Zitto: Serikali iache kutafuta mchawi, iende Mtwara!

Zitto: Serikali iache kutafuta mchawi, iende Mtwara!

Lema yuko kamati kuu amenitumia meseji ili niweze kumrushia , amesisitiza kuwa zit to anakiherere
Mkuu kuwa na busara basi.Hata kama huyo Lema kakwambia wewe kiherehere cha nini?Fitina jambo baya sana.
 
hahahahaahahaha..kazi kweli kweli....

Kilewo nafikiri baadhi ya sahani kichwani kwako zimekaa vibaya au wewe ni taahira hivi kwa akili za kibinadamu kabisa mtu anaweza kukwambia naomba umtukane mtu kwa niaba yangu au akakwambia mtukane fulani matusi haya na wewe ukamtukana kweli una akili au boya?,kutuambia Lema kakwambia useme hivi yuko kwenye kikao na wewe ukatekeleza ni dhahiri kwamba una akili za kushikiwa acha tabia ya kiherehere na kimbelembele
 
Binafsi sioni tatizo lolote la tamko la ndugu ZZK, kwani amelenga kutatua mgogoro huu kwa njia muktadha ya amani...ni neutral speech, na wala haioneshi kuwa ana lengo la kujtengenezea njia kuelekea Uraisi. Mwenyewe ametamka wazi kuwa ameshaandika makala nne kuhusiana na hilo jambo kama Mtanzania yeyote yule. Lengo ni zuri ni wakati wa serikali kupima mapendekezo yake na kama yanafaa wanapaswa kuyatekeleza. Msihusishe siasa na jambo linalotaka kugharimu amani na maisha ya watanzania wengine........kumbuka Mtwara inaundwa na wamakonde na Watanzania wengine wenye makabila mbalimbali kwa sasa....hii inaonesha kuwa bado tu wamoja. Mungu ibariki Tanzania......iepushe na hii sintofahamu inayotukabili kwa sasa.
 
Statement kama hii ilitakiwa itolewe na chama na sio individual. Kama hivi ndio ZZK kasema, jee kesho M/Kiti wake atasema nini?.

Mkuu ZZK, japo ulikiri wazi kuwa hutauzungumzie tena urais 2015, kitendo hiki cha kutoa hii " presidential stetement" iliyokuwa well crafted as if wewe ndio rais, hauoni ni kama kuuzungumzia urais kwa mlango wa nyuma?. Nilikushauri fanya mambo ya kuwadhibitishia Chadema, wewe ndio unae fit kuipeperusha bendera from within, ili Wachadema ndio wakuone unafaa na kukuomba ugombee!, hivi kwa mfano, statement kama hii, ungempa M/Kiti wako aijumuishe kwa press conference yake, huoni ingekuongezea mileage ndani ya chama kuliko kutoka solo?!.

Binafsi ZZK namkubali sana kama ninavyomkubali EL na ikitokea tunatofautia huwa namwambia kama nilivyo mshauri EL asiende Arumeru, angemponza Sioi, alienda na kweli akamponza!, ZZK nilimshauri "" sasa anaendelea, licha ya yeye kuwa ndie the best that Chadema has so far, kama asiposimamishwa kuwa mgombea wa Chadema 2015, asimlaumu mtu, "anayakoroga mwenyewe",atakuwa hana budi, "ayanywe".
Pasco.
Pasco huna haja ya kuki under-estimate chama. Ni uhakika upi ulionano kuwa hii aliotoa ni zaidi ya kile tunachotegemea kutoka kwenye chama? By the way amekiri kuwa chama kimebariki hii press conference yake binafsi. Najitahidi nisizidi kuamini kuwa unafurahishwa na tofauti alizonazo Zitto na viongozi wengine wa Chama
 
Prezzo bado mbinafsi sana, kwa nini hata hakuwa pamoja na Mnyika kama waziri kivuli wa nishati na madini...?
 
Ndugu zangu Hakuna sababu yeyote ya kuweka tafsiri nyingi kuhusu suala hili. Najua kwamba chama chetu kitatoa msimamo wa chama kuhusu suala hili. Press yangu wala haina nia ya kuharibu tamko la chama. Mie nimejibu mapigo ya Simbachawene. Suala hili lina baraka za chama na Kwa kweli Hakuna sababu ya sisi kama chama kutofautiana kwenye suala hili.

Kauli ya chama itatoka

Zitto nimekuelewa sana ila inabidi tuwe waangalifu kwani maadui ni wengi kuliko wanaounga harakati za chama kiukweli tamko lako lipo fresh ila j kamati kuu yote walirizia naona kuna messege kutoka mtu wa kamati kuu . Ushauri wangu jaribu kuwa smart zaidi kushirikiana na wenzako hasa kwenye mambo ambayo yanakuhusu wewe mwenyewe na chama MUNGU bariki Tanzana MUNGU bariki CHADEMA na viongozi wake
 
Mkuu
Kwani kama nikwa maslahi ya taifa na si maslahi binafsi tatizo liko wapi?! Hatukupata ujasiri wa kuyasemea madudu kwenye Tanzanite na Sangara tumeona yaliyo tukuta, kila mwenye uwezo wa kuisemea gasi kwa maslahi ya dongo la taifa hili afanye hivyo hata kama hana kofia ya siasa.

cdm walikua na mpango wa kutoa tamko kama chama sasa je hili ndio tamko la chadema ama la mbunge machachari peke yake na la chama litakuja baadae?

na mbunge machachari anatuambia nyumba inaungua uwezo wa kuzima moto anao lakini anasubiri watu wateketee kwa moto wakati anasubiri ridhaa ya chama!lakini mbona mbunge machachari kwenye kwenda kwenye media kuzungumzia issues huwa hasubiri ridhaa ya chama chake?na kwa nini matamko ya mbunge machachari mengi huwa anayatoa siku za mapumziko mwishoni mwa juma akijua siku hizo huwa hazinaga habari kwa tuliopitia maisha ya news room tunajua hivyo,huwa ni bahati mbaya au ni strategy za kutaka kuonekana starling kama amita bachan enzi zile?
 
Naweka wazi siungi mkono hii press conference ya Zitto . Huu ndio utafutaji wa umaarufu uchwara kupitia media ,acha afurahishe fikra na tabia zake za ubinafsi .Watanzania wa Mtwara na Lindi hawapo /hawasimami na wanaojitafutia umaarufu kwa swala la GAS ,HAPA INASUBIRIWA KAULI YA RAISI JK PEKEE....

GAS KWANZA SIASA ZA VYAMA BAADAE

hata ulivyopigwa chini uongozi kwa magamba wenzio ulipinga kwa kurusha viti.unafuata ya bosi wako mwigulu wala kwenye uungwaji wako mkono hauna tija
 
Kweli Prezzo anatokea Kigoma, anawaza uchawi uchawi tu! Nani kasema serikali inamtafuta mchawi!? Mbona Zitto mwaka huu 2013 umekuja na iman za kishirikina sana?
Mara hakuna panya atakaebaki, leo tena serikali inasaka mchawi, kumbe we unaamini gasi itakuwa maji. Prezzo Masalia likubwa
 
Asante Zitto, waliokuelewa wameelewa achana na magamba. Umeshasema mwenye masikio ma asikie. Mjumbe hauwawi. Mungu akupe maono zaidi achana na magamba
 
Statement kama hii ilitakiwa itolewe na chama na sio individual. Kama hivi ndio ZZK kasema, jee kesho M/Kiti wake atasema nini?. Mkuu ZZK, japo ulikiri wazi kuwa hutauzungumzie tena urais 2015, kitendo hiki cha kutoa hii " presidential stetement" iliyokuwa well crafted as if wewe ndio rais, hauoni ni kama kuuzungumzia urais kwa mlango wa nyuma?. Nilikushauri fanya mambo ya kuwadhibitishia Chadema, wewe ndio unae fit kuipeperusha bendera from within, ili Wachadema ndio wakuone unafaa na kukuomba ugombee!, hivi kwa mfano, statement kama hii, ungempa M/Kiti wako aijumuishe kwa press conference yake, huoni ingekuongezea mileage ndani ya chama kuliko kutoka solo?!. Binafsi ZZK namkubali sana kama ninavyomkubali EL na ikitokea tunatofautia huwa namwambia kama nilivyo mshauri EL asiende Arumeru, angemponza Sioi, alienda na kweli akamponza!, ZZK nilimshauri "" sasa anaendelea, licha ya yeye kuwa ndie the best that Chadema has so far, kama asiposimamishwa kuwa mgombea wa Chadema 2015, asimlaumu mtu, "anayakoroga mwenyewe",atakuwa hana budi, "ayanywe". Pasco.
Simbachawane alimshambulia Zitto personally na sio chama, Zitto amemjibu kwa capacity yake na yupo sahihi. Ni vema tukajadili ideas alizozitoa na ni utoto kumjadili mtoa ideas. Pasco hayo maswala yako ya urais 2015 hayahusiki hapa na yame-shake credibility ya ujengaji hoja unaojaribu kuufanya. watu wanakufa Mtwara tujenge hoja na tuache kujadili majina ya watu hapa.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu zangu Hakuna sababu yeyote ya kuweka tafsiri nyingi kuhusu suala hili. Najua kwamba chama chetu kitatoa msimamo wa chama kuhusu suala hili. Press yangu wala haina nia ya kuharibu tamko la chama. Mie nimejibu mapigo ya Simbachawene. Suala hili lina baraka za chama na Kwa kweli Hakuna sababu ya sisi kama chama kutofautiana kwenye suala hili.

Kauli ya chama itatoka

Nakuunga mkono mkuu, Taarifa ni nzuri na iwapo serikali itafuata ushauri wako naamini mambo yataenda vizuri. Nawashangaa sana wanao pinga taarifa hii, nini maana ya demokrasia. Wengine wanasema ungesubiri, tusubiri mpaka vifo viongezeke ndio watu waseme. Mbona makala ulizotoa kwenye magazeti hakuna aliye hoji. Swala la gas au maliasili kwa ujumla ni zito na serikali haina sera kuhusu hili, kwahiyo mwenye mawazo yoyote mazuri asikae kimya. Mh. Zitto ulicho fanya ni sahihi na usikate tamaa na hao wachache wanao pinga, mwisho wa siku wataona ukweli. Wangapi walikupinga kuhusu Prof. Muhongo? na sasa wanaona ukweli.
 
Iy


Itakuwa ni kiherehere na kutafuta self glory, kwani vikao vya kamati kuu vinaendelea na baraza kuu kesho je alikuwa Hana haraka gani kwani asingeacha Chama kikatoka na tamko Baada ya vikao vya baraza kuu. Lema

kilewo siyo kila unachoambiwa na lema lazima ufanye jaribu kuchuja kwa faida ya umoja wa chama cyo lazima kila mara kuweka tofauti zenu jamvini.wewe ni means ya mawasiliano sometime kutokana na ukaribu wako na wadhifa wako usifanye hivyo.
 
Mohamedi Mtoi naona na wewe ushanunuliwa na kambi ya Zitto mara hii. Kweli Pasco alikuwa sahihi kuwa "penye udhia, penyeza rupia..."
Yeye ameleta taarifa kwani Zitto hapaswi kusema chochote kwa vile wewe hukubaliani naye? Acha watu wawe na uhuru wa kuzungumza tujadili hoja ya msingi sio kupindisha hoja na kuanza kujadili personality
 
Last edited by a moderator:
kitu ilichofanya zitto sio kiherehere but ni jins ya kutoa ufafanuzi wa kile kinachoendelea mtwara na yeye kama mwananchi na nimefurah anaponyesha viongoz badala ya kwenda kushugulikia tatizo wanaanza kuatack watu,Ni vyema alivyofanya wala hamna tatizo kwa maoni yangu
 
Japo namkubali sana ZZK, kwenye ule uzi wangu wa , nilimweleza weakness zake, miongoni mwake ni ni hii ya kukosa subra, ustahimilivu na uvumilivu when it comes to personal attacks!. Japo kwenye suala zima la kujenga hoja na kuwasilisha hoja kuna tofauti kubwa sana kuhusu hoja hiyo imeibuliwa na nani, inajengwa na nani na inawasilishwa na nani!. (Hata ile list of shame, walioijenga tunawajua, kilichofanyika pale Mwembe yanga ni kuwasilishwa tuu). Hakuna ubishi kuhusu uwezo wa ZZK katika kujenga hoja na kuwasilisha hoja ila ZZK anakabiliwa na tatizo kubwa la "ego" linalompelekea kuwa na papara hivyo kum pre empty hata M/Kiti wake!.

Katika ule uzi wangu wa "Chadema Hijajipanga" , pia nililizungumzia hili la "lack of collective responsibilities!", haiwezekani kwenye chama hicho hicho kimoja ni kila mtu anatoa kauli kuhusu jambo hilo hilo moja!. Jana JJ Mnyika, leo Zitto, kesho ndio M/Kiti!. Mlitakiwa muwe na internal discipline mechanism kuwa katika suala la gesi, msemaji ni waziri atatoa msimamo wa wizara kivuli na M/Kiti ndiye atatoa msimamo wa Chama, mlipaswa kumuita ZZK awape full disclosure ya kila anachokijua kufuatia yeye kuwa ndiye Mwenyekiti wa POAC ambapo TPDC iko chini yake!.

Japo sijui ZZK atazungumzia nini, ila kwa vyovyote itakuwa ni kujitetea kwa personal attack alizovurumishiwa na Simbachawene. ZZK ni kijana wenu, akishutumiwa, mmeshutumiwa wote kama alivyo mchuma janga, hula na wa kwao. Haiwezekana mtoto wenu ashutumiwe alafu chama kikae kimya, ndio maana kaamua kujitokeza kuja kujitetea.

Kiukweli Chadema ina tatizo kubwa na "damage control", mgemsoma Nguruvi3 kwenye Duru za siasa - Mgongano wa mawazo kuhusu somo hilo, haya yote yasingetokea!. Kuna shutuma zikivurumishwa, zinatakiwa kujibiwa promptly na sio za kusubiri, japo ZZK ana papara na pupa katika kujibu, kama chama kingekuwa na utaratibu rasmi, ZZK asingefika hapa alipofika!.

Najua wengi wa manazi wa Chadema, mnaamini kuwa ZZK is working in favor of CCM, the time will come, mtawajua wanaoifanyia kazi haswa CCM miongoni mwenu na hamtaamini!.
Pasco.

Mkuu Pasco;
Mahaba yako kwa ZZK yamevuka mpaka. In actual fact sio mahaba kwa ZZK tu, ila ni lengo lango na dhamira yako ya kuona CDM inavurugika ili kuwaondolea vizuizi maCCM! Yaani unajifanya hukubaliani na hatua ya ZZK kutoa tamko kabla ya chama lakini at the same time unampigia ZZK debe la kutosha. Acha unafiki Pasco, ZZK is wrong!
 
Lema yuko kamati kuu amenitumia meseji ili niweze kumrushia , amesisitiza kuwa zit to anakiherere
Sawa. Naamini akimaliza kikao akapata mda wa kusoma aloandika zzk, atamuelewa...
 
Mh. Zitto ana kazi kweli kweli.

Kuna watu hapa hata hawataki kusoma hoja ya Mh. zitto bali wapo kulizodoa jina lake pindi linapotokea janvini.

Press release yake hata haijagusa sera za chama kuhusu gesi........Maana yake nini?...........maana yake huu ni ujumbe toshelezi kuwa hilo siyo tamko la chama bali lake binafsi kuhusu kuzodolewa na viongozi wa serikali.

-Hawezi kujibu bila kutoa angalizi na maoni yake kwa yaliyojili katika sakati hili, ila kwa vile kuna wanazi hawapendi kuliona jina la Mh. zitto kwenye media lazima watafanya kila liwezekanalo ili lisionekane ama lionekane katika angalizo hasi ili asizibe kiwiliwili na kivuli cha "mteuliwa".

Kwa mtindo huu,
STILL LONG WALK TO POWER
 
Back
Top Bottom