Zitto: Nitafanya uamuzi mgumu

Zitto: Nitafanya uamuzi mgumu

Status
Not open for further replies.
Sasa basi huo si uamuzi mgumu huo ni ubishi.. Mkuu kama unafanya kazi kampuni x na ukaona mambo hayaendi unafanyaje?? Unalilia lia tu huku unaskills na uzoefu wa kutosha?? Ni ujinga tu kumuamini huyu.. 2010 alipata kura chini ya 50% jimboni kwake, hata madiwani 10 hana jimboni kwake kigoma nzima mbunge kwa cdm ni yeye tu, hakuna mission aliwahi kuarchieve, si mabilioni ya uswisi wala si buzwagi...huyu anajidanganya na ndio anakufa kama ndugu yanke nyange kabouuru... Atawadanganya wasio mjua mimi nipo kigoma hapa kikazi naelewa sana wakati mgumu alaonao huyu jamaa.. Baada ya kuazsisha mizozo na cdm hapa kigoma watu wamemtoa thamani kabisa, watu wamezidi kujitolea kufungua vijiwe vya cdm kwa gharama zao na kukisapoti chama....

Ni Dr. Walid Amani Kabourou na si mwanamichezo Nyange Kaburu
 
Ben sijui kwann sijui sana siasa ila nilikua naona kama ndio uamuzi sahihi kabisa huo....kama anataka kwenda mbali kwa siasa za kitanzania ni lazima abake CDM tumeona wengi kina kaborou,lamwai walipoishia..kusema tu samahani ni shida gani

Samahani kwa kosa gani?kutaka uenyekiti ni kosa?
 
Kwa sasa ni Zito pekee anayeweza kuamua hatima yake. Ni yeye tu ndiye anayejua alicholipwa kuihujumu CDM!! Nyie wengine msiojua kilicho moyoni mwa Zito mnahangaika bure!! Pesa kala yeye na Wapambe wake, sisi inatuhusu nini? Ila kwa Wapambe wake na labda ukiwemo wewe mna haki ya kufa naye!! Sisi Watanzania wengine tuliomwamini KATUANGUSHA; na namna pekee ya kumuadhibu ni KUMKATAA. CDM amueni na sisi tupo nyuma yenu.

Kumbukeni kuing'oa CCM ni Vita ya kufa na kupona! CCM wa Pesa sana japo ni hizo walizotuibia, wana vyombo vyote muhimu japo ni kama Haramu, Wameweza kutoa ujira kwa masikini wanaojua kusoma na kuandika ili wawatetee kwenye mitandao ya kijamii. Waendelee kufanya hivyo ila asitokee mtu miongoni mwetu akatumika na tukaogopa kumwajibisha, TUTAKOSEA SANA.

Zitto kamuangusha Mbowe tu na wala sio Chadema wala Watanzania.Kamuangusha Mbowe kwa sababu kwa namna walipotoka mbali Mbowe hakutegemea kuwa Zitto atataka tena achukue Uenyekiti wakati anajua kuwa chama kwa nafasi za juu kina wenyewe.
 
Maswali hayo ndiyo wanaojiuliza Watanzania. Zito kwa dharau zake anadhani Watanzania hawawezi kujihoji na kuuliza. Ajue kabisa kwamba watu wenye akili zetu TUNAJIULIZA SANA!!

Wenye akili hutafakari, hawamezi tu waliyoambiwa kama wewe na kuimba kama kasuku.
 
Ni kweli mshauri wake, aombe msamaha kwa kosa gani, na yeye ndio kila kitu chadema hata mwaka jana serikali za mitaa bila yeye chadema wasingeshinda kwa kishindo.....
Zitto, aombe msamaha kwa kosa gani.
 
mkuu nyagakeni asante sana.. bila shaka unaipata hiyo siasa kali kabisa ya wakati huo kabouru akiwa katika kiwango chake cha ubora...., akili nyingi huondoa maarifa...
Ni Dr. Walid Amani Kabourou na si mwanamichezo Nyange Kaburu
 
Kosa la zitto kufukuzwa chadema sio kudai mahesabu na wala sio kutaka kugombea uenyekiti kosa lake kubwa na kuandika waraka wa kimapinduzi wakutaka kupindua viongozi

Makosa ya Zitto yaliyojadiliwa kamati kuu ya kushupalia ruzuku kupitia kamati yake ya PAC bila kuwatonya Chadema.Hiyo ni fact.Huwezi kuikwepa leo.Laiti ingepatika video ya kikao kile watu humu wangeona aibu humu kumuita Zitto msaliti na wangeona aibu aina ya viongozi waliopo Chadema.

Usome ule waraka alafu tuonyeshe hapa ni wapi waraka ule unazungumzia mapinduzi kwa maana ya kupindua?waraka unazungumzia kushiriki uchaguzi wa kidemokrasia na wanachama wa Chadema wachague kwa kura Mwenyekiti ambao kwenye waraka walisema Zitto angefaa.

Ukiusoma waraka ule ni wazi Zitto hakushiriki kuuandaa maana unamzungumzia Zitto pia vibaya sehemu kadhaa.Hivyo kuwa Chadema waraka ule katu hauwezi kusimama popote kuwa sababu kwanza ni mkakati wa kidemokrasia lakin pili Zitto hakushiriki na waraka upo wazi juu ya hilo.

Afadhari umeeleza ukweli kidogo, maana wengine hawajui kuwa zingine zote ni porojo lakini sababu ni UENYEKITI na KUTISHIA MASLAHI YA WATU NDANI YA CHADEMA AMBAO KWAO CHADEMA BI SACCOS YAO.
 
Zitto kachelewa sana, hayo maamuzi magumu alitakiwa ayafanye kabla na sio leo.
 
Naona kwenye Fb yake kasema hatagombea tena ubunge jimbon kwake
 
Nafikiri anataka kutimiza ndoto yake ya kugombea uraisi!,ngoja tusubiri hayo maamuzi magumu!
 
Ni kweli mshauri wake, aombe msamaha kwa kosa gani, na yeye ndio kila kitu chadema hata mwaka jana serikali za mitaa bila yeye chadema wasingeshinda kwa kishindo.....

Mmmmh kushinda kwa kishindo ndio kukoje huko?kupata viti 20 kati ya viti 100 ni kushinda kwa kishindo?labda kiswahili kimebadilika sikuhizi.
 
HUKO FB NDIKO KUNAKOMFAA KUTOLEA MATAMKO.. TAYARI IKO WAZI KUNA KAMANDA WA KUZALIWA KIJIJI CHA KIGANZA NI DAKTARI MATYAZO HOSPITAL ATASIMAMA KWA CDM HAPO KIGOMA KASKAZINI NI MSOMI NA MWENYE UWEZO MKUBWA SANA, ZITTO KASHAPEWA PESA NA CCM ABADILISHANE JIMBO NA MBUNGE WA SASA WA KIGOMA MJINI CCM-Peter serukamba, NA HUYO P. Serukamba NDIYE AENDE KIGOMA KASKAZINI, HALAFU BADO KUNA WATU BADO WANAAMINI ZITTO NI MPINZANI ULIWAHI IONA WAPI HIYO??.........
Naona kwenye Fb yake kasema hatagombea tena ubunge jimbon kwake
 
Upo sahihi kabisa Ben Saanane, kuna haja ya kufanyika maridhiano kati ya CHADEMA na Zitto, kufukuzana katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu ni hatari sana kwa pande zote!

Hakuna atakaefaidi moja kwa moja, iwe Zitto au CHADEMA, kila mmoja atapoteza kwa kiwango chake!

Yaandaliwe mazungumzo yenye lengo la kusameheana, bila kuwekeana masharti yoyote magumu...

Hakuna cha maridhiano,nyie ndo mnampa kiburi,chama lazima kiwe na msimamo juu ya maamuzi yake.
 
Last edited by a moderator:
Huyu dogo mpumbafu sana..wenzako hawakutaki unalazimisha nini si uende ccm au act?
 
Zitto ni makini na washauri wake ni makini pia, huenda maamuzi magumu anayotaka kufanya ni kuendelea na chama kwa kuomba msamaha. Maana hakuna kitu kigumu kama kuomba msamaha.
Kwani amepata washauri wapya!? Kama ni walewale mbona hawakuonyesha huo umakini wakamuacha aende mahakani...hamna kitu hapo,CCM wabaya!
 
Kuna nyepesi mitaa ya kwetu ati ameandaliwa kuwa mgombea mwenza wa Lowasa ili kupata kura za vijana. Labda ndo maamuzi magumu yenyewe hayo. Kugombea kama wagombea binafsi not affiliated na vyama

Mkuu kama ndo hivyo itakuwa hatari,LOWASA na ZITO timu moja 2015 kura zaidi ya 100% au kupita bila kupingwa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom