Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Baada ya maamuzi ya Kamati Kuu chama kimetulia maradufu.Ni mwendawazimu tu atakayedhani eti kuna mgogoro ndani ya Chadema..

Na ndiyo maana wafuasi wote wa Lumumba buku 7 wapo hapa.Utashangaa wana maslahi gani ndani ya Chadema eti wanataka Chadema imrudishe mwanachama wake

Hapana Molemo...Kutulia huko ni dalili ya u imla...chama chochote active lazima kiwe na siasa za ndani za chama...demokrasia ya ndani....Napenda zaidi Zitto arudi CHADEMA...Ingawa asiporudi....sitaiacha CHADEMA kwa sababu nakipenda zaidi chama na sio mtu...ila ni mpumbavu tu anaebeza mchango wa Zitto katika siasa za Upinzani
 
Kurudi anataka ila kufukama hataki,kwani kaenda kumpigia magoti arudi kama sio kumbwelambwela ..na nilisema tu alitaka aitumie escrow ili ajioneshe mpambanaji kumbe chumia tumbo tu
 
Binafsi naamin hata kama zitto atarudi atakuwa mpole,mwenyetahadhari na matendo yake. Kukisambaratisha chama cha upinzani ni dhambi kubwa. Arudi kundini,tusonge mbele
 
Naomba kuweka wazi...

Hakuna aliye juu ya chama.Kuna watu wanatafuta kutaka kuwa maarufu kuliko chama.

Zitto akitaka kurudi Chadema anapaswa kuomba radhi ajutie makosa yake na huu ndiyo msimamo rasmi.

Katiba ya chama iko wazi.Kukipeleka chama mahakamani ni kujifukuzisha mwenyewe ndani ya chama.
Hii inabidi ibadilishwe hii.

Au la katiba ya nchi izuie kuwa na organizations zinazozuia members wake kwenda mahakamani.
 
Kosa la Mwaka ZZK kurudi CDM, aende huko akasaidiane na CCM. Msaliti atatusaliti mara ngapi kabla hajafanikiwa??? MBOWE AND SLAA LET THE PIGLET GO
 
Naomba kuweka wazi...

Hakuna aliye juu ya chama.Kuna watu wanatafuta kutaka kuwa maarufu kuliko chama.

Zitto akitaka kurudi Chadema anapaswa kuomba radhi ajutie makosa yake na huu ndiyo msimamo rasmi.

Katiba ya chama iko wazi.Kukipeleka chama mahakamani ni kujifukuzisha mwenyewe ndani ya chama.
wewe mkuu umenena vema lakini zitto alikua hana jinsi otherwise alikua anatemwa uanachama wake so jamaa kwa kutetea position yake akaamua kufanya alichofanya uancho ona wewe ni kudharirisha chama.
 
Zitto just come back bro. I'm thirsty of you Tanzania needs you kamanda
 
Hapana Molemo...Kutulia huko ni dalili ya u imla...chama chochote active lazima kiwe na siasa za ndani za chama...demokrasia ya ndani....Napenda zaidi Zitto arudi CHADEMA...Ingawa asiporudi....sitaiacha CHADEMA kwa sababu nakipenda zaidi chama na sio mtu...ila ni mpumbavu tu anaebeza mchango wa Zitto katika siasa za Upinzani

Kuvujisha siri za chama mitandaoni ndiyo demokrasia?

Kuanzisha makundi ya uasi ndani ya chama ndiyo demokrasia?

Kutukana viongozi mitandaoni ndiyo demokrasia??

Labda sijui maana ya demokrasia......
 
Uzuri wa siasa za Tanzania, hawa wote wanaojenga hoja na vioja wakisema hawataki Mhe. Zitto arudi CHADEMA, lakini ndiyo hawa hawa ambao kesho kama Mhe. Mbowe au Dkt. Slaa wakisema tunamrudisha Zitto kwenye kundi la CHADEMA, utawasikia tena wakisema, siasa hazina marafiki au maadui wa kudumu.

Siasa za Tanzania ni vichekesho vitupu!.

Ndiyo maana kuna hoja zinasema, siasa za Tanzania zimejaa misukule!
 
Katika siasa hakuna wadhifa wa kudumu, Zitto ni mhimu arejee CHADEMA kwa ajili ya utengemano na hasa wakati huu tunapoelekea uchaguzi. Habari zozote aitakazoonesha Zitto anataka kurejea CHADEMA wahanga wa kwanza wa taarifa hizo watakuwa CCM, CCM siku zote wamekuwa msitari wa mbele katika kuhakikisha Zitto harejei CHADEMA kwa manufaa yao. Namsifu Zitoo kwa kuw imara wakati wote wa mgogoro, hakuonesha kuyumba. Na sas ni wakati wa viongozi wa Chadema kukaa chini na kutafakari ili hatimaye wamrejeshe Zitto kundini kwa mstakabari wa uchaguzi mkuu ujao. Mbowe+Slaa+Alfi+Mnyika+Lisu+Zitto+Lipumba+Seif+Mbatia=kuanguka kwa CCM.
 
Watu tuwe serious Zitto anaweza wekea masharti CHADEMA?

Anatapatapa tu.Nyota yake ya kisiasa imeshaisha.Ni politically frustrated.

Uchaguzi mwakani hajui ashike tawi la chama kipi kugombea mwakani.Kila akiangalia vyama vingine vinavyoonekana imara vimeshaungana kuunda UKAWA.Hivyo akitaka kugombea chama chochote lazima apate approval ya UKAWA ambayo anajua kuipata si rahisi.

Hapo ndipo jasho linamtoka kuwa aweza pigwa chini na vyama vyote vinavyounda UKAWA akashindwa kugombea ubunge ndio anajifanya ohhhh nataka kurudi kwa masharti!!!!!!!!!

Mbona kabla ya mgogoro alishasemaga hana mpango wa kugombea tena?
 
zitto hana option akitaka kuendelea vizuri na siasa arudi cdm kwa kuomba radhi , la hawezi fanya harakati makini nje ya ukawa
 
Yeye aende wala asirudi kwa CDM ni adui Wa Demokrasia nchini!

Km hafahamu kosa lake Basi aende mahakamani akakishitaki chama kwa kumtuhumu mambo ambayo si kweli!
 
hebu mnijuze toka zitto aondoke uthabiti umeongezeka au umepumgua cdm?Hebu jiulize cdm wangalikuwa passive zitto na kafulila wangewamudu wahafidhina wa ccm escrow watu hutegemeana hizo fikra za fulani zaidi huwezi kuwa na chama labdda tff
 
Uko sahihi mkuu...mimi ni moja kati ya watu tuliokuwa na mtazamo hasi juu ya Zitto....lakini kwa sasa CHADEMA wasuluhishe migogoro yao wawarudishe makamanda kama Zitto...huyu hajawahi kukisema chama vibaya wakati huu yuko katika mgogoro....No one is perfect...Zitto ni victim wa siasa anazofanya...We need him back kwa kweli

Naunga mkono hoja kamanda.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom