitoa. Kumbuka Polepole alishawahi kusema kuwa media zimelipwa huku nyingine zikitishwa kutorusha maudhui yake. Hili limethibitika sasa, maana waliokuwa wakiendelea kurusha maudhui hayo ndio kama hawa ambao kama walishindwa...
Raila Odinga afariki dunia nchini India kwa mshtuko wa moyo
Raila Odinga (RAO) afariki dunia huko India. Amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80. R.I.P Papa. Utangulizi Raila Amolo Odinga ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri zaidi katika historia ya Kenya na Bara la Afrika kwa ujumla. Kwa zaidi ya nusu karne, amekuwa nembo ya mapambano ya demokrasia, mageuzi ya kisiasa, na haki za kijamii. Safari yake imejawa na changamoto, mafanikio na matukio makubwa ambayo yameunda sura ya siasa za Kenya. Maisha ya Awali na Elimu Raila alizaliwa tarehe 7 Januari...
Madagascar: Kikosi maalum cha Kijeshi chamwondoa Madarakani Rais Andry Rajoelina
Kikosi maalum cha Kijeshi nchini Madagascar cha 'CAPSAT' kimetangaza kuchukua madaraka, kikimwondoa madarakani Rais Andry Rajoelina, baada ya Wabunge katika Bunge la kitaifa kupiga kura ya kumwondoa, licha ya Rais Rajoelina kutangaza kulivunja kabla ya kura kupigwa.
Madagascar: Rais akimbia nchi ili kulinda maisha yake kufuatia maandamano makubwa ya kitaifa
Rais Rajoelina alitarajiwa kutoa hotuba ya televisheni Jumatatu jioni, lakini hotuba hiyo iliahirishwa baada ya “kikundi cha majeshi yenye silaha kutishia kuchukua udhibiti wa vyombo vya habari vya umma,” kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi yake kupitia Facebook.
TCRA yazuia maudhui ya Mange Kimambi kuonekana Tanzania. Waamuru Meta kufuta post zake!
Mafisadi yamejipanga Kwa njia zote. Leo wameamuru meta ambao ni wamiliki wa Instagram kushusha post zote za kuhusu ufisadi wa serikali Kwamba serikali haitaki kuona post za watoto wa fisadi Seleman Momba ambaye ndo mkurugenzi wa usalama wa Taifa wakichezea mamilion ya USD nyumbani huku wananchi wakikosa hata nafasi katika mwendokasi Serikali haitaki kuona magari ya kifahari ya Abduli Serikali haitaki kuona apartments za Abdul Haitaki wananchi waone manunuzi ya ovyo Mange anahamasisha...
Fanya hivi ili uweze kuperuzi mitandao iliyozuiwa (blocked) bila ya kudownload VPN kwenye Kompyuta yako
Ni wazi kuwa matumizi ya mtandao yameminywa sana Tanzania kwa sababu za kisiasa zinazowekwa kwenye mtazamo wa kiusalamaua na kimaadili, tumefikia kipindi mtu anahitaji kutafuta mbinu za kuweza kupata taarifa kutoka kwenye majukwaa muhimu ya habari kama X na hata sasa Baada ya kusitishwa kwa muda kwa leseni JamiiForums hasa kwa watumiaji wa Tanzania. Mamlaka zimeendambali zaidi hadi kufikia hatua ya kuzuia kuperuzi tovuti za kudownload huduma za VPN. Kwasasa Matumizi ya VPN Tanzania...
Back
Top Bottom