Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Why zito with j.makamba, and not with mnyika, T. Lissu, mdee or lema. Zito hueleweki umezidi kuambatana na hao magamba ndio maana napata wasiwasi kwanini hushirikiani na watu ambao unaoendananao kiitikadi na mara kwa mara kwenye misimamo yako upo na j.makamba?
- Zitto, Januari, Nape ni just a symbolism tu on behalf ya Vijana wengine wote maana huwezi wataja wote kwa majina ni wengi sana,

- HOWEVER: IT IS about time sasa tukajikita kwenye Taifa na Vijana tuangalie the experience ya Vijana kwenye power na hasa kama toka tuanze kuwapa nafasi kuna mabadiliko kitaifa ambayo yanaweza kwua accounted for kwamba ni Vijana ndio sababu yake, kama hayapo then tuachane na Vijana kwenye Taifa, wabaki kwenye vyama tu,

- lakini kumshambulia Zitto kwa sababu za kibinafsi zaisi kuliko mshiko kwa Taifa, inaleta maswali mengi sana kuliko majibu na hasa kama Great Thinkers kweli tupo commited na Taifa au interest za binafsi? I mean hizi never ending Zitto's attacks in unproductive kwa Taifa, mimi sijawahi kusikia Zitto emetoa hoja au maswaada bungeni ambao ni against masilahi ya taifa, sasa tunamuhukumu na makosa gani kwa Taifa?

- Au ni kutaka kwake kuchukua fomu ya Uenyekiti huko CDM ndio dhambi ya kumfanya asifae kua Rais? I mean are we being fair kwa Taifa na Vijana wengine wote kwa sababu kumhukumu Zitto bila hoja na hasa on Ujana wake tunawahukumu vijana wote nchini, Great Thinkers tulitakwia kuona hilo mapema kwamba for that tunawapalilia wazee kuendelea sasa mabadiliko yatatokea wapi ambayo JF tumekuwa tukiyalilia for years!

I mean tufike mahali tutenganishe National interest na personal interest, Zitto ni symbol tu ya Vijana wengi wenye uwezo ambao wanaona wakati ni huu, sasa it should be a National debate kwa kuangalia the history je toka vijana waanze kushika power kwenye vyama mpaka taifa, kuna anything good kwa taifa as opposed na kabla hawajashika?

FMEs!
 
Kwani kuna ubaya kwa Zitto kugombea urais? ni haki yake kikatiba, na chadema ni chama cha kidemocrasia ilani ya chama chetu haimzuii Zitto kufanya hivyo.

Hakuna ubaya kwa Zito kugombea urais, na wala chama chake CDM haikimzuii kugombea; bali katiba iliyopo hairuhusu mgombea chini ya miaka 40. Ninaamini hiyo ndiyo hoja na si kumwandama Zito kama anafaa kugombea urais ama la.
 
Zitto is quality guy, na anafaa sana kuwa rais wa nchi hii, kundi la akina slaa wanamuogopa sana huyu jamaa. Ki ukweli hata CCM wanajua CDM wakimueka huyu jamaa kugombea urais ndo mwisho wao. Slaa hauziki kabisa na eyari ameshajeruhiwa sana kwenye uchaguzi wa 2010 na hakubaliki na makundi yote ya jamii.
BIG UP ZITTO

Wenye akili huwa wanasoma maandishi ukutani kwa jinsi CCM mnavyomwogopa Slaa.Na huwa mnatusaidia sana kumpata mgombea anayefaa kupitia CDM
 
SISI WANACHADEMA TULISHAAMUA NA KUPITISHA KUWA MGOMBEA WETU WA KITI CHA URAIS CHAMANI NI DOKTA WILLIBROAD SLAA, ENYI WANA-CCM MGOMBEA WENU MNAYEMTAMANI SANA KUPITIA CHADEMA HUYO NDIYE NANI HUYO TENA?????????

Haaaa haaa haaaaa haa haa haaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!! Niacheni mie nicheke. Yaani CCM mnavohangaika na mtu mmoja tu ndani ya CHADEMA kwa jina la Dokta WIllibroad Slaa!!!!!!!!!

Eti waraka wa Siri bila mwanzilishi wake wala nembo ya CHADEMA, my foot!!!!!!!!!! Barua kama hiyo hata Ben Sanane hawezi kuandika na kudai ni waraka wa chama achilia mbali hata kisingizio chochote kwa Dogo Zitto Kabwe kuweza kufanya kazi hii ya kihayawani.

Ni kweli tunajua mnavyohaha kushoto na kulia mfanye nini kukiua CHADEMA kabla ya 2015 lakini kwa hapa mmenoa, tafuteni mlango mwingine pa kutokea huko huko kukipa uhai mpya UFISADI nchi lakini si kupitia CHADEMA. Hivi kumbe hata hivi VIRUSI vyenu humu kumbe hawaambieni ukweli kwamba hapa mmekula ya chuya?????

Eeehee, twambieni kwamba tofauti na Dokta wa ukweli kuwa ndiye mgombea wetu rasmi wa kiti cha urais 2015 nyinyi CCM mgombea wenu wa kiti hicho kupitia CHADEMA ni nani huyo??

Hakika kwa mihangaiko yenu hii yote, huyu Mtanzania mwenzetu akidhurika kwa namna yoyote ile; ama kupewa sumu, ajali za kutoelezeka na nini vile, wenzetu msiwe mbali kubeba mzigo huo.

Ndani ya CHADEMA swala la nani ni mgombea urais si swala tena bali tunachojiuliza hapa tu ni kwamba je mfumo wa KIFISADI tunaung'oa lini ili walalahoi tupate ahueni.

Sana sana kinachohitajika hivi sasa kwenu, endeleeni na kazi ya kutimiza zile ahadi 100 zile kwa wananchi na wala msipoteze wakati kwa kubuni hiki na kile kwa CHADEMA maana hakuna hata anayeguswa na hayo.

Wana-CHADEMA sote tunajua tulikotoka, tunafahamu wapi tulipo, na tuna uhakika na wapi huko tunakokusudia kwenda hivyo tumieni muda kutimiza ahadi kwa wananchi badala ya leo hoo mara kesho heee, bure kabisa wala hamna kitu hapo!!

Mwisho kabisa lazima nimpe pongezi nyingi sana Dogo Nape kwamba sasa vijana wake hapa jukwaani wanastahili japo kanyongeza ya mshahara maana wanahangaika kweli kweli sema tu kwamba mambo yenyewe ndi kamwe hayaendi hata kidogo.

Hakika ukweli wa mambo ni kwamba tangu siku nyingi mno WATANZANIA TAYARI TUMEAMUA NA KUWEKA NADHIRI NA CHADEMA CHINI YA UONGOZI IMARA WA DOKTA SLAA NA VIONGOZI WENZAKE KAMA TIMU MOJA.!

Kwa taarifa yenu CHADEMA ni imara kama mwamba leo kuliko hata hapo jana. Wana-CHADEMA wote mshikamano mbeeeeele kama tai tangu mashinani hadi uongozi wetu taifa huku tukiendelea kumunga mkono Dokta Slaa, Freman Mbowe pamoja na viongozi wetu wengine wote pamoja sana!!!!!!!!
 
Mimi sitaki kuizungumzia chochote hiyo habar, tatizo langu kwako zitto ni ''Kwanin Zitto uanze kujisemea mwenyewe kuwa unasifa za kuwa rais wa Tanzania?'' tuache watanzania tukusemee kuwa unazo sifa stahiki za kuwa rais wetu, sio wewe kuanza kututajia sifa zako kama vile wewe ni mgeni kwa watanzania . . . . .ushaur wangu kwako Zitto, fanya majukum yako mwisho wa siku watanzania tutaamua wenyewe, wewe sio mgen kwetu had upoteze muda kututajia sifa zako!!!!?
 
FJM

And who is constantly talking about mining companies to migrate to the new law?

Do you read my work?

Who is asking the government to ensure linkages of the sector?

We have a new law which is far better than the previous. I am very proud to be part of the team, to be the main agitator for the reforms in the sector.

Today no foreigner is allowed to own a licence for gemstone. TanzaniteOne wanahaha sasa kupata leseni.

Kuna aya ya Quran inasema, wana macho lakini hawaoni. Wana masikio lakini hawasikii nk.

Zitto, nafurahi kwamba ngozi yako inazidi kuwa ngumu na unajibu hoja/query hapa jamvini. Great stuff.
Kuna vitu viwili nilitaja:

1. Response yako bungeni baada ya Waziri mkuu kutoa list ya top 15 walipa kodi.Na hapa nikatumia Zitto machachari wa 2007 na Zitto wa sasa. Sina hakika kama Balozi Mwapachu yuko bungeni? Na sina hakika kama hiyo barua naweza kupata nakala yake toka kwenye hansard za bunge? Sina hakika.

2. Kwenye level ya kawaida, nimeonesha wasiwasi wangu kwa kula chakula ambacho 'implicitly' kiko contaminated. Mabati vs kusimamia the very same mabati buyer! Inawezekana immunity level yako iko juu hivyo hautapwata na homa but what if? Na hapa ndio nikasema you are young fine politician, lakini uwe makini na maamuzi yako.

Zitto mimi na wewe tunaweza kulumbana sana hapa JF. But dont forget you are the one vying for an office. You are better off taking whatever contributions written in this forum (bad or bad) and use it to shappen your game. Ni sawa na kupata consultations toka kwa wananchi - for FREE. Watu wanakuambia exactly what they think na wapi pa kuimarisha. Open your mind buddy!

Nirudie nilichosema, I like Zitto wa 2007. He was just Zitto.
 
Zitto Kabwe anaogopa kivuli chake.Nimesoma andiko lake amejaribu kijielezea watu wamjue yeye ni nani.Mwanaharakati wa kweli hatakiwi kujisifia kwa machache mazuri aliyofanya tena ukizingatia anachokipigania bado hajafanikiwa kwa kiwango hicho.

Prof. Baregu,Ananalie Nkya,K. Bisimba,Dr. Slaa,T. Lissu ...nk Hawajatoa mandiko/machapisho ya kujisifia kueleza waliyofa
nya ili wajulikane.Wamejulikana kwa kazi zao .

My take;
Zitto fanya kazi acha kukurupukia social media kujinadi.
 
Kinachokusumbua wewe ni udini tu. Jaribu kuangalia habari imetoka wapi sio kukurupuka. Labda anaongelea urais 2025 Dr Slaa akishamaliza vipindi vyake, which kila mwana CDM atamuunga mkono. Lakini kwa sasa Zitto HAJAKWIVA kuwa rais na hata katiba haimruhusu

inaonekana hujui hata msingi wa hoja,wanaume wanajadili mapungufu ya katiba iliyopo kwenye suala la umri wa kugombea urais,we unajifunika na mwamvuli huohuo wa katiba chakvu kweli mvua ya hoja imeinyea akili yako kiasi kwamba imetota haiwezi kupembua inachokiona!
 
Why zito with j.makamba, and not with mnyika, T. Lissu, mdee or lema. Zito hueleweki umezidi kuambatana na hao magamba ndio maana napata wasiwasi kwanini hushirikiani na watu ambao unaoendananao kiitikadi na mara kwa mara kwenye misimamo yako upo na j.makamba?

Je katiba ya chama chake inamkataza kuwa na ukaribu na Makamba? kama jibu ni ndio kwanini msimvue uanachama? acheni siasa za kijinga wakuu hivi wewe kama ni cdm huna ndugu ambae ni tlp? hamsocialize? kwa kuwa tu huyo ndugu yako hayupo chama kimoja na wewe? au ndugu zako wote ni wa chama unachikisapoort?

Msimsakame Zitto yeye ni mtu jasiri amethubutu kusema tofauti kama wengine wanavyoeleza chini chini au hujasoma hii kitu iliyoandikwa na wabara?

Mshauri mkuu wa chadema ndugu, Kitila Mkumbo alitembelea Uingereza katika miji ya London na Readings kuanzia tarehe 5 Machi na 6 Machi 2012 na kuondoka tarehe 10 Machi, 2012.


Miongoni mwa mambo aliyotueleza ni kuwepo kwa mpasuko wa nani anasitahiri kubeba/kupeperusha bendera ya chadema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kati ya Freeman Mbowe na Dk. Slaa. Mkumbo anasema kuna kambi mbili zinazopingana ndani ya chadema kuhusu suala hilo.

Wanaomuunga mkono Dk. Slaa wanasema kwamba ni mtu anayejua kujenga hoja, ana mvuto, wananchi wanamwamini kuliko Mbowe lakini pia kwamba Dk. Slaa alishinda uchaguzi mkuu wa 2010 kabla ya kuchakachuliwa. Kwa sababu hiyo akipewa nafasi tena 2015 na chadema ikisimamia vyema uchaguzi huo Dk. Slaa anaweza kuwa Rais ajaye.



Kambi ya mbowe inasema kwamba alitumia asilimia 72 ya pesa yake katika kufanikisha kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010, wapo wanaodai chama kirudi mikononi mwa Mbowe kwa sababu hivi sasa ameimarika zaidi kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi mkuu ujao. My take: Kuendeleza huo mpasuko kutaisaidia ushindi wa CCM katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.


Wadau nimeleta kwenu tusaidiane namna ya kutafuta ufumbuzi wa mpasuko wa kambi mbili hizi ili chadema kiendelee kuwa chama kikuu cha upinzani na pengine kushika dola mwaka 2015. Source: Nilikuwa Uingereza miongoni mwa wafuasi wa chadema tuliohudhuria kikao cha kamanda wetu Kitila.

Hatujamsikia Mheshimiwa Mbowe akisema kama anautaka urais ila ukisoma hiyo habari utaona kuwa kuna kundi lake ndio linataka Mhe asimame 2015! Kundi lake linaenda chaka sababu wanayoitoa ni kuwa Mbowe ametumia pesa zake sasa wanamaana inabidi Mbowe awe Rais arudishe pesa zake? mfike mahali muwe mnaleta hoja zisionekana zina maslahi binafsi. Hakuna mtu asietaka kiongozi mwenye uchu wa maendeleo na hakuna atakae kiongozi mwenye uchu wa mali unless/only and if uchu huo huyo mtu atanufaika nao.

Vyama vyote vya siasa vitakuwa na mitikisiko kuelekea uchaguzi wa 2015 cdm hasa wanajf wengi humu mmekuwa mkimshutumu Pro Lipumba kugombea kila mara kama hakuna mtu mwenye uwezo mwingine zaidi yake, kwa kumpinga Zitto na Mbowe na kutaka Slaa aendelee mtajitofautisha vipi na CUF? Mbowe alishajaribu kadhalika na Dr Slaa pia hamuoni sasa apishwe mtu mwingine mwenye ambition atakaeweza kuwawakilisha 2015? nadhani kama mnaamini chama chenu kina sera thabiti swala la nani asimame halitakuwa gumu kwenu.

Tafakari.
 
Ndugu zangu. Naomba msome makala nzima kabla ya kuchangia. Msichangie kwa kusoma kichwa cha habari tu. Hii ni makala nimeandika kama majibu kwa makala ya mwanazuoni mmoja kuhusu umri wa Urais.

Nimesema wazi, kuutaka Urais na kuupata ni mambo mawili tofauti. Kwanza lazima chama changu kiniteue. Kama chama kikiona bado lazima nikubaliane na chama. Kama chama kikiona kuna mwanachama mwingine ana uwezo zaidi yangu lazima nimwunge mkono huyo. Hata kama chama kikiniteua lakini wananchi lazima wakubali. Kwa hiyo unaweza kuutaka Urais lakini usiupate!

Pili nimejibu hoja za ubaguzi, hatari na matabaka za mwanazuoni huyo. Ni vizuri MoD akachukua makala hiyo na kuiweka juu kabisa ili watu wachangie jambo walilolisoma.

Miye nitaweka makala hiyo kwenye blog yangu zittokabwe.com

Mkuu JF siku hizi wachambuaji wa hoja kabla ya kuchangia wamepungua sana kwenye jukwaa la siasa. Pole sana ila ndo Tanzania yetu hii. pole pole tutafika

nakuomba ujitahidi chama kishinde huko Kirumba na uwaunge mkono makamanda wenzio wa arumeru Mashariki ili muongeze mbunge mwingine.
 
The ultimate ambition of ANY politician worth his name is to be a head of state,short of that huna haja ya kujiita mwanasiasa.Anachofanya Mh Zitto hapa ni ku flow na gravity,whether huko njiani atakumbana na magogo,miamba,mabomu ya kutega,maharamia wa majini,mi scud,misumari,tsunami,matingatinga etc that will be entirily another matter.

Nawasilisha,
Bishanga Abashaija Bepari la kihaya.
 
Zitto Kabwe anaogopa kivuli chake.Nimesoma andiko lake amejaribu kijielezea watu wamjue yeye ni nani.Mwanaharakati wa kweli hatakiwi kujisifia kwa machache mazuri aliyofanya tena ukizingatia anachokipigania bado hajafanikiwa kwa kiwango hicho.

Prof. Baregu,Ananalie Nkya,K. Bisimba,Dr. Slaa,T. Lissu ...nk Hawajatoa mandiko/machapisho ya kujisifia kueleza waliyofa
nya ili wajulikane.Wamejulikana kwa kazi zao .

My take;
Zitto fanya kazi acha kukurupukia social media kujinadi.

mkosoe kwa hoja,hakujiunga Chadema baada ya kuchakachuliwa kura na CCM kama wengine,hakuna mwanasiasa asiejisifia,nitajie hata mmoja ili nikiri kuwa sifahamu siasa,hata Mwl Nyrere ambae ndo kioo cha wanasiasa alikuwa akijisifia kwa mazuri alokuwa anafanya, pitia andiko la zitto then edit kila kwenye jina la zitto andika la yule jamaa yako ili uridhike,sera za CDM unazotamba nazo mitaani ni jasho la mboe na zitto upende usipende,usifie usisifie!
 
FJM

And who is constantly talking about mining companies to migrate to the new law?

Do you read my work?

Who is asking the government to ensure linkages of the sector?

We have a new law which is far better than the previous. I am very proud to be part of the team, to be the main agitator for the reforms in the sector.

Today no foreigner is allowed to own a licence for gemstone. TanzaniteOne wanahaha sasa kupata leseni.

Kuna aya ya Quran inasema, wana macho lakini hawaoni. Wana masikio lakini hawasikii nk.

Na wana macho, lakini hawaoni kwayo. Na wana masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni kama nyama howa, bali wao ni wapotofu zaidi. Hao ndio walio ghafilika.
 
Mkuu JF siku hizi wachambuaji wa hoja kabla ya kuchangia wamepungua sana kwenye jukwaa la siasa. Pole sana ila ndo Tanzania yetu hii. pole pole tutafika

nakuomba ujitahidi chama kishinde huko Kirumba na uwaunge mkono makamanda wenzio wa arumeru Mashariki ili muongeze mbunge mwingine.

Bitabo,

Naona sasa mjadala unaanza kuwa balanced.watu wameanza kuelewa kuhusu hii debate..........!

Kuna watu wanapima upepo utawaona watakavyokuja hapa kujifaragua na kujifanya weledi lakini watajenga hoja nje ya mantiki.Kuna wengine watakuja watajenga hoja basid on logic

Zaidi,tusubiri vijigazeti uchwara na siku hizi viko vingi.Anyways,Mwanahalisi halitabaki nyuma katika kujaribu kurudisha imani ya weledi.................!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom