Zitto: Nitafanya uamuzi mgumu

Zitto: Nitafanya uamuzi mgumu

Status
Not open for further replies.
Hiyo ndo ilivyo kutoka kwa watu wa karibu wa kijana huyo alieipenda CHADEMA enzi hizo na kuing'ang'ania CHADEMA kwa sasa ili apate kiinua mgongo cha bunge. ACT mtaisoma no.

CCM tupo imara hatuteteleki

Nakubaliana na wewe maana safari ya jana ya Magdalena Sakaya kuungana na Zito inatoa jibu! Ila propaganda za udini ndio zinazopaliliwa.
 
Upo sahihi kabisa Ben Saanane, kuna haja ya kufanyika maridhiano kati ya CHADEMA na Zitto, kufukuzana katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu ni hatari sana kwa pande zote!

Hakuna atakaefaidi moja kwa moja, iwe Zitto au CHADEMA, kila mmoja atapoteza kwa kiwango chake!

Yaandaliwe mazungumzo yenye lengo la kusameheana, bila kuwekeana masharti yoyote magumu...

Mkuu inasemekana kuwa kuna watu waliwai ku-initiate mazungumzo kati ya CHADEMA na Zitto ila cha kushangaza jamaa akaja na masharti lukuki. Mojawapo ni kuwa yeye anadhani kuwa hana kosa, na kwa hiyo Chama ndio kimuombe radhi. Mimi ni kati ya watu wanaomkubali sana Zitto, ila nadhani ni mtu mwenye UBINAFSI au anayedhani yeye kuwa ni bora kuliko wengine, na ya kwamba yeye ni a perfect person. Na anachotaka kukifanya kwa wana-Kigoma ni kuwaaminisha kuwa YEYE ndio icon ya Kigoma, na kwahiyo ukimgusa yeye umegusa Kigoma. Mbona Kafulila alifukuzwa NCCR-Mageuzi na akugeuza mgogoro wake kuwa ni kati ya watu wa Kigoma na NCCR-Mageuzi? Na mbona Kafulila walimaliza mgogoro wao bila masharti? Kwanini iwe kwa Zitto?
 
Nenda uendako Zitto Zibeir Kabwe … raha ya jamvi ni viraka vyake na ukifika waambie umeshafika.
Nenda Zitto Z Kabwe ukifika tu, waambie umefika.
Tena waambie wewe si popo, mpaka matembezi yako yawe usiku.

Waeleze muda umefika unasema mbele ya mama mkwe kuwa na pale kwake umeianza safari, tena safari hii si kama ile.

Ikiwezekana usisitize kuwa, ile ilikuwa baba mkwe katafuta sifa kwa shemeji, akajaribu utoke kwa siku 90,lakini hii unaianza mwenyewe na ukiwaacha wao hawawezi walau kuiga nyendo zako.

Nasema nenda!
Unajua raha ya jamvi, ni viraka vyake, na ukihitaji kulikalia huna haja ya kuning'iza miguu, wala wasikushangae! kwa nini usiende mtoto wa uswazi ulojitambua, na zaidi hasara wanayo wao kwa upunguani.

Wajua siku ile kwa namna alivyokuwa akisema, nilidhani anabweka, kumbe alitaka sifa, anajua maneno yake ni kama kamba ya Ukili kumfunga Kondoo mwenye juhudi ya mapambano kisha ukamtengea kichwa.

Nenda kijana!
maana muda ungalipo na njia ushaijua, maana wahenga walisema mbali kwenda, kurudi ni kwa jirani. Lakini usisahau!!! kule unapokwenda wapo walimu manyang'au, waliojipanga kujaribu kwenda! Angalia

Wazalendo safari zao haziishi, wakifa huishi katika nyendo zao! Nenda tupo nawe —
 
Zitto usiachie jimbo. Pambana urudi Bungeni. Vi ginevyo umejimaliza kisiasa. Chama ni behewa tu na yako mengi yanakisubiria.

Anaweza kusimamia natamshi yake kuwa ubunge basi labda kwa nafasi ya uraisi. ZZK ni mfanyabiashara tu yule katafuta namna ya kuondoka kwenye siasa ili akatumie rasilimali aliyojikusanyia
 
Mkuu inasemekana kuwa kuna watu waliwai ku-initiate mazungumzo kati ya CHADEMA na Zitto ila cha kushangaza jamaa akaja na masharti lukuki. Mojawapo ni kuwa yeye anadhani kuwa hana kosa, na kwa hiyo Chama ndio kimuombe radhi. Mimi ni kati ya watu wanaomkubali sana Zitto, ila nadhani ni mtu mwenye UBINAFSI au anayedhani yeye kuwa ni bora kuliko wengine, na ya kwamba yeye ni a perfect person. Na anachotaka kukifanya kwa wana-Kigoma ni kuwaaminisha kuwa YEYE ndio icon ya Kigoma, na kwahiyo ukimgusa yeye umegusa Kigoma. Mbona Kafulila alifukuzwa NCCR-Mageuzi na akugeuza mgogoro wake kuwa ni kati ya watu wa Kigoma na NCCR-Mageuzi? Na mbona Kafulila walimaliza mgogoro wao bila masharti? Kwanini iwe kwa Zitto?
upo sahihi mkuu.
100%
 
Zitto usiwalambe miguu hao wafalme,chagua chama kingine uhamie.Waachie chama chao kilichojaa jazba,undugu,ukabila,chuki binafsi,roho mbaya na kutokupenda mawazo tofauti.
 
only83
Mkuu kila mtu ni bora ila challenge inakuja bora kuliko nani, wakati gani na bora kwenye kitu gani. kwa msingi huu usimhukumu/shangae mtu anaposema yeye ni bora. Just take your time and find what is he/she best of
 
Last edited by a moderator:
Ben ndugu yangu. Ushabiki ukizidi unaharibu radha ya "ushindi". Bahati mbaya kwa uwezo wa fikra zako huoni ni jambo gani Zitto anaweza kufanya zaidi ya kuomba msamaha. Sina shaka na uwezo wa Zitto Kabwe kisiasa, lakini nina shaka sana na uwezo wako kisiasa.
uskonde, una haki kikatiba kuamini unachoamini alimradi tu huvunji sheria. hata ukitaka kuamini mbuyu unaweza kugeuka kuwa mchicha wewe amini tu mradi hujavunja sheria yoyote ya nchi
 
Zitto usiwalambe miguu hao wafalme,chagua chama kingine uhamie.Waachie chama chao kilichojaa jazba,undugu,ukabila,chuki binafsi,roho mbaya na kutokupenda mawazo tofauti.
afadhali CDM wao hawakumkolimba zito.ingekuwa ni ccm zito anawaletea hizo siasa uchwara wangeshamzito zamani sana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom