Huyu ni mmoja kati ya waliopewa kazi ya kumchafua JPM, lengo likiwa ni kujaribu kufuta picha ya JPM mioyoni mwa Watanzania walio wengi baada ya kuona kila wakijaribu kufanya nini hawawezi kufikia kasi ya JPM hata kwa 1 ya 10.
Wamefanya utafititi wakagundua kuwa, zaidi ya 90% ya Watanzania bado wanamkumbuka, wanampenda na wanamuenzi JPM kwa kiwango cha juu sana.
Ili kujaribu kupunguza wingi huo wa Watanzania wanaomkubali JPM, wameamua kumshambulia Hayati JPM kwa namna mbalimbali.
Mimi nasema hivi, hata kama watatunga uongo wa kila aina kumchafua JPM, kamwe, kamwe, kamwe, kamwe, kamwe, hawataweza.
MOTO WA JPM siyo wa kitoto. Tofauti na mioto mingine, MOTO WA JPM kila wanapojaribu kuuzima, ndo unawaka mara mia zaidi.
NB:-
JPM mbolea sh.45,000/- na sasa sh.130,000/+