Zitto: Serikali iache kutafuta mchawi, iende Mtwara!

Zitto: Serikali iache kutafuta mchawi, iende Mtwara!

Au watu wangeweza kupigana kwenzi kupitia screen za vipakatwa au tarakirishi wengi wangesha badili vioo maana vingi vingekuwa na nyufa kwa kupigana. Nilicho gundua wengi hawana uvumilivu wa kumeng'eya hoja na kuibomoa hoja kwa hoja! Ni mihemko kwa kwenda mbele! Lol

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Ndio binadamu utakao waongoza ukipewa nafasi,ni wepesi kusifia na ni wepesi sana kulaumu,hawakiwii kusema "mtoto wangu kaenda choo na wala serikali haionekani kuja kumpangusa mwanangu"
 
wakwenda lumumba mimi or ww,nahs nilizaliwa kwa ajili ya chadema na ntafia chadema,mimi sio chadema ya 2010 kama wewe unaejifanya una uchungu na chama,kumbe mnafki na mchonganishi wa siasa,hujatupata bdo ebu 2jalibu tena bdae@pompo wewe

nimekubali pompo ni kihiyo
 
Ngoja tusubiri na tamko la kamati kuu ya chaddema halafu tulinganishe kati ya tamko la kamanda Zitto na la kamati kuu lipi liko vizuri...
luceifel or satan you must be witch how and why lets wait and see if you will increase any political credits gosh what a surpent
 
hahahahaha!mkuu tatizo lake yeye mwenyewe hajitambui kama ni kihiyo,
kaka
kama pompo ndio mpiga debe aliyeteuliwa na chama,basi wamechagua mtu atakayekiangamiza chama kwa maneno na kauri asizozielewa,pompo moja hakai wala mbili hasimami,haelewi anachokiongea,anameza maneno na kuyatafuna baada ya hapo anatapika asichokula.
propaganda zake ni pofu,hazina macho,zinagonga/zinapasuwa/zinaharibu hata chama kilichompa kazi ya propaganda ,hahahahahahaha
 
Binafsi sioni mantiki ya huyu Mheshimiwa kuzungumza kwa leo halafu kesho Mkiti wake Mbowe atoe tamko la Kamati kuu kuongelea kitu hicho hicho.

Huo ni ushauri wangu tu lakini

Mimi Zitto hanishangazi yule yupo miguu yote miwili CCM pale CHADEMA yupo kikazi zaidi, kuhakikisha anakivuruga. Haiwezekani kiongozi wa Chama kutoa tamko ilihali Chama kinajiandaa kutoa Tamko, lakini nionavyo mimi Zitto asipoangalia anachokifanya kitamghalimu sana tuendako kwasababu mbinu za fitna zilishapitwa na wakati kabisa katika Modern politics.
 
Japo namkubali sana ZZK, .............................. ila ZZK anakabiliwa na tatizo kubwa la "ego" linalompelekea kuwa na papara hivyo kum pre empty hata M/Kiti wake!.

......................... mlipaswa kumuita ZZK awape full disclosure ya kila anachokijua kufuatia yeye kuwa ndiye Mwenyekiti wa POAC ambapo TPDC iko chini yake!.
..............................mnaamini kuwa ZZK is working in favor of CCM, the time will come, mtawajua wanaoifanyia kazi haswa CCM miongoni mwenu na hamtaamini!.
Pasco.

Pasco bana!!!!!!!!! Hii siitofautishi na wamama wavumilivu katika ndoa
 
Hata wewe ikikuuma katoa tamko lako, chama kitu gani ebo!!
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), amemtaka Rais Jakaya Kikwete aende Mtwara ili kusikiliza malalamiko ya wananchi katika sakata la gesi asili badala ya kuendeleza malumbano ya kumtafuta mchawi.

Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA (Bara) na Waziri Kivuli wa Fedha, alisema kuwa kama serikali haitashughulikia suala la Mtwara sasa, yatajitokeza matatizo ya aina hiyo katika mikoa mingine yenye rasilimali zisizonufaisha wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Zitto alisema kuwa, hapa nchi ilipofika ni lazima kwanza kusikiliza kilio cha wananchi wa Mtwara ikiwemo kuelewa madai yao.
"Swali kubwa la watu wa Mtwara na Kusini kwa ujumla ni ‘tunanufaikaje?' Jibu la swali hili si ahadi za miradi, bali ni vitendo. Hapa ndipo serikali inaposhindwa kushughulikia suala hili, kutoelewa madai ya wananchi na kuyapotosha," alisema.

Zitto aliongeza kuwa, yafaa viongozi wa kisiasa wenye ushawishi kutoka pande zote, chama tawala na vyama vya upinzani, waende Mtwara kuzungumza na wananchi, lakini wawasikilize kwanza.

Alibainisha kuwa mradi huu wa kutandaza bomba la urefu wa kilometa 542 ni mkubwa sana hapa nchini, na una thamani kubwa zaidi kuliko miradi mingine yote ya miundombinu iliyopata kutokea.
Mradi huu utajengwa kwa mkopo wa dola za Kimarekani 1.2 bilioni kutoka Benki ya Exim ya China.
Alisema kuwa wananchi wa Mtwara kupitia maandamano ya Desemba 27 mwaka jana, wametaka kujua hatma ya maendeleo ya mikoa ya kusini kutokana na mradi huu wa bomba la gesi.
"Serikali imewajibu wananchi hawa kwa kuwaita wahaini, watu hatari na wasioelewa. Imefika mahali inapotosha madai yao kwamba hawataki gesi itoke Mtwara," alisema.
Katika hilo, Zitto alisema Rais Kikwete ana majibu, hivyo ayatoe sasa kwa wana Mtwara. Kwamba kwa mujibu wa mpango kabambe wa umeme nchini (Power System Master Plan), kulikuwa na mradi wa kufua umeme Mnazi Bay, ambao aliagiza utekelezwe mara moja.

Alisema kuwa serikali ieleze umma kuhusu mradi huo wa kujenga kituo cha kufua umeme 300MW Mnazi Bay, Mtwara na kujenga msongo wa umeme wa 300KV mpaka Singida umeishia wapi?
"Ikumbukwe kuwa Oktoba 12 mwaka jana, Rais Kikwete alipokea ripoti ya ujenzi wa mradi huu kutoka makampuni ya China National Machinery & Equipment Import & Export Corporation (CMEC) ya China na Siemens ya Ujerumani, ambayo kwa pamoja yalitarajia kujenga kituo kikubwa cha kuzalisha umeme kutokana na gesi katika eneo la Mnazi Bay, mjini Mtwara," alisema.

Zitto aliongeza kuwa, mradi huo ingehusisha kujenga njia ya kusafirisha umeme ya kilomita 1,100 kutoka Mtwara hadi Singida na ungegharimu dola za Kimarekani milioni 684 na kwamba rais aliagiza utekelezwe haraka sana.
"Huu mradi uliishia wapi? Kwa nini serikali ipo kimya kuhusu mradi huu ambao ungejibu kabisa maswali ya watu wa Mtwara?" alihoji.

Zitto alimsifu Rais mstaafu Benjamin Mkapa, akisema ameshatoa kauli kuhusu suala hilo, na kwamba ni wakati muafaka sasa kwa viongozi wengine kumuunga mkono kwa kwenda Mtwara na kukaa na wananchi wa wilaya zote kusikiliza hoja zao na kuona namna ya kupata ufumbuzi wa suala hilo.
Alisema wakati hatua hiyo inachukuliwa, wananchi waombwe kutulia na kuacha vurugu za aina yoyote ile, na serikali isimamishe mradi mpaka hapo suluhu na wananchi itakapopatikana.

"Serikali iweke wazi mkataba wa ujenzi wa bomba, kwani ni dhahiri gharama za mradi huu ni kubwa mno kulingana na uhalisia wa miradi ya namna hii duniani kote. Katika taarifa zote kwa umma serikali imekuwa ikisema kwamba utagharimu jumla ya dola za Kimarekani 1.2 bilioni," alisema.
Aliongeza kuwa, katika taarifa ya Wizara ya Nishati na Madini, iliyotolewa na George Simbachawene kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini juzi, ilisema mradi utagharimu dola za Kimarekani milioni 875. Kwamba usiri katika mkataba huu unaashiria kwamba serikali inaficha kitu.

Zitto alisema kuwa amelazimika kutoa ufafanuzi huo wakati chama chake kikiandaa tamko, kwa lengo la kujibu kile alichokiita uzushi wa Simbachawene alioutoa kwa wahariri, kwamba yeye anachochea wananchi wa Mtwara na kutumika bila uzalendo.
"Vile vile alitoa vielelezo kadhaa kuonyesha kuwa mradi wa kujenga bomba la gesi ni gharama sawa sawa. Akasisitiza kwamba mimi ni mwongo. Katika kipindi chote cha mgogoro wa gesi Mtwara, sijafika Mtwara. Sijafanya mkutano wowote na waandishi zaidi ya kuandika mawazo yangu, kama Mtanzania kuhusu suala hili," alisema.

Zitto alisema hataki kubishana na naibu waziri huyo ama kiongozi yeyote ya serikali kwa sasa wakati nchi yetu inaungua. Kwamba huu sio wakati wa kutafuta mchawi bali kutafuta majawabu ya changamoto zilizopo mbele yao.

Mtikila anena

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (DP), Christopher Mtikila, amemtaka Rais Kikwete kutumia hekima katika kumaliza mgogoro wa gesi na maslahi ya Mtwara kinyume chake nchi inaweza kugawanyika.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mtikila alisema kuwa madai ya kwamba umeme wa gesi hiyo ufuliwe kulekule Kusini yanatokana na uchungu wa wananchi wote wa Kusini.

Alisema iwapo moto wa mgogoro huo hautauzimwa kwa hekima, si ajabu ukaimeza mikoa yote ya Kusini ikiwemo Lindi, Ruvuma, Mbeya, Iringa, Morogoro na hata Rukwa ambapo matokeo yake ni kuzaliwa mataifa mawili mpaka ukiwa reli ya kati.

Mtikila alisema wakazi wa Kusini hawazuii gesi hiyo isitoke bali wanachotaka umeme huo ufuliwe kule kule, lengo likiwa ni kuwaletea mapinduzi ya maendeleo.

"Wananchi wa Mtwara wanafahamu kwamba sumaku ya mandeleo ya uwekezaji wa miradi mikubwa ya kuwaletea maendeleo ni nishati na miundombinu, lakini watawala wa CCM waliwanyang'anya reli ya kusini kwa uharamia wa kung'oa mpaka mataruma na kufutilia mbali hata na tuta lenyewe," alisema.

Aliongeza kuwa Rais Kikwete analazimika pia kutamka bayana kipaumbele kwa uboreshaji wa bandari kuu ya Mtwara, ikibidi hata kwa kusitisha mradi wa bandari ya Bagamoyo.
Kwamba njia pkee ya kuzima moto huo Kusini na kurejesha amani ni rais huyo kutoa tamko la kukubali kufuliwa umeme huo mkoani Mtwara kwa ajili ya maslahi ya taifa.



[TD="bgcolor: #ffffff"]

[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #FFFFFF, align: center"][/TD]
 
Kiwanda cha Migebuka mbona kipo Congo wakati sehem kubwa ya wanavuliwa upande wa Tz, Bandari ya nchi kavu kupeleka mizigo burundi,Rwanda na congo imejengwa Shinyanga badala ya Kigoma ambapo ndo mpakani,wafanyakaz wengi wa Kambi za wakimbiz wametoka uchagani na karagwe badala ya kigoma.Zitto apiganie hayo Wamakonde wanajimudu kujitetea na kuzungumza na Jk hawatak/ hawahitajii madalali!
 
Kiwanda cha Migebuka mbona kipo Congo wakati sehem kubwa ya wanavuliwa upande wa Tz, Bandari ya nchi kavu kupeleka mizigo burundi,Rwanda na congo imejengwa Shinyanga badala ya Kigoma ambapo ndo mpakani,wafanyakaz wengi wa Kambi za wakimbiz wametoka uchagani na karagwe badala ya kigoma.Zitto apiganie hayo Wamakonde wanajimudu kujitetea na kuzungumza na Jk hawatak/ hawahitajii madalali!
Kumbushia Buzwagi, Jamaa atatoka nduki kweli kwani huo ni msumari wake. Aliianzisha sijui ilifia wapi!
 
Hapo ndipo tunapokosea watanzania. Hii tabia ya kila kitu lazima mwanasiasa azungumze itatuletea matatizo. mimi naamini Ndugu Zitto hata Ohms law hajui ku state, sasa atawezaje kutuambia namna ambavyo gas itazalisha umeme.

Si ndio hapo mkuu, hata mimi simuelewi kabisa!!! Uzalendo gani wa kishinikiza Serikali eti isimamishe mradi huu muhimu iende kuomba ridhaa kwa wananchi?? Kwani Serikali inachaguliwa na wananchi ili ifanye nini?? - Kuna haja gani ya kushikiza Serikali ili ionekane hajiamini katika mahamuzi yake, kila saa inakuwa held at ransom na raia wachache ambao hawaeleweki vizuri nia zao, hasa ili la kusafirisha GESI kuja DAR kwani lina tatizo gani mpaka kufikia hutua ya kuitangazia DUNIA kwamba Watanzania ni watu wenye hulka za vurumai mambo ya kusema ni nchi yenye amani na utulivi ni hadaa tu - wakati hiyo si kweli.

Kusafirisha gesi kuja kufua umeme DSM ndio iwe nongwa ya kukwamisha mradi mzima na kuwatisha Wachina - tukijitia wajuaji watakwenda kuwekeza nchi nyingine ambazo ziko serious - Kenya kwa mfano, hivi tunalitakia mema Taifa letu kweli? Tumekwisha elezwa kiufundi kwa nini ni hasara kufua umeme Mtwara na kusafirisha kuja DSM, ndio maana wameona ni afadhali wasafirishe GAS na kufua umeme hapa hapa DSM with minimum loss - mtu yeyote mwenye uelewa wa nyanja ya usafirishaji wa umeme analijuwa hilo, mwenzangu kazungumzia OHMS LAW kama utani lakini hilo ndio sababu halisi kuhusu uzalishai,usafirishaji na usambazani wa umeme - kwa nini watu wamepania kupindisha mambo!


Gesi inayo safirishwa kuja DAR ni fraction tu ya azina kubwa ya GESI iliyopo Mtwara which means bulky ya GESI itabaki Mtwara kwa ajili ya kuanzisha viwanda vya Mbolea na Saruji nk na nyingine kuisafirisha kwa bomba kwenda nchi jirani, nyingine itasafirishwa kwa njia ya meli kwenda nchi za nje ikitokea huko huko Mtwara - actually kanda ya kusini specifically Mtwara itanufahika zaidi na GESI hii - kwani hilo wanasiasa awalijuhi, mkikaa chini mkawaelimisha wananchi wa kanda ya kusini watashindwa kweli kuwaelewa????


Hizi chochoko za chini chini kupinga WACHINA kusafirisha gesi kuja DAR zilianzishwa na Kampuni shindani ya kizungu inayo safirisha Gesi kutoka Kilwa kuja hapa DAR, mbona wenyewe walipo weka bomba la kusafirisha GESI kuja DAR hakuna mtu yeyote kutoka kanda ya kusini/wanasiasa walio pinga mradi huo wa Wazungu - kunani HAPO!

Mradi mzima unakomaliwa/kupingwa na World Bank, baadhi ya raia na NGOs, wafadhili wa Bajeti ya Taifa ambao wote ni wazungu walikua na nia ya kuwakingia kifua wazungu wenzao waendelee kutunyonya na kuifilisi TANESCO alafu baadae ndio wajikite katika kuzalisha,kusafirisha na kusambaza umeme NCHINI, hilo amlioni/? Kama tungekopa kutoka kwa nchi za magharibi mkopo ungechukua muda gani kuwa approved, Project nzima ingegharimu kiasi gani na kwa masharti gani? Kwanza nchi ya magharibi uchumi wao sio mzuri sana wanakwenda kukopa kwa Wachina hao hao sisi tukifanya hivyo wao wanaona tumefanya makosa.

Tuwe wakweli hapa nchi za magharibi zimepania kupiga vita Wachina kiuchumi by overt/covert means hasa hasa barani Africa, hili la ku-dramatise sakata hili la MTWARA ni moja ya mbinu zao - don't underrate resolve za nchi za magharibi, nimekaa nao nawajuwa vizuri - wana mbinu nyingi SANA!


Mimi ningeshauri mradi uendelee bila ya kuleta mizengwe au kuwekewa spana kwa visingizio mbali mabli, tusitake kuwakwamisha Wachina ambao tunawategemea kwa mambo mengi, kama kuna ujanja ujanja fulani umefanyika katika mradi mzima ni rahisi kuwatia mbaroni wahusika wakuu, kwa kuwa gharama ni rahisi kuzibainisha kuna takwimu za ku-compare na ku-contrast, vile vile Serikali ya Wachina hawana mchezo na mtu yeyote mla rushwa - kwa nini tuwe na wasi wasi, kama kutakuwa na ushahidi kwamba wame-inflate gharama za ujenzi, basi itakuwa rahisi kurudishiwa hela zetu za ziada - mbona BEA imerudisha fedha zilizo zidi katika ununuzi wa RADA, haya ni mambo yanayo zungumzika - after all Wachina ndio wanagharimia Project nzima baada ya kutukabidhi tuna haki ya kupitia kila kitu na kurekebisha walipo tuzidi akili, lakini watu hapa wanakomalia jambo hili kana kwamba ndio mwisho wa DUNIA, tumeingiliwa nini Watanzania WENZANGU.
 
zitto.jpg

Mh Zitto Kabwe Mbunge wa Kikoma Kaskazini


Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu hali ya vurugu zinazoendelea Mtwara katika sakata la mradi wa gesi asilia kuja Dar es Salaam. Picha na Venance Nestory
Na Boniface Meena na Aidan Mhando (email the author)

Posted Jumatatu,Januari28 2013 saa 9:0 AM
Kwa ufupi
“Mradi huu ungegharimu Dola za Marekani 684 na Rais aliagiza utekelezwe haraka. Huu mradi haijulikani umeishia wapi? Kwa nini Serikali ipo kimya katika mradi huu ambao ungejibu kabisa maswali ya watu wa Mtwara?


SHARE THIS STORY

0
inShare​







MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amesema kuwa majibu ya tatizo la wananchi wa Mtwara analo Rais Jakaya Kikwete hivyo ni muhimu akarudi nchini mapema na kuyatoa majibu hayo.

Wakati Zitto akisema hayo, Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila amesema njia pekee ya kumaliza mgogoro huo unaondelea ni Rais Kikwete kutoa tamko la kukubali kufuliwa umeme katika Mikoa ya Kusini.

Katika kipindi cha wiki nne sasa kumekuwa na maandamano, malumbano na vurugu kuhusu mradi wa kujenga bomba la kusafirishia gesi asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam kutokana na wananchi wa Mtwara kutaka kujua ujenzi huo utawanufaisha vipi.

Akizungumzia hali hiyo, Zitto alisema ni muhimu Rais Kikwete akaeleza baada ya kuagiza kufufuliwa kwa mradi wa kufua umeme wa Mnazi Bay utekelezwe mara moja.

“Serikali ieleze umma kuhusu mradi huo wa kujenga kituo cha kufua umeme megawati 300 eneo la Mnazi Bay Mtwara na kujenga msongo wa umeme wa 300KV mpaka Singida umeishia wapi,” alisema Zitto na kuongeza;
“Mradi huu ungegharimu Dola za Marekani 684 na Rais aliagiza utekelezwe haraka. Huu mradi haijulikani umeishia wapi? Kwa nini Serikali ipo kimya katika mradi huu ambao ungejibu kabisa maswali ya watu wa Mtwara?

Alisema ni muhimu Rais Kikwete akarudi kutoka huko aliko ili kuwapa majibu hayo wananchi wa Mtwara ambao wamekuwa wakiandamana kutaka kujua hatma yao.

Zitto alisema kwa hali ilivyofikia ni muhimu vilio vya wananchi wa Mtwara wakasikilizwa na madai yao kueleweka na majibu ya maswali yao yasiwe ni ahadi bali vitendo.

Kwa upande wake, Mtikila alisema Rais Kikwete analazimika kutamka bayana kipaumbele kwa uboreshaji wa Bandari kuu ya Mtwara, ikibidi hata kwa kusitisha mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo.

“Tunatoa tahadhari kwamba hali inayoendelea kuwa mbaya huko Kusini inazidishwa na ukosefu mkubwa wa uzalendo na hekima katika utawala wa CCM,” alisema Mtikila.

Mtikila alibainisha kwamba ni vyema ikaeleweka kwamba madai ya umeme wa gesi ufufuliwe Kusini yanatokana na uchungu wa wananchi wote wa Kusini mwa Tanganyika ‘Mtwara Corridor’.

“Kitu cha msingi kinachotakiwa kufanyika ni kuwasikiliza watu wa Mtwara wanataka nini lakini, siyo kutumia nguvu katika maamuzi (uamuzi) ya kutafuta ufumbuzi wa suala hilo la gesi kwani kufanya hivyo ni kuzidi kuwaongezea uchungu Wanamtwara,” alisema

BONYEZA WEB HII
MICHUZI: MASASI YAZIDI KUCHAFUKA,WATU SABA WADAIWA KUPOTEZA MAISHA
 
Si ndio hapo mkuu, hata mimi simuelewi kabisa!!! Uzalendo gani wa kishinikiza Serikali eti isimamishe mradi huu muhimu iende kuomba ridhaa kwa wananchi?? Kwani Serikali inachaguliwa na wananchi ili ifanye nini - Kuna haja gani ya kuwa na Serikali ambayo ajiamini katika mahamuzi yake, kila saa inakuwa held at ransom na raia wachache ambao hawaeleweki vizuri nia zao ??Kusafirisha gesi kuja kufua umeme DSM ndio iwe nongwa ya kukwamisha mradi mzima na kuwatisha Wachina - tukijitia wajuaji watakwenda kuwekeza nchi nyingine ambazo ziko serious - Kenya kwa mfano, hivi tunalitakia mema Taifa letu kweli? Tumekwisha elezwa kiufundi kwa nini ni hasara kufua umeme Mtwara na kusafirisha kuja DSM, ndio maana wameona ni afadhali wasafirishe GAS na kufua umeme hapa hapa DSM with minimum loss - mtu yeyote mwenye uelewa wa nyanja ya usafirishaji wa umeme analijuwa hilo, mwenzangu kazungumzia OHMS LAW kama utani lakini hilo ndio sababu halisi kuhusu uzalishai,usafirishaji na usambazani wa umeme - kwa nini watu wamepania kupindisha mambo!Gesi inayo safirishwa kuja DAR ni fraction tu ya azina ya kubwa ya GESI iliyopo Mtwara which means bulky ya GESI itabaki Mtwara kwa ajili ya kuanzisha viwanda vya Mbolea na Saruji nk na nyingine kuisafirisha kwa bomba kwenda nchi jirani, nyingine itasafirishwa kwa njia ya meli kwenda nchi za nje ikitokea huko huko Mtwara - actually kanda ya kusini specifically Mtwara itanufahika zaidi na GESI hii - kwani hilo wanasiasa awalijuhi, mkikaa chini mkawaelimisha wananchi wa kanda ya kusini watashindwa kweli kuwaelewa???? Hizi chochoko za Kupinga WACHINA kusafirisha gesi kuja DAR zilianzishwa na Kampuni shindani ya kizungu inayo safirisha Gesi kutoka Kilwa kuja hapa DAR, mbona wenyewe walipo weka bomba la kusafirisha GESI kuja DAR hakuna mtu yeyote kutoka kanda ya kusini/wanasiasa walioyepinga mradi huo wa Wazungu - kunani HAPO! Mradi mzima unakomaliwa/kupingwa na World Bank, wafadhili wa Bajeti ya Taifa ambao wote ni wazungu walikua na nia ya kuwakingia kifua wazungu wenzao waendelee kutunyonya na kuifilisi TANESCO alafu baadae ndio wajikite katika kuzalisha,kusafirisha na kusambaza umeme NCHINI hilo amlioni? Kama tungekopa kutoka kwa nchi za magharibi mkopo ungechukua muda gani kuwa approved, Project nzima ingegharimu kiasi gani na kwa masharti gani? Kwanza nchi ya magharibi uchumi wao sio mzuri sana wanakwenda kukopa kwa Wachina hao hao sisi tukifanya hivyo wao wanaona tumefanya makosa.Tuwe wakweli hapa nchi za magharibi zimepania kupiga vita wachina kiuchumi by overt/covert means, hili la ku-dramatise sakata hili la MTWARA ni moja ya mbinu zao - don't underrate resolve za nchi za magharibi, nimekaa nao nawajuwa vizuri - wana mbinu nyingi SANA!Mimi ningeshauri mradi uendelee bila ya kuleta mizengwe, tusitake kuwakwamisha Wachina ambao tunawategemea kwa mambo mengi, kama kuna ujanja ujanja fulani umefanyika katika mradi huo ni rahisi kuwatia mbaroni wahusika wakuu, kwa kuwa gharama ni rahisi kuzibainisha kuna takwimu za ku-compare na ku-contrast, vile vile Serikali ya Wachina hawana mchezo na mtu yeyote mla rushwa - kwa nini tuwe na wasi wasi, kama kutakuwa na ushahidi kwamba wame-inflate gharama za ujenzi, basi itakuwa rahisi kurudishiwa hela zetu za ziada - mbona BEA imerudisha fedha zilizo zidi katika ununuzi wa RADA, haya ni mambo yanayo zungumzika - after all Wachina ndio wanagharimia Project nzima baada ya kutukabidhi tuna haki ya kupitia kila kitu na kurekebisha walipo tuzidi akili, lakini watu hapa wanakomalia jambo hili kana kwamba ndio mwisho wa DUNIA, tumeingiliwa nini Watanzania WENZANGU.

Adui mkubwa wa Mtanzania na Mwafrika kwa ujumla ni ma -elite wake, ndio wanaoiuza na kuingamiza Tanzania na Afrika kwa ujumla wake, Bw. Zito Kabwe anaelewa kabisa hayo yote uliyoyaandika hapo juu kwa maana yuko ndani ya mfumo mzima, kama kweli Bw. Zito anawajali wananchi wa Kusini kihivyo mbona haongelei au hata kuongoza maandamo kupinga Bomba la Songosongo? Kwa maana kama kuna unyonyaji wa Mtanzania ni kwenye huo mradi lakini hasemi kitu.

Kwa kifupi nchi yetu itatuchukua hata miaka 200 kuja tu kuanza kujitambua achilia mbali maendeleo, na tatizo kubwa ni ma-elite wetu, na haya yananikumbusha kitabu cha Mnigeria nafikiri ni Chinua Achebe kuhusu jamaa aliyesomeshwa na kijiji chake akapelekwa mpaka Ulaya lengo likiwa ni kwamba akirudi aje ashirikiane nao kwenye maendeleo, jamaa alivyorudi kadadilika kabisa na wale wanakijiji waliomtuma akaanza kuwaona hawajastaarabika na washamba, yeye ni full suti na kuvifinjari na wazungu kwenye mji mkuu, bila pia kujua hao wazungu akiwapa tu mgongo wanamuona sokwe tu!

 
Adui mkubwa wa Mtanzania na Mwafrika kwa ujumla ni ma -elite wake, ndio wanaoiuza na kuingamiza Tanzania na Afrika kwa ujumla wake, Bw. Zito Kabwe anaelewa kabisa hayo yote uliyoyaandika hapo juu kwa maana yuko ndani ya mfumo mzima, kama kweli Bw. Zito anawajali wananchi wa Kusini kihivyo mbona haongelei au hata kuongoza maandamo kupinga Bomba la Songosongo? Kwa maana kama kuna unyonyaji wa Mtanzania ni kwenye huo mradi lakini hasemi kitu.Kwa kifupi nchi yetu itatuchukua hata miaka 200 kuja tu kuanza kujitambua achilia mbali maendeleo, na tatizo kubwa ni ma-elite wetu, na haya yananikumbusha kitabu cha Mnigeria nafikiri ni Chinua Achebe kuhusu jamaa aliyesomeshwa na kijiji chake akapelekwa mpaka Ulaya lengo likiwa ni kwamba akirudi aje ashirikiane nao kwenye maendeleo, jamaa alivyorudi kadadilika kabisa na wale wanakijiji waliomtuma akaanza kuwaona hawajastaarabika na washamba, yeye ni full suti na kuvifinjari na wazungu kwenye mji mkuu, bila pia kujua hao wazungu akiwapa tu mgongo wanamuona sokwe tu!

Mkuu Kijakazi sijuhi nikushukuru kivipi! Yaani hata mimi nilikuwa nafikilia kitabu hicho hicho cha Chinua - Siku moja marehemu Samora aliwahi kusema kwamba watu wa kuogapwa sana si Wareno (wakoloni) watu hatari ni Waswahili wenzetu wanao tumiwa na Wareno hao ni rahisi kuwashawishi Waswahili wenzao ku-revort na kuipa wakati mgumu Uongozi ulipo madarakani, Samora alikuwa sahihi kabisa!


Swala la kusafirisha gesi kuja Dar linaeleweka vizuri tu na halina tatizo lolote - cha kusikitisha kuna baadhi ya raia tena wasomi wenye uelewa mkubwa wanajaribu kupindisha mambo kimaksudi, sijui rohoni mwao wanakuwa na mawazo gani au wanataka ku-achieve kitu gani eventually; mpaka najiuliza maswali mengi: Hivi jamaa hawa hawajuhi kwamba kuna Watanzania wengi tu wenye a rasor sharp analytical minds za kuweza kung'amua kinacho jili, mimi nimekwisha kutana na Watanzania ambao wengine wao wameishia shule za msingi lakini wana akili za kuchambanua mambo kwa ufundi sana.

Sasa raia wenye uelewa mkubwa wa kuchambanua mambo wengelezwa ukweli wa mradi wenyewe si ingekuwa raisi kuwaelimisha wenzao ili waone mradi actually utawanufaisha wao zaidi kuliko mikoa mingine - hilo alikufanyika! Badala yake wanawaletea raia horror stories za kuwafanya raia wafikilie Serikali haiwajali - hii nini maanake; nashukuru Mungu kwamba kuna watu humu walisha ling'amua hilo, hata posts zenyewe zinaonyesha hivyo, Watanzania wenzagu inapokuja miradi ya kunufaisha Taifa letu tushikamane tusahau kwa muda mambo ya itikadi za vyama - tusipo kuwa makini majirani zetu watatuacha mbali kimaendekeo; watashirikiana na Wachina kikamilifu sisi tubakie na ngojera zetu zisizo na TIJA.
 
  • Thanks
Reactions: JGG
Zitto Kabwe amekuwa makini katika hili, ukiacha utaratibu wa kawaida wa Serikali ya CCM kujibu kwa kebehi bil akujenga hoja hadi sasa hakuna kiongozi aliyeweza kujibu hoja! Wamekaa kimya, na wanaona haya...uozo wao umebainika!

Najiuliza, wale wabunge wa CCM kule kusini wako wapi? Wale viongozi wanaotoka Kusini wako wapi? Wanawasaliti wenzao nbadala ya kusimama kidete kuwatetea?
 
kuna jambo zito hapo limefichika kwenye issue nzima ya gas, Kitendo cha serikali kushindwa kutoa msimamo wake kunaashilia kunatatizo na hasa la ki maslahi .
 
Back
Top Bottom