Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Hakuna sababu ya kuvuliana nguo kwa kila upande kuomba radhi. Mimi nashauri Mhe. Zitto arudi bila masharti na tuendelee na mapambano kuelekea uchaguzi wa 2015.
 
Haiwi wala haitokuwa! Kwani wewe ndio Zitto? Au Mtama kwa watoto ndio msemaji wa Zitto?

Hao wanao mfisidi Zitto wao niwasemaji wa Chadema au kunya anye kuku tuuuu akinya bata kaharishaa? Waseme kosa la Zitto wa Tanzania wote wasikie Kama hawasemi inamaana walimpikia majungu Na mwenyezi mungu hamfichii dhalim....
 
Last edited by a moderator:
Halafu eti anataka kuombwa radhi huyu mimi nashindwa kumwelewa anataka utukufu bado hajajutia ngoja uchaguzi ujao upite na yeye asote mtaani tuone kama ccm watampatia nini.

Lakini mkuu huenda yale anayoshutumiwa na chama, yeye ana uhakika kuwa hakufanya pia hata kama alifanya basi ana uhakika kuwa si makosa, au kama ni makosa ana uhakika yanasameheka ndio maana anataka iwepo reconciliation baina yake na viongozi wa chama.

Pia tusikariri kuwa mtu akivunja sheria basi ndio hukumu, si sahii hata kidogo, Kwani Sheria nazo huundwa na watu ambapo naturally watu sio wakamilifu hivyo na sheria haiwezi kuwa kamilifu never. ndiomana hata bob Marley aliwahi kusema hivi " I will never be justified by the laws of mens" hivyo hapa chama muhimu watu wakeni chini muhafaka upatikane. OVER
 
Alishaandikiwa Barua kumjulisha Makosa yake akakimbilia Mahakamani.
Huyu mtu vp,?
 
Kat ya watu wanaotakiwa kujiandaa kisaikolojia kutokana na ZITTO kurudi ni pamoja na wewe BEN SAANANE

Kujiandaa kisaikolojia?Mimi?Unajidanganya sana.......!

By the way unaongelea kurudi,ni lini alitoka CHADEMA?
 
Lakini mkuu huenda yale anayoshutumiwa na chama, yeye ana uhakika kuwa hakufanya pia hata kama alifanya basi ana uhakika kuwa si makosa, au kama ni makosa ana uhakika yanasameheka ndio maana anataka iwepo reconciliation baina yake na viongozi wa chama.

Pia tusikariri kuwa mtu akivunja sheria basi ndio hukumu, si sahii hata kidogo, Kwani Sheria nazo huundwa na watu ambapo naturally watu sio wakamilifu hivyo na sheria haiwezi kuwa kamilifu never. ndiomana hata bob Marley aliwahi kusema hivi " I will never be justified by the laws of mens" hivyo hapa chama muhimu watu wakeni chini muhafaka upatikane. OVER

mkuu, zitto amesababisha vijana wengi sana qameangamia kisiasa huku yeye akijifanya mwema..vijana wotebuliowatajabkule juu walihama lwasababu ya zitto wapo akina juliana, mtela, na yuke mwizi wa simu, wako wengi sana...kumwondoa zitto chadema ni kundoa mama wa shetani...
 
Zitto ni CHADEMA damu, anaweza kufarakana na viongozi wake au wanachama wachache kutokana mistakes mbalimbali kama ilivyo kawaida ya ubinadamu, ila kamwe hawezi kukiacha chama (CHADEMA),

Kwa kuweka rekodi sawa, Zitto hata baada ya kufukuzwa CHADEMA hakuthubutu kukipaka chama matope bali yeye alikaa kimya tofauti na wahuni wengine wakina Shonza. (Silence is the source of great power), hali hii inathibitisha kwamba Zitto moyo wake bado upo CHADEMA na sio ACT, Yeye mwenyewe alishasema kuwa atakuwa wa mwisho kuondoka CHADEMA yaani kifo pekee ndiyo kitamtenganisha na CHADEMA na sio ubaya, wema, mtu au mazingira.

Pia lazima tujue hakuna aliyekamilika kwani hata biblia inasema hivi " Kama tukisema hatuna dhambi(mapungufu) tunakuwa tunajidanganya wenyewe nafsini mwetu tena zaidi twamfanya Mungu kuwa ni muongo"

Kwahiyo tunapoendelea kutafakari hoja hii ya uanachama wa Zitto, ni hivi anayejiona mkamilifu na mzalendo zaidi hata ya wale walioanzisha na kuikuza CHADEMA, basi na awe wa kwanza kumpiga Zitto mawe. OVER

Mkuu Shardcole. Hakuna anayepinga Zitto kurudi kundini iwapo atatubu (hata mwana mpotevu katika biblia alijitathmini na kugundua alipomkosea baba yake, aliporudi alijinyenyekeza na kuomba kufanywa mmoja wa watumishi wake,=hakutoa mashart= lakini baba yake akamkumbatia kwa upendo na kumpa nafasi ya juu katika wanae hadi wanae wengine wakaanza kumuonea wivu). hatuhitaji kurudia kumjulisha makosa yake ili aombe radhi, kwa sababu yapo wazi kabisa na yeye anayajua. Na kama anadai hayajui hakuna haja ya kumrudisha kundini maana atatutibua tena. Kutujia na mbwembwe za mashart ni upuuzi ambao nitashangaa sana kama chama kitaintatain. By now Zitto anatakiwa awe ameshajua kosa lake lilikuwa nini na yeye ndiye anayepaswa kukieleza chama na kueleza kwa nini anadhani sasa chama kimpokee. Akifanya hivyo nitakuwa wa kwanza kukisihi chama kimkumbatie na ikiwezekana kimpe mahala pa juu kama ilivyokuwa kwa mwana mpotevu. Kuendelea kujiinua kwa kukipa chama mashart ni muendelezo uleule wa kujiona yeye ni zaidi ya chama. Huo ni utoto - CHADEMA ni zaidi ya mtu yeyote na imebeba dhamana kubwa kuikomboa Tanzania. Yeyote atakayejiona wa maana zaidi ya CHADEMA hatumuhitaji. Hilo ndilo Zitto and the likes wanalopaswa kulijua.
 
Yani ninavyotamani huyu kijana mwenzangu zitto arudi katika chama na kukiendeleza.. Basi tu. Hata kama ni makosa hufanywa na binadam bana..msamaha kwa zitto ndio ukomavu kwa Cdm.
 
ameikana mpaka ACT kweli CDM ni chama chenye matunda mema
 
Kumbe hawa wote walikuwa CDM? Du basi kuna shida CDM kwa nini wapambanaji wote wanapita pale na kukimbia, nadhani kuna shida ya kuadministration ambayo inatakiwa kuwa addressed

Kati ya CHADEMA na CCM ni chama kipi kilichopoteza wanachama watiifu wengi? ni vema ungeizungumzia CCM kwanza kuwa kuna shida kwani wengi unaowaona maarufu sasa katika vyama vya upinzani walikuwa CCM.
 
Yani ninavyotamani huyu kijana mwenzangu zitto arudi katika chama na kukiendeleza.. Basi tu. Hata kama ni makosa hufanywa na binadam bana..msamaha kwa zitto ndio ukomavu kwa Cdm.
tumtamrudisha mkuu usijali
 
Kati ya CHADEMA na CCM ni chama kipi kilichopoteza wanachama watiifu wengi? ni vema ungeizungumzia CCM kwanza kuwa kuna shida kwani wengi unaowaona maarufu sasa katika vyama vya upinzani walikuwa CCM.
CCM ni chama cha wahuni na wapuuzi
 
Mtu kutojua kosa lake ni kosa kubwa kuliko kosa lenyewe.Mtu anayekuwa mgumu kuomba radhi ni hatari sana.Ukiomba radhi unapata muda wa kuonyesha ukweli wako.Ukishindwa kuomba radhi utakaa hivyo 'andiko ukutani'.
 
Naomba kuweka wazi...

Hakuna aliye juu ya chama.Kuna watu wanatafuta kutaka kuwa maarufu kuliko chama.

Zitto akitaka kurudi Chadema anapaswa kuomba radhi ajutie makosa yake na huu ndiyo msimamo rasmi.

Katiba ya chama iko wazi.Kukipeleka chama mahakamani ni kujifukuzisha mwenyewe ndani ya chama.

Wewe ni nani kwenye chama mpaka uongee kwa niaba ya chama?
 
HUELEWKI na umekaa kishabiki zaidi kwa kumchukia zitto UKABILA utakumaliza, jipangeni na litumieni hilo JEMBE mtavuka
kwani mara zote tunawaonya AKILI NDOGO zinawaongozeni MWILI MKUBWA

Kinachowaumiza sana ni kuwa Mliliandaa Bomu(Zitto) na kulitegesha ndani ya CHADEMA ili lilipuke CHADEMA wakagundua na kulihamisha na hadi sasa lipo hewani na hakuna anaetaka kulichukua sasa nashangaa mnabembeleleza bomu hilo lirudishwe CHADEMA. Bomu hilo litaweza kurudishwa CDM pale tu litakapokuwa limeteguliwa na halina madhara tena.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom