Mkuu kuna kisa kimoja cha Nabii Eliya na mtumishi wake Elisha pindi Eliya alipokuwa akielekea mlimani ili atwaliwe na gari la moto na Mungu,
basi walipokuwa wakienda, njiani kila mtu alikuwa akimwambia Elisha ya kwamba je unajua kuwa bwana wako Eliya leo atatwaliwa na gari la moto na kukuacha? Elisha akawajibu na kusema nyamazeni ndiyo najua. Tena walipofika mbele watu wengine wakamuuliza Elisha swali hilo hilo, lakini tena Elisha akawajibu, "Nyamazeni ndiyo najua" na hatimaye Elisha alifanikiwa kufika safari yake na Eliya na hata baada ya kweli Eliya kutwaliwa na gari la moto lakini bado Elisha alifanikiwa kupata upako maradufu ya sehemu ya Eliya. Na hii ndiyo ilikuwa faida ya Elisha kwa kutokukubali kusikia watu wanasema nini na badala yake alifocus kwenye goal yake.
So hapa na sisi goal yetu ni kuona reconciliation inafanyika, Hatupaswi kuangalia au kukumbushana ubaya wetu either wa Zitto au wa viongozi au pengine wetu sisi wanachama juu ya hili, sababu sisi wote TUNAJUA, hapa goal yetu ni kuona muhafaka unapatikana na wote tunarudi kwa pamoja tukiwa wenye afya mifupani mwetu tayari kwa kuendeleza harakati za kumkomboa mtanzania.
Pia siungi mkono hoja eti Zitto au Viongozi watoke hadharani na kuanisha makosa yao huko itakuwa ni kuvuana nguo, bali napendekeza baada ya reconcialition tena ya siri na watu wachache wenye hekima, ndipo tuone viongozi wa chama na Zitto wakitoka nje na kukumbatiana wakiwa wamoja kama zamani. OVER