Zitto: Nitafanya uamuzi mgumu

Zitto: Nitafanya uamuzi mgumu

Status
Not open for further replies.
Wewe ni mm1 mfuasi wa zzk au ni mwingine? Tuanzie hapo tujue kama hili lina ukweli.
 
Akihamia cuf sio mbaya coz bado atakuwa ndani ya ukawa,lakin akihamia kwa waliomtuma atakuwa amejimaliza kabisaaa
 
Magic my foot, tutaona hiyo october sio mbali kabisa. naona harufu ya team Lumumba kuhamia kwa ZZK.
 
Katiba inataka mgombea Urais awe na 40+years , Zitto hatakua na umri huo come October .ni upuuzi kujadili ndoto zako
 
Upo sahihi kabisa Ben Saanane, kuna haja ya kufanyika maridhiano kati ya CHADEMA na Zitto, kufukuzana katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu ni hatari sana kwa pande zote!

Hakuna atakaefaidi moja kwa moja, iwe Zitto au CHADEMA, kila mmoja atapoteza kwa kiwango chake!

Yaandaliwe mazungumzo yenye lengo la kusameheana, bila kuwekeana masharti yoyote magumu...
Ni kweli mkuu BIGURUBE lakini huwezi jua, yanaweza kufanyika maridhiano na kusameheana lakini jamaa akawa kumbe alikuwa hamaanishi; kumbe anaendelea kutumika na Nyinyiem halafu kwenye point za mwishoni akaibua li ugomvi na mmoja wa wategemewa wakafikishana pabaya na jamaa akapoteza sifa za nafasi yake. So kama katiba ya chama imefuatwa mimi sioni tatizo.
 
Katiba inataka mgombea Urais awe na 40 years , Zitto hatakua na umri huo come October .ni upuuzi kujadili ndoto zako

Labda tupo enzi zile za hadithi ya Kalukakange mtoto wa Nyoka ambaye alikuwa ana ongezeka umri kila kukicha. Na zile chale za kwenye makalio anazoziamini kuwa zitatufanya tusahau umri wake kama ambavyo wanaCCM walivyosahau tarehe ya kuzaliwa kwa chama chao.
 
Alisariti nini? Hivi ukihoji Matumizi mabaya ya pesa za chama ni Usariti? Kohoji ukabila na ukanda na mapungufu ya Uongozi ni Usariti? Kumbuka hata chacha Wangwe kabla ya kuuawa na akina Lema na Deus malya alikuwa akihoji sana juu ya Ufujaji wa pesa za Ruzuku na pesa za misaada, pesa yote inamalizikia mifukoni mwa mbowe na watu wake wa Karibu, Wapo watu Chadema wanaamini na kukariri kuwa Mbowe ni Mungu kila analosema linatoka Mbinguni na hasitahili kuulizwa chochote. R.I.P chacha wangwe.

Una mawazo mgando kama akili yako.
 
Zitto ataingia CUF afu atasimamishwa kama mgombea urais kupitia tikiti ya UKAWA...
 
Kuna nyepesi mitaa ya kwetu ati ameandaliwa kuwa mgombea mwenza wa Lowasa ili kupata kura za vijana. Labda ndo maamuzi magumu yenyewe hayo. Kugombea kama wagombea binafsi not affiliated na vyama

Huyu hafai kabisa
 
ZZK kuamua kugombea uraisi wa JMT kptia chama cha ACT is a demon plan, why?? because zitto has magic political power!!! what i mean ni kwamba ZZK atadhoofsha pande zote mbili chama tawala na vyama pinzani,mathematicaly ni hiviii
40%@CCM
30%@UKAWA
25%@ACT
5%@Other parties

Now who is the winner?
Kitakachofata ni vurugu tu.Am out!!!!!!

Umri unaoruhusiwa kikatiba kafikisha? Au katiba itatenguliwta? Wee vipi?
 
Suluhishana na wenzako yaishe Zito, acha kujiona una nguvu sana. Utajimaliza kisiasa, watanzania wa leo sio wa jana. Huko unakotaka kwenda ndio kuna malaika? utakumbana na matatizo yale yale mwisho utakuwa frustrated. Kubali kwamba tabia yako ime efluence matatizo unayokumbuna nayo sasa. Suruhisho ni kuomba msamaha na kisha kusonga mbela na huo ndio ukomavu sio kuzira.
 
Yote afanye lakini sio kuomba msamaha wahafidhina hawana dini, abakie na msimamo wake vile vile. Ajitenge na wahafidhina kwani wako wachache na wafuasi wao wakigundua watamfuata si muda mrefu. Yaani amuombe msamaha tundu lisu! never wengi wa wapambe wa wahafidhina wanaringia ubunge na kiukweli siku zao zinahesabika mno. Asiache siasa huko ndio kafanya vizuri zaidi.

Either aache siasa au aombe msamaha aendelee na siasa
 
Suluhishana na wenzako yaishe Zito, acha kujiona una nguvu sana. Utajimaliza kisiasa, watanzania wa leo sio wa jana. Huko unakotaka kwenda ndio kuna malaika? utakumbana na matatizo yale yale mwisho utakuwa frustrated. Kubali kwamba tabia yako ime efluence matatizo unayokumbuna nayo sasa. Suruhisho ni kuomba msamaha na kisha kusonga mbela na huo ndio ukomavu sio kuzira.

Akili mali yan huoni kama ZITO anaonewa!!!
 
Zitto usiachie jimbo. Pambana urudi Bungeni. Vi ginevyo umejimaliza kisiasa. Chama ni behewa tu na yako mengi yanakisubiria.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom