Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

Zomba tufafanulie tujue yapi yalimkuta bwana ZZK, naona kama uko deep sana na masuala ya CDM
 
Wewe zitto, acha kujikweza huwezi kupata huo uongozi wa cdm, acha nafasi hizo za wachaga. Uking'ang'ania yatakupata ya mh. Wangwe.
 
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Zuberi Kabwe, amesema kuwa hana nia ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama chake katika Uchaguzi wa ndani wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu.

Zitto aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na NIPASHE jijini Mbeya, alikokuwa amekwenda kuongeza nguvu katika kampeni za uchaguzi wa udiwani katika kata ya Kiwira wilayani Rungwe.

Alisema kuwa hana nia ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama hicho kwa sababu anaona timu ya sasa ya uongozi wa chama hicho inatosha na inafaa kuendelea kukiongoza kwa miaka mingine mitano ijayo.

“Sina interest (nia) na sifikirii kama nitagombea uongozi ndani ya chama katika uchaguzi wa ndani wa Chadema mwaka huu, naona timu iliyopo inatosha na inafaa kuendelea kukiongoza chama,” alisema Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini.

Alisema ingawa katika uchaguzi uliopita alijitosa kuwania nafasi ya mwenyekiti wa chama hicho, lakini safari hii nafsi yake haimtumi kufanya hivyo kwa kuwa ana imani kuwa uongozi wa sasa unastahili kuendelea kuwa madarakani kwa manufaa na maslahi ya chama na Watanzania kwa ujumla.


Chanzo: Gazeti la Nipashe

UPDATE:
Kairudia kauli hii Juni 16, 2012 akiwa Iringa (M4C)

Kibano alichokipata wakati alipotaka kugombea uwenyekiti wa CHADEMA, ndio sababu kubwa ya kukaa pembeni safari hii.

Vile vikao vya wazee havikuwa bure, bali viliambatana na vitisho vya kuhatarisha maisha yake. Hali hii iomemfanya Zitto kukiogopa sana chama chake kuliko hata watanzania au hata CCM kAMA WENGI WANAVYOFIKIRI.

Huo ni uamuzi wa Busara, kwani hawa watu wa CHADEMA hawajali maendeleo, hata hivyo usingepata hata kama ungegombea mkwani dDHAMBI YAKO NI KUWA HUKUZALIWA KILIMANJARO/ARUSHA.
 
Bora aache kugombea maana uhusiano wa Zitto na Jack Zoka ni habari mbaya kwa wapambanaji. Uhusiano kati ya Zitto na Jack Zoka ambao uliwekwa wazi na vyombo mbalimbali ni taarifa mbaya kwa wanasiasa na wananchi wanaoipenda taifa lao la Tanzania. Uhusiano huu wa Zitto na Jack Zoka ambaye ni mkurugenzi msaidizi wa TISS (usalama wa taifa) umeripitiwa kuwa na historia ndefu tangu wakati wa uchaguzi mkuu. Wakati Zitto anajitapa kuwa anatetea maslahi ya wananchi, mshirika wake wa chanda na pete Jack Zoka anatuhumiwa na wanasiasa na wanachi kufanya kazi ya kuwadhuru badala ya kulilinda taifa. Kama mshirika wa Zitto anadhuru wananchi ni wazi kuwa naye Zitto ana masalahi binafsi na mabaya kwa wananchi. Maana ukitaka kujua tabia ya mtu, uliza tabia ya rafiki yake. Ni jambo la kusikitisha Zitto kuwa na uhusiano na huyu mfanyakazi wa usalama wa taifa anayedhuru watu na wakati huohuo anajidai kuwa ni mpambanaji. Uhusiano wa Zitto na Jack Zoka ulishawekwa wazi kuwa walikuwa wanawasiliana kwa simu mara kwa mara wakati wa kipindi cha uchaguzi. Tuwe macho na urafiki wao na ambao si mwema hata kidogo kwa wanasiana na wananchi wenye uchungu na taifa letu.
 
Zitto kwanini analazimisha umaarufu huu wa kisiasa kila tukiamka zitto zitto..............
 
Wana JF wenye mapenzi mema kwa CHADEMA, nadhani ni muda muafaka sasa kuanza kutoa maoni kuhusu chama chetu hasa uongozi wake maana uongozi ujao ndio utatupa serikali 2015. kwanza nimpongeze sana Mbowe kwa kweli ameonyesha ujasiri mkubwa na ameongoza chama kwa ujasiri na ukakamavu mkubwa.

Huwezi kuitaja chadema ya leo bila kumtaja Mbowe. Baada ya kazi kubwa na ili kuonyesha chadema kina watu wazuri wengi wanaoweza kuongoza, ningeshauri tu asigombee tena akae pembeni ila abaki kwenye vikao muhimu vya chama.

Nashauri Dr Slaa sasa angeandaliwa kuwa Chairman, Zitto Kabwe awe makamu Bara, atafutwe katibu mkuu msomi mzuri ambaye anaweza kuratibu shughuli za chama kisomi, Naibu katibu pia awe msomi mzuri, tuwe na graduates makatibu wa kila jimbo la uchaguzi ambapo kazi zao itakuwa kufanya uratibu wa chama, hope chadema tutakuwa tumepiga hatua zaidi towards state house. Ni maoni tu. Peoplessssssssssssss Powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Wana JF wenye mapenzi mema kwa chadema, nadhani ni muda muafaka sasa kuanza kutoa maoni kuhusu chama chetu hasa uongozi wake maana uongozi ujao ndio utatupa serikali 2015. kwanza nimpongeze sana Mbowe kwa kweli ameonyesha ujasiri mkubwa na ameongoza chama kwa ujasiri na ukakamavu mkubwa. Huwezi kuitaja chadema ya leo bila kumtaja Mbowe. Baada ya kazi kubwa na ili kuonyesha chadema kina watu wazuri wengi wanaoweza kuongoza, ningeshauri tu asigombee tena akae pembeni ila abaki kwenye vikao muhimu vya chama.

Nashauri Dr Slaa sasa angeandaliwa kuwa Chairman, Zitto Kabwe awe makamu Bara, atafutwe katibu mkuu msomi mzuri ambaye anaweza kuratibu shughuli za chama kisomi, Naibu katibu pia awe msomi mzuri, tuwe na graduates makatibu wa kila jimbo la uchaguzi ambapo kazi zao itakuwa kufanya uratibu wa chama, hope chadema tutakuwa tumepiga hatua zaidi towards state house. Ni maoni tu. Peoplessssssssssssss Powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
Una matatizo mkubwa weye!
Mbowe aondoke?
Halafu chama amwachie nani?
 
Una matatizo mkubwa weye!
Mbowe aondoke?
Halafu chama amwachie nani?
Unataka kutuambia kuwa Mbowe pekee ndie anaweza ndani ya Chadema? Chadema ni chama kikubwa kwa sasa nadhani tutakuwa tunaonyesha njia kama tukiendelea na utaratibu wetu wa kubadilishana kijiti hata kama tuna kiongozi imara kama Mbowe. Nyerere alikuwa kiongozo shupavu ila alifika mahali akaonyesha ukomavu wa kisiasa akang'atuka
 
Mbowe bado ni mtu muhimu sana kwa nafas ya mwenyekiti,slaa ni muhimu kwa ukatibu mkuu,labda zito ndo anapwaya,hajishughulishi kabisa na chama.
 
Maoni yako ni feki, Mbowe elimu alonayo inatosha kabisa kuongoza CDM,wewe yaonyesha humjui Mbowe na CDM. Mbowe ni shupavu, mzalendo, mwaminifu, mhamasishaji na mtu wa watu. Ana umri wa miaka 51 akae pembeni kwa lipi?
 
Slaa hana vigezo vya kuwa Mwenyekiti, kwakuwa si mchaga. Zitto nae pia hana vigezo kwakuwa si wa Kaskazini, si mchaga, na ni muislamu. Labda Selasini au Lema.
 
Maoni yako ni feki, Mbowe elimu alonayo inatosha kabisa kuongoza CDM,wewe yaonyesha humjui Mbowe na CDM. Mbowe ni shupavu, mzalendo, mwaminifu, mhamasishaji na mtu wa watu. Ana umri wa miaka 51 akae pembeni kwa lipi?

Mbowe ana ushupavu wa kuchangisha wananchi vijisenti vyao.
 
Back
Top Bottom