Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Ni kama mwanamke asiye na akili,aliyemsaliti mumewe kwa dharau na kejeli kisa hana pesa na kuhamia kwa mwanaume mwingine,huko mambo yamebuma ndiyo anamkumbuka mume wa awali.
"baby,nimekumic na ninakupenda sana,tuombane msamaha tuyamalize"
Ovyoooo!!
ndo Zitto
 
Zitto analolizungumzia ni la msingi sana,kwanza waaeleze sababu za kutaka kumtimua kwa fact sio kwa maneno kama ya IPTL ambayo yameshindwa kuthibitishwa.Namuunga mkono

Atagombea tu hata bila ukawa,Ukawa wenyewe CUF wanalalamika NCCR wanalamika chadema wanatumia Ubabe sana bila ya busara
 
Naomba kuweka wazi...

Hakuna aliye juu ya chama.Kuna watu wanatafuta kutaka kuwa maarufu kuliko chama.

Zitto akitaka kurudi Chadema anapaswa kuomba radhi ajutie makosa yake na huu ndiyo msimamo rasmi.

Katiba ya chama iko wazi.Kukipeleka chama mahakamani ni kujifukuzisha mwenyewe ndani ya chama.
Saccos yenu haina dira wala mwelekeo hivi sasa
 
acha umbea kwani zitto alikuambia anataka kugombea uraisi

kwani kilichomkosanisha na hao wakuu si kuutaga uenyekiti, au kugombea urais?? we unadhani dr. slaa ataacha kipaji chake cha kugombea kwa zito?? thubutu?? au mbowe asiwe mwenyekiti?? nani kasema. Kama kweli mnania zito arudi mpeni nafasi ya kuwa mwenyekiti japo kwa wiki moja tu.
 
kwani kilichomkosanisha na hao wakuu si kuutaga uenyekiti, au kugombea urais?? we unadhani dr. slaa ataacha kipaji chake cha kugombea kwa zito?? thubutu?? au mbowe asiwe mwenyekiti?? nani kasema. Kama kweli mnania zito arudi mpeni nafasi ya kuwa mwenyekiti japo kwa wiki moja tu.
sina muda wa kushindana na mfu kama wewe
 
This is very funny! Zitto bwana alienda mahakamani kupinga yeye kufukuzwa, kwa hiyo yeye ndio bado anang'ang'ana kubaki! Leo atangaza masharti ya kurudi! Chama hakijamtaka bado!
 
Kwa kauli hiyo sioni nafasi ya muafaka. Upande mmoja lazima ukubali kuwa wenyewe ni wahifidhina, wabadhirifu na wana siasa za majitaka...

Anyway ndio wanasiasa wetu na siasa zao.

Hiyo ni kauli ya wakati ule anatimuliwa, sio kauli ya jana wala juzi.Ni mwaka karibu mmoja uliopita.
 
mkuu, zitto amesababisha vijana wengi sana qameangamia kisiasa huku yeye akijifanya mwema..vijana wotebuliowatajabkule juu walihama lwasababu ya zitto wapo akina juliana, mtela, na yuke mwizi wa simu, wako wengi sana...kumwondoa zitto chadema ni kundoa mama wa shetani...

Mkuu kuna kisa kimoja cha Nabii Eliya na mtumishi wake Elisha pindi Eliya alipokuwa akielekea mlimani ili atwaliwe na gari la moto na Mungu,
basi walipokuwa wakienda, njiani kila mtu alikuwa akimwambia Elisha ya kwamba je unajua kuwa bwana wako Eliya leo atatwaliwa na gari la moto na kukuacha? Elisha akawajibu na kusema nyamazeni ndiyo najua. Tena walipofika mbele watu wengine wakamuuliza Elisha swali hilo hilo, lakini tena Elisha akawajibu, "Nyamazeni ndiyo najua" na hatimaye Elisha alifanikiwa kufika safari yake na Eliya na hata baada ya kweli Eliya kutwaliwa na gari la moto lakini bado Elisha alifanikiwa kupata upako maradufu ya sehemu ya Eliya. Na hii ndiyo ilikuwa faida ya Elisha kwa kutokukubali kusikia watu wanasema nini na badala yake alifocus kwenye goal yake.

So hapa na sisi goal yetu ni kuona reconciliation inafanyika, Hatupaswi kuangalia au kukumbushana ubaya wetu either wa Zitto au wa viongozi au pengine wetu sisi wanachama juu ya hili, sababu sisi wote TUNAJUA, hapa goal yetu ni kuona muhafaka unapatikana na wote tunarudi kwa pamoja tukiwa wenye afya mifupani mwetu tayari kwa kuendeleza harakati za kumkomboa mtanzania.

Pia siungi mkono hoja eti Zitto au Viongozi watoke hadharani na kuanisha makosa yao huko itakuwa ni kuvuana nguo, bali napendekeza baada ya reconcialition tena ya siri na watu wachache wenye hekima, ndipo tuone viongozi wa chama na Zitto wakitoka nje na kukumbatiana wakiwa wamoja kama zamani. OVER
 
Uchaguzi umeshapita, mbowe amejipa uenyekiti sasa ni muda wa muafaka
 
Ili kuepusha haya mambo kujirudia ni mhimu kukaa chini wakazungumza klla upande kuna sehemu uliteleza waelezane ili mwisho wasonge mbele bila maridhiano ya namna hii itachukua mda mrefu sana kuwatoa CCM hakuna kinachoshindikana kama pande zote mbili watakuwa na nia ya maridhiano. Sote tunaelewa tofauti za hapa na pale zilizokuwepo baina ya CDM na CUF lakini leo ni wameungana na wanapiga mzigo...
 


“Ukweli wangu ndani ya Chadema ni nini? Lakini mimi ninaona sina kosa ndani ya Chadema. Ninachotaka mimi nielezwe ukweli bila chembe ya shaka makosa yangu mimi ni nini,” alisema na kuongeza:

“Nitakuwa tayari kuomba radhi hadharani kama ikibainika nilifanya makosa na kama ikibainika chama kilifanya makosa, nacho kiwe tayari kuomba radhi hadharani na ukweli uwe mbele katika maridhiano.

“Kama hakutakuwa na ukweli itakuwa vigumu kupata mwafaka. Mimi sina tatizo. Nirudie nilivyosema bungeni kuwa nina-miss sana (ninapenda sana kuwamo kwenye) harakati za mageuzi kipindi hiki za kuiondoa CCM madarakani.”


Nawasiwasi na itakuwa vigumu kwa milango kuwa wazi kama Kauli zenyewe bado ni kama hizi.Kamati Kuu ya Chama imekaa chini nakufikia tamati ya maauzi leo hii ije hadharani kuwa ilifanya Makosa-lazima mwenye kutegemea hilo anamapungufu na jeuri isiyo na faida.
Mara nyingi akiba ya Kauli na maneno ni silaha ya maisha na mahusiano na watu wengine. Mbunge wangu wa hiari muda mwingine ni vizuri katika mambo mengine ya kuzungumza na kwa mtu binafsi au magazeti akiba ni muhimu sana.
Ni kurejeshe ushauri wa Prof.Mwandosya pale Bungeni majuzi juu ya madai kuwa nawe ulichukua kidogo na ninashukuru uliuzingatia ,hivyo basi si lazima kuwa na majibu ya hapa na pale kila haya magazeti yanoipokufuata kwa maoni.






“No comment (sina maoni) kwa hilo. Siwezi kuzungumzia suala hili katika media (vyombo vya habari),” alisema Mbowe


Ebu cheki hayo majibu hapo juu.Lakini hiyo haitoshi-Mhe.Mbunge hata maoni yako yangeweza kuwa mafupi na yenye kubakiza akiba ya maneno.

Mfano; Suala langu liko mahakamani na “Nilifungua kesi kwa sababu ya kulinda uanachama wangu, lakini mazungumzo yakifanyika kati yetu pengine nafasi ya kusonga mbele kwa amani na ushirikano inawezekana. Hili litategemea ushiriki wa sisi pande mbili kwenye mgogoro huu.





Kuhusu kesi aliyofungua mahakamani dhidi ya Chadema, Zitto alisema:

“Nilifungua kesi kwa sababu ya kulinda uanachama wangu, lakini mazungumzo yakifanyika na kujua kosa langu ni nini, nitaifuta kesi hiyo na kuanza upya harakati.”

Kuhusu taarifa za kujiunga kwake na chama kipya cha ACT-Tanzania alisema, “Hizo ni taarifa ambazo hazina ukweli wowote.”




Haya maneno ya kuweka masharti hayana ladha na hayawezi kuleta suluhu.

 
Mkuu Shardcole. Hakuna anayepinga Zitto kurudi kundini iwapo atatubu (hata mwana mpotevu katika biblia alijitathmini na kugundua alipomkosea baba yake, aliporudi alijinyenyekeza na kuomba kufanywa mmoja wa watumishi wake,=hakutoa mashart= lakini baba yake akamkumbatia kwa upendo na kumpa nafasi ya juu katika wanae hadi wanae wengine wakaanza kumuonea wivu). hatuhitaji kurudia kumjulisha makosa yake ili aombe radhi, kwa sababu yapo wazi kabisa na yeye anayajua. Na kama anadai hayajui hakuna haja ya kumrudisha kundini maana atatutibua tena. Kutujia na mbwembwe za mashart ni upuuzi ambao nitashangaa sana kama chama kitaintatain. By now Zitto anatakiwa awe ameshajua kosa lake lilikuwa nini na yeye ndiye anayepaswa kukieleza chama na kueleza kwa nini anadhani sasa chama kimpokee. Akifanya hivyo nitakuwa wa kwanza kukisihi chama kimkumbatie na ikiwezekana kimpe mahala pa juu kama ilivyokuwa kwa mwana mpotevu. Kuendelea kujiinua kwa kukipa chama mashart ni muendelezo uleule wa kujiona yeye ni zaidi ya chama. Huo ni utoto - CHADEMA ni zaidi ya mtu yeyote na imebeba dhamana kubwa kuikomboa Tanzania. Yeyote atakayejiona wa maana zaidi ya CHADEMA hatumuhitaji. Hilo ndilo Zitto and the likes wanalopaswa kulijua.

Nimekuelewa kamanda, sasa cha muhimu viongozi wakae chini then majadiriano yafanyike na humo ndani ya kikao watapata nafasi ya kujua kila mtu makosa yake na kuombana radhi.
 
Kama Zitto anadai sharti hilo ndo arudi, maana yake tayari hayuko Chadema. Sasa mahakamani alienda kufanya nini. Maana mahakamani alikimbia ili asivuliwe uanachama. Sasa anaweka masharti. Sijamwelewa kabisa. Je mahakama ikiamuru asifukizwe hatorudi hadi aombwe msamaha. Nafikiri bado hajatumia busara. Kusamehana nikuzika tofauti.
 
2015????....sijui ntaponea wapi..?
Nlitaraji kwenda chama kngne cha upinzani..c unajua kwa makamanda nimelikoroga?
NA SASA ndyo kuna hii UKAWA,yarabi toba...
Maskini ubunge wangu..
Magamba nao nimewasaliti..
U lecturer??graduates nao shazi..
USALITI?
 
Kinachowaumiza sana ni kuwa Mliliandaa Bomu(Zitto) na kulitegesha ndani ya CHADEMA ili lilipuke CHADEMA wakagundua na kulihamisha na hadi sasa lipo hewani na hakuna anaetaka kulichukua sasa nashangaa mnabembeleleza bomu hilo lirudishwe CHADEMA. Bomu hilo litaweza kurudishwa CDM pale tu litakapokuwa limeteguliwa na halina madhara tena.QUOTE=11323989]Kujiandaa kisaikolojia?Mimi?Unajidanganya sana.......!
By the way unaongelea kurudi,ni lini alitoka CHADEMA?

[/QUOTE]


Tatizo lako unaweka 'Like popote tu hapo juu unakubali hajaondoka CHADEMA,
Leo Zitto anataka apigiwe magoti na aelezwe makosa yake la sivyo mumuwache asepe viroho vinawadunda washabiki
Mkuu wenu akimpigia magoti mtafahamu? kwani alishagawa Mawaziri vivuli kibao kwa NCCR na CUF hamkubwata leo Mbatia adui wenu na aliyefunga ndoa na CCMkarudi kwenu
 
Chadema hatumuhitaji sana Zitto kama yeye anavyoihitaji Chadema.

Sitarajii kabisa eti viongozi wetu wanamuita zzk katika meza ya mazungumzo ama maridhiano kama anavyosema.

Kama yeye anaomba kukutana na viongozi wetu ili kuzungumzia hatma yake baada ya kubaini kuwa chama chake cha wasaliti ACT hakiwezi kumtoa basi atume maombi rasmi kwa uongozi wetu ili afikiriwe.

Kama anajidanganya kuwa hajui kosa lake basi ni dhahiri kuwa ni mwepesi wa kusahau na asidhani na sisi ni wepesi wa kusahahau. Asifikiri kuwa anaweza kutuchezea akili kwa maneno ya hadaa kuwa hajui kosa lake.

Na mimi niseme wazi kabisa kuwa tangu Zitto "ametimuliwa" kutoka chamani ni ukweli ulio dhahiri kuwa chama kimetulia. Hakuna uvujaji wa taarifa za chama kama ilivyokuwa hapo siku za nyuma wakati aki Naibu Katibu Mkuu. Hakuna maneno ya uchonganishi na fitna baina ya viongozi wetu wa juu. Tangu ameondoka hatujasikia japo tetesi tu za malumbano baina ya viongozi wetu wakuu.

Hii inadhihirisha kuwa pamoja na mambo mengine mengi ya kishenzi aliyokuya anayafanya, zzk alikuwa ni mfitini mkubwa sana. Ndio maana kuondoka kwake imekuwa ni ahueni kwa ustawi wa chama.

Kama yeye anadai kuwa ametu-mis, basi atambue kuwa sisi hatujam-mis hata kidogo.
 
Last edited by a moderator:
Nani amuombe radhi,yaani chama kupitia viongozi wamuombe radhi?
Haitotokea,yeye aombe msamaha ajadiliwe na uamuzi ufanyike. Hakuna aliye juu ya chama. Taasisi ni zaidi ya mtu mmoja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom