Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Tofauti ya Zitto na hawa ni kuwa yeye hajawahi kusimama hadharani na kuitukana Chadema hata siku moja. Hao vijana ni waste product ambayo haifai hata kugusa kwa mkono. Walitumwa watukane basi wacha wakae na matusi yao hukohuko ambako walidhani wamefika ila sasa wamegundua kuwa walitumika kama toilet paper.

Umenena vyema!
 
Naomba kipengele kwenye katiba ya chama inayosema ukitaka kugombea uwenyekiti unanyima ndio mnavyo jidanganya hapo lumumba
HUELEWKI na umekaa kishabiki zaidi kwa kumchukia zitto UKABILA utakumaliza, jipangeni na litumieni hilo JEMBE mtavuka
kwani mara zote tunawaonya AKILI NDOGO zinawaongozeni MWILI MKUBWA
 
Zitto aweke masharti kurudi CHADEMA kwani alitoka?

Anavyoingia bungeni anaingia kama mbunge wa chama gani?

Nimeshangaa sana..

Huyu amekiburuza chama mahakamani...

Kama anaomba msamaha wa chama afute kesi kwanza ndipo aombe radhi..
 
huwezi kumsoma zitto hata siku moja,anaweza akasemehewa ikifika uchaguzi mwakani akaleta madhara au kigeugeu
 
HUELEWKI na umekaa kishabiki zaidi kwa kumchukia zitto UKABILA utakumaliza, jipangeni na litumieni hilo JEMBE mtavuka
kwani mara zote tunawaonya AKILI NDOGO zinawaongozeni MWILI MKUBWA

Eti CCM mnaishauri Chadema

Mtasubiri sana..
 
chadema bila zitto hawawezi kujiendesha kabisa hata iweje tulisema kitambo kwamba watampigia magoti tu.
huu ni uwongo, zitto anahitaji chadema zaidi kuliko chadema inavyomhitaji zitto!
 
Nimeshangaa sana..

Huyu amekiburuza chama mahakamani...

Kama anaomba msamaha wa chama afute kesi kwanza ndipo aombe radhi..

That is not my point though.

Mwanachama ana haki ya kukiburuza chama mahakamani.

Na hajaomba msamaha.
 
chadema_clip.jpg


KWA UFUPI

Ataka aelezwe kosa lake, kama kweli aombe radhi hadharani.


CHANZO: Mwananchi


....Nadhani kosa kubwa litakalozuia kusamehewa na CHADEMA ni hilo la kutojua kosa lake hadi sasa. Iwapo Zitto hajaweza kujua kosa lake hadi leo, basi hastahili kurudi CHADEMA maana atarudia tena. CHADEMA inaweza kumsamehe makosa yote isipokuwa kosa moja tu LA KUTOJUA KOSA LAKE. Na katika hili CHADEMA isijisumbue kujaribu kumjulisha kosa lake maana tayari ilishafanya hilo vizuri sana, huo mchezo wa kitoto wamuachie aendelee kuucheza mwenyewe kama anadhani utamfikisha popote.
 
That is not my point though.

Mwanachama ana haki ya kukiburuza chama mahakamani.

Na hajaomba msamaha.

Isome vizuri Katiba ya Chadema kuhusu kupeleka maamuzi ya Chama mahakamani.
 
Isome vizuri Katiba ya Chadema kuhusu kupeleka maamuzi ya Chama mahakamani.

Siongelei haki ya mwanachama ndani ya CHADEMA.

Why should I do that? I am not CHADEMA.

Naongelea haki ya mwanachama kama Mtanzania.
 
Zitto niwa kuonewa huruma na kwa hakika yuko kwenye state of denial.

Mbali na waraka yeye na kitila waliandaa petition ya kupingana na chama na kitila alichangia 5milioni nyaraka zote zipo halafu mtu huyuhuyu pamoja na kuuza nafasi za ubunge anataka aombwe msamaha na chama.

Labda kama hicho chama ni chauma au act sio chadema

ZZK amesha
 
....Nadhani kosa kubwa litakalozuia kusamehewa na CHADEMA ni hilo la kutojua kosa lake hadi sasa. Iwapo Zitto hajaweza kujua kosa lake hadi leo, basi hastahili kurudi CHADEMA maana atarudia tena. CHADEMA inaweza kumsamehe makosa yote isipokuwa kosa moja tu LA KUTOJUA KOSA LAKE. Na katika hili CHADEMA isijisumbue kujaribu kumjulisha kosa lake maana tayari ilishafanya hilo vizuri sana, huo mchezo wa kitoto wamuachie aendelee kuucheza mwenyewe kama anadhani utamfikisha popote.

Naamini hakuna aliye juu ya Chadema.

Huu ujanjaujanja hautafanikiwa
 
Kwenye mgogoro wote mnapaswa kuingia bila masharti katika kutafuta mwafaka, zitto kama ana lengo la kujiunga na harakati chadema aondoe sharti nje ya hapo atabaki kutangatanga tu!
 
....Hahahaaaaa! Zittto bwana kiboko. Hivi Profesa keshajibu onyo aliloandikiwa na vijana wenye chama?

Zitto ni CHADEMA damu, anaweza kufarakana na viongozi wake au wanachama wachache kutokana mistakes mbalimbali kama ilivyo kawaida ya ubinadamu, ila kamwe hawezi kukiacha chama (CHADEMA),

Kwa kuweka rekodi sawa, Zitto hata baada ya kufukuzwa CHADEMA hakuthubutu kukipaka chama matope bali yeye alikaa kimya tofauti na wahuni wengine wakina Shonza. (Silence is the source of great power), hali hii inathibitisha kwamba Zitto moyo wake bado upo CHADEMA na sio ACT, Yeye mwenyewe alishasema kuwa atakuwa wa mwisho kuondoka CHADEMA yaani kifo pekee ndiyo kitamtenganisha na CHADEMA na sio ubaya, wema, mtu au mazingira.

Pia lazima tujue hakuna aliyekamilika kwani hata biblia inasema hivi " Kama tukisema hatuna dhambi(mapungufu) tunakuwa tunajidanganya wenyewe nafsini mwetu tena zaidi twamfanya Mungu kuwa ni muongo"

Kwahiyo tunapoendelea kutafakari hoja hii ya uanachama wa Zitto, ni hivi anayejiona mkamilifu na mzalendo zaidi hata ya wale walioanzisha na kuikuza CHADEMA, basi na awe wa kwanza kumpiga Zitto mawe. OVER
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom