Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

.....Zito hauna ujanja wa kuipa chadema masharti maana wewe bado ni mwanachama wa chadema
 
Huo ndio ''Msimamo rasmi'' wa CHADEMA?

Tatizo sasa Zitto anasema hajui makosa yake ni yepi na ndio sababu mjadala ni muhimu kufanyika kwa kuwa jambo moja linaweza kuwa na maana tofauti kati ya watu wawili. Kuna mambo ambayo Zitto anaona labda sio makosa (kwa mfano kusema kwamba accounts za chama hazijakaguliwa na CAG..) wakati chama kinaona hilo ni kosa na usaliti wa hali ya juu kwa kuwa Zitto kama Katibu msaidizi, alikuwa na uwezo au nafasi ya kulifanyia kazi kabla ya ''kuropoka'' nje

Nadhani alipokwenda mahakamani aliomba Katibu Mkuu ampatie maamuzi ya Kamati Kuu na alipewa.

Namshauri asome kilichoandikwa mle ndiyo makosa yake.

Mwanasheria wake siku ile pale Serena Hotel alikuwa anasoma nini kama sio makosa yake?

Tuache jamani kujifanya tuko juu ya chama.Huu ni ujinga
 
Asante kamanda Molemo, hakuna aliye juu ya chama.. Chama kwanza mtu baadae..

Unajua sikatai mhalifu yeyote kutubu na kurudi kundini.Ni jambo Jema

Ninachokataa mimi ni kukipa chama masharti.Hilo kamwe sitalikubali.
 
chadema bila zitto hawawezi kujiendesha kabisa hata iweje tulisema kitambo kwamba watampigia magoti tu.


Kauli kama yako hiyo hazimsaidii ZZK bali zinamharibia; hatukatai kwama ZZK ni mwasiasa mahiri; bali hata yeye anajua "he needs a vehicle" and a strong vehicle; a 6x6WD; like CDM to achieve his political ambitions; kubali usikubali; ndio maana hata yeye mwenyewe alimshukuru Cmdr Mbowe kwa namna ya kipekee kwa ushirikiano wake katika sakata la Escrow; bila moral, political and intellectual support waliyompa Wanaukawa, asingetoboa; believe me you!! Ma CCM walikuwa tayari kumchinjia baharini; lakini ile collective voice; strong arguments; patriotic verve; viliwatisha Ma CCM mpaka wakakubali ku-compromise that much kiasi kwamba wamebaki lame ducks! wanaugulia maumivu ya ngumi za uso kutoka UKAWA

Usimuharibie ZZK; mwacheni afanye informed decisions pasi na ushabiki mandazi na fitina!
 
Nadhani alipokwenda mahakamani aliomba Katibu Mkuu ampatie maamuzi ya Kamati Kuu na alipewa.

Namshauri asome kilichoandikwa mle ndiyo makosa yake.

Mwanasheria wake siku ile pale Serena Hotel alikuwa anasoma nini kama sio makosa yake?

Tuache jamani kujifanya tuko juu ya chama.Huu ni ujinga

kamanda Molemo Sidhani kama hao wanao lalamika wanajua katiba ya chama inasemaje hakuna aliye juu ya chama
 
Zitto kumaliza tofauti zake na chama chake ni jambo zuri,LAKINI si kwa kukipangia masharti kama hivyo,hapo ni kutaka kujiweka juu ya chama..na kama anategemea hilo kutokea atasubiri sana vinginevyo wataendelea kushirikiana tu bungeni kwenye maswala yanayohusu taifa na yenye tija kwa taifa letu

Viongozi wakae na Zitto na kumaliza tofauti zao,ndivyo siasa zilivyo hakuna rafiki wala adui wa kudumu. Wafanye hivyo haraka kama mkakati wa kuimaliza ACT na walio kurupuka kwenda huko bila kutumia akili na pia kama maandalizi ya chama kuingia Uchaguzi Mkuu mwakani kikiwa kimeungana! Ni dawa chungu kwa baadhi ya Wanachadema lakini ndiyo tiba ya mpasuko.
 
Kauli kama yako hiyo hazimsaidii ZZK bali zinamharibia; hatukatai kwama ZZK ni mwasiasa mahiri; bali hata yeye anajua "he needs a vehicle" and a strong vehicle; a 6x6WD; like CDM to achieve his political ambitions; kubali usikubali; ndio maana hata yeye mwenyewe alimshukuru Cmdr Mbowe kwa namna ya kipekee kwa ushirikiano wake katika sakata la Escrow; bila moral, political and intellectual support waliyompa Wanaukawa, asingetoboa; believe me you!! Ma CCM walikuwa tayari kumchinjia baharini; lakini ile collective voice; strong arguments; patriotic verve; viliwatisha Ma CCM mpaka wakakubali ku-compromise that much kiasi kwamba wamebaki lame ducks! wanaugulia maumivu ya ngumi za uso kutoka UKAWA

Usimuharibie ZZK; mwacheni afanye informed decisions pasi na ushabiki mandazi na fitina!

Naunga mkono HOJA
 
Hivi mathalani CHADEMA wakikataa hilo sharti alilowapatia Zitto, itakuwaje kwa Zitto?

Mtu mwovu hutanguliza mashaka! Kwani baada ya kumuvua nyadhifa zake zote amekuwaje? Hujasikia kapata kuwa Katibu wa PAC kwa nchi za kusini mwa Afrika! Hujasikia kapata tuzo ya Jamii! Hujasikia akiendelea kuisimamia kamati ya PAC!

Maisha ya siasa yatakuwa vile wakati utakavyoamua ingawa si salama kwa chama kinachokuwa kuanza kuendekeza migogoro ya ndani kwani kupoteza kura hata moja ni hasara kubwa, kupoteza kiongozi mwenye ushawishi na mvuto wa kisiasa ni hasara pia.

Chadema waangalie jinsi ya kumaliza migogoro yao kwani kama kisa kilikuwa enyekiti wa chama basi ulishamalizika na mwenyekiti alishatangazwa.
 
TBS ilidhibitisha kuwa Mh.Zito alibug,sasa ni busara akaomba msamaha,njia ipo wazi
 
Unajua sikatai mhalifu yeyote kutubu na kurudi kundini.Ni jambo Jema

Ninachokataa mimi ni kukipa chama masharti.Hilo kamwe sitalikubali.

Alafu mbaya zaidi siku za nyuma ulikua chini ya mamuzi ya chama leo hiweje ukipangie chama mamuzi? Uvunjifu wa Katiba
 
Si salama kwa chama kinachokuwa kuanza kuendekeza migogoro ya ndani kwani kupoteza kura hata moja ni hasara kubwa, kupoteza kiongozi mwenye ushawishi na mvuto wa kisiasa ni hasara pia.

Chadema waangalie jinsi ya kumaliza migogoro yao kwani kama kisa kilikuwa enyekiti wa chama basi ulishamalizika na mwenyekiti alishapatikana, kama kisa kilikuwa uongozi safu zilishaandaliwa na zinaendelea na kazi.
 
Tatizo la Zitto ni harakati zake za kutaka kugombea Uenyekiti CHADEMA
 
Hili sakata la ZITTO na chama chake likiisha, wa kwanza kujiona MAVI ndani ya CHADEMA atakuwa LISSU na MNYIKA kwa jnsi ambavyo walikuwa wakimtukana ZITTO kwenye vyombo vya habari na majukwaa ya siasa
 
"Kinachoendelea ndani ya chama chetu ni mapambano ya kukuza demokrasia. Ni mapambano baina ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina; waumini wa uwajibikaji dhidi ya wabadhirifu; na wapenda siasa safi dhidi ya watukuzao siasa majitaka."
 
"Kinachoendelea ndani ya chama chetu ni mapambano ya kukuza demokrasia. Ni mapambano baina ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina; waumini wa uwajibikaji dhidi ya wabadhirifu; na wapenda siasa safi dhidi ya watukuzao siasa majitaka."
Tehe teh amewapa WAHAFIDHINA masharti ya kumuomba radhi, tusubiri tuone.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom