Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Kamanda kwenye maisha na siasa sio kila kitu kitapata majibu kama tutakavyo. Kama unaona unaweza kurudi kufanya kazi na CDM ni bora kurejea kwenye meza ya maridhiano bila masharti yeyote.

Mgogoro wa Israel na Palestina unashindwa kupata suluhisho la kudumu kwani pande zote hazikubali kwenda kwenye maridhiano bila masharti yasiyotekelezeka.

Mchawi hayupo zaidi ya wakati. Chama ni watu ambao wanakuja na kutoweka, kufa, kustaafu, kuhama, nk ukitaka majibu yote itakuwa ngumu.

Mtaji mkubwa wa mwanasiasa ni watu. Rudi fanyeni maridhiano , piga kazi andika kitabu weka ukweli wako wazi wacha tusome. Tutaamua. Ila ukitaka chama kikuombe msamaha, sasa mimi niliyeko huku ndandahimba nimekufanya nini? Wewe sema baadhi ya watu muombane msamha kwani kuna watu mlikoseana kibinafsi kwenye ule mgomvi. Ndio maana nakubaliana na msemo wa bakiza na akiba.

vuta pumzi rudi kazini. Ama unataka kuwa kama mandela bila sisulu hurudi?
Mlimwita msaliti, sasa mnambembeleza kurudi?
 
Watu gani wakae chini?

Hivi unacheza na Taasisi iitwayo Chadema?

Si walisema chama kitakufa?

Hivi ulibahatika kushuhudia mkutano mkuu jinsi kulivyokuwa na shamrashamra?

Kweli nijuavyo chadema sipati picha jinsi ilivyotokea huku lakini itumike busara tu binafsi kilichomtokea zito up to now ni tosha kabisa kwake kuwa makin zaid lakini akikubali kosa kama kweli alihasi chama apewe last chance huku wakiwa wanamfuatilia kwa karibu sana
 
Dhambi ya usaliti huwa haiishi kwa mtenda lakini akijirud akakili kosa na kuomba msamaha yapaswa kukaa chino na kuyamaliza hata vitabu vya dini vinatufundsha hivyo rejea kwa petro , mwana mpotezu aliyeamua kurud kwa baba yake
 
Mambo ya cdm waachieni cdm wenyewe. Hivi lengo hasa la ccm kuchombeza kwenye hii issue ni nini? Kama kweli ccm wanaupenda upinzani imara kwa manufaa ya taifa basi na tuone michango ya kujenga.
 
Tatizo lako unaweka 'Like popote tu hapo juu unakubali hajaondoka CHADEMA,
Leo Zitto anataka apigiwe magoti na aelezwe makosa yake la sivyo mumuwache asepe viroho vinawadunda washabiki
Mkuu wenu akimpigia magoti mtafahamu? kwani alishagawa Mawaziri vivuli kibao kwa NCCR na CUF hamkubwata leo Mbatia adui wenu na aliyefunga ndoa na CCMkarudi kwenu

Ukisoma ulichokiandika ukarudia zaidi ya mara 2 utajielewa wewe ni mtu wa aina gani na uwezo wako wa kufukiri unaishia wapi.[/QUOTE]
Jifunze ku-Quote basi maana hapo juu hakuna kielekacho
mm nilikukumbusha kuwa uli-'Like' Post # 127 ya Saa-Nane ulikijua alichosema mwenzako????
 
Kwani Zzk kwa sasa yupo wapi hadi atoe masharti? Si kila mara anajinasibu kuwa yupo CDM?
 
Zito ni tishio kw mafisadi ndio maana chadem tunaona tumetengana na mtu muhimu sana
 
hakuna marefu yasiyokuwa na ncha wakae chini wamalize tofauti zao kama Kafulila na Nccr
 
Acha ujinga wewe, tatizo unadandia treni kwa mbele, ni wapi umeona nimekubali eti chama kimuombe Zitto mkono? Msimamo wangu upo wazi, reconciliation ifanyike kwa siri chini ya viongozi na wazee wachache wenye hekima then watoke nje wakiwa wamoja tujenge chama. Naishia hapa kama huelewi njoo nikupe notes kabisa uzikeshee huenda utanielewa.
we jamaa kama uko akilini mwangu
 
huu ujinga sasa

if you want to clean your dirty laundry, why call the social media??

foook
 
Morinyo wew ndo mpotoshaji mkubwa! Mselewa yupo sawa uanachama wa zitto cdm upo kwa amri ya mahakama so usituletee u magamba


Sasa kama hawajai kumfukuza hilo la mahakama linatoka wapi?
 
Kwenye ukweli lazima tuseme,Tangu waondoke akina Zitto CHADEMA imeonekana kupoteza mwelekeo,Kinapoteza mvuto kwa wananchi na viongozi wengi hawana mvuto kwa wananchi,Angalau Dr Slaa wanamsikiliza lakini hawa wengine ni wepesi mno kisiasa.Zitto bado anakubalika na watu wengi hasa maeneo ya mbali na mijini ambapo ndipo kuna wapiga kura wengi ambao wanampenda mtu na sio chama.Zitto arudishwe chamani haraka na wala hili swala haliitaji mjadala.
 
Vijana wa chadema acheni kumpakazia ZZK toweni ushahidi!Achen kufuata mkumbo?Zitto ni xaid ya wote Chadema!Dogo yuko vzr xn hata sakata la escrow dogo ameshine!Acheni chuki za kijinga hakuna wa kumpambanisha na ZZK chadema!

Sielewi maslahi ya CCM katika hili.

Duh!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom