tatizo la hili jukwaa wote sisi tunajidai ni watu wa kukosoa. Ukiuliza ebu great thinker chagua wizara , shiraka au jimbo moja unaloweza kuwa kiongozi. Taja mikakati mipango na maamuzi gani utafanya. Only few can answer this question
Most of us are just reactive waiting Ziitto to do this or kikwete to do this or Slaa to that.
Please let stop this trend.
Musembi Ungekuwa wewe ndo zitto ungefanya nini?
umeongea kweli ndugu huu ni mkakati ambao una mgongo wa vizito wa chadema nia yao kumuundosha zitto katika duru ya siasa lkn kamwe wakimuuondosha kwa hila yyte ile na wao wajichimbie kaburi lao
Kati ya vitu ambavyo CHADEMA wame-prove kuwa wapo makini ni namna ambavyo wameweza kum-handle Zitto, chama ndiyo kilimfikisha hapo alipo, umaarufu wake ulianza pale alipotolewa bungeni lakini CDM ikaamua kumbeba na kuunganisha watu ili ichukulie kitendo cha kufukuzwa bungeni na matokeoa ya ushujaa wake, na msimamo dhidi ya maslahi ya taifa, kweli watu wakjitokeza kwa wingi baada ili kuitikia wito wa chama.
Alipoona makutano ya watu kiasi kile akajua hii ni shauri ya yeye kama yeye kama Zitto na si chama, imani ikajengeka ndani yake kuwa yeye ni zaidi ya chama, akaanza kufuata utashi na hisia zake, kama treni iliyoacha reli...waandishi waliokuwa wanamsifia wakaona mwelekeo wake hatari, Kibanda akaandika kuonya, Ngurumo akaandika, Happiness Katabazi akaandika, wengi wakaandika, sikio la kufa halisikii dawa, magazeti makini yakaachana naye, akaenda kuibukia kwenye magazeti ya udaku, akayashambulia magazetu yetu kuwa, magazeti ya udaku ndiyo yenye nguvu na yasomwayo na watu wengi duniani, hakufafanua watu wa aina gani. Muda si mrefu urafiki na magazet hayo ukaisha baada ya kuandika skendo zake za ngono na wasichana kadhaa wanaodhani kuwa majina yao ni makubwa hapa nchini, kumbe yanafahamika tu na wala hayana ukubwa wowote.
Turudi kwenye mada...akazua hali ambayo ilitafsiriwa kama kizaazaa ndani ya CDM, nadhani alifanya makusudi ili afukuzwe aondoke "kishujaa"(kama alivyopokewa jangwani) kwasababu kuna watu ndani ya CCM walimdanganya kuwa akifukuzwa na hata akiipoteza nafasi ya ubunge, atapewa wa kuteuliwa na rais, pia kupewa unaibu waziri, na ili kumhakikishia hilo akajengewa ukaribu na idara za usalama na watu mashuhuri walio pretend kwenda kwake kupata ushauri na msaada wa mambo kadhaa, akazidi kuwa jeuri, lakini maskini kijana huyu hakujua kuwa watanzania walishamuona kimeo muda mrefu uliopita kiasi cha viongozi wa CDM kuwekwa katika msukosuko na wananachama wao kuwa kwa nini wanamlea, lakini uongozi ulionyesha ukomavu kwa kuendelea kuwa naye na kumkumbusha maadili ya chama na siasa kwa ujumla.
Kabla ya kampeni mwaka za mwaka jana, alitishia kutogombea, lakinibaadaye akapima akapima akaona namna maisha yatakavyokuwa magumu nje ya siasa, kwani hakuna kazi itakayomlipa kama siasa, ukichukulia kwa muda huo alishaamua kushiriki siasa kwa maslahi binafsi, hivyo akabatilisha msimamo wake na kuamua kutetea kiti chake, kampeni zilipowadia, akijua kuwa chama chake kimesimamisha mgombea wa nafasi ya urais, lakini akaonyesha kuibeza hatua hiyo kwa kusema kuwa, tunakwenda kuchagua wabunge na madiwani kwani rais tayari tunae tumuache amalize muda wake, lakini uongozi wa CDM uliendelea kumvumilia, Kitendo hicho cha uongozi wa CDM kuendelea kumvumilia kimebomoa sana Image ya Zitto kwa jamii,na kuifanya CDM ionekana kama chama imara kinachoweza kuishi pamoja hata inapotokea wakatofautiana mawazo kati yao.....kwa hili CDM nawapa sifa sana. Zitto amechuja lakini hilo halitambui tena kwasababu sasa hivi anaishi kwa kutegemea taarifa za wapambe. Ameaminishwa kuwa kila ampingae ni walewale wanaotumiwa dhidi yake.
Sasa hivi ni naibu Kiongozi wa kambi ya Upinzani bungeni anaongoza watu wasio mkubali watu ambao walipiga kura ya kumkataa, maamuzi ambayo hayakuwahi batilishwa popote pale, lakini kwasababu ya upenzi wake kwa madaraka bila kujari anaongoza kwa mazingira gani as long as anapata chake, katika hili Zitto hataki kutumia akili yake kama mwanasiasa kijana na msomi kama anavyotaka kutambulika, ameamua kung'ang'ania madaraka hayo bila suluhu ya aina yoyote, hataki kupisha nafasi hiyo kwa mtu mwingine anekubalika.
Zitto ambaye nahisi kila aonapo wakina Mnyika, Lema Lissu na wengineo wakitoa hoja zinazotikisa bunge huwa hajisikii vizuri kwa kuumia moyo, akitamani hali hiyo ya bunge kutetemeshwa kwa hoja ingesababishwa na yeye. alijaribu kutengeneza 'msukule/Zombi' wake pale bunge (Kafulila), lakini sijui ulipoishia, japo kuna yule bint, simkumbuki jina lake ila nadhani ni wa viti maalum CDM, lakini wote wapo off-color.
Huyo ndiye Zitto kabwe, ambaye sasa anataka atambulike kama rais mtarajiwa, kwani ameshatangaza dhamira yake ya kugombea urais mwaka 20015, Zitto ambaye watu wakimkubusha wajibu yeye anadhani ni watu wanaomuonea husda kwa 'mafanikio' yake kisiasa, Zitto anayeamini moyoni na kichwani mwake kuwa yeye ni zaidi ya chama, lakini mdomoni anahubiri kuwa hakuna aliye zaidi ya chama.
Nimeandika si kwa mtiririko rasmi wa uandishi na utoaji habari, bali kwa mtindo wa kugusia gusia tu ili kukumbusha, kwa lengo la kuendelea kufikiri na kutafakari kwa pamoja.
Agenda yenu ya kumuuwa Zitto kisiasa kamwe haitafanikiwa, kila ukifungua JF ni Zitto tu, kwani Zitto atakuwa na umri gani 2015, kama sio njama tu za kumuuwa kisiasa. Naona siasa za kupakana matope zinainyemelea CDM. Jengeni hoja mmeandaa mpango gani wa kutatua kero za wananchi mkichukua madaraka, watu wanajua ipi pumba na upi mchele, watachagua tu wanachokitaka
Anazushiwa yapi mkuu.watu hapa wanajadili maneno na vitendo vyake na si mambo ya nyuma ya pazia,utaje huo uzushi basi.mbona akitoa hoja za msingi bungeni kila mtu humu anamsifia?bado naamini Zitto ana move aliyopania kuifanikisha and time will tell kwasababu hawezi kuikimbia cdm kwa mazingira ya sasa ya kisiasa.Nyerere alikuwa Kichwa lakini daima mnyenyekevu na hiyo hata ukimwangalia unaona inatoka moyoni na penye mgongano wa mawazo alitumia nguvu ya hoja na watu wote kumuunga mkono na hatujawahi sikia kuwa aliwahi kushawishi watu kwa hila ili aungwe mkono.kweli mkuu hii ni kweli watz wengi kazi kulalamika tuuuuuuuuuuu lakini ukimwambia toa option hana kabisa ..pale cdm kuna watu kibao wanamuona zitto ni tisho kwao wanakaa wanazusha tuu inakera sana
Wewe mama mtu mzima unasubuliwa na upenzi au maslahi kwa Zito. Huyu si wakumwani kabisa. Mtoa mada ameleza vizuri kabisa kama hujaelewa, basi toa hayo maslahi yako binafsi usome tena. Mimi sina imani na huyu mtu mpaka mwisho wa dunia.Zitto practices modern politics,siasa zinazo endana na dunia ya leo.tatizo wana CDM wengi wapo biased na wmekaa ki chama chama zaidi kuliko ku focus issues...hii kasumba ipo ccm pia,so its the same trend,mzimu huu unawakumba wana CDM bila ya wao kujua..
Mfano: Zitto alipogombea uenyekiti wa CHADEMA ...hapa ndo matatizo yalipo anza na Zitto kuonekana mtovu wa nidhamu,mroho wa madaraka,puppet,ametumwa na mafisadi.kila neno baya alipewa.
Ukweli ni kwamba alikua anatimiza wajibu wake kama mwana chama na kwa kua muda ulikua umefika wa uchaguzi, katiba na kanuni zina mruhusu kugombea alifanya hivyo...
Mbowe na wapambe wake wakati wa uchaguzi wakaleta hoja ya uchanga wa chama,mara chama kitagawanyika na kumshauri zitto ajitoe, yes alikubali. Kama matatizo ya kugawanyika chama na chama kua bado kichanga kuhimili vishido vya uchaguzi, kwanini MBOWE aliye liona tatizo hili mapema asinge jitoa yeye kumpisha Zitto?
Jamani kila siku Zitto, Zitto, Zitto mbona majungu mengi kwa huyu mtoto kuna nini? Hao malaika wenu mbona hamjawahi kuwaandika vibaya au hawana mapungufu kabisa?
Kati ya vitu ambavyo CHADEMA wame-prove kuwa wapo makini ni namna ambavyo wameweza kum-handle Zitto, chama ndiyo kilimfikisha hapo alipo, umaarufu wake ulianza pale alipotolewa bungeni lakini CDM ikaamua kumbeba na kuunganisha watu ili ichukulie kitendo cha kufukuzwa bungeni na matokeoa ya ushujaa wake, na msimamo dhidi ya maslahi ya taifa, kweli watu wakjitokeza kwa wingi baada ili kuitikia wito wa chama.
Alipoona makutano ya watu kiasi kile akajua hii ni shauri ya yeye kama yeye kama Zitto na si chama, imani ikajengeka ndani yake kuwa yeye ni zaidi ya chama, akaanza kufuata utashi na hisia zake, kama treni iliyoacha reli...waandishi waliokuwa wanamsifia wakaona mwelekeo wake hatari, Kibanda akaandika kuonya, Ngurumo akaandika, Happiness Katabazi akaandika, wengi wakaandika, sikio la kufa halisikii dawa, magazeti makini yakaachana naye, akaenda kuibukia kwenye magazeti ya udaku, akayashambulia magazetu yetu kuwa, magazeti ya udaku ndiyo yenye nguvu na yasomwayo na watu wengi duniani, hakufafanua watu wa aina gani. Muda si mrefu urafiki na magazet hayo ukaisha baada ya kuandika skendo zake za ngono na wasichana kadhaa wanaodhani kuwa majina yao ni makubwa hapa nchini, kumbe yanafahamika tu na wala hayana ukubwa wowote.
Turudi kwenye mada...akazua hali ambayo ilitafsiriwa kama kizaazaa ndani ya CDM, nadhani alifanya makusudi ili afukuzwe aondoke "kishujaa"(kama alivyopokewa jangwani) kwasababu kuna watu ndani ya CCM walimdanganya kuwa akifukuzwa na hata akiipoteza nafasi ya ubunge, atapewa wa kuteuliwa na rais, pia kupewa unaibu waziri, na ili kumhakikishia hilo akajengewa ukaribu na idara za usalama na watu mashuhuri walio pretend kwenda kwake kupata ushauri na msaada wa mambo kadhaa, akazidi kuwa jeuri, lakini maskini kijana huyu hakujua kuwa watanzania walishamuona kimeo muda mrefu uliopita kiasi cha viongozi wa CDM kuwekwa katika msukosuko na wananachama wao kuwa kwa nini wanamlea, lakini uongozi ulionyesha ukomavu kwa kuendelea kuwa naye na kumkumbusha maadili ya chama na siasa kwa ujumla.
Kabla ya kampeni mwaka za mwaka jana, alitishia kutogombea, lakinibaadaye akapima akapima akaona namna maisha yatakavyokuwa magumu nje ya siasa, kwani hakuna kazi itakayomlipa kama siasa, ukichukulia kwa muda huo alishaamua kushiriki siasa kwa maslahi binafsi, hivyo akabatilisha msimamo wake na kuamua kutetea kiti chake, kampeni zilipowadia, akijua kuwa chama chake kimesimamisha mgombea wa nafasi ya urais, lakini akaonyesha kuibeza hatua hiyo kwa kusema kuwa, tunakwenda kuchagua wabunge na madiwani kwani rais tayari tunae tumuache amalize muda wake, lakini uongozi wa CDM uliendelea kumvumilia, Kitendo hicho cha uongozi wa CDM kuendelea kumvumilia kimebomoa sana Image ya Zitto kwa jamii,na kuifanya CDM ionekana kama chama imara kinachoweza kuishi pamoja hata inapotokea wakatofautiana mawazo kati yao.....kwa hili CDM nawapa sifa sana. Zitto amechuja lakini hilo halitambui tena kwasababu sasa hivi anaishi kwa kutegemea taarifa za wapambe. Ameaminishwa kuwa kila ampingae ni walewale wanaotumiwa dhidi yake.
Sasa hivi ni naibu Kiongozi wa kambi ya Upinzani bungeni anaongoza watu wasio mkubali watu ambao walipiga kura ya kumkataa, maamuzi ambayo hayakuwahi batilishwa popote pale, lakini kwasababu ya upenzi wake kwa madaraka bila kujari anaongoza kwa mazingira gani as long as anapata chake, katika hili Zitto hataki kutumia akili yake kama mwanasiasa kijana na msomi kama anavyotaka kutambulika, ameamua kung'ang'ania madaraka hayo bila suluhu ya aina yoyote, hataki kupisha nafasi hiyo kwa mtu mwingine anekubalika.
Zitto ambaye nahisi kila aonapo wakina Mnyika, Lema Lissu na wengineo wakitoa hoja zinazotikisa bunge huwa hajisikii vizuri kwa kuumia moyo, akitamani hali hiyo ya bunge kutetemeshwa kwa hoja ingesababishwa na yeye. alijaribu kutengeneza 'msukule/Zombi' wake pale bunge (Kafulila), lakini sijui ulipoishia, japo kuna yule bint, simkumbuki jina lake ila nadhani ni wa viti maalum CDM, lakini wote wapo off-color.
Huyo ndiye Zitto kabwe, ambaye sasa anataka atambulike kama rais mtarajiwa, kwani ameshatangaza dhamira yake ya kugombea urais mwaka 20015, Zitto ambaye watu wakimkubusha wajibu yeye anadhani ni watu wanaomuonea husda kwa 'mafanikio' yake kisiasa, Zitto anayeamini moyoni na kichwani mwake kuwa yeye ni zaidi ya chama, lakini mdomoni anahubiri kuwa hakuna aliye zaidi ya chama.
Nimeandika si kwa mtiririko rasmi wa uandishi na utoaji habari, bali kwa mtindo wa kugusia gusia tu ili kukumbusha, kwa lengo la kuendelea kufikiri na kutafakari kwa pamoja.
Tusimshambulie msembi hayo ni mawazo yake,pia naomba nimuunge mkono msembi,hebu niulize wapenda mageuzi ktk tanzania hii inayomilikiwa na watu wachache,yuko wapi zitto kama yule wakati ni kiongozi UDSM?yukowapi zitto kama yule kabla hajafukuzwa bungeni?yuko wapi zitto kabla hajateuliwa kuwa mwenyekiti kamati ya hesabu za mashirika ya umma?jibu siyo zitto yule tuliyemzoea kabadilika hata ufunguzi wa matawi ya chama chake UDOM,ST JOHNS,MIPANGO,na kwingineko hatujamwona akijihusisha kitu ambacho kwa miaka ya nyuma ni lazima yeye ndo angekuwa mstari wa mbele,ni ukweli usiofichika mh zitto anahitaji kurudi kundini kabla ya huo uamzi wake huo na sisi kama vijana tuko tayari kumpokea kwa gharama yoyote maana hiki ndo chama pekee chenye kutufikisha safari tuliyoianzisha.TOGETHER WE CAN.dalali