Zitto: Serikali iache kutafuta mchawi, iende Mtwara!

Zitto: Serikali iache kutafuta mchawi, iende Mtwara!

ZZK tueleze tunakuelewa maana yako ss wapenda maendeleo tusiofungamana upande wowote,wanaoponda bila hoja ilimradi na yy aonekane amecomment tuwachukulie kama walivyo ni wa kuombewa tu haoooo.
 
Viongozi twendeni Mtwara kusikiliza wananchi wetu.. Mimi nakwenda Mtwara haraka na mara baada ya viongozi wangu wa chama kutoa ridhaa.


ZITTO KABWE

Sidhani kama Chama watakubania Mkuu.........Mostly welcome!!
 
Iy


Itakuwa ni kiherehere na kutafuta self glory, kwani vikao vya kamati kuu vinaendelea na baraza kuu kesho je alikuwa Hana haraka gani kwani asingeacha Chama kikatoka na tamko Baada ya vikao vya baraza kuu. Lema
Lema??
 
Ok ila embu weka kumb; sawa anaenda Kama Chama au Zitto?

Anaenda kama Zitto, binafsi sikubaliani na hii tabia yake ya kivyake vyake kwani ni unafiki na kujitafutia umaarufu yeye binafsi. Lakini hoja niliyoirekebisha ni kwamba anaenda kuzungumzia mapendekezo ya kutatua mgogoro na sio kuzungumzia jinsi gesi itakavyozalisha umeme.
 
Ngoja tusubiri na tamko la kamati kuu ya chaddema halafu tulinganishe kati ya tamko la kamanda Zitto na la kamati kuu lipi liko vizuri...
 
Japo namkubali sana ZZK, kwenye ule uzi wangu wa , nilimweleza weakness zake, miongoni mwake ni ni hii ya kukosa subra, ustahimilivu na uvumilivu when it comes to personal attacks!. Japo kwenye suala zima la kujenga hoja na kuwasilisha hoja kuna tofauti kubwa sana kuhusu hoja hiyo imeibuliwa na nani, inajengwa na nani na inawasilishwa na nani!. (Hata ile list of shame, walioijenga tunawajua, kilichofanyika pale Mwembe yanga ni kuwasilishwa tuu). Hakuna ubishi kuhusu uwezo wa ZZK katika kujenga hoja na kuwasilisha hoja ila ZZK anakabiliwa na tatizo kubwa la "ego" linalompelekea kuwa na papara hivyo kum pre empty hata M/Kiti wake!.

Katika ule uzi wangu wa "Chadema Hijajipanga" , pia nililizungumzia hili la "lack of collective responsibilities!", haiwezekani kwenye chama hicho hicho kimoja ni kila mtu anatoa kauli kuhusu jambo hilo hilo moja!. Jana JJ Mnyika, leo Zitto, kesho ndio M/Kiti!. Mlitakiwa muwe na internal discipline mechanism kuwa katika suala la gesi, msemaji ni waziri atatoa msimamo wa wizara kivuli na M/Kiti ndiye atatoa msimamo wa Chama, mlipaswa kumuita ZZK awape full disclosure ya kila anachokijua kufuatia yeye kuwa ndiye Mwenyekiti wa POAC ambapo TPDC iko chini yake!.

Japo sijui ZZK atazungumzia nini, ila kwa vyovyote itakuwa ni kujitetea kwa personal attack alizovurumishiwa na Simbachawene. ZZK ni kijana wenu, akishutumiwa, mmeshutumiwa wote kama alivyo mchuma janga, hula na wa kwao. Haiwezekana mtoto wenu ashutumiwe alafu chama kikae kimya, ndio maana kaamua kujitokeza kuja kujitetea.

Kiukweli Chadema ina tatizo kubwa na "damage control", mgemsoma Nguruvi3 kwenye Duru za siasa - Mgongano wa mawazo kuhusu somo hilo, haya yote yasingetokea!. Kuna shutuma zikivurumishwa, zinatakiwa kujibiwa promptly na sio za kusubiri, japo ZZK ana papara na pupa katika kujibu, kama chama kingekuwa na utaratibu rasmi, ZZK asingefika hapa alipofika!.

Najua wengi wa manazi wa Chadema, mnaamini kuwa ZZK is working in favor of CCM, the time will come, mtawajua wanaoifanyia kazi haswa CCM miongoni mwenu na hamtaamini!.
Pasco.

Hujui Zitto Yupo kwenye kizazi cha Digitali....nyie mumpe vijembe halafu yeye akae kimya tu uliona wapi, eti asubiri Chama kitoe tamko wakati ni personal attack..Mbona matamko ya Magamba Simbachawene na Muhongo yametofautiana?? nyie wenyewe mnapandana kichwani...kwenda zako kule!!
 
zitto amejibu tuhuma zilizoelekezwa kwake yeye binafsi na wala sio chama au nafasi yake ndani ya chama. Simbachawene alimtaja zito na wala hakutaja chadema na zitto angekuwa punguani. Wapinzani wa zitto jitahidini kufikiri kwa ubongo na sio masaburi kama mnavyofanya. Mkiendelea hivyo hamtamuweza hata kidogo, he is no match of you
 
Sidhani kama Chama watakubania Mkuu.........Mostly welcome!!

hahahahahaha
kila mwanachama wa CDM ni mtabili ama mtoa ruhusa ama muidhinishaji juu ya jambo furani kwa viongozi wa CDM
kazi ipo,
yetu macho
 
zitto daah.. chadema kazi mnayo .. zitto anaweza sana kufutalia mambo na pia anaweza kujenga hoja..
ila honest hii ni weakness kubwa ya zitto. Ego
hii inamfanya amue lolote ili kuimaintain..
ila tunapoenda akichekewa hatakiharibu chama cha demokrasia na maendeleo..
muda utaongea binafsi simwaamini zitto
yawezekana zitto kesha bananishwa kamati sasa anatafuta afueni ....tushajua janja ya nyani...
 
  • Thanks
Reactions: JGG
Ndugu zangu Hakuna sababu yeyote ya kuweka tafsiri nyingi kuhusu suala hili. Najua kwamba chama chetu kitatoa msimamo wa chama kuhusu suala hili. Press yangu wala haina nia ya kuharibu tamko la chama. Mie nimejibu mapigo ya Simbachawene. Suala hili lina baraka za chama na Kwa kweli Hakuna sababu ya sisi kama chama kutofautiana kwenye suala hili.

Kauli ya chama itatoka
 
Wakati anatoa tamko lake viongozi wenzake wote wamejifungia pamoja na wabunge wote wa chama wakiandaa tamko la Pamoja kuhusu gas.

Kwa hiyo kutakuwa na matamko mawili moja la chama litakalotolewa na Mwenyekiti Mbowe na la pili litakalotolewa na Zitto.

Nimeguswa na mjadala huu, lakini napenda kusema mambo mawili. Mosi, nahoji: tunamjadili Zitto au hoja yake? Pili, mimi binafsi najua kuwa chama kinajua na kimemruhusu atoe kauli hii ya utangulizi. Hii ya Zitto inatokana na kauli ya Simbachawene jana, ambayo alii-personalize kwa kumshambulia Zitto. Ukiisoma vema, unaona kuwa hii imelenga kwanza kuweka kumbukumbu sahihi kuhusu kauli za awali za Zitto. Naamini chama kitatoa kauli yenye mwelekeo mwingine wa kisera, si majibizano na Simbachawene. Si lazima tumpende au tukubaliane na Zitto. Katika hili, tusome na kujadili kauli yake.
 
Afadhalu Naona Dr .W. Slaa uko hapa embu tuambie kauli ya zitto ndio kauli ya cdm? Pls Mr Rais wa moyoni mwangu.

Naona anachungulia tu...ngoja tusubirie labda atatokelezea kimaandishi......

There are currently 242 users browsing this thread. (62 members and 180 guests)

 
Binafsi sioni mantiki ya huyu Mheshimiwa kuzungumza kwa leo halafu kesho Mkiti wake Mbowe atoe tamko la Kamati kuu kuongelea kitu hicho hicho.

Huo ni ushauri wangu tu lakini

acha upunguani na ushabiki mgando
 
Yeye si memba humu,mbona hajaweka afu we umwemwekea? au unatafuta ukuu wa wilaya 2015?
 
mwakalinga.una wivu wa kike.take it from pius msekwa
 
chanzo mabadiliko forum
TAARIFA YA NDUGU ZITTO KABWE (MB) KUHUSU YANAYOENDELEA
MTWARA NA MRADI WA BOMBA LA GESI ASILIA
Serikali iache kutafuta mchawi, iende Mtwara

Katika kipindi cha wiki nne sasa kumekuwa na maandamamo, malumbano na vurugu kuhusu mradi wa kujenga bomba la kusafirisha gesi asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam. Mradi huu wa kutandaza bomba la urefu wa kilometa 542 ni mkubwa sana hapa nchini, na una thamani kubwa zaidi kuliko miradi mingine yote ya miundombinu iliyopata kutokea hapa nchini. Mradi huu utajengwa kwa mkopo wa dola za Kimarekani 1.2 bilioni kutoka Benki ya Exim ya China.

Wananchi wa Mtwara kupitia maandamano ya tarehe 27 Desemba 2012 wametaka kujua hatma ya maendeleo ya mikoa wa kusini kutokana na mradi huu wa bomba la gesi. Serikali imewajibu wananchi hawa kwa kuwaita wahaini, watu hatari na wasio elewa. Imefika mahali inapotosha madai yao kwamba hawataki gesi itoke Mtwara.

Kimsingi Serikali haijajibu hoja yeyote ya msingi ya wananchi wa Mtwara kuhusu mradi wa kusafirisha gesi. Badala yake imekuwa ikijaribu kupotosha madai ya watu wa Mtwara kupitia mikutano na vyombo vya habari.

Tangu maandamano haya yatokee, na baadaye mikutano ya hadhara na
hatimaye matukio ya kusikitisha ya kuharibu mali za watu, mauaji ya
watu na majeruhi mbalimbli, Serikali na hasa Wizara yenye dhamana ya
mradi huu, imekuwa ikitoa matamko kwenye vyombo vya habari badala ya
kwenda Mtwara kuzungumza na wananchi, kusikiliza madai yao na kuona
namna ya kutekeleza madai hayo. Kutokana na Serikali kutofanya hivyo,
kusikiliza na kuzungumza na wananchi wa Mtwara, vurugu mbaya sana zimeendelea mkoani humo.

Mwezi uliopita, Desemba 2012, tatizo lilionekana kuwa ndogo na lenye kuhusiana zaidi na ukosefu wa kushirikishwa kwa wananchi. Badala ya kushughulikia
tatizo likiwa bado ndogo, Serikali imeona njia pekee ya kushughulikia suala hili ni kutafuta mchawi na kwa wiki zote hizi imekuwa ikisemakuwa wanasiasa na makampuni ya uwekezaji ya nje yanachochea mgogoro
huu.

Leo hali iliyopo mkoani Mtwara inasikitisha sana, maana mali za wananchi zinaharibiwa, nyumba zinachomwa moto na watu wanapoteza maisha. Tunalaani matukio haya kwa nguvu zetu zote, maana kinachotokea Mtwara si Utanzania. Tusipowasikiliza wananchi na kutatua mgogoro huu kwa kuwashirikisha, hali itazidi kuzorota wakati tukitupiana lawama.

Hivi sasa serikali imeona njia pekee ya kushughulikia suala hili ni kutafuta mchawi na kwa wiki zote hizi imekuwa ikisema kuwa wanasiasa na makampuni ya uwekezaji ya nje yanachochea mgogoro huu.

Kwanza, Serikali imekuwa ikiaminisha umma kwanza suala hili limechukuliwa kisiasa. Pili, Serikali imekuwa ikirudia kusema kuwa baadhi ya makampuni ya uwekezaji nchini na mataifa ya Magharibi yamekuwa yakichochea wananchi wa Mtwara.

Katika mwendelezo wa mtindo wa Serikali wa 'management by press conferences' jana Jumamosi Naibu Waziri wa Nishati na Madini ndugu George Simbachawene aliwaambia wahariri kwamba mimi Zitto Kabwe ninachochea wananchi wa Mtwara, ninatumiwa, na si mzalendo. Vile vile alitoa vielelezo kadhaa kuonyesha kuwa mradi wa kujenga bomba la gesi ni gharama sawasawa. Akasisitiza kwamba mimi ni mwongo.

Katika kipindi chote cha mgogoro wa Gesi Mtwara, sijafika Mtwara. Sijafanya mkutano wowote na waandishi zaidi ya kuandika mawazo yangu, kama Mtanzania kuhusu suala hili.

Nimeandika makala nne na zimechapishwa katika magazeti kadhaa hapa nchini na kwenye blogu yangu (www.zittokabwe.com).

Niliandika: Utajiri wa Gesi Asilia: Tuwasikilize Watanzania wa Mtwara na Lindi. Nikaandika tena: Tusipuuze mandamano dhidi ya Bomba la Gesi: Kilio cha Uwajibikaji; Nikaandika tena: Mtwara : Serikali inavunja nchi kwa kutosikiliza Wananchi; ni baadhi ya makala nilizoandika kuhusiana na suala la Mtwara.

Sitaki kubishana na Naibu Waziri ama Kiongozi yeyote ya Serikali kwa sasa. Hatuwezi kuendelea kulumbana, kuzozana, kuzodoana na kurushiana maneno wakati nchi yetu inaungua. Huu sio wakati wa kutafuta mchawi bali kutafuta majawabu ya changamoto zilizopo mbele yetu.

Yanayotokea Mtwara ni fundisho kwetu kwa Taifa namna ya kukabili changamoto za utajiri wa rasilimali, ili kuweka mkakati, mambo haya yanayotokea Mtwara yasitokee tena Tanzania. Tutaweza kuzuia maafa haya iwapo tutaweka uwazi katika mikataba, tutashirikisha wananchi kwenye unyonyaji wa maliasili za nchi, na iwapo tutaweka uwajibikaji.


Rais Kikwete Kikwete ana majibu; ayatoe sasa kwa wana Mtwara

Kwa mujibu wa Mpango Kabambe wa Umeme nchini (Power System Master Plan), kulikuwa na mradi wa kufua umeme MnaziBay, ambao Rais Jakaya Kikwete aliagiza utekelezwe mara moja. Serikali ieleze umma kuhusu mradi huo wa kujenga kituo cha kufua umeme 300MW MnaziBay Mtwara na kujenga msongo wa umeme wa 300KV mpaka Singida. Umeishia wapi? Ikumbukwe kuwa mnamo tarehe 12 Oktoba 2012, Rais Jakaya Kikwete alipokea ripoti ya ujenzi wa mradi huu kutoka makampuni ya China National Machinery & Equipment Import & Export Corporation (CMEC) ya China na Siemens ya Ujerumani, ambayo kwa pamoja yalitarajia kujenga kituo kikubwa cha kuzalisha umeme kutokana na gesi katika eneo la Mnazi Bay, mjini Mtwara na pia kujenga njia ya kusafirisha umeme ya kilomita 1,100 kutoka Mtwara hadi Singida. Mradi huu ungegarimu dola za kimarekani milioni 684 na Rais aliagiza utekelezwe haraka sana. Huu mradi uliishia wapi? Kwa nini Serikali ipo kimya kuhusu mradi huu ambao ungejibu kabisa maswali ya watu wa Mtwara? Taarifa ya Ikulu kuhusu mradi huu imeambatanishwa hapa.

Tufanyeje?

Hapa tulipofikia ni lazima kwanza kabisa kusikia kilio cha wananchi wa Mtwara ikiwemo kuelewa madai yao. Swali kubwa kubwa la watu wa Mtwara na Kusini kwa ujumla ni ‘tunanufaikaje'? Jibu la swali hili si ahadi za miradi bali ni vitendo. Hapa ndipo serikali inaposhindwa kushughulikia suala hili, kutoelewa madai ya wananchi na kuyapotosha.Viongozi wa kisiasa wenye ushawishi kutoka pande zote, chama tawala na vyama vya upinzani, waende Mtwara kuzungumza na wananchi, lakini wawasikilize kwanza.


  1. Lazima viongozi tujenge utamaduni wa kusikiliza wananchi na si kuwahutubia tu. Wananchi wa Mtwara wana madai ambayo lazima viongozi tukae kitako kuwasikiliza kisha kufanya nao majadiliano ambayo yatatoa mwafaka. Rais mstaafu, Ndugu Benjamin Mkapa ameshatoa kauli kuhusu suala hili. Ni wakati mwafaka sasa kwa viogozi wengine kumuunga mkono kwa kwenda Mtwara na kukaa na wananchi wa Wilaya zote za Mtwara, kusikiliza hoja zao na kuona namna ya kupata ufumbuzi wa suala hili. Wakati hatua hii inachukuliwa, wananchi waombwe kutulia na kuacha vurugu za aina yeyote ile, na Serikali isimamishe mradi mpaka hapo suluhu na wananchi itakapopatikana.


  1. Wakati juhudi hizo zinaendelea Serikali iweke wazi mkataba wa ujenzi wa bomba, kwani ni dhahiri gharama za mradi huu ni kubwa mno kulingana na uhalisia wa miradi ya namna hii duniani kote. Katika taarifa zote kwa umma Serikali imekuwa ikisema kwamba mradi utagharimu jumla ya dola za kimarekani 1.2 bilioni, lakini katika taarifa ambayo Wizara ya Nishati na Madini imesambaza jana kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini imesema mradi utagharimu dola za kimarekani milioni 875. Usiri katika mkataba huu unaashiria kwamba Serikali inaficha kitu. Hivyo njia pekee ni kutaka mkataba uwe wazi kwa wananchi.


  1. Wakati tunawataka wananchi wa Mtwara kuruhusu utulivu, ni vema Serikali ijiandae kutoa majawabu ya madai ya wananchi hao. Majawabu ya Serikali yajikite kueleza wananchi wa Mtwara wanafaidikaje na rasilimali ya gesi asilia kwa maendeleo yao. Wananchi wa Mtwara wanataka uwajibikaji wa Serikali kwenye utajiri wa nchi, na wamechoka na porojo za orodha ya miradi isiyotekelezwa.

Viongozi twendeni Mtwara kusikiliza wananchi wetu. Nchi inaungua na hatuwezi kuendelea kuzozana badala ya kuzima moto huu hatari kama vita vya MajiMaji. Mimi nakwenda Mtwara haraka na mara baada ya viongozi wangu wa chama kutoa ridhaa.


ZITTO KABWE
Mbunge, Kigoma Kaskazini (Chadema)
Waziri Kivuli wa Fedha
Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni
Statement kama hii ilitakiwa itolewe na chama na sio individual. Kama hivi ndio ZZK kasema, jee kesho M/Kiti wake atasema nini?.

Mkuu ZZK, japo ulikiri wazi kuwa hutauzungumzie tena urais 2015, kitendo hiki cha kutoa hii " presidential stetement" iliyokuwa well crafted as if wewe ndio rais, hauoni ni kama kuuzungumzia urais kwa mlango wa nyuma?. Nilikushauri fanya mambo ya kuwadhibitishia Chadema, wewe ndio unae fit kuipeperusha bendera from within, ili Wachadema ndio wakuone unafaa na kukuomba ugombee!, hivi kwa mfano, statement kama hii, ungempa M/Kiti wako aijumuishe kwa press conference yake, huoni ingekuongezea mileage ndani ya chama kuliko kutoka solo?!.

Binafsi ZZK namkubali sana kama ninavyomkubali EL na ikitokea tunatofautia huwa namwambia kama nilivyo mshauri EL asiende Arumeru, angemponza Sioi, alienda na kweli akamponza!, ZZK nilimshauri "" sasa anaendelea, licha ya yeye kuwa ndie the best that Chadema has so far, kama asiposimamishwa kuwa mgombea wa Chadema 2015, asimlaumu mtu, "anayakoroga mwenyewe",atakuwa hana budi, "ayanywe".
Pasco.
 
Ngoja tusubiri na tamko la kamati kuu ya chaddema halafu tulinganishe kati ya tamko la kamanda Zitto na la kamati kuu lipi liko vizuri...


......Kamanda omeona mbali.....

....Kombora bila coordinates haliwezi kurushwa
....kumbuka Chadema ni chama MAKINI..
 
Hapa anazungumzia suala la majibu wanayoyataka na manufaa ya mradi wa gesi kwa wakazi wa Mtwara.Hazungumzii suala la mabilioni ya uswiss wala urais.Usipotoshe fikra za great thinker,hawa wapo kazini bwana.Mabilioni na urais ni mada nyingine tofauti na hii.
 
Back
Top Bottom